Meneja: Uwanja wa ndege Chato unahudumia abiria 250 kwa mwezi

Meneja: Uwanja wa ndege Chato unahudumia abiria 250 kwa mwezi

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Serikali ifanye uamuzi mgumu, hii ni biashara ya hasara, nadhani ATCL wajikumbushe sababu zilizofanya ATC ikafilisika, abiria sita ni sawa na milioni mbili laki nne kwa nauli ya laki nne, Dar-Chato direct flight, maana yake kama ni dreamliner siti nyingi hazikaliwi,inaenda tupu kwa asilimia 98

======
Kamati ya Barabara ya mkoa wa Geita imefanya ziara ya kukuagua barabara mkoani humo kikiwemo kiwanja cha ndege cha Geita kilichopo wilayani Chato na kuridhishwa na mwenendo ukamilishaji ujenzi wa kiwanja hicho sambamba na utoaji huduma ya usafirishaji

"Tumeshahudumia abiria – in-bound na out-bound – kama 3000. Yani kwa mwezi, on average, ni kama abiria 250 mpaka 300 ambao wanatumia kiwanja hiki" Amesema afisa wa Chato Airport

Naye Rosemary Senyamule, Mkuu wa Mkoa wa Geita, amesema:

"Tumeuona ni mradi ambao una viwango ambavyo ni vya juu na haujawahi kupata ufa, haujawahi kupata ajali yoyote. Ni uwanja ambao tangu umejengwa ni imara na umeendelea kutumika mpaka sasa...

… sanasana tuendelee kualika abiria. Tuna safari mbili kwa sasa lakini tunategemea kupata safari tatu kwa wiki. Tuendelee kuwakaribisha watu waendelee kuutumia uwanja huu kwani ni mzuri na wenzetu wa ATCL wametuletea ndege zinakuja. Tuendelee kuunga mkono juhudi kwa kuutumia uwanja huu kama ambavyo wengine wanaendelea kufanya.

Bado tunawakumbusha wenzetu wa ATCL waturudishie route tuwe na siku tatu kwasababu abiria ni wengi. Mnaosimamia hapa muendelee kutunza miundombinu hii… kama ambavyo serikali imewekeza fedha nyingi katika eneo hili

Tumeambiwa zaidi ya bilioni 59 zimetumika kuweza kukamilisha hizi hatua ambazo zipo…"


=====

Screenshot_20220127-153217_1.jpg
 
#miradiYAhovyo

Mama apige chini uendelezaji wa kiwanja hiki, kilipofikia panatosha, bilioni karibu 200 unajengea watu sita? Pengine ni wanafamilia wa mwendazake tu wanaopenda kuangalia kaburi
 
Umekosea hesabu mkuu, sidhani kama ina safari za kila siku. Assume ina safari nne kwa mwezi itakuwa ni abiria 50 kwa safari. Labda hoja iwe uwekezaji mkubwa uliofanyika kwenye uwanja kwamba haukuwa na maslahi kiuchumi.
 
Mimi nashauri siku maji yakizidi unga tukope hela nyingiii halafu bondi tuweke huu uwanja wauchukue tu🐒
Naunga mkono hoja, Wachina ndio wanapenda bond za hivi, tuchukuwe pesa za wachina tuwaachie uwanja huo useless kabisa.
 
Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Chato amesema uwanja huo umefikia 95% ya ujenzi wake na kwamba uwanja huo umekuwa msaada mkubwa sana kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na nchi jirani.

Meneja amesema mpaka sasa kwa wastani wana hudumia abiria 250 kwa mwezi na ndege za Shirika la ATCL zinatua uwanjani hapo mara 3 kwa wiki. Pia Shirika la TANAPA wanatumia mara kwa mara uwanja huo kwa shughuli zao za uhifadhi.

My take.
Huu ni uthibitisho tosha kuwa kila alichofanya Magufuli alifanya kwa masilahi ya taifa hili, na ujumbe huu uwafikie wote wenye roho za korosho na wapinga maendeleo wote ikiwemo timu gaidi.

 
Back
Top Bottom