Meneja wa TRA Kibondo akamatwa na meno ya tembo

Meneja wa TRA Kibondo akamatwa na meno ya tembo

Hii nchi imekuwa ya hovyo, mtu anayelipwa milioni 3 kwa mwezi gross anakatwa kodi karibia laki 6 na ushee.....wakati wafanya biashara wakubwa wenye mitaji ya milion 50 na zaidi hawalipi kodi ipasavyo. Serikali inawabana sana watumishi private na public kwa kodi kubwa ya PAYE. Na ndio kodi wanayoitegemea sana.
Bora kutafuta suluhu mtaani. Mwamba kapambana.
Kapambana kipo wapi mzee???

Wote wewe mfanyakazi na wafanyabiashara tunajua kuna mianya yenu ya upigaji ridhikeni nayo msiende kwenye jinai mbaya kama hizi ona kijana fresh alitegemea afanye mengi kwenye maisha yake lakini sasa kazi hana na bangili amekula.
 
Aisee! Tuseme kwamba mshahara anaopata pamoja na marupurupu ya Cheo Cha Umeneja wa TRA havitoshelezi mahitaji yake ya msingi ya kiuchumi? Is it??

Ama kweli kwamba Ufisadi ni tabia, Wala siyo kwa sababu ya kipato kidogo kisichokidhi mahitaji.

Kwani huoni matozo yanavumbuliwa kila leo! Srkl haitosheki na ilichonacho

Kweli peponi wataingia wachache sana
 

Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma linamshikilia Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Wilayani humo Irving Mutegeki kwa tuhuma za kukutwa na meno ya Tembo.

Mutegeki Bagasheki amekamatwa na nyara hizo za Serikali Wilaya ya Kibondo Julai 2, 2024 akiwa kwenye gari binafsi majira ya usiku na anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Meneja huyo wa TRA anadaiwa amekuwa akifanya biashara ya meno ya Tembo kutoka Wilaya ya Kibondo na Kakonko kwenda mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi ikiwemo Burundi.
Tamaa mbaya ...
 

Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma linamshikilia Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Wilayani humo Irving Mutegeki kwa tuhuma za kukutwa na meno ya Tembo.

Mutegeki Bagasheki amekamatwa na nyara hizo za Serikali Wilaya ya Kibondo Julai 2, 2024 akiwa kwenye gari binafsi majira ya usiku na anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Meneja huyo wa TRA anadaiwa amekuwa akifanya biashara ya meno ya Tembo kutoka Wilaya ya Kibondo na Kakonko kwenda mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi ikiwemo Burundi.
alikuwa anatumia gari ya serikali au vipi? pia, hapo mbona rahisi tu, atauza nyumba, analipa kwa plea bargaining, imeisha hiyo. tembo nadhani gharama yake kama 30m, wakipiga mara tatu 90m anatoka fresh. ila kazi ndio hana tena. wao wanaita hizo ni bahati mbaya kazini. inawezekana kashakusanya nyingi zaidi ya hizo, na mawakili wa serikali walivyo wabaya watapora hata nyumba na magari aliyonayo.
 
Siku hizi TRA hakuna maokoto ya kutosha mpaka viongozi mnafanya biashara haramu?

top level manager kabisa, umezingua sana
TRA maokoto ya kawaida sana,, ishu ni chocho la kula pesa haramu kama wale wazee wa bandari tu ,labda wale wa vyeo vya juu maokoto yana maajabu kidogo, ila huku kwa wakina ofisa ni kawaida sema njia za kula nje ya mshahara ndo nyingi
 

Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma linamshikilia Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Wilayani humo Irving Mutegeki kwa tuhuma za kukutwa na meno ya Tembo.

Mutegeki Bagasheki amekamatwa na nyara hizo za Serikali Wilaya ya Kibondo Julai 2, 2024 akiwa kwenye gari binafsi majira ya usiku na anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Meneja huyo wa TRA anadaiwa amekuwa akifanya biashara ya meno ya Tembo kutoka Wilaya ya Kibondo na Kakonko kwenda mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi ikiwemo Burundi.
Awaambie alikua anaenda kutengenezea tusker amwagilie moyo
 
Back
Top Bottom