Niliichukia Real Madrid baada ya kuwatoa Bayern Munich kwa kubebwa hapo Bernabeu,na kiukweli nimefurahi kufungwa kwao na Barca ingawa sio mpenzi wa Barca.
Lakini kuna tofauti katika hivi vikosi,Madrid Wengi wa wachezaji wake ni Wazee na wameshachoka baada ya kufikia kilele cha mafanikio,Ronaldo hana njaa tena na ameridhika na mataji na mataji binafsi na record alizoweka au kuvunja na umri pia umeshamtupa mkono kimpira,mara nyingi wanashinda kutoka na Ujuzi binafsi na Uzoefu,hawana Mpira wa kutisha kama tulivyoizoea Real Madrid kwa misimu miwili mitatu iliyopita walipokuwa kwenye peak,then bado Zidane ana mbinu za kizamani katika ufundishaji wake,mifumo ya miaka ya 2000's ya Uingereza,Timu yake haina radha ya Mpira magoli mengi ni ya either kuvizia or counter attack,ndio mana Perezi pamoja na kushinda Kombe la UEFA bado hajaridhishwa na kiwango cha Zizou katika ufundishaji,Zidane sio muumini wa wachezaji Wenye Vipaji ndio mana unaona Mtu kama Hames Rodriguez akiwa banch au Morrata huku Benzema akipata nafasi kwenye kikosi chake.
Kwa Upande wa Barcelona,nayo now wanajijenga upya baada ya kuanguka katika msimu ya hivi karibuni,baada ya kuondoka Pep Gurdiola Barcelona ilipoteza ufalme wake bara ni Ulaya,wachezaji wengi waliokuzwa pale wameuzwa au kumfata Pep mfano Pedro,Alcantra n.k,so timu imekosa warithi wa Xavi,Iniesta,Mess,hivyo sasa kutegemea Zaidi Miujiza ya Mesi kama alivyofanya jana.
Hawa Watu watatu Xavi,Iniesta na Mess peke yao walikuwa na uwezo wa kupiga pasi si chini ya 600 per game.
Game na Man united pale Wembley walipiga pasi Zaidi ya 1000 huku Xav peke yake akipiga pasi si chini ya 400,utaona hiyo kasi,nguvu na skills hadi Fegurson akatetemeka, hakuamini kilichokuwa kinafanyika uwanjani utafikiri Play station.
Mess akienda ukingoni mzigo mkubwa unahamia kwa Neymar,na ndio mana nao sasa wanaingia sokoni kutafuta wachezaji badala la kutegemea la Masia kuziba nafasi za wakongwe na kurudisha soka lao la pasi nyingi.
Kiwango cha jana cha Mess ni hasira baada ya kushindwa kuperform kwenye game ya Juve na alijuwa udhaifu wa timu yake na Mzigo alioubeba.
Sitoshangaa kuja kwa Coutihno pale Barca,Griezman au hata Hazard kama watakuwa na mfuko mrefu.