Messi bado ni mchezaji mzuri sana

Messi bado ni mchezaji mzuri sana

Huyu Messi nilitamani sana siku moja kumwona akicheza EPL, kama ni mpunga tu watu waliweka mezani wa kutosha. Nilijiuliza sijui nini kilitokea, nilibaki na jibu moja tu, huenda hakuwa na mapenzi ya kucheza EPL au labda kuwa na ile fear ya jina lake kufunikwa au kupotea ghafla kulingana na nature ya ligi hiyo kinachopelekea yeye ku opt kwenda ligi nyepesi nyepesi.
EPL ndo ligi ngumu? Ligi ambayo mtu anabeba makombe kadri atakavyo? Emb pga hesabu vizuri uone takribani miaka 15 UEFA imenasa wapi hasa. EPL ni ligi ya kawaida tu, hiki ni kipindi ambacho vilabu vikubwa ulaya vimeanza kupoteza muelekeo hasa Spain na Italy.
 
Lakini tukumbuke pia Messi amezifunga timu zote kubwa za EPL alizokutana nazo

Man united
Chelsea
Man city
Liverpool
Arsenal

Na zote amewahi kuzifunga siyo chini ya goli mbili...sasa hii inadhihirisha hata angecheza EPL bado angewafunga tuu kama timu kubwa hizi kazifunga basi hao kina newcastle, everton na Westham angezifunga tuu...
Tukumbuke pia alizifunga zikiwa ktk ubora wao, Totenham alichapwa 2 na Messi, Lloris akiwa golini pale England.

Na zile goli mbili za Messi zote zilikuwa za ukatili, Lloris aliruka basi tu.

Hapo tuweke mbali akina Buffon, Neur wa Beyern, Iker Cassilas, Van Der Sa wa Man U n.k
 
Ongeza na Spurs hapo.
Watu wanajisahaulisha kuhusu Messi, tatizo tuna vijana wengi ambao wanaojua mpira kuanzia miaka ya 2018, hawa watakwambia kabisa Mbappe ni bora saaana kuliko Messi. Wasichojua ni kwamba kwa umri wa Mbappe, Messi kwa umri huo alikiwasha balaa, hakukuwa na dau la kumtoa Barca.
 
Miye ni timu Ronaldo Lia Lia
Jana CR7 kaiwezesha A Nassr kuingia semi final,hivyo na Messi,sijawahi kumkubari Messi,ila Kwa anayoyafanya uwanjani hakuna namna

Ile faulo ya Messi ni konyo

alicheza na nani? wacheza NFL wa California
 
Ronaldo anacheza na wauza kachori na wauza tende huko Saudia anapiga ndondo na akina Raja na Zamalek. Mashabiki wenzako wa Ronaldo wamekaa pembeni wanakuchora unambishia GOAT La pulga🐐.

Ronaldo anacheza na Benzema, Mahrez, Mane, Kante, Savic, Fabinho, Firmono, Banega, Messi anacheza na nani?
 
Ronaldo anacheza na Benzema, Mahrez, Mane, Kante, Savic, Fabinho, Firmono, Banega, Messi anacheza na nani?
MLS>Kebab league. Messi kaenda timu ya mkiani MLS kaeinua overall performance ya Inter miami wakati huo Ronaldo wote tumeona alichokifanya na Al Nassr
 
MLS>Kebab league. Messi kaenda timu ya mkiani MLS kaeinua overall performance ya Inter miami wakati huo Ronaldo wote tumeona alichokifanya na Al Nassr

Kwa maelezo yako Umethibitisha kuwa MLS ni circus
 
Back
Top Bottom