Messi Vs Pele

Mjadala wa Messi na Pele unakaribia kuisha now ni Messi na Mbappe

Mbappe ana hattrick kwenye fainali wc, Messi ana nini?

Wengi humu wapo kishabiki zaidi ya uhalisia wenyewe.. yani mbappe unamcompare na Messi kweli!!
 
Umeshawekewa sababu ya kwanini hilo lilitokea lakino bado unabisha

Sasa tutaweka rule kuwa kila mchezaji anatakiwa acheze ligi zetu

Na mwisho Messi atakosa sifa kwasababu hatujamuona kwenye NBC
Sasa kwakuwa Chama hajacheza Ulaya tunaweza kusema ndio best midfielder in the world?
 
Kwa hiyo kama Pele hatujawahi kumshuhudia unaliwekaje hili jambo?
Kama hatukuwahi kumshuhudia, inakuaje tuseme ni bora kumzidi Messi ambae tumemshuhudia? Kwamba tutumie clips za YouTube kujiaminisha kua Pele ni bora zaidi ya Messi tunaemuona day in day out?

Ni uongo!

Hoja kuu ya mashabiki wa Pele ni kwamba Pele alishinda world cup tatu. Tumewaambia, kushinda world cup sio kazi ya mtu mmoja. Ni kazi ya team nzima. Sote tumeona ambavyo Mbappe amekiwasha kwenye hii world cup japo France hawakubeba kombe. Je ni sahihi kusema Dybala ni mkali kuliko Mbappe, eti kwakua Dybala ameshinda world cup mwaka huu ambao Mbappe hajashinda?

Ndio maana wengi wetu tunaamini Messi angeendelea kua GOAT hata bila kushinda world cup.

Huyu Pele hata rekodi zake hazieleweki. Vijana wa sasa wakizifikia, anasogeza tena ili tu aonekane kua yeye ni bora zaidi. Ndio maana sisi ambao hatukumshuhudia akicheza, tunashindwa kuamini hizo takwimu zake. Hawa akina Messi na Ronaldo, kila kitu chao kipo recorded na tunashuhudia.


Anaanza Messi, then Ronaldo, alafu ndio hao wazee wanafuatia. Mimi sioni Pele anamzidi vipi Cristiano Ronaldo!
 
Mkuu ni kweli mpira wa zamani ulikuwa hardcore tofauti na sasa

Angalia kitu kidogo tu kama hiki



Huo ndio mpira uliokuwa unatumika miaka ya nyuma kipindi cha kina Pele, ni mpira ambao umeumdwa kwa material fulani non leather ambayo yanafanya mpira uwe mzito halafu hautembei chini

Katika kizazi hiki cha wapiga cross wangepata shida sana kwenye mpira huu.

Kuna mambo mengi sana juu ya changamoto ya aina hiyo ya huo mpira nikipata wasaa nitaelezea vizuri

Lakini kumbuka hicho ni kitu kidogo chenye kubeba hoja ya msingi
 
Pele hana hiyo hattrick, kwahyo Mbappe ni bora kuliko pele?
Umekuja sasa kwenye hoja yangu

Ni kwamba huwezi kumfananisha Messi na Pele na kuamua kuwa Messi ni bora kuliko Pele kwa kuangalia aina fulani ya mashindano ambayo hakushiriki
 
Umekuja sasa kwenye hoja yangu

Ni kwamba huwezi kumfananisha Messi na Pele na kuamua kuwa Messi ni bora kuliko Pele kwa kuangalia aina fulani ya mashindano ambayo hakushiriki
Pele alishiriki Ligi la bara (Copa)
Alichukua?
Messi kachukua mwaka jana
 
Kama hujawahi kumshuhudia Einsten utaona hiyo sio sababu ya kumtofautisha na lecture wako wa chuo?
 
Pele alishiriki Ligi la bara (Copa)
Alichukua?
Messi kachukua mwaka jana
Sheria za Copa America za miaka ya nyuma zilikuwa sio rafiki

Pele katika michuano hiyo alikuwa ndio top score na siku ya fainali walikutana na Argentina mpira ukaiha 1-1

Hawakwenda matuta, lakini kombe likaenda Argentina kwasababu walionekana kuwa na rekodi nzuri kwenye mashindano

Hiyo ndio sababu iliyomkosesha Pele kuchukua kombe
 
1800 ulikuwepo?

Sasa mmetoka kwa ronaldo na mmehamia kwa pele 😀😀 aise huyu messi atawapa presha..
Ndo miaka hiyo hiyo inayoelezea ma legend wenu kina mkwawa na machief wengine

Ambao huwezi kubisha kuwa hawakuwepo
 
In summary hakuchukua
 
Kama hujawahi kumshuhudia Einsten utaona hiyo sio sababu ya kumtofautisha na lecture wako wa chuo?
Hii hoja haina uhalisia. Shughuli ya Einstein haikuhusisha maonyesho. Ni vitu ambavyo vinathibitishika kwa majaribio ya kisayansi, na kanuni za kimahesabu.

Kesi ya Pele inahusisha maonyesho. Ucheze mpira, watu wakuone, ndio wajue kiwango chako. Hiki sio kitu kinachothibitishika kwa majaribio ya kisayansi, wala kanuni za kimahesabu.

Kwa mantiki hiyo, naweza kumuamini Einstein ambae sikumuona ila kazi zake zinathibitishika, kuliko Pele ambae kazi zake hazithibitishiki. Yani niamini eti Pele ni bora kuliko Messi au Ronaldo, eti kwakufuatisha masimulizi yenu? Hapana bana Scars!
 
Pele kupoteza mipira kufanyaje?!!
 

Kuna viumbe hawampendi lakini moyoni wanamkubali na kuhofia huenda itachukua karne na karne kuja kufikia uwezo wake..
 
Nani ambaye angetegemea kumuona mtu anatoa sifa kwa mchezaji mwingine tofauti na yule aliyemchora mwilini mwake kwa tattoo???
 
Siku tutayoamua kuuza nchi, wewe utasimama kama dalali

Unaongea sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…