Messi Vs Pele

Messi Vs Pele

Mjadala wa Messi na Pele unakaribia kuisha now ni Messi na Mbappe

Mbappe ana hattrick kwenye fainali wc, Messi ana nini?

Wengi humu wapo kishabiki zaidi ya uhalisia wenyewe.. yani mbappe unamcompare na Messi kweli!!
 
Umeshawekewa sababu ya kwanini hilo lilitokea lakino bado unabisha

Sasa tutaweka rule kuwa kila mchezaji anatakiwa acheze ligi zetu

Na mwisho Messi atakosa sifa kwasababu hatujamuona kwenye NBC
Sasa kwakuwa Chama hajacheza Ulaya tunaweza kusema ndio best midfielder in the world?
 
Kwa hiyo kama Pele hatujawahi kumshuhudia unaliwekaje hili jambo?
Kama hatukuwahi kumshuhudia, inakuaje tuseme ni bora kumzidi Messi ambae tumemshuhudia? Kwamba tutumie clips za YouTube kujiaminisha kua Pele ni bora zaidi ya Messi tunaemuona day in day out?

Ni uongo!

Hoja kuu ya mashabiki wa Pele ni kwamba Pele alishinda world cup tatu. Tumewaambia, kushinda world cup sio kazi ya mtu mmoja. Ni kazi ya team nzima. Sote tumeona ambavyo Mbappe amekiwasha kwenye hii world cup japo France hawakubeba kombe. Je ni sahihi kusema Dybala ni mkali kuliko Mbappe, eti kwakua Dybala ameshinda world cup mwaka huu ambao Mbappe hajashinda?

Ndio maana wengi wetu tunaamini Messi angeendelea kua GOAT hata bila kushinda world cup.

Huyu Pele hata rekodi zake hazieleweki. Vijana wa sasa wakizifikia, anasogeza tena ili tu aonekane kua yeye ni bora zaidi. Ndio maana sisi ambao hatukumshuhudia akicheza, tunashindwa kuamini hizo takwimu zake. Hawa akina Messi na Ronaldo, kila kitu chao kipo recorded na tunashuhudia.


Anaanza Messi, then Ronaldo, alafu ndio hao wazee wanafuatia. Mimi sioni Pele anamzidi vipi Cristiano Ronaldo!
 
Scars unachokifanya, ni kudokoa kihoja kimoja kidogo kabisa kwenye rundo la hoja then unakikomalia.

Hiyo comment uliyoiquote, hoja yake kuu ni kupinga kwamba mpira wa zamani ulikua mgumu kuliko wa sasa. Hebu jikite kwenye hoja ya msingi. Unapinga au unakubali?
Mkuu ni kweli mpira wa zamani ulikuwa hardcore tofauti na sasa

Angalia kitu kidogo tu kama hiki

Screenshot_20221226-220830.png


Huo ndio mpira uliokuwa unatumika miaka ya nyuma kipindi cha kina Pele, ni mpira ambao umeumdwa kwa material fulani non leather ambayo yanafanya mpira uwe mzito halafu hautembei chini

Katika kizazi hiki cha wapiga cross wangepata shida sana kwenye mpira huu.

Kuna mambo mengi sana juu ya changamoto ya aina hiyo ya huo mpira nikipata wasaa nitaelezea vizuri

Lakini kumbuka hicho ni kitu kidogo chenye kubeba hoja ya msingi
 
Pele hana hiyo hattrick, kwahyo Mbappe ni bora kuliko pele?
Umekuja sasa kwenye hoja yangu

Ni kwamba huwezi kumfananisha Messi na Pele na kuamua kuwa Messi ni bora kuliko Pele kwa kuangalia aina fulani ya mashindano ambayo hakushiriki
 
Umekuja sasa kwenye hoja yangu

Ni kwamba huwezi kumfananisha Messi na Pele na kuamua kuwa Messi ni bora kuliko Pele kwa kuangalia aina fulani ya mashindano ambayo hakushiriki
Pele alishiriki Ligi la bara (Copa)
Alichukua?
Messi kachukua mwaka jana
 
Kama hatukuwahi kumshuhudia, inakuaje tuseme ni bora kumzidi Messi ambae tumemshuhudia? Kwamba tutumie clips za YouTube kujiaminisha kua Pele ni bora zaidi ya Messi tunaemuona day in day out?

Ni uongo!

Hoja kuu ya mashabiki wa Pele ni kwamba Pele alishinda world cup tatu. Tumewaambia, kushinda world cup sio kazi ya mtu mmoja. Ni kazi ya team nzima. Sote tumeona ambavyo Mbappe amekiwasha kwenye hii world cup japo France hawakubeba kombe. Je ni sahihi kusema Dybala ni mkali kuliko Mbappe, eti kwakua Dybala ameshinda world cup mwaka huu ambao Mbappe hajashinda?

Ndio maana wengi wetu tunaamini Messi angeendelea kua GOAT hata bila kushinda world cup.

Huyu Pele hata rekodi zake hazieleweki. Vijana wa sasa wakizifikia, anasogeza tena ili tu aonekane kua yeye ni bora zaidi. Ndio maana sisi ambao hatukumshuhudia akicheza, tunashindwa kuamini hizo takwimu zake. Hawa akina Messi na Ronaldo, kila kitu chao kipo recorded na tunashuhudia.


Anaanza Messi, then Ronaldo, alafu ndio hao wazee wanafuatia. Mimi sioni Pele anamzidi vipi Cristiano Ronaldo!
Kama hujawahi kumshuhudia Einsten utaona hiyo sio sababu ya kumtofautisha na lecture wako wa chuo?
 
Pele alishiriki Ligi la bara (Copa)
Alichukua?
Messi kachukua mwaka jana
Sheria za Copa America za miaka ya nyuma zilikuwa sio rafiki

Pele katika michuano hiyo alikuwa ndio top score na siku ya fainali walikutana na Argentina mpira ukaiha 1-1

Hawakwenda matuta, lakini kombe likaenda Argentina kwasababu walionekana kuwa na rekodi nzuri kwenye mashindano

Hiyo ndio sababu iliyomkosesha Pele kuchukua kombe
 
1800 ulikuwepo?

Sasa mmetoka kwa ronaldo na mmehamia kwa pele 😀😀 aise huyu messi atawapa presha..
Ndo miaka hiyo hiyo inayoelezea ma legend wenu kina mkwawa na machief wengine

Ambao huwezi kubisha kuwa hawakuwepo
 
Sheria za Copa America za miaka ya nyuma zilikuwa sio rafiki

Pele katika michuano hiyo alikuwa ndio top score na siku ya fainali walikutana na Argentina mpira ukaiha 1-1

Hawakwenda matuta, lakini kombe likaenda Argentina kwasababu walionekana kuwa na rekodi nzuri kwenye mashindano

Hiyo ndio sababu iliyomkosesha Pele kuchukua kombe
In summary hakuchukua
 
Kama hujawahi kumshuhudia Einsten utaona hiyo sio sababu ya kumtofautisha na lecture wako wa chuo?
Hii hoja haina uhalisia. Shughuli ya Einstein haikuhusisha maonyesho. Ni vitu ambavyo vinathibitishika kwa majaribio ya kisayansi, na kanuni za kimahesabu.

Kesi ya Pele inahusisha maonyesho. Ucheze mpira, watu wakuone, ndio wajue kiwango chako. Hiki sio kitu kinachothibitishika kwa majaribio ya kisayansi, wala kanuni za kimahesabu.

Kwa mantiki hiyo, naweza kumuamini Einstein ambae sikumuona ila kazi zake zinathibitishika, kuliko Pele ambae kazi zake hazithibitishiki. Yani niamini eti Pele ni bora kuliko Messi au Ronaldo, eti kwakufuatisha masimulizi yenu? Hapana bana Scars!
 
Mpira si magoli tu, Ingekuwa hivyo basi viungo wasingeingia ktk list ya wachezaji bora duniani.

By the way, Messi alianza kama Winger, lazima ufungaji wake uwe mdogo kuliko forward. Hata hivyo mpaka sasa Messi keshamzidi Pele idadi ya Magoli na Assists. Lakini ukiacha yote hayo, Messi ana uwezo mkubwa wa kukusanya kijiji kuliko Pele. Pele alikuwa mwepesi wa kupoteza mpira kuliko Messi
Pele kupoteza mipira kufanyaje?!!
 
Hii hoja haina uhalisia. Shughuli ya Einstein haikuhusisha maonyesho. Ni vitu ambavyo vinathibitishika kwa majaribio ya kisayansi, na kanuni za kimahesabu.

Kesi ya Pele inahusisha maonyesho. Ucheze mpira, watu wakuone, ndio wajue kiwango chako. Hiki sio kitu kinachothibitishika kwa majaribio ya kisayansi, wala kanuni za kimahesabu.

Kwa mantiki hiyo, naweza kumuamini Einstein ambae sikumuona ila kazi zake zinathibitishika, kuliko Pele ambae kazi zake hazithibitishiki. Yani niamini eti Pele ni bora kuliko Messi au Ronaldo, eti kwakufuatisha masimulizi yenu? Hapana bana Scars!

Kuna viumbe hawampendi lakini moyoni wanamkubali na kuhofia huenda itachukua karne na karne kuja kufikia uwezo wake..
 
Kwa kigezo cha World Cup, Pele ametwaa World Cup 3.

Ya kwanza ni mwaka 1958 pale Sweden akiwa na miaka 17 yaani alikuwa mchezaji chipukizi wala sio tegemeo kwa timu.

Mara ya pili akatwaa mwaka 1962 pale Chile. Mechi ya pili tu Pele akaumia na hakucheza tena michuano hiyo lakini akavaa medali.

Mara ya tatu akatwaa mwaka 1970 pale Mexico katika michuano ambayo Brazil inachukuliwa kama timu bora ya wakati wote wakiwemo akina Tostao, Jairzinho, Captain Carlos Alberto.

Katika michuano yote hiyo, Pele hakuwahi kuwa mchezaji bora wa mashindano, wala kuwa mfungaji bora.

Messi ametwaa World Cup moja lakini imebidi aibebe timu mabegani mwake ili waweze kutwaa ndoo tofauti na Pele aliyebebwa na mafanikio ya wenzake.

Kwa kuhitimisha, kwangu mimi Messi ni mchezaji bora kumzidi Pele ila kwaluwa wahafidhina wa soka wanapenda mambo ya zamani watamtetea Pele
Nani ambaye angetegemea kumuona mtu anatoa sifa kwa mchezaji mwingine tofauti na yule aliyemchora mwilini mwake kwa tattoo???
 
Kwa lugha rahisi ni kwamba Kombe la nguvu za Pele ni hilo la 70 na kwenyewe hakuwa best scorer sasa wanapodai ndiye bora wakati hata mashindano husika hakuwa mchezaji bora wanadhihirisha wana nongwa na Messi tu maana Messi ipo clear anaupiga mwingi every tournament
Huyu Pele hata rekodi zake ni za kuungaunga kabisa hadi zinakosa uhalisia mfano ile update ya magoli baada ya kufikiwa idadi ya magoli na Ronaldo akaongeza eti alifunga 1000 na mamia huko ili tu asiwe chini ya mwingine
Siku tutayoamua kuuza nchi, wewe utasimama kama dalali

Unaongea sana
 
Back
Top Bottom