Mfahamu Meja Jenerali Muhiddin Kimario. Ukisikia mzalendo ndio huyu

Mfahamu Meja Jenerali Muhiddin Kimario. Ukisikia mzalendo ndio huyu

Pichani ni Marehemu Major Generali Muhiddin Kimario, ni moja kati ya mawaziri wawili tu waliowahi kudumu katika nafasi zao za wizara ya mambo ya ndani kwa muda wa miaka mitano (5) katika Historia ya Tanzania.

Mwaka 1978 alitumwa kwenda mkoani Mwanza na Mwalimu Nyerere kwenda kuwaaga Wanajeshi waliokuwa wanakwenda kupigana Vita vya Kagera kumn'goa Idd Amin Dada, wakati akitoa Hotuba yake ndani ya Viwanja vya Nyamagana ghafla aliamua kujivua uwaziri na kuamua kwenda vitani "Mkuu wa Mkoa ninaomba ufikishe taarifa hii kwa mh Rais kwamba najivua Uwaziri na ninaamua kurudi jeshini kuungana na wenzangu leo kwenda kumshikisha Adabu Amin"

View attachment 1498576
humpati wa hivi kwa kipindi Cha Sasa walivyo wabinafsi
 
hapa ndo ninapoichukia tz story Kama hizi zilipaswa zitolewe na chanel au gazeti la jeshi kuleta hamasa na kutunza heshima Ila Sasa kwetu mwanajeshi kuogopwa ndo sifa
 
Nadhani umekosea kwa bahati mbaya kuandika Shamim, ni Tamim. Ni kweli jamaa alipitia kipindi kigumu baada ya vita. Alikua ni askari mwaminifu na mtiifu kwa jeshi na nchi yake na alikua amepigana vita ya Uganda akiwa ni miongoni mwa makomandoo wa Tanzania waliotoa mchango mkubwa sana kwa ushindi wetu dhidi ya Amin.

Miaka miwili baada ya vita yaani 1981 alitumwa kwenye mission fulani nyeti nje ya nchi. Kwa kifupi mission ile haikua inajulikana na uongozi wa juu kabisa wa nchi. Kukawa na fununu kua waliomtuma walikua mbioni kuteuliwa kwenye nafasi kubwa sana jeshini na wakati huo kukawa na tetesi pia za malalamiko za hiyo nchi alipokwenda Tamimu kwenye operation aliyotumwa.

Kilichotokea ni kwamba hao waliomtuma kwa hofu ya kukosa nafasi kubwa za uteuzi wakiamini mamlaka ya uteuzi itachukizwa na operation ile wakamkana Comandoo Tamim kua hawakumtuma na kwamba eti ALIASI JESHI!!!! Commando Tamim akakatiwa support aliyotakiwa kupewa akiwa huko na akjikuta akiwa vulnerable huku akisakwa na kuwindwa kama digidigi ili kuuwawa huko alipotumwa. Ni kwa mbinu zake, juhudi na mafunzo aliyopewa ndio akaweza kutoroka na kurudi Tanzania

Aliporudi hakuamini kikichotokea. Alikutana na mashtaka ya uasi na kupelekwa court martial!!! Kifupi aliondolewa jeshini kwa dhulma na alijua na sababu za kuamini kwamba hata hapa kwenye nchi aliyoioenda sana alikua anawindwa auwawe! Kwakweli ilimchanganya sana. Inawezekana hii ndiyo ilisababisha ikawa rahisi Comandoo Mohamed Martin Tamimu kushawishika kuingia kwenye njama chafu na ovu za kutaka kupindua serikali. Ni kweli pia yote aliyopitia haihalalishi yeye kuingia katika njama za uhaini na kosa lake liko palepale lakini fact ipo palepale Tamim aliuzwa na kusalitiwa na wenye tamaa ya madaraka na wakamnyima fursa ya kuitumikia nchi yake ambayo miaka michache tu iliyopita alijitoa muhanga kufa uwanja wa vita akiitetea

Ama kuhusu shahidi X na shahidi Y ni kwamba mmoja ameshatangulia mbele za haki na mwingine ni yule aliyemfyatulia risasi Tamimu sina hakika kama alishapona maradhi yake yaliyomfanya awe kwenye coma kwa muda mrefu
Msukuma yule aliyepooza ni ndugu yangu; sina taarifa zake kwa muda mrefu sana, na wala sijui kama bad yupo hai. Ila enzi zake alikuwa anakula bata sana na pia alikuwa na maisha ya hatari na ya usiri sana; aliponea kuuwawa mara nyingi sana ndani na nje ya nchi.
 
hapa ndo ninapoichukia tz story Kama hizi zilipaswa zitolewe na chanel au gazeti la jeshi kuleta hamasa na kutunza heshima Ila Sasa kwetu mwanajeshi kuogopwa ndo sifa
tanzania hatujui kutumia opportunity, vipo vingi tu tumeshindwa kuvitumia vizuri mfano; rasilimali nyingi za kuvutia watalii ambazo zingetuwezesha kupandisha zaidi GDP lakini hatuzioni, wakenya wangefanikiwa kuwa na amani na mafanikio ya kijeshi na viongozi wazalendo kama tanzania, wangekuwa mbali sana, lakini ahsante sana magu, pamoja na mapungufu mengi umeanza kutuamsha
 
Amefariki 2005, ila Kisa chake cha kusikitisha ndio hiki
Kuna askari wengi waliokuwa mstari wa mbele wanasema Lupogo alishindwa KABISA kuendesha vita na kurudishwa makao makuu. Kikosi chake cha 205 kuchukuliwa na Kimario. Kimario aliendesha mapigano makali na kikosi chake cha 205 kiliweza kukata katikati ya Uganda mpaka Nimule kwenye mpaka wa Uganda na Sudan. 205 ndiyo kikosi kilichopoteza kifaru kimoja baada ya mapigano makali ya masaa 8 ili kuteka daraja muhimu la Maporomoko ya Karuma Kwa maajabu,Mwl Nyerere alimpandisha cheo Lupogo kuwa Meja Jenerali na kumuacha yule aliyepiganisha vita na kushinda Kimario. Wewe jiulize inakuaje aliyeshindwa vita kupandishwa cheo na yule liyeshinda kuachwa mpaka alipopandishwa cheo na Rais A.H Mwinyi.Hizo ndizo changamoto za Mstari wa mbele walizokuwa wanazipata wapiganishaji wetu
Kuna hoja ya ukabila pia hapo labda
 
Next 2025 anatakua mpentekoste,
Hii ya wakatoliki ni mpaka leo mkuu, inavyosemekana ukiwa muislam huwez kuongoza nchi km sio mslamu wa Bakwata, na ukiwa mkristo lazma uwe Catholic na ndio sababu pia ya kumkata mamvi (ukaskazini+Ulutheran)
 
tatizo la huyu 'mangi' lilikuwa ufisadi na ma-deal, hata mwalimu alikuwa anaishi naye kimachale machale tuu……………….
 
Huu nao ni uwongo mwingi sana. Ni kweli Tamimu aliuwawa Kinondoni kutokana na uhusika wake katika njama za kupindua serikali mwaka 1982; hakuuzwa bali alijiunga na akina Zakaria Hanspope, Uncle Tom, Badru Kajaja na wengineo katika njama za kutaka kuipindua serikali kutokana na maisha magumu yaliyofuatia baada ya vita.

Tanzania ya leo tumelogwa nini kuamini hizi conspiracy theories kupita kiasi?
Kama hujui kisa cha Tamimu kuasi na kujiunga na uasi dhini ya sirikali kilikuwa ni hasira za kuingizwa 'choo cha kike' na 'wanene' akiwa kama mwana usalama wa jeshi
 
Kisa cha Kanali Mahfoudh nacho ni cha kusisimua sana. Kinahitaji uzi wake maalum. Amefariki miaka ya hivi karibuni akiwa kapata hadhi ya utumishi uliotukuka wa idara nyeti huko Msumbiji
Naam pamepita miamba nchi hii ambayo haikuwa midomoni wala vitabuni ila ilofanya mambo yaliyotukuka nchini petu.
 
Kumbe alitoka kwa mkulu mwenyewe.. kumbe kelele zote za ukabila yeye alijaza wadosi tuu toka musoma.haaa
Yaah tena majirani kabisa nadhani mwendo wa dakika kumi kwa miguu kutoka kwa mwalimu mpaka kwa geral
 
Back
Top Bottom