Mfahamu Meja Jenerali Muhiddin Kimario. Ukisikia mzalendo ndio huyu

Mfahamu Meja Jenerali Muhiddin Kimario. Ukisikia mzalendo ndio huyu

Amefariki 2005, ila Kisa chake cha kusikitisha ndio hiki
Kuna askari wengi waliokuwa mstari wa mbele wanasema Lupogo alishindwa KABISA kuendesha vita na kurudishwa makao makuu. Kikosi chake cha 205 kuchukuliwa na Kimario. Kimario aliendesha mapigano makali na kikosi chake cha 205 kiliweza kukata katikati ya Uganda mpaka Nimule kwenye mpaka wa Uganda na Sudan. 205 ndiyo kikosi kilichopoteza kifaru kimoja baada ya mapigano makali ya masaa 8 ili kuteka daraja muhimu la Maporomoko ya Karuma Kwa maajabu,Mwl Nyerere alimpandisha cheo Lupogo kuwa Meja Jenerali na kumuacha yule aliyepiganisha vita na kushinda Kimario. Wewe jiulize inakuaje aliyeshindwa vita kupandishwa cheo na yule liyeshinda kuachwa mpaka alipopandishwa cheo na Rais A.H Mwinyi.Hizo ndizo changamoto za Mstari wa mbele walizokuwa wanazipata wapiganishaji wetu
Hii nayo ni uwongo mtupu; Muhidini Kimario baada ya vita alikuwa waziri wa mambo ya ndani kuanzia mwaka 1983. Hata ukienda tovuti ya Wizara hiyo utakuta kuwa yeye aliendelea kuongoza wizara hiyo hadi 1988, yaani miaka kumi baada ya vita. Kabla ya Vita alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

Hizi conspiracy theories mnazitoa wapi?
 
Huyu anayesifiwa tbccm kila siku kwenye vipindi vya kusifu na kuabudu kuwa ni mzalendo namba 1 ni wa hovyo kabisa.
 
Alifariki 2014 Moshi
Sio mzalendo aliwahi funguliwa kesi ya uhujumu Uchumi, soon baada ya awamu ya Tatu kuingia...
Aliwahi kukataliwa Jimbo la Moshi Mjini

Mtoto wake mmoja ndio alikuwa mpambe wa Rais, Yule anayevaa magwanda ya jeshi nadhani siku hizi amekuwa muambata kwenye balozi zetu hu
 
Amefariki 2005, ila Kisa chake cha kusikitisha ndio hiki
Kuna askari wengi waliokuwa mstari wa mbele wanasema Lupogo alishindwa KABISA kuendesha vita na kurudishwa makao makuu. Kikosi chake cha 205 kuchukuliwa na Kimario. Kimario aliendesha mapigano makali na kikosi chake cha 205 kiliweza kukata katikati ya Uganda mpaka Nimule kwenye mpaka wa Uganda na Sudan. 205 ndiyo kikosi kilichopoteza kifaru kimoja baada ya mapigano makali ya masaa 8 ili kuteka daraja muhimu la Maporomoko ya Karuma Kwa maajabu,Mwl Nyerere alimpandisha cheo Lupogo kuwa Meja Jenerali na kumuacha yule aliyepiganisha vita na kushinda Kimario. Wewe jiulize inakuaje aliyeshindwa vita kupandishwa cheo na yule liyeshinda kuachwa mpaka alipopandishwa cheo na Rais A.H Mwinyi.Hizo ndizo changamoto za Mstari wa mbele walizokuwa wanazipata wapiganishaji wetu
Meja jeneral muhiddin Kimario(kamanda mbogo) alifariki mwaka 2014
 
Nahisi msumuliaji alikufa vitani yeye akwshindwa kuendelea na simulizi!
 
Alifariki 2014 Moshi
Sio mzalendo aliwahi funguliwa kesi ya uhujumu Uchumi, soon baada ya awamu ya Tatu kuingia...
Aliwahi kukataliwa Jimbo la Moshi Mjini

Mtoto wake mmoja ndio alikuwa mpambe wa Rais, Yule anayevaa magwanda ya jeshi nadhani siku hizi amekuwa muambata kwenye balozi zetu hu
Acha uongo Brigedia Ibrahim Kimario(mpambe wa Rais kikwete) sio mtoto wa Meja jeneral kimario japo wana undugu kwenye ukoo wa kimario.
 
Kuna kisa kingine cha kusikitisha cha jamaa mmoja alikua Captain wa Jeshi akiitwa Mohamed Martin Tamimu(Comandoo). Huyu aliuzwa vibaya sana kwa kupelekwa nje ya nchi kufanya kazi ambayo yeye akiamini ni yakulitumikia taifa.

Yalitokea mambo kadhaa. Waliomtuma wakamgeuka na kumruka, akawa adui wa huko alipotumwa na adui wa nchi iliyo mtuma! Akajikuta analazimika kuingia kwenye uasi/uhaini na aliuwawa pale Kinondoni Mkwajuni kwa kufyatuliwa risasi na mwanasiasa maarufu sana hapa nchini ambaye habari zake za mwisho alikua upinzani
Huyu huwa natamani sana nijue habari zake..
 
Kama kitu wewe hukijui usiseme kua hakipo au hakikuwahi kuwepo. Unajua baada ya kutoka vitani Tamimu alikua wapi na alikua anafanya nini?

Vita iliisha mapema 1979 baada ya Amin kuikimbia Uganda na Majeshi ya Tanzania yakatwaa Mamlaka ya kuiongoza nchi hiyo hadi walipochaguana wenyewe. Mwl. Nyerere alianza kuwaingiza wanajeshi wa Tanzania kwenye shughuli za siasa na kazi nyingine za umma

Njama za uhaini zilipangwa mnamo 1982 na ni sahihi unaposema Tamimu alikuwepo kwenye njama hizo. Lakini unajua kabda ya hapo alikua wapi? Unazijua mission zote alizotumwa na wakubwa zake akazitimiza kwa ufanisi na uaminifu mkubwa kabda ya kuuzwa na kusalitiwa na haohao waliomtuma na akajikuta sio tu kapoteza kazi yake bali pia akiwindwa ili auwawe? Kama hujui uliza mkuu wangu, wengine hatujasimuliwa tumeyaishi haya
Kwa hiyo unataka kusema kuwa Tamim aliuzwa baada ya vita ndipo akaamua kuja kujiunga na njama za mapinduzi? Halafu tunapobishana katika mswala haya jitahidi pia kuniambia kama unawajua shahidi X na shahidi Y kwenye kesi ile ya uhaini ya mwaka huo. Hapa kuna vitu vingi sana vya kusimuliwa ambavyo havilingani na rekodi zenyewe halisi.
 
Meja Muhidin Kimario.. daa umenikumbusha mbali jiran yangu pale moshi. Huyu mzee cku zake za mwisho mwisho alikuwa na mlinz wake mkurya kila cku wanalewa gongo chakar wanaimba barabara nzima. Ila tukiwa wadogo tulikuwa tunasikia anaish dodoma. Mi nilikuja kumjua uzeen sana. Tulikuwa tunakula tende nyumban kwake. Ngoja niishie hapo.
 
Kwa hiyo unataka kusema kuwa Shamim alizwa baada ya vita ndipo akaamua kuja kujiunga na njama za mapinduzi? Halafu tunaposihana katika mswala haya jitahidi pia uniambia kama unawajua shahidi X na shahidi Y kwenye kesi ile ya uhaini ya mwaka huo. Hapa kuna vitu vingi sana vya kusimuliwa ambavyo havilingani na rekodi zenyewe halisi.
Nadhani umekosea kwa bahati mbaya kuandika Shamim, ni Tamim. Ni kweli jamaa alipitia kipindi kigumu baada ya vita. Alikua ni askari mwaminifu na mtiifu kwa jeshi na nchi yake na alikua amepigana vita ya Uganda akiwa ni miongoni mwa makomandoo wa Tanzania waliotoa mchango mkubwa sana kwa ushindi wetu dhidi ya Amin.

Miaka miwili baada ya vita yaani 1981 alitumwa kwenye mission fulani nyeti nje ya nchi. Kwa kifupi mission ile haikua inajulikana na uongozi wa juu kabisa wa nchi. Kukawa na fununu kua waliomtuma walikua mbioni kuteuliwa kwenye nafasi kubwa sana jeshini na wakati huo kukawa na tetesi pia za malalamiko za hiyo nchi alipokwenda Tamimu kwenye operation aliyotumwa.

Kilichotokea ni kwamba hao waliomtuma kwa hofu ya kukosa nafasi kubwa za uteuzi wakiamini mamlaka ya uteuzi itachukizwa na operation ile wakamkana Comandoo Tamim kua hawakumtuma na kwamba eti ALIASI JESHI!!!! Commando Tamim akakatiwa support aliyotakiwa kupewa akiwa huko na akjikuta akiwa vulnerable huku akisakwa na kuwindwa kama digidigi ili kuuwawa huko alipotumwa. Ni kwa mbinu zake, juhudi na mafunzo aliyopewa ndio akaweza kutoroka na kurudi Tanzania

Aliporudi hakuamini kikichotokea. Alikutana na mashtaka ya uasi na kupelekwa court martial!!! Kifupi aliondolewa jeshini kwa dhulma na alijua na sababu za kuamini kwamba hata hapa kwenye nchi aliyoioenda sana alikua anawindwa auwawe! Kwakweli ilimchanganya sana. Inawezekana hii ndiyo ilisababisha ikawa rahisi Comandoo Mohamed Martin Tamimu kushawishika kuingia kwenye njama chafu na ovu za kutaka kupindua serikali. Ni kweli pia yote aliyopitia haihalalishi yeye kuingia katika njama za uhaini na kosa lake liko palepale lakini fact ipo palepale Tamim aliuzwa na kusalitiwa na wenye tamaa ya madaraka na wakamnyima fursa ya kuitumikia nchi yake ambayo miaka michache tu iliyopita alijitoa muhanga kufa uwanja wa vita akiitetea

Ama kuhusu shahidi X na shahidi Y ni kwamba mmoja ameshatangulia mbele za haki na mwingine ni yule aliyemfyatulia risasi Tamimu sina hakika kama alishapona maradhi yake yaliyomfanya awe kwenye coma kwa muda mrefu
 
Navutiwa na story yako na ni ukweli kuwa ilisemekana yale mapinduzi hayakuwa ya kisiasa ila dissatisfaction ya baadhi ya watu ama manyanyaso..

Ukifinguka zaidi japo kwa codes inaweza kupendeza zaidi
Nadhani umekosea kwa bahati mbaya kuandika Shamim, ni Tamim. Ni kweli jamaa alipitia kipindi kigumu baada ya vita. Alikua ni askari mwaminifu na mtiifu kwa jeshi na nchi yake na alikua amepigana vita ya Uganda akiwa ni miongoni mwa makomandoo wa Tanzania waliotoa mchango mkubwa sana kwa ushindi wetu dhidi ya Amin.

Miaka miwili baada ya vita yaani 1981 alitumwa kwenye mission fulani nyeti nje ya nchi. Kwa kifupi mission ile haikua inajulikana na uongozi wa juu kabisa wa nchi. Kukawa na fununu kua waliomtuma walikua mbioni kuteuliwa kwenye nafasi kubwa sana jeshini na wakati huo kukawa na tetesi pia za malalamiko za hiyo nchi alipokwenda Tamimu kwenye operation aliyotumwa.

Kilichotokea ni kwamba hao waliomtuma kwa hofu ya kukosa nafasi kubwa za uteuzi wakiamini mamlaka ya uteuzi itachukizwa na operation ile wakamkana Comandoo Tamim kua hawakumtuma na kwamba eti ALIASI JESHI!!!! Commando Tamim akakatiwa support aliyotakiwa kupewa akiwa huko na akjikuta akiwa vulnerable huku akisakwa na kuwindwa kama digidigi ili kuuwawa huko alipotumwa. Ni kwa mbinu zake, juhudi na mafunzo aliyopewa ndio akaweza kutoroka na kurudi Tanzania

Aliporudi hakuamini kikichotokea. Alikutana na mashtaka ya uasi na kupelekwa court martial!!! Kifupi aliondolewa jeshini kwa dhulma na alijua na sababu za kuamini kwamba hata hapa kwenye nchi aliyoioenda sana alikua anawindwa auwawe! Kwakweli ilimchanganya sana. Inawezekana hii ndiyo ilisababisha ikawa rahisi Comandoo Mohamed Martin Tamimu kushawishika kuingia kwenye njama chafu na ovu za kutaka kupindua serikali. Ni kweli pia yote aliyopitia haihalalishi yeye kuingia katika njama za uhaini na kosa lake liko palepale lakini fact ipo palepale Tamim aliuzwa na kusalitiwa na wenye tamaa ya madaraka na wakamnyima fursa ya kuitumikia nchi yake ambayo miaka michache tu iliyopita alijitoa muhanga kufa uwanja wa vita akiitetea

Ama kuhusu shahidi X na shahidi Y ni kwamba mmoja ameshatangulia mbele za haki na mwingine ni yule aliyemfyatulia risasi Tamimu sina hakika kama alishapona maradhi yake yaliyomfanya awe kwenye coma kwa muda mrefu
 
Back
Top Bottom