Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

nilisoma kitu kama hicho mahali fulani, kwamba baada ya malaika kujifanyia mwili wa kibinadamu na kulala na wanawake matokeo ndio hayo majitu....na kile kitabu kilieleza kuwa gharika ilipokuja iliangamiza wote japo malaika waliacha mwili na kuondoka,

Leo nimepata kitu kingine hapa,
Ila kuna hoja moja hapo juu kuhusu mfalme OG kwamba alishikiria boti ya nuhu sijaielewa vizuri.
Kama malaika waliacha miili na kukimbia kwanini kipindi hiki hawavai tena miili na kuja kulala na binadamu?
Au binadamu wa sasa hawawavutii
 
zitto junior. Kuna vitu tumefichwa lakini ukweli ni kuwa Mungu alimuumba mwanadamu kukiwa kuna maisha ya viumbe kama binadamu tayali.
Na sijui kwanini Mungu aliamua kutupunguzia maisha wakati viumbe wake waliotutangulia ndio wametufanya tuingie katika majaribu ya kutuhadaa

Ushahidi wa viumbe waliokuwepo kwa mjibu wa Biblia

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanzo 3 :5

Hapa Mungu anatufananisha na viumbe waliotangulia hapa kuna kitu ukitafakari unapata jibu la kuwepo maisha yaliyoendelea

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
Mwanzo 6 :3
Kwanini Mungu atupunguzie umri ili hali yeye ndiye katuumbia vitu vya kutupotosha?

Kwanini Mungu asingetupeleka sayari nyingine tuanze maisha yetu yasiyo na mchanganyiko wowote?

Kwanini Mungu asinge tupeleka hata kwenye nyota (jua) proxima century mbali na hapa tukawa mbali na wanefili?

Maana wanefili bado wanaishi ila Mungu kawapunguzia uwezo wa nguvu lakini ndiyo jamii zenye ushawishi na nguvu kiuchumi kuindesha Dunia ndio wazungu wenye macho njano.

Kwa picha hii ni uthibitisho tosha kuwa wapo ila hawana nguvu za mwili ila wamebaki kiakili
 

Attachments

  • tallest-and-shorte_1559059i.jpg
    tallest-and-shorte_1559059i.jpg
    31.7 KB · Views: 239
  • IMG_20180430_104940_824.jpg
    IMG_20180430_104940_824.jpg
    23.8 KB · Views: 225
Kama malaika waliacha miili na kukimbia kwanini kipindi hiki hawavai tena miili na kuja kulala na binadamu?
Au binadamu wa sasa hawawavutii
walikua ni malaika walio hasi na kuwa watumwa washetani na bila shaka hata kizazi cha leo hayo mambo yapo....kuna watu wanazaa na majini/mapepo.

Mshana atakua anajua zaidi kwenye haya mambo.

Cc Mshana Jr
 
Hatujaambiwa walikuwa jinsia gani so huenda kulikuwa na wanefili wa kiume na wakike. Ila uzao wao upo mfano huyu mfalme ogu alikuwa anatawala MAJIJI 60 kwenye himaya ya jamii yake ikimaanisha aliweza kuwa na uzao ingawa hatujaelezwa huyo mke wake alikuwa wa aina gani kma naye ni alikua mnefili ama lah ila kwa kujibu swali lako tuamini tu kuwa kulikuwa na wanawake wanefili pia hivyo walilala nao hao hao
Maana yake ni kwamba, wakati malaika wanalala na binadamu, watoto walozaliwa walikuwa wa kike na kiume.
 
Hakuna malaika maana biblia inatuambia walikuwepo wana wa Mungu
Soma hapo chini

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
 
zitto junior. Kuna vitu tumefichwa lakini ukweli ni kuwa Mungu alimuumba mwanadamu kukiwa kuna maisha ya viumbe kama binadamu tayali.
Na sijui kwanini Mungu aliamua kutupunguzia maisha wakati viumbe wake waliotutangulia ndio wametufanya tuingie katika majaribu ya kutuhadaa

Ushahidi wa viumbe waliokuwepo kwa mjibu wa Biblia

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanzo 3 :5

Hapa Mungu anatufananisha na viumbe waliotangulia hapa kuna kitu ukitafakari unapata jibu la kuwepo maisha yaliyoendelea

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
Mwanzo 6 :3
Kwanini Mungu atupunguzie umri ili hali yeye ndiye katuumbia vitu vya kutupotosha?

Kwanini Mungu asingetupeleka sayari nyingine tuanze maisha yetu yasiyo na mchanganyiko wowote?

Kwanini Mungu asinge tupeleka hata kwenye nyota (jua) proxima century mbali na hapa tukawa mbali na wanefili?

Maana wanefili bado wanaishi ila Mungu kawapunguzia uwezo wa nguvu lakini ndiyo jamii zenye ushawishi na nguvu kiuchumi kuindesha Dunia ndio wazungu wenye macho njano.

Kwa picha hii ni uthibitisho tosha kuwa wapo ila hawana nguvu za mwili ila wamebaki kiakili
Huyu hawezi hata kuinua mfuko wa simenti.
 
Hakuna malaika maana biblia inatuambia walikuwepo wana wa Mungu
Soma hapo chini

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
Mkuu kwanini hao wana wa mungu hawaji tena kwenye zama hizi kuzaa na binadamu?
 
kuna jambo linakanganya!! kama unaamin kwamba kuna gharika ilitokea bas huna budi kuamini kuna Mungu. ukiamin juu ya Mungu maana yake unaamini Mungu ni mkuu kuliko huyo Og!! hivyo bas iweje apone na huku lengo la Mungu ni kuangamiza kizazi chote kitakachokua nje ya safina??

lugha rahisi huyu Og alimshinda hadi Mungu. hiyo haiwezekani. ila asante kwa habar yenye kufikirisha
 
Hakuna malaika maana biblia inatuambia walikuwepo wana wa Mungu
Soma hapo chini

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4

Neno wana wa Mungu lililotumika hapo ni "B'nai Elohim" ambalo kwenye Biblia ya Kihebrania linamaanisha Malaika.
 
Nadharia No2 mkuu naipinga japo sio msomaji wa bible vizuri ,ila kibinadamu.

Hata angekuwaje hivi kama inavyosema biblia kuwa maji yalijaa duniani kote mikono kumi na tano (mikono kumi na tano ya wakati huosio sasa) ina maana yalikua maji marefu yenye nguvu unadhani kuna kiumbe kingeweza kabisa kushika safina ili kisiangamie kingali nje ya safina?


Na hio hoja ya kusema kuwa watu wangemvamia.. mkuu maji unayajua nadhani hivi yanavyojua kuwa na nguvu mtu unaweza kumvamia mwenzio? au hata kufikiria kumvamia bila kujiokoa.. Haiwezekani kwakweli.
Tuelimishane vizuri
Hio nadharia ya 3 naweza kuikubali ina make sense mkuu.
 
Back
Top Bottom