Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Halafu msipende kuwafananisha malaika na majini jaman ni viumbe wawili tofauti kabisa jaman majini ni kama sisi tu wanadam baadhi ya sifa zao na zetu zinafanana
Majini ni malaika waovu, ni waasi walifukuzwa mbinguni wakatupwa hapa duniani
 
Goliath hakuwa na jipya sana zaidi ya ukubwa wa mwili tu ambao hata kaka zake wale 4 walikuwa na ukubwa sawa na wake tu...... Yote kwa yote wote ni uzao wa kinefili hivyo goliath ni kama kitukuu cha Huyu OG

Ila kwa kuwalinganisha huyu mfalme ogu amemzidi mwili na maarifa maana aliweza kuacha nyaraka ila goliath hakuacha maandiko yeyote yale

Pili mfalme Ogu aliweza kusimamisha majiji 60 na kuyatawala kwa kipindi kirefu hii inaelezea pia alikuwa ni kiongozi haswaa maana kutawala miji yote hyo bila kupinduliwa wala vita za ajabu ajabu basi aliweza kuwadhibiti tofauti na goliath sikuoma kokote alikoonyeshwa kuwa ni kiongozi mzuri

Tatu ogu anasifika kwa ushujaa wake wa kupona kwenye gharika kitu ambacho kwa akili ya kawaida hakiwezekani wengine wote wafe ww upone ila goliath sikuona kwenye simulizi yeyote alifanya mambo ya kutisha ila alikuwa maarufu sababu ya size tu wala hakuna jipya

Hizo ni baadhi ya tofauti nikiwalinganisha ila huyu mfalme og inaoneokana alikuwa tishio zaidi dunia nzima ndio maana kuna mistari zaidi ya 20 ya manabii tofauti inazungumzia ushindi wa waisraeli dhidi ya OG na wanakumbuka kisa kile hadi leo na kipo kwenye vitabu vyao vya kiyahudi!! Tofauti na goliath sioni kokote akitajwa tajwa sana na manabii wa baadae
Mku nmekusoma pooooote lkn uliposema tu alikua tishio dunia nzima ndo ninapokataaga je alishawai kuja kupigana na wahehe, au akina Zwangendaba, mkuu siku utakapopata historia za nyumbani ndo utakapojua nasi tuna hadithi zetu
 
assumption kuwa jamaa alikuwepo:
turudi kwenye situation ya maji yaliyosemwa katika mwanzo.

kama ilivyovigumu kusimama kwenye mafuriko ya maji ya mto msimbazi. Atawezaje kusimama kwenye maji ambayo sio tu yanatoka juu bali ardhi ilikuwa pia ikitoa maji.
Pili lengo la Mungu lilikuwa ni kuwaangamiza wanadamu wote kwa staili ile, je atawezaje kiruhusu aina ya maangamizi ambayo yatampa fursa mmojawapo kutoroka?

Yale maji yalikuwa ni combination ya "Fountain of the deep" na "product ya Windows of heaven"

maelezo yako bado kama yanatoa nafasi finyu hau haipo kabisa kwa huyo kiumbe kuescape ikiwa unakubaliana na complications za yale mafuriko kama yanavyoelezwa hapo mwanzo.
Possibility kuwa maji yalijaa mikono 15 zaidi ya mlima mrefu ikimaanisha huyu Ogu kma alikuwa na urefu wa zaidi ya futi 15 ina maana basi anaweza kuwa maji aliyazidi kimo kuendana na hoja hii ya MIKONO 15!!! Other factors remaining constant ingawa ni finyu kma unavyosema ila kwa msimamo huu wa biblia je haiwezekani??
 
Zitto junior

Hebu tuanzie hapa kwanza afu tuendelee naimani tutapata kitu

Ogu
BibliaJinaKumbukumbu la Torati

640px-Ostjordanische_Amoriterreiche.png



Ogu ni jina la mfalme wa Waamorialiyetawala sehemu za Bashani. Ogu anatajwa katika Biblia kwenye vitabuvya Hesabu 21 na Kumbukumbu la Torati 3, kwa kifupi pia katika Zaburi135:11 na 136:20. Inawezekana ya kwamba kutajwa kwa "Mwamori" katika Amosi 2:9 ni pia kuhusu Ogu.

Ogu katika Biblia
Katika vitabu vya Hesabu na Kumbukumbu la Torati anaonyeshwa kama mfalme ambaye aliyekataa ombi la Wanaisraeli la kupita katika nchi yake wakitokea Misri na kuelekea Kanaani. Ogu alikataa akakusanya jeshi lake na kuwashambulia Wanaisraeli. Karibu na mji wa Ederei (leo: Dar'a nchini Syria) alishindwa. Wanaisraeli waliteka nchi yake ikawa makazi ya kabila la Manase.

Ogu anakumbukwa katika masimulizi ya Biblia kama jitu akiwa na kitandachenye urefu wa mikono yaani dhiraa10 sawa na mita 4-5.

Katika masimulizi ya Wayahudi sifa hiyo iliendelea kuongezeka; katika Kitabu cha Amosi 2,9 anatajwa (bila kusema jina) kama "Mwamori" "nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni".

Ogu katika mapokeo ya Kiyahudi
Wataalamu Wayahudi wa baadaye waliona ya kwamba vipimo vya Kumb. 3 kuhusu kitanda chake chenye urefu wa mikono yaani dhiraa 10, sawa na mita 4-5, vilihusu mkono wa hilo jitu lenyewe, hivyo walimwona mkubwa zaidi tena.

Kwenye kitabu Berakhot cha TalmudiOgu anasimuliwa ya kwamba aliweza kuinua mlima aliotaka kurusha dhidi ya Wanaisraeli, lakini Mungu alimzuia Katika kitabu cha Nidah katika Talmudi Ogu anasemekana ni mtu aliyeishi kabla ya gharika kuu ya Nuhu akiwa ni mmoja wa wale ambao walitunzwa.

Ogu nje ya Biblia
Kwa jumla habari haba zilizohifadhiwa juu ya Ogu ziko ndani ya Biblia. Nje yake jina la Ogu linaonekana kwenye kigae cha mwandiko wa kikabarikutoka mji wa Biblos

Ogu katika Uislamu
Masimulizi ya Kiyahudi yalipokewa na Waislamu na kubadilishwa tena. Hapa anajulikana kwa Kiarabu kama ‘Uj bin Unuq / ‘Anaq عوج بن عنق. Ushahidi uko kwa Al Tabari aliyeandika ya kwamba maiti ya Udj ilikuwa kama daraja juu ya mto Naili, pia wengine.

Kutoka mapokeo hayo ya Kiislamu jina lilifika pia katika hekaya za Waswahilikwa umbo la Unju bin Unuk


Kwa msaaada wa mtandao

Asalaam kudo
Duu huyu ni abnormal imagine daraja la mkapa eti ndo maiti ilitumika kama daraja la MTO Nile,maajabu
 
Mku nmekusoma pooooote lkn uliposema tu alikua tishio dunia nzima ndo ninapokataaga je alishawai kuja kupigana na wahehe, au akina Zwangendaba, mkuu siku utakapopata historia za nyumbani ndo utakapojua nasi tuna hadithi zetu
Naposema Dunia kwa context ya agano la kale ni mashariki ya kati pekee ndio ilikuwa dunia..... Enzi hizo watu waliishi maeneo ya mesopotamia hadi eridu mpaka misri basi na walikuwa hawazidi hata million 5 dunia nzima!!

Enzi za mfalme ogu afrika ilikuwa inaishia libya na misri tu hivyo hakukuwa bado na matishio huku afrika ingawa najua baadae afrika ilikuja kupata watu mashujaa ila all in all huyu Ogu alikuwa ni MWEUSI sababu anatambuliwa kma muamori ambaye ni jamii ya HAMITES ngozi nyeusi kabisa walioishi canaan/palestina-israel ya sasa takriban miaka 6000 iliopita hivyo ni ''mwenzetu'' huyo!!
 
Nadhani huyu mfalme OGU ana undugu na UNJU bin UNUQ
Inasemekana mkuu ndio mtu mmoja ila wazungu wanamuita OGU ila alikuwa mweusi ndio maana hata kwenye biblia anatajwa kuwa yupo kwenye uzao wa HAM ambao watoto wake walikuwa weusi mf mizraim phut cush n.k hivyo kuna ukweli kuwa UJ BIN ANAQ ama OG OF BASHAN ndio UNJ BIN UNUQ !!
 
Naposema Dunia kwa context ya agano la kale ni mashariki ya kati pekee ndio ilikuwa dunia..... Enzi hizo watu waliishi maeneo ya mesopotamia hadi eridu mpaka misri basi na walikuwa hawazidi hata million 5 dunia nzima!!

Enzi za mfalme ogu afrika ilikuwa inaishia libya na misri tu hivyo hakukuwa bado na matishio huku afrika ingawa najua baadae afrika ilikuja kupata watu mashujaa ila all in all huyu Ogu alikuwa ni MWEUSI sababu anatambuliwa kma muamori ambaye ni jamii ya HAMITES ngozi nyeusi kabisa walioishi canaan/palestina-israel ya sasa takriban miaka 6000 iliopita hivyo ni ''mwenzetu'' huyo!!
Asante mkuu ila naomba Critically hebu dhania kama Afrika hii ya kwetu enzi hizo kulikua hakuna watu au ilikuaje, saa ingine nadhan biblia iliandikwa kwa mujibu wa watu wa mashariki ya kati miksa Misri. Labda nasi tuna historia yetu nyingine kabisa labda na Nuhu wetu au Ogu wetu ila kwa vile hatuna namna ya utunzaji kumbukumbu nso maana tunasemaga tu alikua hatari dunia nzima au aliipiga dunia nzima au alitawala dunia nzima
 
Hawa wanefili ni matokeo ya malaika kuzaa na binadamu na inasemekana waliangamia na hawapo tena
Kwanini hawa malaika waliozaa na binadamu huwa hawashuki tena duniani na kuja kuzaa na mabinti wengine baada ya gharika hadi mpaka sasa?
Nini kimewazuia
Mie nadhani bado malaika huwa wanashuka aisee...rejea marehemu masogange...duuhhh...alikuwa kamili kila idara...sihaba malaika walitia nakshi kikatokea kitu kile....au hata shemela wetu kwa brother kiba...daah.
 
Kwanza kuna kitu hakileti ukweli katika Biblia maana hapa katika maandiko ya mwanzo kuna mkanganyiko inaonyesha WANEFILI WALIKUWEPO KABLA YA BINADAMU

1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6 :1

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
Wee mkuu nimekuelewa vizuri aisee...ujuwe manefili walikuwepo kitambo...sasa wakawa tishio kwa wanadamu...so mungu kutubust akili na maarifa akawatuma malaika wazae na mabinti zetu ndio wakatokea vizazi vyenye akili za kuwazidi manefil....good idea.
 
Naposema Dunia kwa context ya agano la kale ni mashariki ya kati pekee ndio ilikuwa dunia..... Enzi hizo watu waliishi maeneo ya mesopotamia hadi eridu mpaka misri basi na walikuwa hawazidi hata million 5 dunia nzima!!

Enzi za mfalme ogu afrika ilikuwa inaishia libya na misri tu hivyo hakukuwa bado na matishio huku afrika ingawa najua baadae afrika ilikuja kupata watu mashujaa ila all in all huyu Ogu alikuwa ni MWEUSI sababu anatambuliwa kma muamori ambaye ni jamii ya HAMITES ngozi nyeusi kabisa walioishi canaan/palestina-israel ya sasa takriban miaka 6000 iliopita hivyo ni ''mwenzetu'' huyo!!
Unamaanisha nini kusema hivi?

Louis Seymour Bazett Leakey alituambia kua Mtu wa Zamani/Kale zaidi aliishi Tanzania, na aliigundua hii kitu baada ya kupata Fuvu la Binadamu huyo. Kama unaelewa issue za Zinjanthropus
 
kuna movie niliionaga zuku movies Nuhu anasaidiwa kujenga safina na THE WATCHERS ...majitu hayaeleweki eleweki kama yamejengwa na mawe halafu macho yao ni mwanga mkali...

Sikuielewa ,japo pia sielewi Watchers kwa kiswahili ni nini? wakuu tufafanulieni
 
Possibility kuwa maji yalijaa mikono 15 zaidi ya mlima mrefu ikimaanisha huyu Ogu kma alikuwa na urefu wa zaidi ya futi 15 ina maana basi anaweza kuwa maji aliyazidi kimo kuendana na hoja hii ya MIKONO 15!!! Other factors remaining constant ingawa ni finyu kma unavyosema ila kwa msimamo huu wa biblia je haiwezekani??
mkuu assumptions hizo inabidi na Uhusika wa Mungu kwenye hilo zoezi hilo uwe neglected.
pia baadhi ya commentary zinasema kutumika kwa neno la kiebrania linaloendana na wanefili wa zamani sio lazima awe nefili aliyetoroka kichapo cha mafuriko, bali ni lugha kuwakilisha ufanano wa hilo jitu na majitu ya kale. maana ukiliita hivyo kwa waebrania wataelewa zaidi.

lkn kabla haijatajwa futi 15, fungu la nyuma linasema milima yote ilifunikwa (kufunikwa milima yote, assumption ilikuwa ni grobal flood hata everest yenye zaidi ya futi 20,000, yawezekana hiyo 15 foot ni kwa vimilima ambavyo vilikuwa karibu, ila lile fungu la nyuma lilipozungumzia milima yote sidhani kama huyo jamaa angeweza kusurvive).

Ikiwa ni futi 15 flat worldwide nadhani kuna sehemu zitakuwa hazijafunikwa na maji kama mlima kilimanjaro, kitu ambacho kitakanusha sentesi milima yote ilifunikwa.

Pia nawaza kwa assumption ya uwezekano wa kutoroka kwa huyo jamaa kutokana na umbo lake kuwa kubwa kuliko kimo chake.
mambo kadhaa yataibuka.
1: Mungu ataonekana ni unintelligent being kutoa adhabu ambayo kuimbe wake anaweza kuikwepa. kitu ambacho hakiungani na sifa za Mungu.
2:Mikono 15 ya watu wa enzi za nuhu ni tofauti na mikono ya kipindi hiki. kumbuka kabla ya mafuriko watu walikuwa ni wakubwa sana, na wenda ilichukuliwa reference ya mikono ya hayohayo manefili maana lengo la mafuriko pamoja na yote hao ndio walikuwa walengwa wakuu.
3:Gharika ilidumu juu ya nchi zaidi ya siku arobaini. huyo OG alitakiwa asimame kwenye maji yenye nguvu bila kula siku arobaini. Kumbuka kwao mvua ilkuwa ni mshtukizo japo nuhu alihubiri na kutoa tahadhari miaka 120. hivyo huyo jamaa hakujiandaa kisaikolijia, pia kusema alikula Mizoga kwa wigo wa bibilia watu walianza kula nyama baada ya gharika.
sidhani kama angepata stamina ya kusimama siku zote hizo. Kumbuka nguvu ya maji pia mkuu na huyo kiumbe hajawahi kukutana na hayo mazingira.

4:Mvua ilinyesha Siku 40, maji yakadumu siku 150 siku karibu 200 huyo mdau alikuwa yuko majini. na Mungu akimuangalia tu. Zaidi ya nusu mwaka. mkuu biologically kwa non-aquatic being kuwa hai majini hata kama ni maji ya kiuno?



najaribu kufikiri na kuvaa viatu vya OG napata shida inabidi assumptions nyingi sana ziongezeke, na constants nyingi sana ziondolewe na uwezo wa Mungu na nia yake udogoshwe kabisa awe kama nyampala flani tu ambaye alikiwa anaadhibu vijana wake na baadhi wakamchenga.


nawaza mkuu.
assumption kuu. Yale maji hayakuwa tulivu kama ya kwenye swimming pool hadi mdau apate kusimama raha mstarehe miezi sita, bali yalikuwa ni zaidi ya tsunami kwa maana ya nguvu na vurugu zake.
 
Back
Top Bottom