Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mkuu ukiwa msomaji wa biblia utaelewa hoja yangu kivipi Mungu anaweza toa hukumu ila akaruhusu masalia wabaki na amefanya hivyo hata kwa wanefili wa baada ya gharika (Waamori)ambayo ni familia ya mfalme Ogu

Twende taratibu

1. Mungu anamuamuru waisraeli waue wakaanani WOTE wasibakize kitu

Kumbukumbu la torati 20
16 Lakini katika miji ya mataifa haya akupayo BWANA, Mungu wako, kuwa urithi, usihifadhi kuwa hai kitu cho chote kipumzikacho;
17 lakini uwaangamize kabisa, Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, kama alivyokuamuru BWANA, Mungu wako
;

2.Tukisoma kwenye joshua baada ya kuwa wameikamata canaani waliweka makubaliano na hawa wanefili ya kuwaacha hai!!

Joshua 9:15
15 Naye Yoshua akafanya amani pamoja nao, na kufanya agano nao, ili kwamba waachwe hai; na wakuu wa mkutano wakawaapia

3.Kinyume kabisa na maagizo ya Mungu ya kwanza tunaona wagibeoni wakiachwa hai na waliingia agano ambalo Mungu alisupport

Kumbukumbu 7
1 BWANA, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang?oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe;
2 wakati BWANA, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao


4.mpaka hapa unaweza kufikiri waliamua wenyewe waisrael lahasha..... Huko mbeleni tutaona MUNGU akiwaadhibu waisraeli kwa kuvunja agano hilo la kuwaacha waamori/wagieboni hai

2 samuel 21
1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa BWANA. BWANA akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni.

Je unataka kusema Mungu ni kigeugeu au utakubaliana na mimi kuwa Mungu aliamua kuwaacha hao wagibeoni kwa kusudi lake???

Na je kama tunaona hapa Mungu aliamrisha waue waamori WOTE ila baadae Mungu alitaka wengine wabakizwe je huoni hoja ya kusema Ogu kuwa mnefili pekee kuachwa kwenye gharika kuwa ina mashiko maana tumeona kumbe Mungu akitoa hukumu ya WOTE huwa anaacha exceptions!!!

Karibu tuelimishane mkuu wangu
Cc SALA NA KAZI Malcom Lumumba Eiyer popbwinyo Kudo900

mkuu asante kwa elimu.
kama nilivyowasilisha hoja huko nyuma.
1:Bibilia inasema katika mwanzo hakupona mtu zaidi wa watu wanane. na kutoka kwa wanane hao Mungu akawaambia waijaze nchi na kuitiisha.
2:Miaka zaidi ya 2000 nadhani baadae anakuja Mungu kwa umbile la wanadamu kwa jina la Yesu. Anatukumbusha stori hiyo hiyo na kisisitiza kiwa walipona watu wanane, wengine wote waliangamia.
3:Miaka kadhaa baada ya Kupaa Yesu, Anaandika Petro kwa watu wote nikiwemo mimi na wewe kuwa
"Wala hakuuachilia ulimwengu wa Kale, bali alimuhifadhi nuhu mjumbe wake, na watu wengine saba, hapo alipoileta gharika juu ya ulimwengunwa wasiomcha Mungu" 2Petro 2:5.

######
Mkuu hoja yako nimeipata kwa uzuri. kuwa ikiwa hukumu nyingine kuna watu waliponyoka hivyo kuna uwezekano watu wakapona kwenye kila hukumu ya Mungu.
yawezekana sodoma na ghomora kuna waliopona kwa hekima hiyohiyo, wenda kwa hekima hiyohiyo hata kiyama cha mwisho kuna uwezekano wakawepo watakaokwepa (nimeexagerate kidogo kuleta maaa.).

Mkuu unazungumziaje kwa hukumu hiyo na idadi ya watu waliopona kuthibitishwa kuwa ni wanane tu na vyanzo tofautitofauti vilivyoongozwa na roho mtakatifu?.
Mungu anapomuagiza mwanadamu atekeleze hukumu zake, naye akafanya tofauti nadhani ni tofauti na Mungu akitekeleza Hukumu zake.

mfano, Mungu hakumuambia NUHU awaangamize watu, bali yeye aliifanya hiyo kazi mwenyewe kwa ufanisi wote. Kuhusu kugeuka baadae. Mungu katika operations zake agano la kale kuna mahala anaonyesha kuheshimu makubaliano ya watu. mfano Hesau alipomuuzia yakobo uzao wa kwanza. Yakobo aliirithi ahadi wakati kiuhalisia Mungu alipaswa kumpa huo urithi mkubwa yaani Hesau. Lkn Mungu akaweka kumbukumbu sawa kuwa "Basi zamani zile za ujinga Mungu alijianya kama hazioni, Bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu" Matendo 17:30


nakubaliana na wewe pia, tunapaswa kujadili hao watu wenye sifa za wanefili au waliotambulishwa kama wanefili baada ya Gharika.

maswali kadhaa yanaibuka.
Je, Hicho kitendo kilichotokea kabla ya gharika kikazaa wanefili hakiwezi kutokea baada ya gharika?

Kwa nini hakitokei sasa?

Je hawa watu warefu wa sasa ambao si wakawaida wanauhusiano wowote na Og au ni genetics za kawaida?

kitanda cha og? je tunamaarifa yoyote juu ya vitanda vya wakati huo? kuna maandiko yanaonyesha watu wa kale hasa wafalme walikuwa wanaexaggerate vipimo vya vitanda ili waonekane warefu zaidi? cc http://jbqnew.jewishbible.org/assets/Uploads/401/jbq_401_og.pdf


Kwa mujibu wa chanzo hapo juu, makadilio ya urefu wa OG au Goriath ni kama mara mbili ya urefu wa Mtu wa kawaida, Je hili ni jambo la ajabu sana?

kwa genetics za kawaida inashindikana kuwepo mtu wa namna hiyo?
 
Aisee umenisaidia kuanza kusoma biblia
kweli mkuu, hata jamaa zitto junior anatusaidia kurudia kuisoma bibilia kwa akili na kwa maarifa.
anachokifanya waumini wengi hatujui, ikiwa sio mfuatiliaji utaona ni mambo mapya.

huyu jamaa, alinifanya nisome document moja ambalo nililichukua kutoka kwa mwanatheolojia mmoja msabato aliyofundishwa huko chuoni bugema uganda. Lilinishinda kuelewa, ila baada ya kukutana na bandiko lake la epics of gilgamesh na hadithi za zamani za mafuriko ya nuhu, akkida, summerian flood etc nilirudi fasta na nikajikuta nasoma kama maji na kuongeza uelewa...

tusome bibilia mpendwa...
 
Mwanzo 6
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
3 BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.


Ukisoma kwa umakini utagundua mstari wa pili ndipo walipoanza kuzaliana.... Na hao wanefili wamekuja kutajwa mstari wa 4 ikimaanisha ni zao la mstari wa 2.....

Kuhusu neno WANA WA MUNGU WA KWELI labda muandishi alitaka aweke tu msisitizo ila bado maana ni ile ile kuwa ni WANA WA MUNGU haijalishi alimaanisha wana wa Mungu yaani malaika ama alimaanisha wana wa Mungu yani watu waliokuwa wanamuabudu ila naona hiyo WA KWELI kama msisitizo tu wa sentensi kuonyesha utofauti wa hao wana wa Mungu wa kweli kulinganisha na wanadamu wengine ambao walikuwa hawamuabudu Mungu au vilevile alitaka kuweka msisitizo juu ya Mungu anaeongelea kuwa ni YHWH na sii mwingine

Che mittoga SALA NA KAZI
Mkuu mistari inachanganya sana ,hasa wa3-4
mstari wa tatu una maana kumbwa japo sielewi
na wa 4 pia mbona kama unawatofautisha wanefili na hao wana wa watoto wa Mungu na binadamu? ina maana wanefili walikua watu hodari na wenye sifa?[emoji23]

Naona kunahaja ya kutafakari hio mistari.
Mwenye bible jamani aniazime
 
Hivi hatuwezi kumpata mtu akaenda kuuliza swali hili kwa mtu kama Titus Amigu au kiongozi yeyote wa dini akatupa muongozo ulionyooka?
 
Mkuu mitale na midimu nashkuru kwa bandiko lako lililoshiba maarifa kiukweli we ni mtu makini sana na unajibu kwa busara sana bila mihemko na kashifa wala kejeli za "wajuaji" wengine....

Nkirudi kwenye mada literature ya biblia ni ngumu kidogo ndio maana kuna sehemu biblia inasema alilisha watu elfu 5000 ila kiuhalisia wanawake hawakuhesabiwa hata adam alizaa mtoto wa kike baada ya cain ila hatajwi kokote sababu ya mila na desturi za enzi hizo katika definition ya MTU ni nini kuwa tofauti na sasa

Kingine biblia kuna mahali inasema enoko ni MTU wa saba baada ya Adamu ilihali mpaka enoko anazaliwa walishapita watu maelfu na zaidi ila aliitwa MTU wa saba sababu ya KUANGALIA kizazi hivyo wanaweza kusema watu 8 ila hapo walihesabu namba ya VIZAZI vilivyopo humo na sio watoto wala wajakazi n.k sijui inaleta maana??

So licha ya kwamba biblia inasema watu 8 it's not final ila inaweza kuwa ina maana pana zaidi kma ile ya ENOCK MTU WA SABA BAADA YA ADAM!! So huenda Mungu alikuwa hachukui hesabu za watoto wa CAIN na hivyo ogu aliweza kuwa termed kma mnyama au ''machine'' hivo haingii kwenye list ya WATU 8

Najaribu kufikiri tu mkuu
Barikiwa
 
Mkuu mistari inachanganya sana ,hasa wa3-4
mstari wa tatu una maana kumbwa japo sielewi
na wa 4 pia mbona kama unawatofautisha wanefili na hao wana wa watoto wa Mungu na binadamu? ina maana wanefili walikua watu hodari na wenye sifa?[emoji23]

Naona kunahaja ya kutafakari hio mistari.
Mwenye bible jamani aniazime

3 BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Hapa naona Mungu anasema hatashindana na mwanadamu sababu dhambi zilizidi na hayo maasi hivyo akaona awape hukumu kuwa baada ya miaka 120 gharika litakuja..... Na huu mstari wa 3 unatakiwa usome book of watchers nzima inaelezea enoko alivyokuwa anawaasa hawa wanefili waache kupambana na Mungu maana kuna wakati ulifika hadi walimtuma enoko akamwambie Mungu kuwa wanataka kupambama naye vitani.... Hata book of giants inaeleza hapo kuhusu WANADAMU KUSHINDANA NA MUNGU kwa upana zaidi ila naona hapa wamesummarise tu

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.

Hapa ni simple tu inatakiwa usome mstari wa pili kabla ya wanne.... Utagundua uzao wa wana wa Mungu na wanadamu ndio ulileta hao WANEFILI ambao walikuwa hodari.... Mfano jitu kama NIMROD alikuwa mnefili ambaye biblia ilimuita HODARI kwenye mwanzo 10..... So kabla ya mstari wa pili hakukuwa na wanefili ila walikuwepo SIKU ZILE baada ya mstari wa pili unaosema wana wa Mungu walioa wanadamu
 
3 BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Hapa naona Mungu anasema hatashindana na mwanadamu sababu dhambi zilizidi na hayo maasi hivyo akaona awape hukumu kuwa baada ya miaka 120 gharika litakuja..... Na huu mstari wa 3 unatakiwa usome book of watchers nzima inaelezea enoko alivyokuwa anawaasa hawa wanefili waache kupambana na Mungu maana kuna wakati ulifika hadi walimtuma enoko akamwambie Mungu kuwa wanataka kupambama naye vitani.... Hata book of giants inaeleza hapo kuhusu WANADAMU KUSHINDANA NA MUNGU kwa upana zaidi ila naona hapa wamesummarise tu

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.

Hapa ni simple tu inatakiwa usome mstari wa pili kabla ya wanne.... Utagundua uzao wa wana wa Mungu na wanadamu ndio ulileta hao WANEFILI ambao walikuwa hodari.... Mfano jitu kama NIMROD alikuwa mnefili ambaye biblia ilimuita HODARI kwenye mwanzo 10..... So kabla ya mstari wa pili hakukuwa na wanefili ila walikuwepo SIKU ZILE baada ya mstari wa pili unaosema wana wa Mungu walioa wanadamu
mkuu zito bible ya kiswahili please
 
Mkuu swali ni hili naona hatuelewani

Mnefili alikuwepo kabla ya gharika..... Akawepo baada ya gharika je iliwezekanaje ilihali Mungu alishaapa kuwafuta wote kasoro Nuhu ambaye hakuwa ameoa WANADAMU yaani watoto wa CAIN

Hapa tu nisaidie
Nafikiri uelewi wanefili walizaliwa tena baada ya gharika kumbuka uzao wao ulitokana na Nalaika kuingilia wanadamu hii tabia iliendelea ndo maana kama utawaelewa waamori wanefili wanetokea hapo maana yake uzao wa hao malaika hao waamori kizuri zaidi na kipo wazi nimrodi hakuwa mtu wa kawaida nikujulishe tu hawakuwa tu hao hadi wana wa anaki kwanini utaki kusoma makabila hayo utafute sifa zao humo humo kwenye Biblia.
Wakati wa ujenzi wa mnara ndio hao hao walikuwa chanzo sasa ukijua nimrodi katokea Wapi ña zile kabila za hamu hautasema wanefili walibakia labda haujaelewa huo mstari uliokazania.
 
Jamani jamani muangalie kabila la waamori ukisoma kwa makini tangu linatajwa mpaka tu kwa ogu utagundua malaika waouvu waliendelea na tabia ya kuwaingilia watu na kuzaa Major. Maana malaika walikuwa wana wa Mungu saaa ukisema mwandishi kafanyaje unalosea hao ndo wana wa Mungu walioasi akiwemo shetani mwenyewe wanakuja kupotea baada ya agano jipya yesu kumfungia kuzimu shetani shetani añandilandi tena duniani.
 
Mkuu swali ni hili naona hatuelewani

Mnefili alikuwepo kabla ya gharika..... Akawepo baada ya gharika je iliwezekanaje ilihali Mungu alishaapa kuwafuta wote kasoro Nuhu ambaye hakuwa ameoa WANADAMU yaani watoto wa CAIN

Hapa tu nisaidie
Kwani malaika walikufa? Sí tunaambiwa chanzo cha hayo manefili ni muingiliano wa wanadamu na malaika kwani wanadamu hawakuzaliwa tena namalaikakuzini tena? Nikujibu hivyo usipoelewa endelea na tafiti yako
 
Kwani malaika walikufa? Sí tunaambiwa chanzo cha hayo manefili ni muingiliano wa wanadamu na malaika kwani wanadamu hawakuzaliwa tena namalaikakuzini tena? Nikujibu hivyo usipoelewa endelea na tafiti yako
Jamani jamani muangalie kabila la waamori ukisoma kwa makini tangu linatajwa mpaka tu kwa ogu utagundua malaika waouvu waliendelea na tabia ya kuwaingilia watu na kuzaa Major. Maana malaika walikuwa wana wa Mungu saaa ukisema mwandishi kafanyaje unalosea hao ndo wana wa Mungu walioasi akiwemo shetani mwenyewe wanakuja kupotea baada ya agano jipya yesu kumfungia kuzimu shetani shetani añandilandi tena duniani.
Nafikiri uelewi wanefili walizaliwa tena baada ya gharika kumbuka uzao wao ulitokana na Nalaika kuingilia wanadamu hii tabia iliendelea ndo maana kama utawaelewa waamori wanefili wanetokea hapo maana yake uzao wa hao malaika hao waamori kizuri zaidi na kipo wazi nimrodi hakuwa mtu wa kawaida nikujulishe tu hawakuwa tu hao hadi wana wa anaki kwanini utaki kusoma makabila hayo utafute sifa zao humo humo kwenye Biblia.
Wakati wa ujenzi wa mnara ndio hao hao walikuwa chanzo sasa ukijua nimrodi katokea Wapi ña zile kabila za hamu hautasema wanefili walibakia labda haujaelewa huo mstari uliokazania.
Okay nimekuelewa mkuu kuwa baada ya gharika malaika walizaa tena na wanadamu !!! Ila je malaika gani hao mbona biblia inasema walipofanya uzinzi kma sodoma na gomorrah walifungwa kuzimu

Yuda
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.


Hivyo kama malaika walishapewaga hukumu kwa uasherati waliofanya kwa kufungwa chini ya dunia kusubiri hukumu je hao waliozaa na wanadam baada ya gharika walitoka wapi

Kingine Mungu alileta gharika ili kuharibu uzao huo sasa angekuwa wa ajabu kiasi gani atoe adhabu ambayo anajua kesho tena malaika watarudia huo huo ujinga wa kuzalisha wanadamu hivyo ina maana gharika isingekuwa imesaidia lolote

Najaribu kuwaza tu
 
Sijaelewa ulichotaka kutuambia ila naamini ulitaka kutuambia kitu flani muhimu,lakini pia ungelijaribu kutupa na wew ushahidi wako ikibidi na baadhi ya nukuu ili twende sawa kuhusu kusalia kwa mtu huyo au kufa kwa mtu huyo wakati wa garika maana nukuu nyingi sana zinaonesha uwezekano wa Ogu kusalia na tayari watu wengi wamechangia hapa na nukuu zao kutoka vitabu tofauti tofauti
Well,nilichotaka kusema hapa ni kwamba kuna uwezekano mkubwa sana wa mtu huyu kuwepo lakini kama ni kweli alikuwepo basi si kweli kuwa alikuwa na kimo na umbo analodaiwa kuwa nalo na mwandishi wa thread hii kwasababu kuwepo kwa mtu wa namna hii kwa maana ya kimo chake na size ya mwili wake isingekuwa ajabu kwasababu kun a ushahidi mwingi sana unaonesha kuwa Wanefili wa wakati ule walikuwa na kimo kama cha huyu jamaa anayeelezwa hapa...

Kwa sasa sina ushahidi wa kuweka hapa isipokuwa nina uhakika mkubwa sana wa ninachkiandika hapa.Nitaweka ushahidi hapa nikiwa nimetulia na kufukua makabrasha yangu...
Lakini pia naomba nikuulize swali moja Hope utatusaidia

Nuhu aliwezaje kujenga safina ile kubwa peke yake? Na aliwezaje kupata mbao au miti mingi vile kujengea na aliitoa wapi ikiwa sehemu alikokuwa akiijengea kulikuwa ukanda wa jangwa?
Mkuu,hili swali lako ni dogo sana kama tu utaelewa kuwa the whole shaw ilisimamiwa na Mungu ambaye HAKUNA kinachomshinda.Ni sawa na mtu aanze kuwaza kuwa waliokuwemo kwenye safina walikula nini kwa siku 40 wakati huo huo Yesu aliweza kulisha watu,tena wanaume 5000 kwa mikate mitano tu na samaki wawili...

Mungu kama alivyo ukimuelewa vyema haya maswali yanapotea yenyewe tu.Nadhani unamkumbuka kisa cha unga usioisha kwenye Biblia.Kama kuna mtu alitumia unga bila kuisha,inashindikana nini watu saba kutumia chakula kidogo [kama kilikuwa kidogo kweli] kilichokuwa kwenye safina kwa siku zote 40? Au ni kwanini tu asifunge matumbo yao kupata njaa kwa siku hizo 40? Hili ni jambo zaidi ya dogo sana kwa Mungu,yaani ni ilivyo rahisi kwa Mungu kutenda hili ni sawa na wewe ilivyo rahisi kumnyanyua sisimizi. Umehoji kuhusu uwezo wa Nuhu. Mungu anashindwaje kumpa Nuhu uwezo unaohitajika ili aijenge Safina kama hakuwa nao?

Brother/Sister,kumbuka tunamjadili Mungu asiyeshindwa CHOCHOTE hapa....
 
Back
Top Bottom