fidel castro wapili
JF-Expert Member
- Mar 18, 2017
- 3,497
- 2,911
Walikuwa watu walioshiba. Cku ya kiama patakuwa na BINAADAM dizain tofauti tofauti.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Daah una hazina kubwa saana ila ningekuomba tu mkuu ufafanue kidogo kuhusu makazi ya hawa jamaa huko chini lkn pia kuhusu Obama,Asante sana!!Mkuu,kwa namna ninavyoelewa mimi ni kwamba,kwanza suala au dhana ya malaika "kufungwa" kwa upande wangu bado halijakaa sawa....
Nasema hivui kwa sababu sijawahi kuelewa huko "kufungwa" ni kwa namna ipi,lakini pia bado sijaelewa kama walifungwa kweli walifungwa wakati upi. Nasema hivi kwasababu kwenye kitabu cha Ayubu ule ukurasa wa kwanza tu kuna kisa cha Shetani kujumuika na Malaika [Wana wa Mungu] mbinguni huko na alipoulizwa alisema kuwa ametokea duniani alikokuwa anazunguka zunguka. Ukiacha tukio hili kuna tukio la Shetani kufungwa miaka 1000 kwenye kitabu cha Ufunuo baada ya ile dhiki kuu.Hapa inaonekana huyu balaa alikuwa hajafungwa au kuwepo kifungoni...
Ayubu 1:7
7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
Ufunuo wa Yohana 20:1-3
1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.
Sasa kwa mantiki hii ni vigumu sana kuhitimisha tu wamefungwa kuzimu na hawatoki humo [kwa maana ya wengi na iliyopelekea kuleta swali uliloniuliza] na kufanya swali la kizazi chao kuwa kuendelea kuwepo kuwa ni gumu zaidi...
Jambo la msingi ambalo wengi hapa wanapaswa walielewe ni kwamba Wanefili walikuwepo hata baada ya Gharika.Waliendelea namna ipi hilo ni jambo la kufanyia utafiti lakini kuna nadharia moja inaeleza kuwa,kwasababu viumbe hawa [Wanefili] walikuwa wanauelewa mkubwa sana wa kanuni za maumbile [physical law] waliweza kupona kwenye gharika kwa namna moja au nyingine au hawakupona lakini malaika wale waliendeleza kizazi kile kwa namna ile ile kwasababu wao gharika haikuwahusu...
Ukiniuliza mimi binafsi naelewaje au kufahamuje viumbe hawa waliwezaje kupatikana baada ya gharika,kama msingi wa swali lako ulivyo ukweli ni kwamba hadi sasa sijapata jibu lenye mashiko au niseme tu kuwa sifahamu ilikuwaje wakaendelea kuwepo lakini nina uhakika kuwa waliendelea kuwepo....
Nina dhana nyingi tu ambazo zinajaribu kuelezea hawa majitu waliendeleaje kuwepo na bado naendelea kufuatilia....
Kwanza mkuu nianze kwa kukueleza kuwa ishu ya Yericko ni tofauti sana na hii japokuwa inahusiana pia. ni tofauti kwasababu Rahabu [kama sijakosea] alitoa msaada kwa wapelelezi wa Israeli na wakamuahidi watamuacha hai.Hapa kuna jambo kubwa sana mkuu kwasababu bloodline ya huyu mwanamke ndiyo hii tunayokuja kuipata kwa Yesu.Yaani uzao wa Rahabu ndio blood line ya Yesu. Hili niliache kwa sasa maana kuna mengi hapo,lakini pia unapaswa ukumbuke kuwa maelekezo ya Mungu ya kuwaangamiza Wakanaani ilikuwa ni wanaume wote na wanawake waliomjua mwanaume.Jambo hili linasababishwa na suala hili hili la Wanefili.Hili nalo lina mengi lakini ninachotaka ukione hapa ni kwamba kitendo cha Mungu kuruhusu Rahabu kuendelea kuishi bila kujali alikuwa ni kahaba na kitendo cha kuwa kahaba kina maana kuwa na uwezekano wa kuwa na watoto wenye damu hii ya Wanefili kinaleta maswali mengine magumu sana...
.....sasa basi,kunakuwa na sababu ya kahaba huyo kuachwa hai,je kuna sababu ipi ya Wanefili wa kabla ya gharika kuachwa? [Japokuwa sijasema hawakuachwa] Dhana ya huyu OG kumsaidia nuhu ni ya kufikirika zaidi kwasababu haina ushahidi wa kimaandiko kuwa alimsaidia Nuhu,ni mawazo ya watu tu. Kwa maoni yangu,kama walipona basi huenda ni kwa sababu ambayo huenda hatujaijuwa bado....
Kuhusu Tekinolojia ya wakati huo ni kwamba mimi binafsi ninaamini kuwa wakati ule kulikuwa na maendeleo ya kiteknolojia zaidi ya wakati huu.Ninasema hivi kwasababu nimepitia dicumentary nyingi tu zikielezea maendeleo ya hatari ya wakati huo.Kwa kukuonesha hili nenda katafute documentary moja inaitwa "Technology of the Fallen" utapata mwanga.Maendeleo haya yalitumiwa na binadamu wengine,sisemi kuwa Nuhu aliitumia isipokuwa nataka tu nianze kubadili mtazamo wako kuwa zamani hizo hawakuwa na maendeleo au maendeleo yao yalikuwa duni kuliko leo....
....Mungu kaka alivyo yeye ndiye baba wa teknolojia yote,malaika waasi waliona namna Mungu alivyokuwa anaweka kanuni zote za Physics na vitu vyote kwa ujumla wake na wakaweza kuwa na uelewa mkubwa sana wa kanuni hizo na zingine nyingi.Kumbuka tu ni malaika hao hao waliokuja kuleta maarifa haya kwa binadamu,maarifa ambayo kimsingi binadamu hakupaswa kuyafahamu,maarifa haya yanaitwa "forbiden knowledge".Binadamu hakupaswa kuyaelewa maarifa haya kwasababu hakuumbwa kuyahimili na ndiyo maana walipoyajuwa walianza kuangamizana wao kwa wao na hata leo unaona yanavyotutesa.Sasa kama hawa waliona tu na wakawa na ujuzi huo,vipi Mungu mwenyewe ambaye ndiye alikuwa msimamizi mkuu wa kujengwa safina hadi gharika yenyewe ambaye ndiye mwenye kanuni na ujuzi huo?
Ninachotaka ukielewe hapa ni kwamba,jambo lilalosimamiwa na Mungu mwenyewe weka pembeni yanayowezekana na yasiyowezekana kwa binadamu. Kwa hiyo dhana ya huyo OG "kumsaidia" Nuhu siioni kama ina mashiko kwasababu tu Nuhu "asingeweza" kuijenga mwenyewe....
Hawa Wanefili hawajaisha mkuu,tena nasema hivi kwa uhakika kabisa...
Ni nini kinanipa uhakika mkubwa hivi?
Vipo vingi tu na cha kwanza ni Biblia yenyewe....
Mosi,Biblia yenyewe inakiri Wanefili walikuwepo hata baada ya gharika [mwanzo 6:6],kama walikuwepo baada ya gharika basi watakuwepo hadi leo maana sijaona sababu ya kutokuwepo kwao....
Pili,Yesu mwenyewe alisema "kama ilivyokuwa nyakati za Nuhu ndivyo itakavyokuwa wakati wa kuja kwake mwana wa Adamu" hii inamaana kuwa,moja ya alama za kurudi Yesu mara ya pili ni uwepo wa mambo kama ya nyakati za Nuhu na moja ya mambo ya wakati ule ni uwepo wa Wanefili...
Tatu,utafiti ambao umeshafanywa na watu wengi sana unaonesha kuwa Majitu haya yapo hadi leo hivyo sina sababu ya kupinga na nimeshaangalia video moja kutoka kwa mtu aliyeshuhudia kuona majitu haya kwenye D.A.M.Bs [Deep Underground Military Bases] zilizoko karibu dunia nzima chini ardhini na yanachapa kazi kabisa. Kilichoko huku juu ni mfano wa kilichoko huko chini.Majiji unayoyaona huku juu ni madogo sana kwa size ya majiji yaliyoko huko chini ardhini ma majiji yote yameunganishwa kwa barabara zilizojengwa kwa viwango vya hali ya juu kiteknolojia,ngoja niishie hapa kwenye hili...
Nadhani swali litakalofuatia hapa ni kuhusu sababu za majitu haya kufichwa au kujificha.Sababu namba moja iliyofanya haya ni udanganyifu....
Ni udanganyifu namna gani?
Kwanza kabisa baada ya gharika Shetani aliamua kutengeneza namna mpya ya kukabiliana na Mungu na njia hiyo ni udanganyifu. Udanganyifu wa kwanza kabisa ni kuhakikisha kile ambacho Mungu anawaeleza binadamu kionekane ni uwongo.Mojawapo wa mfano wa jambo hili ni suala hili la uwepo Mjitu haya.Shetani aliamua kuendesha harakati zake mafichoni huko na siyo wazi maana kama ikiwa siyo mafichoni watu wataona majitu haya na kuverify maelezo ya kwenye Biblia kuwa ni kweli yalikuwepo majitu na hili lina madhara makubwa sana kwao maana kuna mtaalam mmoja wa masuala ya Evolution alisema kuwa kama itaonekana ni kweli kulikuwepo Wanefili basi evolution inakufa kifo cha kibudu.Kuna aina nyingi sana za udanganyifu haswa kwenye historia ambako ndiko kwenye msingi mkubwa sana wa kuona Mungu anasema kweli namna ipi kwenye kwenye Biblia na maeneo mengine.
Hii ndio sababu moja na ndogo sana na zipo nyingi sana na nadhani hii inatosha kwa hapa....
Ni kweli kuwa viongozi wa dunia wengi ni bloodline isiyokuwa na asili ya binadamu,Moja ya damu inayosadikiwa haina asili ya binadamu inaitwa RH-Negative,nakupa kazi mkuu kafukue ufahamu mengi kuhusu group hili la damu....
Kuna namna ambayo unaweza kuwa na bloodline ya Wanefili na hutakuwa na umbo kubwa na hili linaratibiwa kwenye DNA yako na hiki ndicho alichokifanya shetani ili kuendelea kufanya kazi yake kwa kutumia kizazi chake.Kwa namna hii hata leo tuna "Wanefili" lakini hawaonekani kwa namna inayotarajiwa na wengi kuwa Mnefili ni mwenye umbo kubwa...
Hii siyo ajabu kwasababu ukiwafuatilia marais wa Marekani kwa mfano unaona kabisa ni bloodline moja na inakwenda kuungana na bloodline ya Royal Family kule UK.Brad Pit naye ni blood line hii,ukiangalia hakuzaa na Angelina Jolie kwa bahati mbaya maana naye pia ni bloodline hii hii...
Nadhani kuna mtu anaweza hoji juu ya Barack Obama na bloodline yake,ninachotaka kusema hapa ni kwamba kuna mengi ukiyajuwa kuhusu mtu huyo unaweza baki mdomo wazi...
Acha niishie hapo kwa leo mkuu....
Mungu akubariki sana..
Tuombe uzima tuendelee kupeana kiduchu kiduchu namna hii....
Utanitag mkuu hiyo madaAiseeee.... Mkuu Eiyer indeed wewe ni true great thinker maana umenipa material zaidi ya niliohitaji na nimegundua sifahamu hata 2% ya mambo ya sirini ya dunia hii ila umenipa mwanga nitatafiti hayo ulionitonya ili niongeze maarifa na kupata majibu ya maswali ninayojiuliza.
Once again nashkuru kwa kuja kutupa darasa murua kabisa ila usiende mbali sana kuna mada nyingine nimeipandisha ila mods hawajaiachia na nategemea utakuja kutupa darasa tena
Kudos!
Umeelewa nilichoandika?Waamori ni uzao wa nimrodi unafikiri nimrodi alikuwa nani ni yale yale majitu soma mwanzo hakunahaja ya kukimbia mbele mwazo 10:8-20
Je nimrodi si alizaliwa na kushi mwana wa hamu mzao wa nuhu je nuhu hakuwa mabaki ya gharika au nini tena
Amina ndugu,Ahsante Chief mungu awe nawe kwa kila jambo utendalo na akusamehe makosa yako maana hujui utendalo
Enenda katika imani ya bwana na yafanye matendo yako yawe nguzo njema ya maisha yako bila kumchukiza muumba wako
Bwana awe nawe na ninamwomba mungu amfanye ndugu yangu Da'vinsi asipite huku maana shetani anaweza kuijaribu imani yake.
Umepitia aina ya maneno waliyotumia walio ni quote?Mkuu popbwinyo kwanza punguza mihemko kama una hoja unaweza ileta tu kistaarabu bila kushambulia mtu yeyote humu mbona kina mitale na midimu au mkuu Eiyer wamepinga hoja yangu ila tumeeleweshana kwa vifungu na facts na mjadala umeenda vizuri tu sasa kejeli matusi ya nini tujifunze kuweka mahaba ya kiimani pembeni tunapojadili mada kama hizi
1. Kwanza toka mwanzo nimesema source zangu ni VITABU tofauti yaani biblia quran na vitabu vya wayahudi kma tanakh,torah au talmud pia pseudepigraphi kama book of jubilees,jasher,book of giants n.k sasa sielewi kwanini mada ya kihistoria nikiquote vitabu vinginr igeuke ya VIJIWENI ina maana hata historia ya nyerere itageuka ya vijiweni kisa haipo kwenye biblia??? Kwanini tunapenda kujifunga sana ina maana hiyo biblia ilishushwa tu au ulitegemea ingeandika kila kitu
Kwa mfano wwe nilikuhoji unaweza niambia biblia inaongeleaje kuhusu kifo cha ogu??? Kama haiongelei je ukitaka kujua alikufaje utafanyeje?? Kwanini hatupendi kupanua ufahamu kisa tu KWENYE BIBLIA HAIPO
Kitabu nilichoquote baadhi ya simulizi kutoka kitabu cha Yasher wwe umeita za vijiweni lakini nabii musa na waandishi wengine 3 wa biblia wanakitambua hata book of Enoch biblia kupitia kitabu cha YUDA inakitambua sasa ww ni nani kuita za kijiweni ina maana unajua sana kuliko musa au daudi ama Yuda??
Joshua 10:13
Hayo, je! Hayakuandikwa ndani ya kitabu cha Yashari
2 Samuel 1:18
18 (kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema,Wana wa Yuda na wafundishwe haya
2. Kingine hii historia ya waisraeli imeandikwa kwenye vitabu vingi tu vya kihistoria vya waisraeli na wanavitumia kma official factbook sasa iweje historia ya nchi yao wameandika wenyewe ila mtanzania wa kutoka kakonko kigoma aseme historia hiyo ni ya uongo kisa biblia haijaandika?? Kweli tumefikia hapo kiasi kwamba historia za nchi zetu tunazipuuza kisa imani za kidini?? Yaani leo hii historia ya nchi flani huitambui kisa biblia haijaandika?? Ulitegemea biblia itaandika kila kitu??
3. Kingine vipimo vya ogu niliviweka hapa kwamba alikuwa na zaidi ya futi 13 kulingana na vipimo vya muandishi wa hesabu ingawa wachambuzi wanasema kulingana na tafsiri ya orijino biblia ya kiebrania wanasema amezidi futi 28!! Sasa hiyo ya Amos nimeweka ili kuonyesha kuwa ALIKUWA mrefu na mkubwa hta kama hafikii MNAZI.... Ila kma hoja ni urefu takwimu za kibiblia unazotaka nmeshaweka ssa sijaelewa kipi unachoamua kubisha
Ni hayo tu
Barikiwa
Basi sawa mkuu ila jaribu kupunguza jazba haina haja ya kumrushia mtu maneno makali kisa naye kakurushia sasa busara yako ya 43 iko wapi?? 2 wrongs don't make a rightUmepitia aina ya maneno waliyotumia walio ni quote?
Hebu yapitie uone km haikuwa sahihi mm kuwajibu hivyo,
Am 43 mtu ananiita mtoto kisa tu nimejibu kwa kuchelewa hoja zungumzwa,sasa ulitegemea nijibu vipi,acha unafki
Asante sana kwa kunionesha busara ya vitabuni na siyo busara halisiBasi sawa mkuu ila jaribu kupunguza jazba haina haja ya kumrushia mtu maneno makali kisa naye kakurushia sasa busara yako ya 43 iko wapi?? 2 wrongs don't make a right
Uwe na jioni njema
Samahani mkuu niliquote kwa bahati mbayaUmeelewa nilichoandika?
acha kuwa mgumu mimi nimesema malaika hao wamefungwa??Ufunuo 20:1-3
1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.
Hapa Shetani alifungwa kuzimu na hii ni baada ya kufufuka Yesu.....
Dhana na kuwa malaika wamefungwa kwa maana physical huwa ina matatizo mengi sana.Ukiangalia kinachoendeleaduniani leo ni ngumu sana kuona kuwa ni kweli kafungwa kwa namna mnayoisema ninyi....
Ninaamini maandiko yalikuwa yanamaanisha kitu kingine kabisa yaliposema "wamefungwa"...
acha kuwa mgumu mimi nimesema malaika hao wamefungwa??
Au hukuelewa nimesema aliyefungwa ni shetani na ninakazia tena ni baada ya yesu kufufuka kama nilikosea kuandika nisamehe kwa hilo mkuu
Kingine ujue kama shetani angeoparate duniani mpaka Leo ungewaona wanefili wa kizazi kipya but wanao oprate now ni malaika Walio chini yake. Tena hawana nguvu wala haki hiyo kwa sababu kabla ya agano jipya walijiamlia kumwingia mwanadamu watakavyo.ila sio kama sasa hawa malaika kukutumikisha jua umeamua mwenyewe uliza tena mkuu nakukaribisha kwa upendo
Wewe usituharibie mada, kaa kimya watu tupate ilimu, kama huamini katika hilo wewe pita hiviKwani yesu alikufa ??? unao ushahidi ??
Wewe usituharibie mada, kaa kimya watu tupate ilimu, kama huamini katika hilo wewe pita hivi
Sio maudhui ya mada hiiMbona unakimbia swali ki aina aina ???
Mimi nimekuuliza kama ulivyoandika , jee yesu alikufa ??? unao ushahidi ?? kuamini au kutoamini ni jambo jengine
tuwekee ushahidi yesu alikufa wapi ???
1 uko sahihi kabisa kwa mujibu wa biblia ila vitabu vya wayahudi wenye nchi yao alipoishi ogu wanasema alikuwepo kabla ya gharika ndio maana nikaleta uzi humu ili tujue nani mkweli nani anapotoaha.... Wanadai hata hao waamori ni zao lake yeye ndio maana alikua mfalme wao miaka yote.Mi kwa uelewa wangu nadhani mnachanganya
OGU Alitoka kwenye jamii ya amorites people
Na AMORITES ni uzao wa CAANAN mwana wa Nuhu.
Na biblia iliposema alibaki OGU kati ya Giants ni kwamba yeye ndio alikuwa wa mwisho kwa duniani kusumbua kipindi kile.
SWALI MUHIMU NI KUWA: WALIRUDIJE BAADA YA GHARIKA??
Ndio wengi tunarudi kwa Ham baba yao na mama yao ambae haongelewi na huyo mtoto wa CAANAN why alizaa GIANTS mbona watoto wengine wa HAM hawakuzaa GIANTS??
SO CAANAN NDIO SHIDA HAPA YEYE NDIO WA KUDADAVUA.....(NA WHY NUHU ALIMLAANI)...KWA CAANAN NDIO PENYE JIBU LA KWELI
Hii mada kuhusu canaan kulaaniwa na sio ham ni pana sana itabidi nipandishe uzi kabisa wa kujitegemea watu wafungukeSO CAANAN NDIO SHIDA HAPA YEYE NDIO WA KUDADAVUA.....(NA WHY NUHU ALIMLAANI)...KWA CAANAN NDIO PENYE JIBU LA KWELI
kaulize bibliaKwani yesu alikufa ??? unao ushahidi ??