Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Well,nilichotaka kusema hapa ni kwamba kuna uwezekano mkubwa sana wa mtu huyu kuwepo lakini kama ni kweli alikuwepo basi si kweli kuwa alikuwa na kimo na umbo analodaiwa kuwa nalo na mwandishi wa thread hii kwasababu kuwepo kwa mtu wa namna hii kwa maana ya kimo chake na size ya mwili wake isingekuwa ajabu kwasababu kun a ushahidi mwingi sana unaonesha kuwa Wanefili wa wakati ule walikuwa na kimo kama cha huyu jamaa anayeelezwa hapa...

Kwa sasa sina ushahidi wa kuweka hapa isipokuwa nina uhakika mkubwa sana wa ninachkiandika hapa.Nitaweka ushahidi hapa nikiwa nimetulia na kufukua makabrasha yangu...

Mkuu,hili swali lako ni dogo sana kama tu utaelewa kuwa the whole shaw ilisimamiwa na Mungu ambaye HAKUNA kinachomshinda.Ni sawa na mtu aanze kuwaza kuwa waliokuwemo kwenye safina walikula nini kwa siku 40 wakati huo huo Yesu aliweza kulisha watu,tena wanaume 5000 kwa mikate mitano tu na samaki wawili...

Mungu kama alivyo ukimuelewa vyema haya maswali yanapotea yenyewe tu.Nadhani unamkumbuka kisa cha unga usioisha kwenye Biblia.Kama kuna mtu alitumia unga bila kuisha,inashindikana nini watu saba kutumia chakula kidogo [kama kilikuwa kidogo kweli] kilichokuwa kwenye safina kwa siku zote 40? Au ni kwanini tu asifunge matumbo yao kupata njaa kwa siku hizo 40? Hili ni jambo zaidi ya dogo sana kwa Mungu,yaani ni ilivyo rahisi kwa Mungu kutenda hili ni sawa na wewe ilivyo rahisi kumnyanyua sisimizi. Umehoji kuhusu uwezo wa Nuhu. Mungu anashindwaje kumpa Nuhu uwezo unaohitajika ili aijenge Safina kama hakuwa nao?

Brother/Sister,kumbuka tunamjadili Mungu asiyeshindwa CHOCHOTE hapa....

Sawa Chief hapo nimekwelewa
 
Okay nimekuelewa mkuu kuwa baada ya gharika malaika walizaa tena na wanadamu !!! Ila je malaika gani hao mbona biblia inasema walipofanya uzinzi kma sodoma na gomorrah walifungwa kuzimu

Yuda
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.


Hivyo kama malaika walishapewaga hukumu kwa uasherati waliofanya kwa kufungwa chini ya dunia kusubiri hukumu je hao waliozaa na wanadam baada ya gharika walitoka wapi

Kingine Mungu alileta gharika ili kuharibu uzao huo sasa angekuwa wa ajabu kiasi gani atoe adhabu ambayo anajua kesho tena malaika watarudia huo huo ujinga wa kuzalisha wanadamu hivyo ina maana gharika isingekuwa imesaidia lolote

Najaribu kuwaza tu
Umesoma nani anayeongea na wakati gani mkuu
Malaika walifungwa kuzimu nani kasema unajua maana ya agano jipya na la kale su imagino ri agano jipya su la kale ni vitabu vya biblia tu malaika mkuu shetani yuko kuzimu baada ya yesu kufufuka na wangine ndo unasikia wanataabisha watu kabla ya yesu shetani hakuwa kuzimu alikuwa duniani soma uelewebiblia na nyakati na majira ya biblia mkuu unapouliza swali kama hilo nazidi kuona ulivyo lalia vitabu vya miongozo yaani vilivyoongezwa tu
Zaidi ya kuchambua ndani ya Biblia mkuu hakuna malaika aliyekuwa kuzimu na kuzimu kulikuwa na wafu tu
Angalia mwazilishi wa vita na wanadamu alikuwa shetani mwenyewe ndo maana sodoma na gomora ilikuwa hatari mbona Leo Mungu ajawateketeza baadhi watu waovu kama sodoma ujue agano ni nini na linamaanisha nini su nifupishe
Hao malaika walitupwa Wapi baada ya kuasi katika agano la kale weka reference hapa
Au ujue kuwa walioperate mpaka yesu alipofufuka ndo kufungiwa tena aliyefungiwa ni shetani ambaye ni kiongozi wao na jamaa bado wapo ila uwezo wa kuingilia walimwengu umekua tofauti kwa sababu Baba lao lilitupwa kuzimu na limefungwa kwa kunyanganywa mamlaka so hautawaona wanefili tena kipindi hiki
 
Mkuu Eiyer habari za siku.... Umepotea sana jukwaani ila nmefurahi sana umeweza kuja na kutupa elimu adimu kama kawaida yako great thinker

Nkirudi kwenye mada...kwa kuzingatia objections zako za ''kisomi'' nina maswali kadhaa naomba utujuze

1. Je wanefili waliwezaje kurudi baada ya gharika if at all waliangamizwa wote kwenye gharika?? Na biblia iko wazi kuwa wale malaika walifungwa kuzimu kusubiri hukumu siku ya mwisho je hiyo bloodline yao iliponaje gharika sasa ambapo tukikataa ogu alisalimika.
Mkuu,kwa namna ninavyoelewa mimi ni kwamba,kwanza suala au dhana ya malaika "kufungwa" kwa upande wangu bado halijakaa sawa....

Nasema hivui kwa sababu sijawahi kuelewa huko "kufungwa" ni kwa namna ipi,lakini pia bado sijaelewa kama walifungwa kweli walifungwa wakati upi. Nasema hivi kwasababu kwenye kitabu cha Ayubu ule ukurasa wa kwanza tu kuna kisa cha Shetani kujumuika na Malaika [Wana wa Mungu] mbinguni huko na alipoulizwa alisema kuwa ametokea duniani alikokuwa anazunguka zunguka. Ukiacha tukio hili kuna tukio la Shetani kufungwa miaka 1000 kwenye kitabu cha Ufunuo baada ya ile dhiki kuu.Hapa inaonekana huyu balaa alikuwa hajafungwa au kuwepo kifungoni...

Ayubu 1:7
7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

Ufunuo wa Yohana 20:1-3

1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.

2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;

3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.




Sasa kwa mantiki hii ni vigumu sana kuhitimisha tu wamefungwa kuzimu na hawatoki humo [kwa maana ya wengi na iliyopelekea kuleta swali uliloniuliza] na kufanya swali la kizazi chao kuwa kuendelea kuwepo kuwa ni gumu zaidi...

Jambo la msingi ambalo wengi hapa wanapaswa walielewe ni kwamba Wanefili walikuwepo hata baada ya Gharika.Waliendelea namna ipi hilo ni jambo la kufanyia utafiti lakini kuna nadharia moja inaeleza kuwa,kwasababu viumbe hawa [Wanefili] walikuwa wanauelewa mkubwa sana wa kanuni za maumbile [physical law] waliweza kupona kwenye gharika kwa namna moja au nyingine au hawakupona lakini malaika wale waliendeleza kizazi kile kwa namna ile ile kwasababu wao gharika haikuwahusu...

Ukiniuliza mimi binafsi naelewaje au kufahamuje viumbe hawa waliwezaje kupatikana baada ya gharika,kama msingi wa swali lako ulivyo ukweli ni kwamba hadi sasa sijapata jibu lenye mashiko au niseme tu kuwa sifahamu ilikuwaje wakaendelea kuwepo lakini nina uhakika kuwa waliendelea kuwepo....

Nina dhana nyingi tu ambazo zinajaribu kuelezea hawa majitu waliendeleaje kuwepo na bado naendelea kufuatilia....
2. Hoja ya kusema Mungu alisimamia gharika hivo basi hakuna mnefili ambaye angepona sababu Mungu alishadhamiria..... Mbona wakati ukuta wa yeriko unaangushwa yule malaya alisalimika kwa Mungu kuacha nyumba yake pekee je haiwezi kuwa case kwa Nuhu ukizingatia alimsaidia kwenye ujenzi hasa kufuata miti iliyotumika kwenye ujenzi haikuwa ikipatikana mashariki ya kati na vilevile ukubwa ule wa meli usingeweza kuwa assembled na binadamu wa kawaida kwa teknolojia ya enzi hizo ila huyu ogu alikuwa msaidizi mkubwa je haiwezi kuwa sababu ya Mungu kumpa neema yake asife kwenye gharika kma alivompa yule malaya wa yeriko??
Kwanza mkuu nianze kwa kukueleza kuwa ishu ya Yericko ni tofauti sana na hii japokuwa inahusiana pia. ni tofauti kwasababu Rahabu [kama sijakosea] alitoa msaada kwa wapelelezi wa Israeli na wakamuahidi watamuacha hai.Hapa kuna jambo kubwa sana mkuu kwasababu bloodline ya huyu mwanamke ndiyo hii tunayokuja kuipata kwa Yesu.Yaani uzao wa Rahabu ndio blood line ya Yesu. Hili niliache kwa sasa maana kuna mengi hapo,lakini pia unapaswa ukumbuke kuwa maelekezo ya Mungu ya kuwaangamiza Wakanaani ilikuwa ni wanaume wote na wanawake waliomjua mwanaume.Jambo hili linasababishwa na suala hili hili la Wanefili.Hili nalo lina mengi lakini ninachotaka ukione hapa ni kwamba kitendo cha Mungu kuruhusu Rahabu kuendelea kuishi bila kujali alikuwa ni kahaba na kitendo cha kuwa kahaba kina maana kuwa na uwezekano wa kuwa na watoto wenye damu hii ya Wanefili kinaleta maswali mengine magumu sana...

.....sasa basi,kunakuwa na sababu ya kahaba huyo kuachwa hai,je kuna sababu ipi ya Wanefili wa kabla ya gharika kuachwa? [Japokuwa sijasema hawakuachwa] Dhana ya huyu OG kumsaidia nuhu ni ya kufikirika zaidi kwasababu haina ushahidi wa kimaandiko kuwa alimsaidia Nuhu,ni mawazo ya watu tu. Kwa maoni yangu,kama walipona basi huenda ni kwa sababu ambayo huenda hatujaijuwa bado....

Kuhusu Tekinolojia ya wakati huo ni kwamba mimi binafsi ninaamini kuwa wakati ule kulikuwa na maendeleo ya kiteknolojia zaidi ya wakati huu.Ninasema hivi kwasababu nimepitia dicumentary nyingi tu zikielezea maendeleo ya hatari ya wakati huo.Kwa kukuonesha hili nenda katafute documentary moja inaitwa "Technology of the Fallen" utapata mwanga.Maendeleo haya yalitumiwa na binadamu wengine,sisemi kuwa Nuhu aliitumia isipokuwa nataka tu nianze kubadili mtazamo wako kuwa zamani hizo hawakuwa na maendeleo au maendeleo yao yalikuwa duni kuliko leo....

....Mungu kaka alivyo yeye ndiye baba wa teknolojia yote,malaika waasi waliona namna Mungu alivyokuwa anaweka kanuni zote za Physics na vitu vyote kwa ujumla wake na wakaweza kuwa na uelewa mkubwa sana wa kanuni hizo na zingine nyingi.Kumbuka tu ni malaika hao hao waliokuja kuleta maarifa haya kwa binadamu,maarifa ambayo kimsingi binadamu hakupaswa kuyafahamu,maarifa haya yanaitwa "forbiden knowledge".Binadamu hakupaswa kuyaelewa maarifa haya kwasababu hakuumbwa kuyahimili na ndiyo maana walipoyajuwa walianza kuangamizana wao kwa wao na hata leo unaona yanavyotutesa.Sasa kama hawa waliona tu na wakawa na ujuzi huo,vipi Mungu mwenyewe ambaye ndiye alikuwa msimamizi mkuu wa kujengwa safina hadi gharika yenyewe ambaye ndiye mwenye kanuni na ujuzi huo?

Ninachotaka ukielewe hapa ni kwamba,jambo lilalosimamiwa na Mungu mwenyewe weka pembeni yanayowezekana na yasiyowezekana kwa binadamu. Kwa hiyo dhana ya huyo OG "kumsaidia" Nuhu siioni kama ina mashiko kwasababu tu Nuhu "asingeweza" kuijenga mwenyewe....
3. Je Hawa wanefili waliishia wapi mkuu.... Kuna mmoja hapa katoa hoja kuwa damu yao bado ipo na kuna viongozi wakubwa wa dunia hii wana damu za kinefili je kuna ukweli hapa au conspirancy?? Na kma sio kweli je hawa wanefili waliishia wapi mbona leo hii hatuoni majitu ya size hiyo??

Ni hayo tu kwa sasa

Cc: Malcom Lumumba Kudo900
Hawa Wanefili hawajaisha mkuu,tena nasema hivi kwa uhakika kabisa...

Ni nini kinanipa uhakika mkubwa hivi?

Vipo vingi tu na cha kwanza ni Biblia yenyewe....

Mosi,Biblia yenyewe inakiri Wanefili walikuwepo hata baada ya gharika [mwanzo 6:6],kama walikuwepo baada ya gharika basi watakuwepo hadi leo maana sijaona sababu ya kutokuwepo kwao....

Pili,Yesu mwenyewe alisema "kama ilivyokuwa nyakati za Nuhu ndivyo itakavyokuwa wakati wa kuja kwake mwana wa Adamu" hii inamaana kuwa,moja ya alama za kurudi Yesu mara ya pili ni uwepo wa mambo kama ya nyakati za Nuhu na moja ya mambo ya wakati ule ni uwepo wa Wanefili...

Tatu,utafiti ambao umeshafanywa na watu wengi sana unaonesha kuwa Majitu haya yapo hadi leo hivyo sina sababu ya kupinga na nimeshaangalia video moja kutoka kwa mtu aliyeshuhudia kuona majitu haya kwenye D.A.M.Bs [Deep Underground Military Bases] zilizoko karibu dunia nzima chini ardhini na yanachapa kazi kabisa. Kilichoko huku juu ni mfano wa kilichoko huko chini.Majiji unayoyaona huku juu ni madogo sana kwa size ya majiji yaliyoko huko chini ardhini ma majiji yote yameunganishwa kwa barabara zilizojengwa kwa viwango vya hali ya juu kiteknolojia,ngoja niishie hapa kwenye hili...

Nadhani swali litakalofuatia hapa ni kuhusu sababu za majitu haya kufichwa au kujificha.Sababu namba moja iliyofanya haya ni udanganyifu....

Ni udanganyifu namna gani?

Kwanza kabisa baada ya gharika Shetani aliamua kutengeneza namna mpya ya kukabiliana na Mungu na njia hiyo ni udanganyifu. Udanganyifu wa kwanza kabisa ni kuhakikisha kile ambacho Mungu anawaeleza binadamu kionekane ni uwongo.Mojawapo wa mfano wa jambo hili ni suala hili la uwepo Mjitu haya.Shetani aliamua kuendesha harakati zake mafichoni huko na siyo wazi maana kama ikiwa siyo mafichoni watu wataona majitu haya na kuverify maelezo ya kwenye Biblia kuwa ni kweli yalikuwepo majitu na hili lina madhara makubwa sana kwao maana kuna mtaalam mmoja wa masuala ya Evolution alisema kuwa kama itaonekana ni kweli kulikuwepo Wanefili basi evolution inakufa kifo cha kibudu.Kuna aina nyingi sana za udanganyifu haswa kwenye historia ambako ndiko kwenye msingi mkubwa sana wa kuona Mungu anasema kweli namna ipi kwenye kwenye Biblia na maeneo mengine.

Hii ndio sababu moja na ndogo sana na zipo nyingi sana na nadhani hii inatosha kwa hapa....

Ni kweli kuwa viongozi wa dunia wengi ni bloodline isiyokuwa na asili ya binadamu,Moja ya damu inayosadikiwa haina asili ya binadamu inaitwa RH-Negative,nakupa kazi mkuu kafukue ufahamu mengi kuhusu group hili la damu....

Kuna namna ambayo unaweza kuwa na bloodline ya Wanefili na hutakuwa na umbo kubwa na hili linaratibiwa kwenye DNA yako na hiki ndicho alichokifanya shetani ili kuendelea kufanya kazi yake kwa kutumia kizazi chake.Kwa namna hii hata leo tuna "Wanefili" lakini hawaonekani kwa namna inayotarajiwa na wengi kuwa Mnefili ni mwenye umbo kubwa...

Hii siyo ajabu kwasababu ukiwafuatilia marais wa Marekani kwa mfano unaona kabisa ni bloodline moja na inakwenda kuungana na bloodline ya Royal Family kule UK.Brad Pit naye ni blood line hii,ukiangalia hakuzaa na Angelina Jolie kwa bahati mbaya maana naye pia ni bloodline hii hii...

Nadhani kuna mtu anaweza hoji juu ya Barack Obama na bloodline yake,ninachotaka kusema hapa ni kwamba kuna mengi ukiyajuwa kuhusu mtu huyo unaweza baki mdomo wazi...

Acha niishie hapo kwa leo mkuu....

Mungu akubariki sana..

Tuombe uzima tuendelee kupeana kiduchu kiduchu namna hii....
 
Umesoma nani anayeongea na wakati gani mkuu
Malaika walifungwa kuzimu nani kasema unajua maana ya agano jipya na la kale su imagino ri agano jipya su la kale ni vitabu vya biblia tu malaika mkuu shetani yuko kuzimu baada ya yesu kufufuka na wangine ndo unasikia wanataabisha watu kabla ya yesu shetani hakuwa kuzimu alikuwa duniani soma uelewebiblia na nyakati na majira ya biblia mkuu unapouliza swali kama hilo nazidi kuona ulivyo lalia vitabu vya miongozo yaani vilivyoongezwa tu
Zaidi ya kuchambua ndani ya Biblia mkuu hakuna malaika aliyekuwa kuzimu na kuzimu kulikuwa na wafu tu
Angalia mwazilishi wa vita na wanadamu alikuwa shetani mwenyewe ndo maana sodoma na gomora ilikuwa hatari mbona Leo Mungu ajawateketeza baadhi watu waovu kama sodoma ujue agano ni nini na linamaanisha nini su nifupishe
Hao malaika walitupwa Wapi baada ya kuasi katika agano la kale weka reference hapa
Au ujue kuwa walioperate mpaka yesu alipofufuka ndo kufungiwa tena aliyefungiwa ni shetani ambaye ni kiongozi wao na jamaa bado wapo ila uwezo wa kuingilia walimwengu umekua tofauti kwa sababu Baba lao lilitupwa kuzimu na limefungwa kwa kunyanganywa mamlaka so hautawaona wanefili tena kipindi hiki
Ufunuo 20:1-3
1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.

2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;

3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.




Hapa Shetani alifungwa kuzimu na hii ni baada ya kufufuka Yesu.....

Dhana na kuwa malaika wamefungwa kwa maana physical huwa ina matatizo mengi sana.Ukiangalia kinachoendeleaduniani leo ni ngumu sana kuona kuwa ni kweli kafungwa kwa namna mnayoisema ninyi....

Ninaamini maandiko yalikuwa yanamaanisha kitu kingine kabisa yaliposema "wamefungwa"...
 
Mkuu ili kujifunza lazima upanue ufahamu kwa kutafiti huko na huko hakuna story inayoweza kuwa kamili kwa kutumia chanzo kimoja tu kuna visa biblia haiviongelei hivyo ni lazima uvikute nje ya biblia ili story iweze kuwa moja

Sielewi kwanni tunapenda kuamini kitabu kimoja ndio sawa kuliko kingine hyo ya safina kutokwenda mbali na ilipoondokea ipo kwenye vitabu vya waisraeli wenyewe hata ya kunyanyua mlima ipo kwenye vitabu vya kiyahudi ambavyo wanatumia kusalishana kila siku ssa iweje mtanzania ukatae kitu ambacho waisrael wenyewe wanakubali? Kwanni tunalazimisha kuwa chochote kisicho kwenye biblia ni uongo

Embu tupende kujifunza kitu kipya tusiingize mahaba ya dini kwenye kila kitu
Kwangu mimi hao wanaoitwa Wayahudi siyo Wayahudi watoto wa Yakobo....
 
Aiseeee.... Mkuu Eiyer indeed wewe ni true great thinker maana umenipa material zaidi ya niliohitaji na nimegundua sifahamu hata 2% ya mambo ya sirini ya dunia hii ila umenipa mwanga nitatafiti hayo ulionitonya ili niongeze maarifa na kupata majibu ya maswali ninayojiuliza.

Once again nashkuru kwa kuja kutupa darasa murua kabisa ila usiende mbali sana kuna mada nyingine nimeipandisha ila mods hawajaiachia na nategemea utakuja kutupa darasa tena

Kudos!
 
Hakuna ukweli wowote hapa na hizo nadharia zako pitia maandiko matakatifu then njoo tena
Nilipitia ndio uwezo wangu ukaishia hapo ndio maana nikafungua thread so nategemea wasomaji kma ww ndio mtusaidie kupata majibu so karibu utuambie ukweli ni upi

Ahsante
 
Aiseeee.... Mkuu Eiyer indeed wewe ni true great thinker maana umenipa material zaidi ya niliohitaji na nimegundua sifahamu hata 2% ya mambo ya sirini ya dunia hii ila umenipa mwanga nitatafiti hayo ulionitonya ili niongeze maarifa na kupata majibu ya maswali ninayojiuliza.

Once again nashkuru kwa kuja kutupa darasa murua kabisa ila usiende mbali sana kuna mada nyingine nimeipandisha ila mods hawajaiachia na nategemea utakuja kutupa darasa tena

Kudos!
Tuko pamojakiongozi...

Tunachojuwa ni kama punje moja ya mchanga wa bahari,ni kama hatujuwi kabisa...

Tuendelee kuombeana uzima tuendelee kujuzana kadiri ya tunavyowezeshwa na Mungu wetu...

Barikiwa sana mkuu...
 
Chief umeelekezwa vizuri sana tena Sana na watu wengi sana wamekoment hapa na ushahidi wao wenye kuleta kujifunza mapya na tusioyajua,ni aibu kutunisha misuli kwa Simba alieshiba ikiwa wewe una njaa ya kiu na chakula.

Inaonesha huna ukijuacho kabisa na hujahangaika kusoma maoni ya watu au ya Zitto junior mwenyewe kuanzia mwanzo lakini pia hajasema tufuate alichosema ila ametaka tujifunze wote na tumfunze pia asioyajua kuhusu Ogu.

Ogu kaongelewa vitabu vingi sana tena sana na ninashangaa wewe unaejua biblia umeshindwa walau kujua maajabu yalioongelewa ya mfalme Ogu.

Ogu ametajwa hata kwenye vitabu visivyo vya kidini na umbo lake kubwa,lakini ni jamii za wanefili zilizokuwa na watu kama yeye na wengineo ambao hawakupata kuwa Maarufu enzi hizo.

Acha kuleta mbwembwe za kunya juu ya chupa ikiwa hujui kimo na upana wa mdomo wa chupa.

Huna unalolijua Chief japo sikujui vyema ila kwa maandiko tu yawezekana nyie ndo wale mnaotembea na kalamu siku ya ibada kisha mnachora mistari kwenye Bible baada ya kusomewa vifungu na wachungaji afu unatoka kifua mbele bila kuelewa mistari hiyo na maana zake.

Kasome ulipoelekezwa na Zitto unaeza kuja na jipya na sisi tukajifunza kuliko kukomenti kwa mihemko utadhani wote uliotukuta tunajadili hii mada hatujui tunachojadili au kama unavyosema biblia

Kasome
Rudi kwenye siasa,maana siasa ndo huhitaji kurembesha unachoongea,biblia haina kutembesha wala kukoleza,ni black inatamkwa black white inatamkwa white,hakuna sehemu ya biblia inayotamka hayo aliyoyamka na unayolazimisha wewe kuwa huyo mtu aliyafanya,narudia aliyafanya siyo kutajwa kwake jina,nnachoamini binafsi ni simulizi za biblia na siyo simulizi za mtaani,na nnaongelea kile nnachokisoma,km unajua na siyo kukarilishwa,nipe mstari ama sura ama ukurasa unaoongelea hayo juu ya mtu hyu,
Mngeongelea kadri ya hadithi zenu za vijiweni na siyo kuamunisha watu kuwa matendo yote mlomjazia jamaa yamenenwa ktk biblia,
Usiumie na mm kusema haya,
Acha blah blaha,
 
Mkuu ili kujifunza lazima upanue ufahamu kwa kutafiti huko na huko hakuna story inayoweza kuwa kamili kwa kutumia chanzo kimoja tu kuna visa biblia haiviongelei hivyo ni lazima uvikute nje ya biblia ili story iweze kuwa moja

Sielewi kwanni tunapenda kuamini kitabu kimoja ndio sawa kuliko kingine hyo ya safina kutokwenda mbali na ilipoondokea ipo kwenye vitabu vya waisraeli wenyewe hata ya kunyanyua mlima ipo kwenye vitabu vya kiyahudi ambavyo wanatumia kusalishana kila siku ssa iweje mtanzania ukatae kitu ambacho waisrael wenyewe wanakubali? Kwanni tunalazimisha kuwa chochote kisicho kwenye biblia ni uongo

Embu tupende kujifunza kitu kipya tusiingize mahaba ya dini kwenye kila kitu
Tatizo lako unataka kulazimisha mambo na uelewa wako ukawa sahihi,
Nnachokataa Mimi ni kuisingizia biblia,
Unapoongea jambo bainisha kipi kimesemwa na biblia na kipi hakijasemwa ila umekipata kwingine,
Rudia kusoma mafungu aliyotoa,halafu wianisha na matendo yaliyohadithiwa kwa kukolezwa juu ya mtu huyu,
Narudia kuongea hadithi kwa mujibu wa biblia juu ya mtu huyu hazipo hivyo,kwa hiyo tunapo ongelea jambo tubainishe kuwa hili ni la chanzo cha biblia na hii ni la vyanzo vingine km hadithi za mtaani ama kwenye kahawa ama vitabu vingine,usisingizie vyanzo ili kutaka kuaminika,
 
Shida yako mkuu unapinga tu bila kusoma!! Sasa sijui unataka kubishana na nabii amos

Amos 2:9
9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini.


Mierezi kwa kiingereza ni CEDAR tree haya tusome kidogo kuhusu ukubwa wa mti huu

View attachment 764058
Cedar trees are large, evergreen trees of the family Cupressaceae. Cedar trees will usually grow to a height of up to FIFTY FEET, but others can reach one hundred or more feet in height.

Pia tunaambiwa na BIBLIA kuwa alikuwa na nguvu kma mierezi ambayo ilikuwa pia ni miti migumu zaidi huko mashariki ya kati na mbao ngumu kabisa na ndio maana hta waandishi wa biblia wanauzungumzia sana kwenye mifano yao

Zaburi 92:12
,
"Wenye haki watastawi kama mtende]], watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni".

Sasa kama biblia inamuelezea mtu huyu kwa staili hii iweje wwe upinge kma ana uwezo wa kuwa mrefu kuliko mlima ama anauwezo wa kunyanyua mlima ama nguvu za kubeba mlima hata kma sio wote unapinga kwa minajili ipi??? Mbona biblia inaprove kuwa alikuwa na nguvu za ajabu??
Nianze na fungu ulilotoa,
Nioneshe wapi amosi kasema jamaa alitaka kuinua mlima,
Lkn nikusihi usisome biblia kimbumbumbu,usisome biblia km style anayotumia bata kula,
Usimeze vizima vizima,cheua,
Biblia inapofananisha mtu na kiumbe kingine haiwianishi kwa vigezo unavyodhania ww,biblia hutamka sifa hizo km mifano ya sifa ktk kuwafahamisha watu juu ya jambo siyo uwiano wa jambo km lilivyotajwa,(vivumishi)
Mf.biblia ilipomuita Petro mwamba unataka kusema ilimaanisha petro kaumbwa kwa lava km mwamba?,ama mwili wake unaugumu na tabia na hali sawa na mwamba? Kiasi ambacho hata uzito na uimara wa mwili wa petro ulifanana na mwamba?
Jiulize hili na utafakari,
Mf.mwingine ni km biblia ilipotaja 666,haikumaanisha namba zenye umbile huo tajwa,lilikuwa ni neno la kumteta ama kumzungumzia adui yao kimafumbo japo mbumbumbu wa biblia wanalimeza na kulitafsiri zimazima wanapotoka,
Biblia imewafananisha watu na tabia za vitu vingi sana,
Mf.mwingine,Yesu anaitwa mwanakondoo,inamaana anamanyoya km kondoo,alikuwa na kimo umbile na nguvu km kondoo?
Yesu anaitwa pia simba wa yuda inamaana alikuwa physically km simba?
Ili ujue kilichowianishwa kwa huyo mtu siyo kimo sahihi cha mti ila ni muonekano wake awapo ktk kundi la watu nijuze km miti yooote ya aina tajwa ina height sawa na uliyosema,
Acheni blah blah
Na msichukie kuambiwamnaongea na kutafsiri kipotofu,
Wapo watu walifananishwa na tai si kwamba wanaruka km tai,
 
Rudi kwenye siasa,maana siasa ndo huhitaji kurembesha unachoongea,biblia haina kutembesha wala kukoleza,ni black inatamkwa black white inatamkwa white,hakuna sehemu ya biblia inayotamka hayo aliyoyamka na unayolazimisha wewe kuwa huyo mtu aliyafanya,narudia aliyafanya siyo kutajwa kwake jina,nnachoamini binafsi ni simulizi za biblia na siyo simulizi za mtaani,na nnaongelea kile nnachokisoma,km unajua na siyo kukarilishwa,nipe mstari ama sura ama ukurasa unaoongelea hayo juu ya mtu hyu,
Mngeongelea kadri ya hadithi zenu za vijiweni na siyo kuamunisha watu kuwa matendo yote mlomjazia jamaa yamenenwa ktk biblia,
Usiumie na mm kusema haya,
Acha blah blaha,


Kuwa mpole Chief huko tushatoka tangu Jana na kuendeleza mjadala uliofungwa ni kujirudisha utoto

Tuache utoto tungojee thread nyingine iliozuiliwa na Mods

Watu kama nyinyi hata darasani walikuwepo,hawakupenda kushea mambo wanayoyajua na wengine na hata kama hawajui hawakutaka kuonekana hawajui

Chief maandiko yoote na vifungu watu wameweka kweli wewe hujaona hata kimoja? Chenye kukupa uchangamsho wa fikira! Japo ili angalau uje hapa utufunze na sisi wenye simulizi za vijiweni ?

Chief umeshindwa kuja kutuelimisha na mandiko ya biblia kuhusu upotoshaji wa simulizi zetu za vijiweni kweli?

Hebu jipange hata kwa nusu saa tu pengine waeza rudi na nondo nzuri zaidi ukatushawishi kuanza upya mjadala
 
mkuu unatufikirisha vizuri lakini neno "kama" mbona ni ufananisho sidhani ni uhalisia.

Mfano:
Tulikiwa machoni pao kama nzige.???
Shetani ni kama simba aungurumaye?
Yesu kama mwanakondoo asubiriye kuchinjwa??
Zaburi 1:3 naye atakuwa kama mti uliopandwa kati ya maji.

Isaya 40:31 wamngojea bwana watapaa juu kama mbawa za tai.

mkuu binafsi bibilia naipa Highest authorty kuliko vitabu vingine, lkn pia nakubali kujifunza kutoka katika vitabu vingine lakini sio kama vyenye msawazo sawa na bibilia. naamini maneno ya agano la kale aloyotumia yesu ndiyo tunayotumia sisi kujenga hoja licha ya uwepo wa mavitabu mengi enzi hivyo ambavyo havikuwa endorsed na mwokozi.


bibilia imejaa ufananisho wa watu na viumbe vya asili katika mantiki mbalimbali, tunajifunza kwa urahisi lwa kuangalia viumbe asili zaidi ya masomo dhaania.

maoni na mtazamo juunya comment yako mkuu.
Definetly
Wasoma vijarida vya sani wamegeuka wataalamu wa maneno yaMungu,
 
Mkuu wanaposema KAMA ni kweli haimaanishi ndio uhalisia ila ni ULINGANISHO kuwa kitu kitakuwa kwa mithili hiyo huwezi ukaniambia mtu akimuelezea magufuli atasema MREFU KAMA MNAZI haiwezekani sababu hata haikaribii nusu ya ukweli ila kwa mtu kama Hasheem thabeet kidogo inaweza onekana kuna kamfananisho kwa mbali

Hivyo hapa muandishi hata kma hamaanishi kuwa ogu alikuwa mrefu kama huo mti ila anajaribu kutuonyesha kuwa alikuwa MREFU SANA na MWENYE NGUVU SANA bila kujalisha ni kama hiyo miti au mbao ila ndio alichotaka tuelewe hivyo kwa mstari huu mtu akisoma atajua jamaa alikuwa na NGUVU SANA bila kujalisha kuwa alifikia hiyo mierezi na mialoni.

Na ndio maana hata mwandishi wa zaburi anatoa mfano kuwa wenye haki Watastawi na kuwa kama MIEREZI ya lebanon.... Akimaanisha watakuwa IMARA bila kujalisha utafikia uimara wa huo mti au lah.

Che mittoga SALA NA KAZI Malcom Lumumba
Ulichoongea saa hizi ni tofauti na ulichoongea awali hadi ukatuletea actual height ya huo mti ili tu kutulinganishia urefu,
Nadhani umegundua kuwa ulipotoka ktk ufahamu wako wa jambo hili na umeshindwa kukiri ulipotoka sasa unaamua kujitutumua kuwa ulimaanisha hili,
Kili ulipotoka
NB.hatupingi kuwa hakuwepo
Hatupingi kuwa hakuwa na nguvu zaidi ya binadamu wa kawaida
Hatupingi kuwa hakuwa na kimo zaidi ya binadamu wa kawaida,
Tunapinga chumvi za mtaani,
Tunapinga ulinganishaji wa kimbumbumbu
 
Kuwa mpole Chief huko tushatoka tangu Jana na kuendeleza mjadala uliofungwa ni kujirudisha utoto

Tuache utoto tungojee thread nyingine iliozuiliwa na Mods

Watu kama nyinyi hata darasani walikuwepo,hawakupenda kushea mambo wanayoyajua na wengine na hata kama hawajui hawakutaka kuonekana hawajui

Chief maandiko yoote na vifungu watu wameweka kweli wewe hujaona hata kimoja? Chenye kukupa uchangamsho wa fikira! Japo ili angalau uje hapa utufunze na sisi wenye simulizi za vijiweni ?

Chief umeshindwa kuja kutuelimisha na mandiko ya biblia kuhusu upotoshaji wa simulizi zetu za vijiweni kweli?

Hebu jipange hata kwa nusu saa tu pengine waeza rudi na nondo nzuri zaidi ukatushawishi kuanza upya mjadala
Unaposema utoto unajitambulisha ulivyo km kipofu aliyepata nafasi ya kuona na akaona punda hivyo kila kitu ukimuambia anawianisha na punda,
Unataka kunambia huwa ktk mijadala hakuna nyongeza,
Huwa hakuna kujibu ulichoulizwa Jana,
Walioongea wameingelea ufahamu wao,Na mm niliyenukuliwa napaswa kujibu ufahamu wangu maana mm ndo nilinukuliwa,
Tabia yako ya kushinda humu sababu ya kukosa majukumu mengine siyo kipimo cha usahihi wa namna tunavyopaswa kuenenda ktk mijadala ya humu,
Muda ww unapokuwa humu fulltime mm nakuwa nakuandalieni ada na mengineyo,
 
Mkuu utawezaje kujua kama Padre Titus Amigu ndo Zitto Junior ama ndo Mitale na Midimu?
Duuh hapo sasa ila yatupasa kuwa tunawatafuta hawa watu physically kwa majina yao halisi kuliko haya ya bandia
 
Unaposema utoto unajitambulisha ulivyo km kipofu aliyepata nafasi ya kuona na akaona punda hivyo kila kitu ukimuambia anawianisha na punda,
Unataka kunambia huwa ktk mijadala hakuna nyongeza,
Huwa hakuna kujibu ulichoulizwa Jana,
Walioongea wameingelea ufahamu wao,Na mm niliyenukuliwa napaswa kujibu ufahamu wangu maana mm ndo nilinukuliwa,
Tabia yako ya kushinda humu sababu ya kukosa majukumu mengine siyo kipimo cha usahihi wa namna tunavyopaswa kuenenda ktk mijadala ya humu,
Muda ww unapokuwa humu fulltime mm nakuwa nakuandalieni ada na mengineyo,

Ahsante Chief mungu awe nawe kwa kila jambo utendalo na akusamehe makosa yako maana hujui utendalo

Enenda katika imani ya bwana na yafanye matendo yako yawe nguzo njema ya maisha yako bila kumchukiza muumba wako

Bwana awe nawe na ninamwomba mungu amfanye ndugu yangu Da'vinsi asipite huku maana shetani anaweza kuijaribu imani yake.
 
Back
Top Bottom