Kwa mfano tunauza karanga sote najua nafanyaje ili nichukue wateja wako kwa mfano karanga wewe unakaanga Tu hautoi Ganda la juu Mimi natoa Ganda la juu hapo naiba wateja kirahisi au unakaanga na Mimi nakaanga basi naongeza za kuchemsha mbinu kutoa barabarani na mwanzo nakubali nipate hasara ili utoke barabarani ili niteke sokoUlishawahi kufanya biashara zinazofanana zimepangana Ata frame tano mtiti wake ulivyo
Tusichanganye kati ya biashara na faida,,faida ni baada yakufanya biashara,mchakato ni biashara,unaifanyaje?hadi kufikia kupata faida?ndo ngoma iko hapo.Tuseme Nina guest house alafu nikwambie Nina vyumba 20 naingiza laki nne kwa siku Sasa hapo mshindani wangu atanipiku kivipi
Kwani kutaja mapato ndio kutoa code?Tuseme Nina guest house alafu nikwambie Nina vyumba 20 naingiza laki nne kwa siku Sasa hapo mshindani wangu atanipiku kivipi
Mkuu upo mwanza nipo Tanga nipe code za biznes namimi nikimbize hukuHata mimi mwenyewe siwezi mpa mtu siri za faida zangu
Kuna mwamba yupo gavo kuna michezo alikua anaichezesha kujipatia pesa hapo ndio nikagundua kwenye maisha siri haikosekani jamaa anaiibia gavo ila kwa siri sana na cha ajabu hajawahi kushtukiwa yupo tangu enzi za nkapa anaiibia serikali na hawamshtukii anaiba kwa siri sana kumshtukia ni ngumu sanaHakuna atakaekupa code zote na njia anazopita hiyo sahau. So wale tunaofuatana DM kuulizana mjifunze hapa, pesa ina Siri na biashara ni Siri ya anayeifanya. Hivo msihangaike wewe andaa mfumo wako nawe utembee mbele kwa mbele hivo ndivo ilivo.
Ukweli kabisaHata mimi mwenyewe siwezi mpa mtu siri za faida zangu
Hua ni mwiko kuuza code , code ndio uhai wa biashara yako ni sawa na umevaa uamue kuvua nguo mchana mbele za watuKwani kutaja mapato ndio kutoa code?
Au unadhani CocaCola na PepsiCo huwa hawatangazi mapato na matumizi yao kila mwaka. Na wakati huo formula ya syrup na concentrate hawatoi.
Kutaja mapato ni kujiropokea tu. Alafu hiyo kiasi ni ghafi, faida yake baada ya gharama ni ipi. Na mchakato wa kupata faida na kuendesha ni upi.
Usipokuwa makini utakurupuka umuulize muuzaji maarufu wa bangi mtaani kwako, akwambie mauzo ya debe labda ni 800,000 alafu ukurupuke kuagiza madebe nawewe. Kumbe yeye kwenye hiyo laki 8 kuna mgawo wa afisa wa polisi wa mtaa na mwenyekiti, na vilevile huyo jamaa ana ndugu yake fisadi la CCM Halmashauri au kaka yake idara ya polisi huo mkoa analindwa. Wewe unakurupuka na madebe yako unaenda jela unahonga mtaji mzima.
Unarudi unajiuliza wanafanyaje, sasa unataka akwambie ana kaka yake afisa wa polisi makao makuu ya mkoa, anawapa mgawo viongozi wa mtaa na anahonga polisi ili kuwatuliza? Ukitoka hapo si unamtangaza?
Codes ni hizi mkuu tafuta heka moja ya ardhi ulime tikiti maji na kuanzisha ufugaji wa kware na mayai yake niamini baada ya miezi mi3 utakuja kunishukuru.Kabisa mkuu hii platform hatujuani wala nini mpe mtu maujuzi akafie mbele uko
Sema nini ni uchoyo tu
Hii imekaa kiujumla zaidi bado inahitaji kufunguliwa zaidiCodes ni hizi mkuu tafuta heka moja ya ardhi ulime tikiti maji na kuanzisha ufugaji wa kware na mayai yake niamini baada ya miezi mi3 utakuja kunishukuru.
vp na wewe ukampa code mdogo wako aliyeko mwanza niliko mimi?Sasa unaongezaje mpinzani haliyakuwa anaekuuliza yupo mwanza wewe upo dar hususani humu mitandaoni
Mwanza kubwa mkuu hawezi kuwa ulipo wewevp na wewe ukampa code mdogo wako aliyeko mwanza niliko mimi?
Biashara ni code hata Elon hawezi kutoa code zake kirahisi hii ni dunia nzimaHuku mikoani tunaumoja wetu wa biashara inayofanana niliingia umoja huo kwa kuhisi may be tutapeana uzoefu wapi wenzetu wanatoa mzigo ambao kidogo bei imepoa ajabu ni kwamba siawahi ona mtu kapost tuungane wafanybiashara walau watano tuagize mzigo kwa pamoja ... wanahofia ushindani nikaamin kweli wafanybiashar hawatoi code bwana..