DOKEZO Mfanyabiashara wa Magari, Gideon Mlokozi Mashankara amepotea

DOKEZO Mfanyabiashara wa Magari, Gideon Mlokozi Mashankara amepotea

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Yaani buu utawala umejaa ushetani mkubwa. Mbona inakuwa ni zaidi hata ya utawala wa awamu ya 5?
Asitekwe Lissu, Mbowe,Mwambukusi au Mdude Nyagali atekwe mtu ambaye hata nyumbani kwake hana ushawishi? kuweni seriuous eti kwa sababu ameandikwa mwanaharakati basi mnaona serikali imemteka!

Wafanyabiashara wa magari wengine baadhi yao ni matapeli,wanajihusisha na wizi wa magari na dhuruma. Hilo ndio lingeangaliwa kwanza. Alimdhuruma/alimtapeli nani?
 
Sisi wananchi ni wajinga.Tumesema siku zote mkiona magari hayana namba na wanataka kumchukua mtu pigeni filimbi watu waje ili walizingile hilo gari na kulichoma moto pamoja na waliomo vinginevyo hiyo biashara ya kuteka watu itaendelea
Tatizo hayo maelekezo yapo mitandaoni na hayatolewi na jeshi la polisi wala mamlaka za serikali napo ndipo mamlaka za serikali zinapo husishwa na madhila haya wanayo yapitia watanzania sasa
 
Anaitwa GIDEON MLOKOZI MASHANKARA ana umri wa miaka 30,mkazi wa Tabata Segerea,

Kazi yake ni mfanyabiashara wa kuuza magari lakini pia ni mwanaharakati huru wa mitandaoni,hajulikani alipo siku ya saba leo baada ya kutekwa na kupotezwa.

Alitekwa na watu waliojitambulisha kuwa ni askari wa jeshi la Polisi siku ya Ijumaa ya tarehe 02 August 2024 majira ya Saa 2 :00 usiku.

Akiwa katika ofisi ya magari ya rafiki yake inayojulikana kama RAPHAEL STAR iliyopo maeneo ya Segerea Stand.

Watu hao waliojitambulisha kama askari wa Jeshi la polisi walikuwa watano,walivamia ofisi hiyo wakiwa wamevalia kiraia na kumuweka Chini ya ulinzi.

Ndipo alipowahoji waoneshe vitambulisho lakini wakakaidi na kudai wanampeleka kituo cha polisi Tabata,atajua huko huko.

Walitumia nguvu na kumfunga pingu kisha wakamuingiza kwenye gari walilokuja nalo aina ya Landcruiser hardtop, ikiwa haina namba

Lakini mashuhuda waliokuwa nje ya ofisi wanasema,gari hilo halikuwa na namba kwa nyuma ila kwa mbele liliandikwa "STL" tu.

Gari hilo halikuelekea Kituo cha polisi Tabata kama walivosema bali lilielekea njia ya kwenda kinyerezi.

Familia ilianza juhudi za kumtafuta vituo vyote vya Polisi Jijini Dar es saalam bila mafanikio

Tulianza kituo cha polisi Tabata, tukaambiwa hayupo na hawana taarifa zake,Tukaenda kituo cha polisi cha Staki Shari,Kinyerezi na Buguruni pia hawakuwa na taarifa zake

Kesho yake asubuhi tuliendelea na vituo vingine tulianzia Central, Oysterbay na vituo vyote bila Mafanikio

Tumezunguka Hospitali zote jijini Dar es saalam na vyumba vya kuhifadhia maiti "Mortuary" bila Mafanikio.

Tulifungua taarifa kituo cha Polisi cha Staki Shari na kupewa RB namba STK/RB/6642/024

Baada ya siku ya tano bila Mafanikio tumeenda Central polisi kufungua jalada la Uchunguz,tumeambiwa upelelezi unaendelea.

Kwa niaba ya Familia tunaomba mtu yoyote mwenye taarifa kuhusu ndugu yetu awasiliane na Baba yake GIDEON kwa namba 0786878133 au kwa namba ya rafiki yake ambayo ni 0624497811

Asante sana.
Mh ! 🤔🤔🤔
 
Wabongo wangi ni wajinga tu yaani wanakuja watu from no where wanamchukua mshaji wako kibabe na ww upo tu unaangalia?
Musipokua na umoja mtapotezwa kama kuku endeleni na ujinga wenu.
Ukiaacha tu kuaangalia
Ukisema umpambanie basi uende na plastic bag ya kuwekea ubongo wako
Tanzania my motherland nakulilia
 
Watanzania TUANZE KUJILINDA.

Hayawani vichwa vimepata moto. Ogopa sana mwanamke akishaonja damu ya mtu

Mlinipuuza niliposema tukaipinge sheria inayowapa kinga TISS wanapoamua kuua

Kumbukeni Dotto Magari ni chawa kiherehere hivyo kumuuza mtu adakwe ni chap kwa haraka
=Survival of my fittest.

-Survival for the fittest.
 
Back
Top Bottom