Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mtu mwenye akili timamu anaelewa vizuri tu kama taarifa amecopy kutoka kwa ndugu na ameisambaza hapa.Hii habari ni ya siku nyingi kidogo mwanzo wa mwezi hivyo edit habari ili kutoa mkanganyiko "amepotea leo siku ya 7".
Weka na picha pia mkuu isaidie watu kumtambua.
Uko sahihi Profesa ,inawezekana sina akili.Mtu mwenye akili timamu anaelewa vizuri tu kama taarifa amecopy kutoka kwa ndugu na ameisambaza hapa.
Ukipata mkanganyiko ndio ujijuwe huna akili.
Wewe umeelewa ni ya siku nyingi, nasema ambaye hatoelewa ndio ajijuwe akili hana.Uko sahihi Profesa ,inawezekana sina akili.
Yaani huwa ninajiuliza hilo swali. Watu huwa wanatuma clip za matukio yasiyo na tija hili hamna hata picha?Hivi ni kwanini mtu anapochukuliwa na watu msiowajua msifuatilie hilo gari mpk mwisho mjue anapelekwa kituo gani iwe rahisi kufuatilia?
Sasa kila mtu akimiliki silaha si itakuwa ni suicide missions tu kila uchao. Maana ishu inakuwa sio kutekwa tena ni kupigwa njugu na wasiojulikana unaachwa ufie hapo hapo getini kwako.Ili kukabiliana na huu utekaji wa kikosi kazi ambacho kipo chang'ombe Kwa mujibu wa hotuba ya mh mbowe,serikali inatakiwa ilegeze masharti ya umiliki wa siraha kama ilivyo marekani ili tuwashughulikie Hawa wahuni wanaojifanya hawajulikani wakati wanajulikana na niwajingawajinga ambao uwezo wao wa kuchanganua mambo ni sifuri.
"Mtanikumbuka si kwa mabaya bali kwa mema 😂"Yaani buu utawala umejaa ushetani mkubwa. Mbona inakuwa ni zaidi hata ya utawala wa awamu ya 5?
Unapambana kumtetea mwana wanakukariri, kesho wanakujia wewe unaisha😂Tatizo hayo maelekezo yapo mitandaoni na hayatolewi na jeshi la polisi wala mamlaka za serikali napo ndipo mamlaka za serikali zinapo husishwa na madhila haya wanayo yapitia watanzania sasa
Hili nalo ni shida imgine hadi leo ndio taairifa zinasambaa wakati ilitakiwa usiku huo huo ziwe viral.Upole una faida na hasara zake. Mfano hapo hata kama si polisi hakuna raia waliohoji mnaangalia tu mwenzenu akipotea.
Magufuli pamoja na ukatili wake hakuwahi kuwakati watu laki 1 maji,umeme,afya na elimu wala kufuta vijiji vyao na kuwakosesha kupiga kura. Nadhani atavunja rekodi ya dunia."Mtanikumbuka si kwa mabaya bali kwa mema 😂"
Nimekuelewa mkuu✊✊Wewe umeelewa ni ya siku nyingi, nasema ambaye hatoelewa ndio ajijuwe akili hana.
Mema yaapi yeye ndiye ameridmthisha haya."Mtanikumbuka si kwa mabaya bali kwa mema 😂"
Kwenye sekta ya utekaji kuna awamu itazidi ya Magu?"Mtanikumbuka si kwa mabaya bali kwa mema 😂"
Nadhani tuwe na sheria ya kumiliki silaha ya lazima kwa kila raia. Sababu ni kuwa inawezekana kuna organized crimes ambapo kuna mafia group watu wakidhulumiana basi kinatumwa kikundi kumteka mtuAnaitwa GIDEON MLOKOZI MASHANKARA ana umri wa miaka 30,mkazi wa Tabata Segerea,
Kazi yake ni mfanyabiashara wa kuuza magari lakini pia ni mwanaharakati huru wa mitandaoni,hajulikani alipo siku ya saba leo baada ya kutekwa na kupotezwa.
Alitekwa na watu waliojitambulisha kuwa ni askari wa jeshi la Polisi siku ya Ijumaa ya tarehe 02 August 2024 majira ya Saa 2 :00 usiku.
Akiwa katika ofisi ya magari ya rafiki yake inayojulikana kama RAPHAEL STAR iliyopo maeneo ya Segerea Stand.
Watu hao waliojitambulisha kama askari wa Jeshi la polisi walikuwa watano,walivamia ofisi hiyo wakiwa wamevalia kiraia na kumuweka Chini ya ulinzi.
Ndipo alipowahoji waoneshe vitambulisho lakini wakakaidi na kudai wanampeleka kituo cha polisi Tabata,atajua huko huko.
Walitumia nguvu na kumfunga pingu kisha wakamuingiza kwenye gari walilokuja nalo aina ya Landcruiser hardtop, ikiwa haina namba
Lakini mashuhuda waliokuwa nje ya ofisi wanasema,gari hilo halikuwa na namba kwa nyuma ila kwa mbele liliandikwa "STL" tu.
Gari hilo halikuelekea Kituo cha polisi Tabata kama walivosema bali lilielekea njia ya kwenda kinyerezi.
Familia ilianza juhudi za kumtafuta vituo vyote vya Polisi Jijini Dar es saalam bila mafanikio
Tulianza kituo cha polisi Tabata, tukaambiwa hayupo na hawana taarifa zake,Tukaenda kituo cha polisi cha Staki Shari,Kinyerezi na Buguruni pia hawakuwa na taarifa zake
Kesho yake asubuhi tuliendelea na vituo vingine tulianzia Central, Oysterbay na vituo vyote bila Mafanikio
Tumezunguka Hospitali zote jijini Dar es saalam na vyumba vya kuhifadhia maiti "Mortuary" bila Mafanikio.
Tulifungua taarifa kituo cha Polisi cha Staki Shari na kupewa RB namba STK/RB/6642/024
Baada ya siku ya tano bila Mafanikio tumeenda Central polisi kufungua jalada la Uchunguz,tumeambiwa upelelezi unaendelea.
Kwa niaba ya Familia tunaomba mtu yoyote mwenye taarifa kuhusu ndugu yetu awasiliane na Baba yake GIDEON kwa namba 0786878133 au kwa namba ya rafiki yake ambayo ni 0624497811
Asante sana.
Ni kweli nakumbuka kwa mbali hii Taarifa ni ya siku nyingi.Mtu mwenye akili timamu anaelewa vizuri tu kama taarifa amecopy kutoka kwa ndugu na ameisambaza hapa.
Ukipata mkanganyiko ndio ujijuwe huna akili.
Tofauti ni moja huu wa sasa wahusika wameshatambulika ila bado serikali imetia pamba.Kwenye sekta ya utekaji kuna awamu itazidi ya Magu?