Mfanyakazi/Mwajiriwa sasa kupewa TIN Number ili kutambulika kama mlipa kodi kupitia PAYE

Mfanyakazi/Mwajiriwa sasa kupewa TIN Number ili kutambulika kama mlipa kodi kupitia PAYE

Kuna taarifa inasambazwa kwa video clip na magazetini ikiwa imetolewa na TRA kuwataka waajiliwa wote kuwa na TIN. Ni taarifa ambayo naona kama inatokana na uongozi wa TRA wenye mapungufu ya hekima. Kwanza imeletwa ikiwa na kikomo (ultimatum) wakiamini wanayo nguvu hiyo ya kuwapa ultimatum waajiliwa wote. Pili imetolewa utadhani ni jambo la dharula. Tatu imetolewa kwa lugha ya hovyo, isiyo na uungwana pamoja na tishio la kuzuia mshahara wa mwajiliwa.

Naomba TRA wasijitwishe madaraka yasiyo yao. Mwajiliwa yeyote hajawahi kuwa na mkataba wa aina hiyo na TRA. Kama TRA wanaleta utaratibu mpya, wanatakiwa wawe waungwana (reasonable). Walete taarifa ya kiungwana na siyo kutishia wakati hakuna mwenye makosa. Labda wanaiga lugha za viongozi wanaomiliki vyombo vya dola. TRA hana nguvu ya aina hiyo na ni makosa kutishia watu wasio na mkataba wa aina hiyo.
Hao ndio watoza ushuru. Wanakubambikia kodi...wanakuja kudai cha kwao...halafu baadae wanasema tumekusaidia. Rushwa iliyoko ndani ya hii nchi itaisha lini? Tunataka haki. Haki itamalaki ili Taifa liweze kwenda mbele na kufanikiwa
 
Mkuu unahitaji elimu, suala la TRA kutaka kila mwajiriwa awe na Tin ni jambo la busara sana. Kumekuwa na ukwepaji wa kodi mkubwa sana utakuta kampuni inawajiri hta 100 alafu paye wanasema wana waajiri 50. Huenda hata wewe hapo ulikuwa unakatwa paye kwenye msahara lakn haifiki serikalini muhasibu au mwajir anafaidi anakula.

Huu mfumo mpya ni mzuri kabisa kwasababu mfanyakazi nae analipa kodi ukiachana na mfanyabiashara tena kuna wafanyakazi wanalipa kodi kubwa kushinda hata hao wafanyabishara.

TRA ni chombo cha serikali hivo kinapokea maagizo kutoka juu. Na suala la kutumia TIN taarifa ilitoka muda sana.ulikua wapi boss??
Huyu atakuwa wazee CPA, maana anavyotoa POVU kana kwamba TRA wamekosea.

Pinga pinga kila kitu haitofikisha hata atawale malaika.
 
Kuna taarifa inasambazwa kwa video clip na magazetini ikiwa imetolewa na TRA kuwataka waajiliwa wote kuwa na TIN. Ni taarifa ambayo naona kama inatokana na uongozi wa TRA wenye mapungufu ya hekima...
Waajiriwa taarifa wanazo tangu Julai 2020 na deadline ilikuwa September.

Kwa taarifa yako/yenu haichukui nusu saa mtumishi kuwa na TIN number ilimradi awe na kitambulisho cha taifa NIDA.

Watumishi wa Umma 99% wanavyo vitambulisho au number za nida
 
Waajiriwa taarifa wanazo tangu Julai 2020 na deadline ilikuwa September.
Kwa taarifa yako/yenu haichukui nusu saa mtumishi kuwa na TIN number ilimradi awe na kitambulisho cha taifa NIDA.
Watumishi wa Umma 99% wanavyo vitambulisho au number za nida
Tatizo kupata hiyo TIN online ni shida.
Kwangu niliomba online TIN Tarehe 25/9/2020 lakini mpaka leo inaniandikia
"Your TIN status is in progress, You will be notified through your contacts".
Inanipasa tu nitembelee ofisi zao maana huku online naona kama imeshindikana.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Waajiriwa taarifa wanazo tangu Julai 2020 na deadline ilikuwa September.
Kwa taarifa yako/yenu haichukui nusu saa mtumishi kuwa na TIN number ilimradi awe na kitambulisho cha taifa NIDA.
Watumishi wa Umma 99% wanavyo vitambulisho au number za nida
Mkuu mbn kama unatuchamba ?!
 
Tin no ni usajili wa mlipa kodi yeyote na kwa kuwa wafanyakazi wanalipa kodi wanapaswa kuwa nayo ni mawazo yangu lkn mkuu
Vipi kuhusu wafanyakazi wanaolipwa kima cha chini ?
Hawa pia wanatakiwa kuwa na TIN Number wakati hawalipi Kodi ?
 
Mhhhh labda uelewa wangu mdogo maana ukiuza gari unaenda kubadili ownership na unalipa TRA kwa gari ndogo nadhani 70000
Ukiuza gari, nyumba nk lazima ulipe 10% ya bei uliouza inaitwa capital gain, so hio kodi huwez kwepa why? Ukiuza gari au kununua ili ubadilishe umiliki lazma ulipe hio 10% bila kulipa hautofanikiwa
 
Tin no ni usajili wa mlipa kodi yeyote na kwa kuwa wafanyakazi wanalipa kodi wanapaswa kuwa nayo ni mawazo yangu lkn mkuu
Mawazo yako ni mgando. Hata kabla ya uhuru watumishi wa uma hulipa kodi kwa utaratibu ulioainishwa,ambao upo wazi, sasa hiyo TIN NUMBER kwa mtumishi itaongeza nini?
 
Back
Top Bottom