Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Imeelezwa kuwa mfumo wa mgawanyo wa madaraka na utayari wa kimapambano ni mmoja ya mifumo bora katika vyama vya utetezi wa haki kwani huwa daima hautingishiki kutokana na vifo vya viongozi wao wakuu.
Kutokana na mfumo huo nafasi yoyote inayoaachwa wazi basi huwa kuna makundi ya waliotayarishwa kushika nafasi hiyo.Kwa mfano Hassarn Nasrallah mwenyewe alishika nafasi muda mfupi tu baada ya kuuliwa mtangulizi wake .Mousa Mossawi mwaka 1992.
Hivi karibuni kuna makamanda wakuu wa kundi hilo ambao waliuliwa na papo hapo nafasi zao kujazwa na kuendeleza majukumu waliyokuwa wakiyasimamia.
Shambulio la kutumia simu za mkononi liliwajeruhi wanachama wa Hizbullah karibu 1500 na hata hivyo hakuna kilichosimama siku moja tu baada ya tukio hilo.
Hassan Nasrallah kila siku alikuwa akijihisi kwamba wakati wowote angeuliwa na hivyo alikuwa ameshatayarisha makumi ya wasaidizi wake ili kumrithi nafasi yake.
Mfumo huo wa uendeshaji umeelezwa na Andreas Krieg wa chuo kikuu cha Kings huko Uiengereza.
Kwa hali hiyo mtafiti huyo amesema iwapo Israel itaamua kuvutka mpaka kuingiza vikosi vya ardhini nchini Lebanon inaweza ikakutana na upinzani mkali kutoka makundi ya kivita ya Hizbullah ambayo yanajiendesha yenyewe bila kusubiri amri kutoka uongozi wa juu wa chama hicho.Hilo linaweza likawapa kipingamizi kikubwa IDF.
Kutokana na mfumo huo nafasi yoyote inayoaachwa wazi basi huwa kuna makundi ya waliotayarishwa kushika nafasi hiyo.Kwa mfano Hassarn Nasrallah mwenyewe alishika nafasi muda mfupi tu baada ya kuuliwa mtangulizi wake .Mousa Mossawi mwaka 1992.
Hivi karibuni kuna makamanda wakuu wa kundi hilo ambao waliuliwa na papo hapo nafasi zao kujazwa na kuendeleza majukumu waliyokuwa wakiyasimamia.
Shambulio la kutumia simu za mkononi liliwajeruhi wanachama wa Hizbullah karibu 1500 na hata hivyo hakuna kilichosimama siku moja tu baada ya tukio hilo.
Hassan Nasrallah kila siku alikuwa akijihisi kwamba wakati wowote angeuliwa na hivyo alikuwa ameshatayarisha makumi ya wasaidizi wake ili kumrithi nafasi yake.
Mfumo huo wa uendeshaji umeelezwa na Andreas Krieg wa chuo kikuu cha Kings huko Uiengereza.
Kwa hali hiyo mtafiti huyo amesema iwapo Israel itaamua kuvutka mpaka kuingiza vikosi vya ardhini nchini Lebanon inaweza ikakutana na upinzani mkali kutoka makundi ya kivita ya Hizbullah ambayo yanajiendesha yenyewe bila kusubiri amri kutoka uongozi wa juu wa chama hicho.Hilo linaweza likawapa kipingamizi kikubwa IDF.