TEAM 666
JF-Expert Member
- Dec 7, 2017
- 4,399
- 8,594
Mtanzania aliyehukumiwa kwa kuhusika katika shambulio la kigaidi lililotokea mwaka 2015 katika chuo kikuu kimoja nchini Kenya na kusababisha watu 148 kufariki , amejiua mwenyewe akiwa gerezani , vyombo vya habari vya Kenya vimeripoti.
Washambuliaji wanne waliuawa kwa kupigwa risasi na wanajeshi wa Kenya katika chuo kikuu cha Garissa ,lakini Rashid Charles Mberesero, na wenzake wawili walikamatwa na mwaka jana walihukumiwa kwa kuhusika katika ugaidi.
Hukumu hiyo ilimpa bwana Mberesero kifungo cha maisha gerezani.
Taarifa zinasema alikuwa na matatizo ya akili wakati akiwa gerezani na alikuwa anamuona mtaalamu wa afya akiwa gerezani.
Gazeti la Daily Nation linasema Mberesero alijinyonga mwenyewe aliwa gerezani kwa kutumia blanketi lake.
Shambulio kubwa kutokea mwaka 2015 liliacha simanzi kubwa .
Al-Shabab ilisema imekuwa katika vita na Kenya tangu askari wa Kenya kuingia Somalia mnamo Oktoka 2011.
Rashid Charles Mberesero ni nani?
Habari kwamba raia mmoja wa Tanzania ni miongoni mwa washukiwa watatu waliopatikana na hatia ya kupanga na kutekeleza shambulio katika chuo kikuu cha Garissa nchini Kenya 2015 ziliwaacha wengi na mshangao.
Rashid Charles Mberesero ambaye alikamatwa na watu wengine wanne muda mfupi baada ya mkasa huo wa Garissa uliosababisha vifo vya wanafunzi 148, alipatikana na hatia hiyo wakati mahakama moja nchini Kenya ilipotoa uamuzi wake baada ya takriban miaka minne.
Katika uamuzi huo raia huyo wa Tanzania pamoja na Hassan Edin na Mohammed Abdi jina jingine Mohamned Ali Abikar walipatikana na hatia ya kupanga shambulio hilo chini ya ushirikiano wa wanachama wa kundi la Al-Shabab.
View attachment 1638171
Washambuliaji wanne waliuawa kwa kupigwa risasi na wanajeshi wa Kenya katika chuo kikuu cha Garissa ,lakini Rashid Charles Mberesero, na wenzake wawili walikamatwa na mwaka jana walihukumiwa kwa kuhusika katika ugaidi.
Hukumu hiyo ilimpa bwana Mberesero kifungo cha maisha gerezani.
Taarifa zinasema alikuwa na matatizo ya akili wakati akiwa gerezani na alikuwa anamuona mtaalamu wa afya akiwa gerezani.
Gazeti la Daily Nation linasema Mberesero alijinyonga mwenyewe aliwa gerezani kwa kutumia blanketi lake.
Shambulio kubwa kutokea mwaka 2015 liliacha simanzi kubwa .
Al-Shabab ilisema imekuwa katika vita na Kenya tangu askari wa Kenya kuingia Somalia mnamo Oktoka 2011.
Rashid Charles Mberesero ni nani?
Habari kwamba raia mmoja wa Tanzania ni miongoni mwa washukiwa watatu waliopatikana na hatia ya kupanga na kutekeleza shambulio katika chuo kikuu cha Garissa nchini Kenya 2015 ziliwaacha wengi na mshangao.
Rashid Charles Mberesero ambaye alikamatwa na watu wengine wanne muda mfupi baada ya mkasa huo wa Garissa uliosababisha vifo vya wanafunzi 148, alipatikana na hatia hiyo wakati mahakama moja nchini Kenya ilipotoa uamuzi wake baada ya takriban miaka minne.
Katika uamuzi huo raia huyo wa Tanzania pamoja na Hassan Edin na Mohammed Abdi jina jingine Mohamned Ali Abikar walipatikana na hatia ya kupanga shambulio hilo chini ya ushirikiano wa wanachama wa kundi la Al-Shabab.
View attachment 1638171