Mfunze Mwanao kujiajiri, mwambie maisha hayaanzi akiajiriwa, wasomi wakiwa wengi ajira zinakuwa chache

Mfunze Mwanao kujiajiri, mwambie maisha hayaanzi akiajiriwa, wasomi wakiwa wengi ajira zinakuwa chache

Yani kwa Tanzania ya sasa uanze kuuza nyanya uwe milionea thubutu semeni tu waajiriwa wasikae kizembe wafanye chochote wapate hata hela ya bando ila kwa bongo hii ya 2020 utoke from zero uwe milionea sahau....
Walianzaje, do you know their backgrounds?

Maana hata Dewji ni billionaire, watoto wa marehem mengi wale mapacha wawili pia ni millionaires japo hawajui hata andazi linapikwa vipi na linauzwaje mtaani!

Nioneshe huyo billionaire alieanza biashara mwaka jana tu baada ya kumaliza chuo na leo amefikia ubilionea!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio poyoyo mleta mada yuko sahihi labda wewe hujamwelewa.

Kiukweli ajira hamna na Wasomi ni wengi. Ukweli utabaki

Wasomi waangalie namna ya kujiajiri...anapokuwa shule asiwaze ajira awaze kutafuta pesa....

Biashara wala haihitaji uzoefu toka kwa wazazi hayo ni mawazo tu mgando....you can make your own life....

Anyway

Mimi nitawaelimisha watoto wangu kuwa usomi sio ajira wajifunze namna ya kutafuta pesa nje ya ajira. Na nitawapeleka veta.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mawazo duni kabisa. Hakuna wakati ajira ziliwahi kutosha wote.

Kumbuka argument yangu ni kuwa huwezi kumfundisha mtoto kujiajiri kwa mdomo na porojo, ni lazima vitendo. Ukaja na misconception kuwa uache kazi ujiajiri. Mbona wengi sana tena sana wameajiriwa na wao ni waajiri na wana biashara zao mbali mbali. Lakini sikushangai, kwani wewe ni "English Lady" and I guess you are blonde too.

Narudia, mleta mada ni poyoyo asiyeelewa maisha yakoje. Mada yake ni bogus kabisa na siiungi mkono hata kidogo.

Ni ujinga pia kufikiri kuwa elimu ndiyo inamfanya mtu asijiajiri au kuajiriwa kuna mfanya mtu asijiajiri. Ni ujingw pia kufikiria unaweza kumfundisha mtoto kwa maneno tu akakuelewa, ujinga tu kufikiria hivyo.
 
Hata hivyo bado hatujachelewa tunaweza kubadilisha huu mfumo wa elimu kama mada ikiwekwa mezani bungeni.
Panda juu ushuke mfumo hutoweza kuubadili.

Anza kubadilika mwenyewe nyumbani. Jiajiri japo part time, Anza kuuza juice unaporudi nyumbani au kila Jumamosi na Jumapili na wanao wakuone unafanya hivyo na unafurahia na unaingiza pesa. Hapo inakuwa unatoa mafunzo ya kujiari kwa vitendo si kwa maneno.
 
Umesema vizuri sana fursa za biashara Tz bado zipo nyingi.Ukosefu wa bunifu unafanya zionekane ngumu.
Kuna mtu aliwah kuzumgumzia juu ya kuongezea bidhaa thamani,hakuna anayefikiria hayo.Kazi/shughuli nyingi bado zinafanywa KIJIMA mno!

Kuna miji mingi sana mpaka sasa bucha zake hazina mashine ya kukatia nyama!(fursa!)
Kuna gereji za magari mpaka sasa hazina vifaa vya kisasa,hata carwash! (fursa)
Maji bado yanauzwa kwa kuzungushwa na mkokoten! (fursa)
Mji mkubwa tena katikati ila mamantilie wanahudum kwa uduni mnoo, ukiboresha biasha ya mgahawa siyo lazima bei ya chakula ipae(fursa)
Watu wabo wanalima kwa jembe la mkono, trekta kodisha lima mashamba uza(fursa)
MAMBO NI MENGI, WATENDA KAZI NI WACHACHE, KISA WAMESOMAMO, ETI HAWANA MITAJI(MBONA MAMILION YA KULIPIA SHULE YALIPATIKANA??


When your toddler was learning to walk, you’d encourage her to get back up after she fell down,Parents should practice that approach as their children get older.
[c] CcCentia. Family zetu za kitanzania zina shida moja kwy kutafuta Ada wapo tayari hata kukopa pesa lakini ukishamaliza shule ndio wanakuwa wamemtelekeza Kijana kwy ulingo wa AJIRA ambao uko ndio maisha yapo na inakuwa ni shida sana, mfano na vijana wengi wa kitanzania yupo tayari akasome degree ya political science na wakati ana malengo yoyote ya siasa izi ndio changamoto na Kingine umasikini ni kitu kibaya sana kinaondoa maarifa unakuta baada ya kusoma vitu vyenye dili tunasoma vitu vya ARTS ambavyo havina FUTURE kama vilivyo muhimu kama kusoma maswala ya magari, kilimo, mifugo na afya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nunua maharage kilo mbili na cement mifuko mitatu kisha jenga mgahawa. Baada ya miezi saba utakuwa na five star hotel na zaidi ya bilion mia tatu benki!

Alisikika motivational speaker kwenye viunga vya stendi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio Enstein, ni Einstein.

Ujinga ni ujinga tu, hakuna ujinga mkubwa na mdogo.
Kweli ujinga ni ujinga tu. Nilikuwa naonesha jina huanza kwa herufi kubwa. Ulichofanya wewe ni kama kuweka spelling kwa Kiingereza Sawa, ungeweka kwa Kijerumani ungekuwa nawe si mjinga kwani hakuwa Mwingereza huyo.
 
Hata mi nawaza hili. Kumpa mtoto life skills za kusaka noti. Na zaidi sana napingana sana na usemi mtoto urithi wake elimu mi nimejipangia kupambana niwezavyo niwape mali...kabla sijafa sio aje arithi nikiwa mfu.


Kuna dogo mmoja ana urafiki na ndugu yangu...ndugu yangu alifeli kidato Cha nne zeroo...akajifunza udereva mitaani nikamtafutia leseni.... yuko anapiga zake kazi za udereva, ana maisha yake na mke na mtoto kukiwa na Jambo kwenye familia anachangia. Sasa huyu rafiki ake Ni msomi wa digrii ametoka zake huko mkoa anamsumbua ndugu yangu amtafutie ajira na anaishi kwake hana analofanya zaidi ya kusumbua kwa simu apate ajira. Ndugu yangu anahangaika sana....

Mfano wa pili huyu ndugu yangu ni age mate na mdogo angu wa kiume.....ye kasoma digrii na amesoma school of law hana ajira mpk Leo hi hopeless hana analofikiri zaidi ya kula bata tu...hakuna analoweza walikuwa wakimcheka huyu ndugu kuwa hana elimu...lkn ana maisha yake...anajitegemea..... Yaani huyu dogo anashindwa hata kufikiri kutumia taaluma yake ya sheria kujiajiri hana...anawaza tu kuajiriwa.

Yani kuliko mtu apoteze mamilioni kulipia chuo kikuu kusoma theories miaka 3-7 ni aheri aende NIT apate cheti cha udereva aanze harakati zake mapema tu au akasomee technical skills nyingine ambazo zitamnufaisha moja kwa moja akitoka chuo kama capentry, cherehani ama welding.

Sitarudia hili kosa kwa mtoto wangu. Shule ya msingi atasoma nzuri ya sekondari kawaida form 4 breki. Short course kisha mtaji aingie zake mtaani kupambana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom