You are very right Madam, tatizo watu wengi hawana msingi wa elimu za biashara hata kama ni informal inasaidia sana kujua abcs za business.
Binafsi niliingia kwenye biashara baada ya kumaliza form 4, na hapo sijui ilitokeaje nikakosa post ya form 5 na nilikuwa na division 2 na kwa miaka hiyo ilikuwa ni pass mark nzuri sana.
Kutokana na changamoto za kifamilia sikuweza kuafford private school nikazama mtaani. Nikafanya business kwa miaka 4 then nikaenda advance baada ya hapo chuo nikaunga.
Nilipomaliza nami nikajikuta kwenye mtego wa wahitimu wa kusaka ajira wakat nilikuwa na balance nzuri tu baada ya kutoka chuo kwa kuwa muda wote nasoma nikiwa likizo nilikuwa napiga mishe zangu nasave pesa.
Baada ya kuapply kwa miezi kadhaa huku nikitumbua 'mafao' yangu, nikatafakari hapa nisipojiongeza nitaishiwa. Nikaamua kuset deadline ya kutafuta ajira (mwaka mmoja tu) ndio muda niliojipa tangu nitoke chuo. Ulivopita sikuapply tena na hata ndugu na jamaa walipo nitonya kuna nafasi mahali niliitikia ila kiukweli sikuapply kabisa.
Sent using
Jamii Forums mobile app