Mgao ujao wa umeme…

Mgao ujao wa umeme…

Inadaiwa mgao wa umeme unakuja. Inadaiwa unaanza tarehe 1 mwezi ujao wa Februari.

Sababu ya huo mgao eti ni matengenezo ya mitambo yao ya wapi wapi huko sijui…

Sasa kwa akili zangu hizi za kidato cha nne, ni kama vile sielewi elewi.

Mbona nchi zingine huwa hakuna migao inayosababishwa na matengenezo ya mitambo ya umeme?

Au zipo? Kama zipo, basi sawa. Ila kwa nchi nizijuazo mimi, kamwe hata mara moja sijawahi sikia eti kutakuwepo na mgao au migao ya umeme kwa sababu mitambo ya kuzalisha au kusambaza umeme inafanyiwa ukarabati.

Hao wenzetu wao mitambo yao huwa haihitaji ukarabati? Kama huwa inahitaji ukarabati, wanawezaje kuepuka migao ya umeme?

Kwa nini sisi kila mitambo inapohitaji ukarabati [ kama ni kweli inahitaji huo ukarabati] basi kunakuwepo na mgao?

Manake hili si jambo geni. Limekuwepo siku zote. Sasa miaka yote hii hawa watu hawajaweza tu kubuni namna ya kuikarabati hiyo mitambo bila kuleta usumbufu wa migao?

Tanesco….and whoever else involved….seriously????
Tangu Magufuli ameondoka basi kila kitu kimekuwa hovyo tu.
 
Kila hitilafu ikitokea inakuwa oh...fulani angekewepo isingetokea!!
Hata mashine zinachoka na kuhitaji ukarabati...
"Mpaka mvua ikichelewa kunyesha itasemwa kwa kuwa fulani hayupo.."
Tusubiri wahusika watujulishe sababu ya mgao na sio kuangalia nani yupo nani kaondoka...
 
Hadi mwaka jana, inakadiriwa kuwa uzalishaji wa umeme kwenye gridi ya taifa ulikuwa 1,604MW, huku mahitaji kwenye grid yalikuwa 1,180MW...

Sasa ikitokea chanzo kimoja kikubwa kimezimwa, ndipo hapo upungufu unapojitokeza...

Kitu ambacho nadhani Waafrika kimekuwa kikitukwamisha, ni kutojua au kutilia maanani vipaumbele...

1604MW, kiwango hiki ni chini ya matarajio ya sera ya nishati, ambayo ilikadiria kuwa hadi kufikia 2020, Tanzania ingekuwa ikizalisha si chini ya 5,000MW za umeme kwenye gridi ya taifa, hasa baada ya ugunduzi wa gesi asilia...

Huu ndio ule wakati Waziri Muhongo na wanasiasa wengine walijigamba kuwa mgao wa umeme kuwa historia Tanzania...

Kwa mujibu wa takwimu, matumizi ya bomba kubwa la gesi lile la (Mtwara <> Dar) ni asilimia 6 tu, huku asilimia 94 zikiwa hazitumiki...

Iwapo bomba hilo lingetumika kwa uwezo wake kwa angalau asilimia 50 tu, lingesaidia kuongeza umeme wa uhakika...
 
Kuna Muda Natamani hata nisingezaliwa Tanzania
Unaweza kupata uraia wa nchi yeyote unayotaka si lazima uwe mzaliwa wa hapo.....
Kama kuwa Mtanzania kunakukera badilisha uraia hujachelewa
 
Hadi mwaka jana, inakadiriwa kuwa uzalishaji wa umeme kwenye gridi ya taifa ulikuwa 1,573.7MW, huku mahitaji kwenye grid yalikuwa 1,180MW...

Sasa ikitokea chanzo kimoja kikubwa kimezimwa, ndipo hapo upungufu unapojitokeza...

Kitu ambacho nadhani Waafrika kimekuwa kikitukwamisha, ni kutojua au kutilia maanani vipaumbele...
Kwa nini hawana mitambo ya ziada?

Miaka 60 ya uhuru bado tunahangaika na migao ya umeme tu!
 
Hiyo mitambo haikufanyiwa marekebisho kwa muda mrefu sababu wahusika waliogopa kutumbuliwa (hili waziri alishasema)

Sababu za mgao ni kufanya ukarabati na bila kufanya huo ukarabati kipindi hiki huenda hata huo umeme wa mgao usiwepo.....hivyo Watanzania ondoeni wasiwasi kwani hayo matengenezo ni muhimu kipindi hiki.
 
Inadaiwa mgao wa umeme unakuja. Inadaiwa unaanza tarehe 1 mwezi ujao wa Februari.

Sababu ya huo mgao eti ni matengenezo ya mitambo yao ya wapi wapi huko sijui…

Sasa kwa akili zangu hizi za kidato cha nne, ni kama vile sielewi elewi.

Mbona nchi zingine huwa hakuna migao inayosababishwa na matengenezo ya mitambo ya umeme?

Au zipo? Kama zipo, basi sawa. Ila kwa nchi nizijuazo mimi, kamwe hata mara moja sijawahi sikia eti kutakuwepo na mgao au migao ya umeme kwa sababu mitambo ya kuzalisha au kusambaza umeme inafanyiwa ukarabati.

Hao wenzetu wao mitambo yao huwa haihitaji ukarabati? Kama huwa inahitaji ukarabati, wanawezaje kuepuka migao ya umeme?

Kwa nini sisi kila mitambo inapohitaji ukarabati [ kama ni kweli inahitaji huo ukarabati] basi kunakuwepo na mgao?

Manake hili si jambo geni. Limekuwepo siku zote. Sasa miaka yote hii hawa watu hawajaweza tu kubuni namna ya kuikarabati hiyo mitambo bila kuleta usumbufu wa migao?

Tanesco….and whoever else involved….seriously????
Nafikiri kwa muda mrefu Tanesco wamekuwa wakiendesha hiyo mitambo bila periodic maintenance kwa kuhofia kuonekana saboteurs baada ya serikali kuahidi hamna mgao. Now the chickens have come home to roost maana wakizidi kuiendesha ita collapse kabisa. Hawana jinsi bali wafanye the long over due maintenance.

Amandla...
 
Subiri subirini kidogo bado tunamalizia keki ya birthday tukimaliza tuhudhurie kongamano moja,teuzi kidogo na semina elekezi tumalizie na birthday ya pinda .Tukimaliza tutaangalia angalia nafasi ikiwepo tutajadili hili swala
 
Back
Top Bottom