Mgao wa Maji umerudi Dar?; Kunduchi-Mtongani wiki inaisha bila maji kutoka

Mgao wa Maji umerudi Dar?; Kunduchi-Mtongani wiki inaisha bila maji kutoka

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Salaam ndugu,

Ni hatari kwa afya kumaliza wiki nzima bila kupata maji. Labda sijui walitangaza kutakuwa na mgao wa maji, lakini hakuna mgao unaokwenda mpaka wiki nzima bila maji kutoka. Tunajipa matumaini labda maji yatatoka usiku lakini wapi!

Nilitegemea mvua nyingi zilizonyesha hivi karibuni zingetatua shida ya uhaba wa maji kwa muda mrefu, lakini hiki kinachoendelea kimenishangaza sana.

Hata kama kungekuwa na hitilafu kubwa labda bomba kubwa kupasuka nk, ndio lisirekebishwe wiki nzima?

DAWASA sisi wananchi wa huku tunawalilia, hali ni mbaya sana. Wengine maji ya chumvi ambayo ndio yanuzwa sana mtaani kwa sasa hatuyawezi. Tunataka maji tuendelee na shughuli zetu. Sasa hivi hata kwenda chooni unajipimia ili kubana matumizi ya maji. Kuna jirani yangu mtoto wa mama karudi kwao kisa mtaani hakuna maji.
 
MTAANYOOKA MWAKA HUU.

MPKA MTAMBUE UMUHIMU WA KUDAI HAKI ZENU NA KATIBA MPYA.

Mwanamke hafai kwa uongozi kabisaa
 
Kaka sijui unakaa kunduchi mtongani sehemu gani hasa, kuna ndugu zangu wanaishi mitaa hiyo hata jana nilipita hapo maji yapo na wala sijawahi kusikia hayo malalamiko yawezekana labda bomba kubwa linaloleta maji mtaani kwenu lina shida, jaribu kufuatilia.
 
Wananchi wa makao makuu ya nchi dodoma, mrejesho tafadhali. Mnapata maji ya uhakika kweli kutoka kwa ndugu zenu wa Duwasa? Au bado ni mpaka wiki ipite?
 
Kaka sijui unakaa kunduchi mtongani sehemu gani hasa, kuna ndugu zangu wanaishi mitaa hiyo hata jana nilipita hapo maji yapo na wala sijawahi kusikia hayo malalamiko yawezekana labda bomba kubwa linaloleta maji mtaani kwenu lina shida, jaribu kufuatilia.
Hapa maarufu kama baa ya Kyaroni, mita 100 kutoka barabara kuu ya Bagamoyo.
 
Back
Top Bottom