Mgao wa mali za Jide, Gadner 'UTATA'


Gadner kawekeza TBL na Kwa Bibi.
 
Bora akajipange tu maana mwanaume kukomalia mali duh!!
 

shikamooo mkuu
 
Issue zingine mbona ndogo sana......JIDE kubadili majina ya umiliki wa mali zake haitosaidia labda kama hayatotumia majina yake kwenye ownership kule BRELA na usajili mwingine kama TIN n.k ......kama bado umiliki ni wake bado Gadner ana haki zote maana ndoa haijavunjwa rasmi kisheria.....chochote atakachonunua sasa Gadner au JIDE itabaki kuwa mali zao wote hadi pale ndoa itapokufa kisheria.......pengine wanataka kutumia skendo hii kibiashara ........
 
Kuandika mali kwa jina lako hakumnyimi mwanandoa mwenzio haki kisheria kama mlichuma kipindi cha uhai wa ndoa.Zile utazochuma baada ya ndoa kuvunjika kisheria ndio zitakuwa zako.
 
Hapo mwanamke ndo angefanyiwa hivi kama anavyofanyiwa gardner humu pasingekalika

Tena n maneno mazito kma wamechuma wote shurti mgao pasu kwa pasu istoshe jamaa ana haki zake katumia nguvu sana kupromote kazi z wife kma meneja wke
 
Kuna siku humu niliwahi kuandika kuwa ule Mgahawa wala sio wa Jide bali pale ni Wapangaji kama wapangaji wengine waliopanga kwenye lile jengo acha #warumi team jide anitukane, nikaamua nipotezee tu. Kwenye hilo bandiko lako ulilokopi toka grobal ndo wamemaliza ubishi wako kuwa lile jengo anapanga. Sijaona unakanusha kama grobal ni waongo bshaka ndo ukweli wenyewe na huo ubishi tumeuzika leo kuwa jide mpangaji pale.

Tatizo Gadner anashindwa kuelewa kuwa zile mali zimetokana na kipaji cha Jay Dee na yeye alikua ni Meneja wa jide bshaka alikua analipwa mshahara. Unaposhindwana na bosi wako unabwaga unaenda kutafta maisha sehemu nyingine. Haki za wanawake huwezi kuzililia zifanye kazi upande wa pili wa jinsia.
 
gadner arudi kwa mke wake wa kwanza wakagawane mali alizo chuma wakiwa wote aking'ang'ania za jide anatia aibu nani hajui alimkuta jide na mali zake utakoma kaka jipange komando jide kile kichwa hhh hati zote kwa jina la demu hunachako hapo bro anza kuchuma vyako.
 
Mapenzi ya nguvu ya soda ni balaa!yakikatika inakua chui na paka
 

kashaolewa hana khabari na ana good life gadner hana maana yule na hawakua na chochote
 
Hakuna kwenye utata kwenye hili swala sema Global wanajaribu lionekane lina utata!

Hawa watu wanajulikana walifunga ndoa lini na wana cheti cha ndoa!
Hawa watu vitu vyote walivyo vinunua vina vielelezo vilinunuliwa lini ...

Kama kweli Jide amendika jina lake mali zote lakini lazima kuna makubaliano kwanini alifanya hivyo na lazima kuna mali G hana mchango wowote!

Pamoja na hayo yote Gardner ana mchango katika maendeleo ya Jide na wala hili haliitaji ushahidi..

Hili swala halina utata kabisa maana kila kitu(Mali) kina vielelezo hivyo kila mtu atapata kulingana na mchango wake kwenye kila kitu!
 
Kichwa cha nyumba bila pesa? ni ngumu mno. Enzi bible inaandikwa, wanaume walikuwa bread earners so automatically walikuwa vichwa vya nyumba. Hawa wanaume wa sasa wamesahau majukumu ya utafutaji na kuhudumia familia, ni ngumu sana kuwa father house

Ndio tatizo linapoanzia hapo wanaume wa siku hizi wanaoa mwanamke kwa kuangalia kipato chake na atasaidia vipi familia! Ndio maana nasema Gadner kama hana hata mali moja iliyoandikwa kwa jina lake mimi siwezi muelewa kwanini aliacha mali zote zikawa ktk jina la mkewe? Gadner amekuwa ndani ya ajira zaidi ya 10yrs nadhani lazima alikuwa na mchango/kipato chake kama baba wa familia, kuacha mali zote ziwe chini ya mkewe ni sawa na kuwa mke ndie alikuwa kichwa cha nyumc
 

Nakubaliana nawe 100% Kwamba Gadner ana mchango mkubwa sana ktk mafanikio yao.Gadner hakusimama kama mwanaume wa kiafrika na kuwa na akili angalau kwa namna moj naye awe mmiliki wa kitu fulani ktk hivyo walivyochuma. Kumwachia mwanake umiliki wote inaleta picha ni namna gani Gadner alikuwa mzembe au akinyanyasika ndani ya mahusiano. Ndoa ambayo mwanamke anamiliki kila kitu hazidumu sababu wanawake wengi wanavumilia kukaa ktk ndoa sababu ya mali.
 

Mali ni za jaydee sasa suala la kuruhusu mtu kuandika jina lake kwenye vitu anavyomiliki ni vibaya? Cha muhimu ajipange tu kimaisha aanze upyaaa
 

Ivi utangazaji na wenyewe ni kazi ya kufanya mtu ajishebedue nayo? Mi nilikuwa sijiu
 

Angekuwa mwanamke mngesema sana, ooh alkuwa anampikia chai, anamfulia chupi, sheria msumeno , umetaka talaka kila kitu kiwekwe kati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…