Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
Ijumaa nilimpokea mgeni, ambaye ni shangazi yake waifu. Ametoka mkoani na yupo hapa Dodoma akifuatilia mafao yake baada ya kustaafu. Hawa wenzetu askari hustaafu wakiwa na umri mdogo ukilinganisha na waajiriwa wengine.
Siku ya jumapili aliaga mapema kuwa ataenda kuutembelea familia ya rafiki yake pamde za Nkuhungu. Tukawa hatuna pingamizi.
Ikafika saa moja kimya, saa mbili kimya, saa mbili na nusu nikamwambia wife, mcheki shangazi yako. Maana ni mgeni na muda unasonga kwa kasi.
Alipompigia akapokea akiwa kwenye kelele nyingi, ila akasema atarudi mida ya saa tano au sita wanasherehekea ushindi wa Simba na marafiki zake.
Saa sita kimya, sita na nusu kimya, saa saba kasorò nane, geti linagongwa kwa nguvu sana, wife akataka aende kumfuñgulia shangazi yake. Nikamzuia, nikamwambia wee lala, wewe sio baba mwenye nyumba.
Basi nikaenda nikamfungulia, huko nikamkuta yuko na kajaa fulani hivi wamelewa chakari,chakari chakari chakari chakari , wananyonyana ndimi kilevi.
Nikafungua, kisha nikasalimia kwa kumwambia auntie uko poa? Akaniambia niko poa, nimekuja na mjomba wenu.
Tayari mi nilikuwa nimekereka na sikutaka kumuaibisha kwa wakati huo, nikaona niwe mpole tu, muda utamsuta.
Basi nikawaacha waingie ndani, nikaifunga nyumba kisawasawa, nikamjulisha waifs naingia lindo namsaidia mlinzi, maana leo ndio off yake.
Basi auntie na ngosha wake wakazama chumbani kwao, sikuwajali, nilikuwa busy na jambo moja tu, ulinzi.
Nilikaa nje hadi saa 12 na nusu, nilipoingia ndani nikamwambia waifu aandae breakfast kwa wingi kwani tunatarajia mgeni.
Nikaingia ndani nikalala kama mfu. Saa nne kasoro nikaamka, nikaoga kisha nikawa nimekaa mezani, nile kisha niingie misele.
Nilikaa mezani kama dakika kumi tu, kisha nikatoka kwenda mishe. Sikuwa na shughuli nyingi, kwani mara nyingi jumatatu huwa hazisomeki.
By saa tisa nilikuwa home, naulizwa na wife, mbona hamna mgeni aliyekuja kula breakfast? Nikamuuliza shangazi yako amekula, akanijibu akasema shangazi kasema anahitaji kupumzika, hata nje hajatoka.
Nikiwa hapo sebuleni napitia JF, mara nikasikia mlango wa chumbani kwa auntie ukifinguliwa. Auntie anatoka huku anaona aibu, akaja kunisalimia huku analia, kapiga magoti anaomba msamaha.
Mara wife akatokea akawa anashangaaa maana sikumweleza chochote, so akawa anashangaa kwanini shangaziye analia?
Nikamwambia mimi sina nongwa, mlete mgeni wako mle mpate nguvu. Jamaa anaona aibu na jezi yake ya Simba, anakula chakula hakishuki, anatiatia tu huruma.
Nikawaacha na kusepa zangu.
Wapendwa ukifurahi, hakikisha unafurahi kwa kiasi, usizidi kipimo.
Siku ya jumapili aliaga mapema kuwa ataenda kuutembelea familia ya rafiki yake pamde za Nkuhungu. Tukawa hatuna pingamizi.
Ikafika saa moja kimya, saa mbili kimya, saa mbili na nusu nikamwambia wife, mcheki shangazi yako. Maana ni mgeni na muda unasonga kwa kasi.
Alipompigia akapokea akiwa kwenye kelele nyingi, ila akasema atarudi mida ya saa tano au sita wanasherehekea ushindi wa Simba na marafiki zake.
Saa sita kimya, sita na nusu kimya, saa saba kasorò nane, geti linagongwa kwa nguvu sana, wife akataka aende kumfuñgulia shangazi yake. Nikamzuia, nikamwambia wee lala, wewe sio baba mwenye nyumba.
Basi nikaenda nikamfungulia, huko nikamkuta yuko na kajaa fulani hivi wamelewa chakari,chakari chakari chakari chakari , wananyonyana ndimi kilevi.
Nikafungua, kisha nikasalimia kwa kumwambia auntie uko poa? Akaniambia niko poa, nimekuja na mjomba wenu.
Tayari mi nilikuwa nimekereka na sikutaka kumuaibisha kwa wakati huo, nikaona niwe mpole tu, muda utamsuta.
Basi nikawaacha waingie ndani, nikaifunga nyumba kisawasawa, nikamjulisha waifs naingia lindo namsaidia mlinzi, maana leo ndio off yake.
Basi auntie na ngosha wake wakazama chumbani kwao, sikuwajali, nilikuwa busy na jambo moja tu, ulinzi.
Nilikaa nje hadi saa 12 na nusu, nilipoingia ndani nikamwambia waifu aandae breakfast kwa wingi kwani tunatarajia mgeni.
Nikaingia ndani nikalala kama mfu. Saa nne kasoro nikaamka, nikaoga kisha nikawa nimekaa mezani, nile kisha niingie misele.
Nilikaa mezani kama dakika kumi tu, kisha nikatoka kwenda mishe. Sikuwa na shughuli nyingi, kwani mara nyingi jumatatu huwa hazisomeki.
By saa tisa nilikuwa home, naulizwa na wife, mbona hamna mgeni aliyekuja kula breakfast? Nikamuuliza shangazi yako amekula, akanijibu akasema shangazi kasema anahitaji kupumzika, hata nje hajatoka.
Nikiwa hapo sebuleni napitia JF, mara nikasikia mlango wa chumbani kwa auntie ukifinguliwa. Auntie anatoka huku anaona aibu, akaja kunisalimia huku analia, kapiga magoti anaomba msamaha.
Mara wife akatokea akawa anashangaaa maana sikumweleza chochote, so akawa anashangaa kwanini shangaziye analia?
Nikamwambia mimi sina nongwa, mlete mgeni wako mle mpate nguvu. Jamaa anaona aibu na jezi yake ya Simba, anakula chakula hakishuki, anatiatia tu huruma.
Nikawaacha na kusepa zangu.
Wapendwa ukifurahi, hakikisha unafurahi kwa kiasi, usizidi kipimo.