Mgodi wa Shantamine Chunya unakusanya dhahabu nyingi lakini hauna impact yoyote nchini

Mgodi wa Shantamine Chunya unakusanya dhahabu nyingi lakini hauna impact yoyote nchini

Inaonekana unaokoteza manebo ua mitaani badala ya kuitafuta ukweli.

Shanta mine, siyo sawa na Bulyanhulu, Buzwagi, Geita au North Mara.

Mgodi huo wa Shanta mine ni mgodi wa kati, siyo mgodi mkubwa - ni ML (Mining License). Hiyo mingine niliyoitaja ni SML (Special Mining License).

ML - uwekezaji wake si zaidi ya $100m. SML - ni uwekezaji wa zaidi ya $100m.
Haiwezekani mgodi wa kati ukatoa dhahabu nyingi kuliko mgodi mkubwa?
 
Kwakumalizia ni kwamba, ukubwa wa mgodi hupimwa kwa ukubwa wa skwea mita za eneo pamoja na miundo mbinu iliyopo.
Pia uzaishaji wa mgodi hupimwa kwa wingi wa rakili (ngapi) hupatikana katika kila kifusi madini cha tani moja.
 
Kwanza ujue mrabaha hautozwi kwenye faida. Pili shanta ni mgodi wa kati,a mining licence,ukubwa wa mgodi unakuwa determined na capital investment.

Huwezi kusema mgodi ni mkubwa sababu tu macho yako yameona mchanga mwingi umerundikwa au mataa mengi yanayomeremeta ndani ya mgodi.
Huu ujinga wa miccm,tubadili sheria basi.mchanga ukiwa mwingi ndo uwe kigezo cha mgodi mkubwa.tunapigwa Sana na hii miccm
 
Ukiona wanapakia pale songwe airport ujue wana clearance zote na washalipa kila kitu
Dhahabu haiondoki bila kuwepo tra,watu wa tume ya madini na vyombo vya ulinzi na usalama
Kama unajua wanaotorosha madini,isaidie nchi yako kwa kutoa taarifa tume ya madini/wizara ya madini.
Nje ya mada: Mkuu naweza kuja PM ukanipa ABC's za taratibu za kupeleka madini ya dhahabu nje ya nchi (Vyote kama mchimbaji au mnunuzi mkubwa ''agent")
Hasa dhahabu ya Chunya.
 
Huwezi kupima mgodi ukubwa kulingana na uzalishaji wake? Wanaweza weka mtaji mdogo lakini wakazalisha dhahabu nyingi kuliko migodi 'mikubwa' ya kanda ya ziwa.
Kabla mgodi kuanzishwa kunakuwa na study ya deposit ya madini na hiyo document inatakiwa kuambatishwa upon an application of licence..
Hiyo pamoja na mingine vitadetermine aina ya leseni
 
Moja kati ya mambo yanayonisikitisha nchi hii, ni sera ya serikali kwenye nishati na madini. Nchii ina kila aina ya madini. Lakini maeneo ya madini yana ufukara unaotisha. Hakika nchi hii tuna laana ya asili.

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
Sera zinaweza zisiwe mbaya, tatizo likawa kwenye utekelezaji wake.
Lakini kitu kingine kinacholeta shida ni namna ambayo "sisi wazalendo" tunavyoyaangalia na kuyapima MANUFAA ya migodi.

1. Kuna kodi na tozo ambazo wanalipa kwenye vyombo mbalimbali vya serikali.
2. Kuna ajira za moja kwa moja wanazotoa.
3. Kuna ajira zisizo za moja kwa moja wanazotoa.
4. Kuna michango yao ya kusaidia jamii katika nyanja mbalimbali kama shule, hospitali, huduma za maji n.k (Corporate social responsibility)
5. Kuongeza mzunguko wa fedha katika enjoy husika pamoja na kukuza fursa za kibiashara.

Sasa sisi wananzengo tunataka kupima manufaa ya madini kwa idadi ya mabilionea waswahili (akina Laizer) kama ndio kipimo pekee cha rasilimali tajwa.
 
Mkuu, kwanza mleta mada hajazungumzia swala la Shanta Mine kupata hasara.
Pili, migodi (dhahabu) ni biashara kama biashara zingine na hivyo basi hasara ni sehem ya biashara na hutokea kwenye migodi pia.
Ukisema mbona hawaondoki, manayake kwangu inanipa jibu rahisi kwamba bado haujui lolote kuhusu migodi/dhahabu ama biashara.
Kwakifupi ni kwamba, mtu anapo wekeza fedha nyingi kwenyw biashara flani na akawa anapata faida, then ikatokea biashara ile ikayumba kidogo na akajikuta anapata hasara, hii haimaanishi basi kwamba aondoke. Kumbuka hapo kabla alikua anapata faida na pia amewekeza mtaji mkubwa pamoja na kujenga miundo mbinu.
Miaka 10 unaclaim hasara KILA siku, si uongo huo.
 
Kwanza Shanta haipo Chunya mkuu, Shantamine ipo karibu na Mkwajuni, Saza na Patamela na upo katika wilaya ya Songwe, Katika Mkoa wa Songwe na sio Mbeya.

Pili kuhusu ukubwa ni kweli nadhani Shanta ni wa pili kwa ukubwa Tanzania kama sikosei baada ya GGM. Sijajua ni kwa nini hausikiki kabisa, lazima kuna matatizo sehemu.
Hata Chunya kuna wachina wamewekeza mgodi huko kuna Siku nilikuona Mkuu wa Wilaya na Chalamila wakiweka mambo sawa.

Pili nadhani unakumbuka sakata la utoroshaji madini mkoa wa mbeya badala ya kuuza kwenye soko la madini Chunya.

Huo mgodi kwa nini hautoi mapato kwenye Halmashauri za Chunya na Songwe kama ilivyo kwa Geita na Kahama
 
Mbona wengi mnawatetea hao wezi? Seems wanufaika wa hongo mko wengi Ili msiseme ukweli.

Serikali chunguza hii kampuni
 
Ule mgodi unasemekana ni wa kikwete unasimamiwa na ridhiwan

Kuna kipindi fulani ilikua kila jumamosi choppa inatua kuchukua mzigo na kusepa.
Kila kitu nchi hii ni cha Kikwete, gas Kikwete, mahotel mbugani ni Kikwete, mgodi wa Tanzanite one mirerani ni Kikwete, dhahabu ni Kikwete nk.. come on... give me a break! Acheni ujinga. Tufanye basi huo mgodi ni wa baba yako!
 
Shanta umeanza kazi nafikiri 2012 ni mpya sana, hiyo GGM au North Mara na Buly ni migodi ya zamani.

Kiukubwa sijui kama operation zimefikia capacity za hiyo migodi ya zamani.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Kila kitu nchi hii ni cha Kikwete, gas Kikwete, mahotel mbugani ni Kikwete, mgodi wa Tanzanite one mirerani ni Kikwete, dhahabu ni Kikwete nk.. come on... give me a break! Acheni ujinga. Tufanye basi huo mgodi ni wa baba yako!
OK
 
Ule mgodi unasemekana ni wa kikwete unasimamiwa na ridhiwan

Kuna kipindi fulani ilikua kila jumamosi choppa inatua kuchukua mzigo na kusepa.
Hawa kina Patel wana uhusiano gani?
 
Ukiona wanapakia pale songwe airport ujue wana clearance zote na washalipa kila kitu
Dhahabu haiondoki bila kuwepo tra,watu wa tume ya madini na vyombo vya ulinzi na usalama
Kama unajua wanaotorosha madini,isaidie nchi yako kwa kutoa taarifa tume ya madini/wizara ya madini.

Well said
 
Hata Chunya kuna wachina wamewekeza mgodi huko kuna Siku nilikuona Mkuu wa Wilaya na Chalamila wakiweka mambo sawa.

Pili nadhani unakumbuka sakata la utoroshaji madini mkoa wa mbeya badala ya kuuza kwenye soko la madini Chunya.

Huo mgodi kwa nini hautoi mapato kwenye Halmashauri za Chunya na Songwe kama ilivyo kwa Geita na Kahama
Chalamila alikua RC wa mkoa Mbeya, inakuaje ukamwona "akiweka mambo sawa" kwenye mkoa mwingine (Mgodi upo mkoani Songwe).

Ukisema ulimwona kabla mkoa wa Mbeya haujagawanywa, swali langu litakuja kwako kwamba ulimwona akifanya hivyo angali ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa ?
(Chalamila kawa RC wa Mbeya baada ya kugawanywa).
Naomba ufafanuzi wa ulichokiona mkuu
 
Back
Top Bottom