Baadhi ya dinari na pareshi zilivutiwa na sera zake hadi kupelekea wasiwasi kwa viongozi wa dayosisi na kanisa anglikana kwa ujumla.
Kamati ya uchaguzi iliondoa jina lake tena wakati uchaguzi ukiwa umeshafanyika kwa madai kuwa Kuta hana vigezo,jambo mojawapo lililosemwa ni kuwa bwana Kuta anajihusisha na masuala ya mapenzi ya jinsia moja.Ikumbukwe kuwa Kuta anatokea maeneo ya kanda ya Mlali ambapo ndipo hasa kwenye mgogoro mkubwa,baada ya kuondolewa kwake zaidi ya makanisa 80 yaliyopo kanda hiyo ya Mlali yaliamua kujitoa dayosisi ya Mpwapwa.