Mgogoro wa Israel na Palestine - Safari ya Tera

Mgogoro wa Israel na Palestine - Safari ya Tera

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
1621343437747.png

Na, Robert Heriel Tz

PART 1: SAFARI YA TERA

Huwezi zungumzia Taifa la Israel bila kumzungumzia Tera. Wazo la Israel kwenda Kanaani (Palestine) ya leo liliasisiwa Tera.

Tera ndiye Baba wa Abraham, Nahori na Harani. Tera alikuwa akiishi Uru ya Ukaldayo (Kati ya nchi ya Shinari na bara Aram) hata hivyo eneo hilo kwa wakati huo lilifahamika Kama nchi ya Aram ambapo waliishi Waram alioongea kiaramu.

Tera mbali na kuwa mfugaji pia alikuwa ni mchongaji wa vinyago na sanamu ambapo kazi hiyo ilimpa kipato kutokana na wakazi wa Uru walipenda kuabudu miungu ya sanamu.

Tera Kama binadamu mwingine aliamua kutafuta fursa sehemu zingine kuongeza pato lake kutokana na shughuli yake ya uchongaji na ufugaji (hasa ule ufugaji wa kuhama hama Kama wamasai, wasomi huutambua Kama Nomadic life)

Eneo nyeti Kwa wakati huo lilikuwa ni Kanaani, ambayo ilikuwa na malisho Kwa mifugo, na pia ilikuwa Route muhimu kuingilia Afrika na kwenda nchi za Mashariki ya mbali. Hivyo kibiashara Kanaani Tera aliiona ingemfaa Kwa kazi yake ya uchongaji.

Mambo ya Tera yakazidi kuwa magumu hasa baada ya mtoto wake wa kiume aitwaye Harani Kufariki. Hii ikamfanya azidi kuichukia nchi ya Uru na kuongeza ari ya yeye kuhama nchi hiyo. Kama haitoshi, mkwe wake Sarai ambaye ni mke wa Ibrahimu naye mambo yalikuwa magumu kwani alikuwa Tasa. Hii ikamfanya Tera aone nchi ya Uru haimfai kwani inamletea majanga katika familia yake. Hivyo ahame nchi nyingine (shabaha yake ikiwa Kanaani) kutafuta bahati yake.

Kizamani kufiwa na mtoto lilikuwa ni Jambo baya zaidi lisilosemeka. Ilifahamika kuwa mzazi ndio alipaswa kufa kabla ya mtoto. Hivyo Tukio la kifo cha Harani kiliusononesha moyo wa Tera. Na baadhi ya vitabu vinaeleza kuwa maisha ya Tera yalianza kuharibika kuanzia hapo.

Tera akaondoka Uru ya Ukaldayo akiwa na Ibrahimu mwanaye, Sarai mkwewe, Lutu mtoto wa Harani, na watumishi wengine, hapa Nahori hajatajwa ingawaje Nahori alioa binti wa Harani aitwaye Milka.

Inaendelea...

PART 1: SAFARI YA TERA

Na, Robert Heriel Tz

Kusema Nahori alichukua binti ya Harani (nazungumzia nchi sio Harani ndugu yake). Tera akaondoka Uru wa Ukaldayo na akatembea maili nyingi akielekea Kanaani, safari yake iligota katika nchi ya Harani. Hapo alikaa Kwa muda mrefu mpaka umauti ulipomfika, akafa na ndoto yake ya kufika Canaan.

Pengine sababu ya kukaa muda mrefu yaweza kuwa ni kuona jina la mwanaye Harani likifanana na jina la nchi hiyo, Harrani ingawaje hakukuwa na mahusiano ya kimaana baina ya majina hayo. Kuishi Harani pengine kulimpa faraja pale asikiapo jina hilo likitajwa.

Pia, sababu ya pili yawezakuwa ni uwepo wa baadhi ya ndugu katika nchi ya Harani hasa ndugu zake Labani ambao baadaye kupitia ukoo huo Isacka alimpata Rebeka, na Yakobo akapata wake zake yaani RRaheli na Leah binadamu zake kutoka Kwa mjomba wake Labani.

Safari ya Tera iliishia hapo nchi ya Harani, akiwa Mzee wa miaka Mia mbili na tano -205. Safari ya Tera ukawa turning point Kwa Ibrahim na waisrael mpaka hivi leo.

Tera alipokufa, Ibrahimu hakutaka kuendelea kuishi nchi ya Harani, Maandiko yanasema Mungu aitwaye Yahwe alimtokea na kumwambia aende Mpaka nchi atakayomuagiza, akiirejelea nchi ya Kanaani ambayo Baba yake, Mzee Tera ndio ilikuwa ndoto yake.

Ibrahimu akakusanya virago, mke, na Lutu mtoto wa ndugu yake, pamoja na yote waliyoyapata wakiwa Harani wakachanganya Mbariga kuelekea Kanaani.

TUNAENDELEA PART 3

Isemayo, SAFARI YA ABRAHAM

Uru ya Ukaldayo, Kwa Leo ndio Iraq mji wake Mkuu ilikuwa mesopotamia. Harani hivi leo ni Uturuki ya Kusini, Canaan kwa leo ni Gaza, westbank, ndio Palestine, na Maeneo ya Jordan.

Ulikuwa nami

Robert Heriel
Taikon WA fasihi
06933223000

Hadi kesho tena.

Part 2
Post in thread 'Mgogoro wa Israel na Palestine -- safari ya Tera' Mgogoro wa Israel na Palestine -- safari ya Tera
 
Simulizi nzuri.

Binafsi nashauri mama afanye ziara Israel awaalike waje hapa Tz kama wawekezaji sababu tunamaeneo makubwa. Waje waishi huku na kuiendeleza Tanzania kwapamoja.
 
PART 2: SAFARI YA ABRAHAM KUTOKA HARANI KWENDA CANAAN/PALESTINE



Na, Robert Heriel


Kabla hatuenda mbali, tuzingatie Jambo hili.

Tera mwenye asili ya Uru wa Ukaldayo, huko Mesopotamia, Iraq ya leo, aliondoka Uru kuelekea Kanaani na Safari yake kukomea Harani Uturuki ya Kusini karibu na Mpaka wa Ashuru, Syria ya leo. Akiwa na sababu zifuatazo;



1. Kutafuta maisha, Fursa za malisho ya mifugo

i. Biashara yake ya kuuza vinyago na sanamu ambavyo alikuwa akichonga



2. Kutafuta bahati na tumaini jipya baada ya nchi ya Uru kumfanyia mikosi na majanga Kama alivyoona.



3. Sababu ya Kisiasa.

Mgogoro wake na Mfalme Nimrodi ambaye aliazimia kuwatumikisha jamii ya Shem na Japheti.



Hata hivyo Tera aliikwama Haran na kufia huko.



Abraham naye akaanzia Harani, Uturuki ya Kusini kuelekea Canaan ndio Palestine, Gaza, westbank, maeneo machache ya Jordan, na Lebanon. Akiwa na Sarah mkewe, Lutu mtoto wa ndugu yake, na wajakazi pamoja na Mali zake.



Hapo akapitia Ashuru ndio Syria na kuingia Kanaani akakuta Makabila ya wakanani na Wafilisti.

Akakaa huko mpaka njaa ilipoingia Kanaani.



Akaondoka yeye na familia yake tena kuelekea Kusini kabisa ambapo angepita Jordan akielekea Misri, kemet ambapo hapakuwa na njaa.



Uzuri wa Sarah ukampa hofu Ibrahimu, akahisi wamisri wangemuua na kumchukua Mkewe. Akadanganya kuwa Sarah sio mkewe Bali Dadaake. Baadaye ikafahamika aliongopa, Fatao akampa Mali Kama dhahabu, Fedha, Shaba na Mali nyingi mno. Ibrahimu akaondoka Misri kurudi Kanaani akiwa na UTAJIRI wa kutosha.



Maisha mapya ya Kanaani yalianza, Abraham akiwa na Utajiri alioupata Misri.

Mali na hapa ni mifugo ilipoongezeka mgogoro ukazuka baina ya watumishi wake na watumishi wa Lutu mwanaye(mtoto wa Haran nduguye).



Abraham akatengana na Lutu akimuambia achagua upande wa kuelekea. Lutu akachagua Kusini lilipo bonde la sodoma na Gomora lenye rutuba, bonde Hilo lilikuwa na mifumo ya umwagiliaji kutokana na mto Jordan. Sodoma na Gomora ipo nchi ya Jordan hivi leo.



Abraham akanunua ardhi na kuifanyia kazi zake. Sasa alihitaji watoto lakini wapi angewapata ikiwa mke wake alikuwa Tasa. Kwa nasibu, Sarah akamruhusu Ibrahim amuingilia Kijakazi wake aitwaye Hajiri ambaye ni Mmisri, waliyempata kipindi walipoenda Misri siku zile njaa ilipopiga nchi.

Akazaliwa Ishmael, ndio Baba wa waishmael ambao walikuwa mashuhuri Kwa kutembea na misafara jangwani ya biashara.



Baadaye Isaka akazaliwa, akatafutiwa Mke kutoka Harani kulekule alipofia Tera walipo watu wa damu Yao, ndugu zao ukoo wa Labani.

Mkewe ndiye Rebeka.

Isaka akamzaa Yakobo ndiye Israel, na Esau ndiye Edomu.



Hivyo Yakobo ndiye Baba wa Taifa la Israel kupitia watoto wake kumi na mbili ambao waliunda Makabila kumi na mbili.



Esau ndio Baba wa taifa la Waedomu ambao baadaye waliwasumbua Sana waisrael wakitokea Misri.



Yakobo akakaa Kanaani na wakeze, na watoto wake. Mpaka njaa ilipoingia Kanaani.

Hapo wakaenda Misri Kwa ufadhili wa Ndugu yak aitwaye Yusufu, mtoto wa Raheli mkewe Yakobo.



Huko wakakaa mpaka alipozaliwa Amram Baba yake na Musa kupitia mkewe aitwaye Yokobedi.

Nduguze Musa ni pamoja na Miriam mtoto wa Kwanza, Musa, nawa mwisho Haruni wote kutoka Kabila la Lawi.



Safari ya Abraham inaishia hapa.



Tutaendelea Part 3

Isemayo

SAFARI YA MUSA KUTOKA MISRI KWENDA KANAAN



Hizi zote ni Zionism Movements ambazo ni kizamani.

Tutafika mpaka Zionism movement under Theodore, Balfour, mpaka kuanzishwa Kwa nchi ya Israel mnamo 4May 1948.



Robert Heriel

Taikon wa Fasihi

0693322300
 
Safi sn mkuu,Unai summarise vizuri sn na inaeleweka .Najiona km nasoma Bibila iliyokuwa summarised

Ila mpaka hapa Nina maswali mawili kwako;
1.Ikiwa Tera alikuwa mwenyeji wa Iraq ya sasa it means kwamba alikuwa mwarabu,kama sivyo naomba unielezee vizuri chimbuko la race ya waarabu,waturuki na hawa waisrael ,na mtiririko wa kizazi vyao Hadi kutokea taifa la Israel ya sasa ambao siyo waarabu
NB:kuna Stori nyingi huku mtaani zinasema waisrael asilia ni weusi,wengine wameenda mbali zaidi na Kusema Yesu alikuwa mweusi pia

2.Umesema Lutu alienda upande wa Sodoma na Gomorra,ni Sawa,ndivyo Biblia inavyosema pia.Lakini Kwa location ya eneo ilipo Sodoma na Gomorra ya sasaambayo wewe umeitaja km nchi ya Jordan ni tofauti na maandiko mengine ya historia niliyosoma yanayosema kwamba mabaki ya mke wa lutu aliyegeuka sanamu la jiwe la chumvi baada ya kugeuka nyuma yanapatikana eneo la Iraq..hebu fafanua kidogo hapa mkuu
 
Agano La Mungu Na Abramu

1Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono:

“Usiogope, Abramu.

Mimi ni ngao yako,

na thawabu yako kubwa sana.”

2Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?” 3Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”

4Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.” 5Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”

6Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.

7Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”

8Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”

9Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”

10Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili. 11Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.

12Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake. 13Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne. 14Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi. 15Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema. 16Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”

17Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama. 18Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati, 19yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni, 20Wahiti, Waperizi, Warefai, 21Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
 
Umechanganya madesa.

Tafuta tofauti ya Jericho na Yordan.

YERIKO ndiko ambako Kuna Dead see.
Kuna sanamu ya chumvi ya mke Wa Rutu.
 
Back
Top Bottom