Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

Cosovo

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2018
Posts
667
Reaction score
1,810
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika. Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti.

Wote wanatokea familia masikini ila familia ya mwanamke ina ahueni kidogo maana wazazi wake wanaishi nyumba ya kudumu ingawa ni ya zamani na imechakaa ila kwa mwanaume wazazi wake wanaishi nyumba za tembe na makuti.

Wote walikopa hela bank kama million 25 kwa kutaka angalau wawajengee wazazi na wakakubaliana kuanza kuwajengea wazazi wa mwanaume. Baada ya hela kuingia mwanamke amegoma kutoa hela anataka awajengee wazazi wake kwanza maana wamesumbuka kumsomesha.

Mwanaume anakataa anasema makubaliano yaheshimiwe lakini mwanamke anakataa. Baadae mwanaume akapendekeza basi hiyo hela wanunue kiwanja wajenge nyumba yao, mwanamke akasema sawa wewe kama mwanaume nunua kiwanja mimi nitajenga msingi wa nyumba panapobaki umalizie hela yangu inayobaki niwajengee wazazi maana wamenitoa mbali.

Mwishowe mwanamke akasema hivi ungenioa bila kazi ungesema hayo unayotaka nifanye, wewe kama mwanaume wajibika kuwajengea wazazi wako, kisha jenga nyumba yetu na mimi niwajengee wazazi wangu.

Jamaaa anawaza sana anatishia kuvunja ndoa, nini kifanyike? NB, Jamaa ana umri wa miaka 36 hivi mke wake miaka 27

1626759720275.png
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti
Ubinafsi kwenye ndoa ni janga linaloangamiza. Hapo hawawezi kuongea lugha moja tena, ni heri busara ikatumika.
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti
Unachukuaje pesa ya mwanamke na kwenda kujenga nyumbani kwenu?[emoji848]

Kesho akikudharau?
 
Mimi nafikiri wote wawili mawazo yao ni tofauti na kila mmoja ana mtazamo wake. Hii ndoa hata mgogoro huo utaisha lakini mbeleni sioni uhai wake, namshauri mwanaume afanye kazi kwa kujituma sana tena sana aelewe jukumu lake kubwa na kinachosababisha anafanya kazi kwa nguvu na maarifa ni familia yake pamoja na wazazi wake.

Inatakiwa ajibike kujenga nyumba yao na wazazi wake, pili nyumba atakayojenga asikubali mwanamke kuchangia hata cent yeyote na uwanja/nyumba iandikwe jina la mtoto ili kuepusha sintofahamu ya mbeleni.
 
Mimi nafikiri wote wawili mawazo yao ni tofauti na kila mmoja ana mtazamo wake. Hii ndoa hata mgogoro huo utaisha lakini mbeleni sioni uhai wake, namshauri mwanaume afanye kazi kwa kujituma sana tena sana aelewe jukumu lake kubwa na kinachosababisha anafanya kazi kwa nguvu na maarifa ni familia yake pamoja na wazazi wake. Inatakiwa ajibike kujenga nyumba yao na wazazi wake, pili nyumba atakayojenga asikubali mwanamke kuchangia hata cent yeyote na uwanja/nyumba iandikwe jina la mtoto ili kuepusha sintofahamu ya mbeleni
Nyumba iandikwe jina la mwanaume kwa sababu tayari kuna mgogoro. Then kila kitu cha familia akiongoze mwanaume tu.

Hii ndiyo shida ya kuoa mke mnayelingana kipato[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Huo ni upumbavu unaoa ili mwanamke akusaidie kwenye mambo yako simply kila mtu kasomeshwa kama vipi kila mmoja ajenge kwao kwa hela yake mbona simple, et anatishia kuvunja ndoa ni upimbi huo, Miaka 36 unasubiri uoe ndo ujenge kwa mshahara wa mkeo au ujenge kwa mkopo nyumba ya wazazi na yako utajenga vipi.
 
Mke ana point. Kila mtu awajibike kwa wazazi wake. Binafsi wala siwezi mwomba mume wangu ajengee wazazi wangu.Ugomvi mwingine wakujitakia.
Sasa kama ndivyo ule uhalisia wa ndoa uko wapi wa kuwa mwili mmoja?
 
Mwanaume mjinga sana. Mwanaume Ana wajibu wa kutunza familia yake. Mke wangu sijawahi kumuuliza mshahara wake.
Natoa pesa ya kila kitu na kukamilisha majukumu yote Kama baba.

Pesa yake Kama akiamua kuileta kwenye familia sawa. Akiamua kuwapa ndugu zake atajijua mwenyewe. Lakini hatakiwi kuniuliza pesa ya kuhonga natoa wapi? Na hatakiwi kujua mapato yangu yote. Hayamuhusu
 
Kumbe ni makosa
Kwa macho ya kawaida siyo kosa, ila ukishaingia kwenye ndoa na bahati mbaya mmoja akawa mbinafsi basi KIPATO KULINGANA inakuwa kosa. Imagine mume angekuwa na kipato Mara tatu zaidi ya mke wake, ni wazi kwamba mwanamke angekubaliana na mpango wa kuwajengea wote kirahisi sana ila kwakuwa anajua wote wako sawa so Kila mtu anaamua anachotaka[emoji847]
 
Mimi nafikiri wote wawili mawazo yao ni tofauti na kila mmoja ana mtazamo wake. Hii ndoa hata mgogoro huo utaisha lakini mbeleni sioni uhai wake, namshauri mwanaume afanye kazi kwa kujituma sana tena sana aelewe jukumu lake kubwa na kinachosababisha anafanya kazi kwa nguvu na maarifa ni familia yake pamoja na wazazi wake. Inatakiwa ajibike kujenga nyumba yao na wazazi wake, pili nyumba atakayojenga asikubali mwanamke kuchangia hata cent yeyote na uwanja/nyumba iandikwe jina la mtoto ili kuepusha sintofahamu ya mbeleni
Sio mbaya kwa nyumba yao wakachangia ila kulazimishana et achukue mkopo mkajengee wazazi wako ni non sense
 
Mwanaume mjinga Sana.
Mwanaume Ana wajibu wa kutunza familia yake.
Mke wangu sijawahi kumuuliza mshahara wake.
Natoa pesa ya kila kitu na kukamilisha majukumu yote Kama baba.
Pesa yake Kama akiamua kuileta kwenye familia sawa. Akiamua kuwapa ndugu zake atajijua mwenyewe.
Lakini hatakiwi kuniuliza pesa ya kuhonga natoa wapi?
Na hatakiwi kujua mapato yangu yote. Hayamuhusu
Je na kama ukigundua hela yake anamhonga ex wake wa chuoni unafanyaje?
 
Tunajua ni wewe na unataka tusaport ujinga wako ila nikwambie tu hicho kitu unachokifanya ni mambo ya wavulana na sio wanaume,na kama ulioa mfanyakazi ili akufaidishe umeula wa chuya
Siyo mimi ila nipo upande wa mwanaume, maana mpaka wanakubaliana walikubali kuchangiana ili kutatua matatizo madogo madogo na makubwa, pia kuoana watumishi ni kuondoa utegemezi, inakuwaje hela ya mwanamke ni ya mwanamke ila ya wanaume ni ya woteee?
 
Siyo mimi ila nipo upande wa mwanaume, maana mpaka wanakubaliana walikubali kuchangiana ili kutatua matatizo madogo madogo na makubwa ,pia kuoana watumishi ni kuondoa utegemezi ,inakuwaje hela ya mwanamke ni ya mwanamke ila ya wanaume ni ya woteee?
Sio wa kwanza kutokea kwenye familia maskini, sema hana akili.
 
Back
Top Bottom