Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

Mnakimbilia kuoa mwisho mnaishia kwenye matatizo kama haya.. Mimi kaka angu wa kwanza baada ya kupata kazi aliwajengea kwanza wazazi nyumba na kuwapa usafiri wa gari dogo na miradi ya ufugaji kisha akaoa.
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti
 
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]pesa ya kuhonga[emoji119]
Mwanaume mjinga Sana.
Mwanaume Ana wajibu wa kutunza familia yake.
Mke wangu sijawahi kumuuliza mshahara wake.
Natoa pesa ya kila kitu na kukamilisha majukumu yote Kama baba.
Pesa yake Kama akiamua kuileta kwenye familia sawa. Akiamua kuwapa ndugu zake atajijua mwenyewe.
Lakini hatakiwi kuniuliza pesa ya kuhonga natoa wapi?
Na hatakiwi kujua mapato yangu yote. Hayamuhusu
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti

Wote wanatokea familia masikini ila familia ya mwanamke ina ahueni kidogo maana wazazi wake wanaishi nyumba ya kudumu ingawa ni ya zamani na
Wewe ndo umekosea na umefanya jambo baya sana kumlazimisha mkeo pesa zake akajenga kwenu.

.pengine alikubali ili usimuone hawapendi wazazi wako.

Au pengine alikubali kwa wakati huo pengine mlikuwa mnaishi vizuri lakini anaona umebadilika.
Au alikubali huwezi kujua alikuwa yupo katika mood gani.

Mkuu acha hiyo kitu ya kwwmba pesa ya mkeo ukajenge kwenu.

Mbona wewe hutaki pesa yako akajenge kwao ?

Kinachokufanya ukatae wewe kumjengea wazazi wake kwa pesa hiyo ni kipi ?

Acha ubinafsi mkuu,huo ni utoto unafanya.Mali ya mke iwe ya mke,na mi ya mume iwe ni ya mume,kama hamfati msingi huu mtagombana kila siku kwa kujifanya mna share saaana.

Mali ina mipaka yake katika ndoa,jambo mkikubaliana ndio mfanye hilo,kama hamjakubiana usitake kutia uanaume wako tena.

Kwa taarifa yako hata kwa Mungu dhambi hapati hiyo mwanamke,kila mtu ana uchungu na wazazi wake anajua mwenyewe alivyolelewa.

Mali ya mke ibaki kuwa ya mke,na mali ya mume ibaki kuwa ya mume,mume jukumu lako kumhudumia mkeo.

Na mke hawajibiki kwa CHOCHOTE kukuhudumia wewe mume wala hawajibiki kuwahudumia watoto,iweje unataka kumuwajibisha kuwahudumia wazazi wako wewe ambae yeye hawajibiki kukuhudumia ?

Acha ushamba mkuu.
 
Inaonesha dhahiri huyu ni mwanamke mwenye kisirani na gubu
 
Mwanaume wajengee wazazi wako, ukisha maliza anza msingi wa nyumba yenu, mshahara wa mwanamke haukuhusu kabisa.. kama ataamua kujenga kwao ni makosa yako kuoa mke mbinafsi
Hapana sio mke mbinafsi mkuu.

Huyu mume akiamua kujenga kwaao basi na yeye aitwe mbinafsi pia kwa sababu hajjaanza kujenga kwa wazazi wa mwanamke.

Mkuu wanawake nao mishahara yao wana matumizi nayo,hata kama hawatumii anauwezo wa kusema sikupi chochote katika mali yangu na bado akawa hana tatizo.

Majukumu yote ya kugharamia familia ni ya mume.

Mwanamke hawajibiki kwa chochote juu ya wazazi wa mumewe zaidi ya kuwaheshimu na kutowatovukia adabu na kuwahudumia sio kuwagharamia
 
inakuwaje hela ya mwanamke ni ya mwanamke ila ya wanaume ni ya woteee?
mahari ulilipa wewe hhamkulipa wote kuonesha kwamba cha mwanamke ni chake na cha mume(kwa mipaka) ni cha wote.

Mkuu sio DINI WALA sheria za nchi hizi zote zimempa mume wajibu wa kumgharamia mkewe na watoto.

Ndio maana mume ukienda kulalamika serikalini kwamba mkeo halishi familia utaonekana mpuuzi tu.

Mume ndio mwenye majukumu katika ndoa,hiyo ndio asili mzee,msiwatwishe wanawake mizigo isiyowahusu
 
Hapa ndio nimeanza kuamini la saba ndio waifu matirio na si graduates wala waajiriwa ona sasa hawa wenzetu wanagombania mkopo utadhani umeingia kwenye akaunti ya ndoa na wote watawajibika kulipa benki.
Kama ni wewe mtoa uzi, nashauri tafuta pesa na usitegemee ya mwanamke hata kidogo.
 
Sijui jamaa ako aliwaza nini kukubaliana na mkewe kuwa washirikiane kuwajengea wazazi wao.
Kuhusu kushirikiana kujenga nyumba yao si shida ila za wazazi jamaa aliyumba kinoma wala hakutakiwa kumahirikisha kuhusu yeye kuwajengea wazazi wake kafanya upuuzi hapo. Na kinachoonekana hawaaminiani hao watu.

Jamaa angejitutumua ajenge kwao na ikiwezekana asaidie na kujenga ukwenii dadadeki sio kulia lia ujengewe na mkeo.
Kwa mimi naamini majukumu yote ya nyumbani ni ya mume, mke anipe heshima na upendo nizidi kuzisaka asiponiheshimu sitasita kuachana nae.

Hiyo ndoa sijui kama itadumu.
 
Kwanza hii habari haina ukweli kuna mambo yamerukwa hapa.Mara wakajenge kwao mwanaume Mara wajenge kwa wakwe ,Mara wajenge nyumba yao.

Kweli MTU aliye ajiliwa anaanzaje kujenga ukweni kabla hajajenga nyumba yake-huku hiyo hela uliyokopa utakatwa zaidi ya miaka 2.
 
Sijui jamaa ako aliwaza nini kukubaliana na mkewe kuwa washirikiane kuwajengea wazazi wao.
Kuhusu kushirikiana kujenga nyumba yao si shida ila za wazazi jamaa aliyumba kinoma wala hakutakiwa kumahirikisha kuhusu yeye kuwajengea wazazi wake kafanya upuuzi hapo. Na kinachoonekana hawaaminiani hao watu.

Jamaa angejitutumua ajenge kwao na ikiwezekana asaidie na kujenga ukwenii dadadeki sio kulia lia ujengewe na mkeo.
Kwa mimi naamini majukumu yote ya nyumbani ni ya mume, mke anipe heshima na upendo nizidi kuzisaka asiponiheshimu sitasita kuachana nae.

Hiyo ndoa sijui kama haitadumu.
Ndio matatizo ya kujifanya unampenda MTU kumbe unaharibu,sio kila kitu cha kumwambia Mwanamke.
Wanawake 99% ni wabinafsi tofauti kabisa na wanaume,hawezi kukubali umjengee mzazi wako kabla ya wa kwake.
 
Kwanza hii habari haina ukweli kuna mambo yamerukwa hapa.Mara wakajenge kwao mwanaume Mara wajenge kwa wakwe ,Mara wajenge nyumba yao.

Kweli MTU aliye ajiliwa anaanzaje kujenga ukweni kabla hajajenga nyumba yake-huku hiyo hela uliyokopa utakatwa zaidi ya miaka 2.
Kabla ya kuchukua mkopo walikubaliana wakichukua waanze kuwajengea wazazi wa mwanaume maana wanaishi kwenye nyumba za ajabu huko kijijini,baada ya kuchukua mwamke akachenji mara baada ya hela kuingia kwa account, akaanza kudai awajengee wazazi wake maana ndo walimsomesha

Na utaanzaje kujenga nyumba yenu na wazazi wanalala kwenye makuti huko kijijini na nyie mmepanga mjini mnaishi angalau nyumba nzuri?
 
Ndio matatizo ya kujifanya unampenda MTU kumbe unaharibu,sio kila kitu cha kumwambia Mwanamke.
Wanawake 99% ni wabinafsi tofauti kabisa na wanaume,hawezi kukubali umjengee mzazi wako kabla ya wa kwake.
Yaah kabisa mkuu, sijui jamaa aliwaza nini, ina maana hakua na mpango wa kuwasaidia wazazi wake bila usaidizi kweli.??
 
mahari ulilipa wewe hhamkulipa wote kuonesha kwamba cha mwanamke ni chake na cha mume(kwa mipaka) ni cha wote.

Mkuu sio DINI WALA sheria za nchi hizi zote zimempa mume wajibu wa kumgharamia mkewe na watoto.

Ndio maana mume ukienda kulalamika serikalini kwamba mkeo halishi familia utaonekana mpuuzi tu.

Mume ndio mwenye majukumu katika ndoa,hiyo ndio asili mzee,msiwatwishe wanawake mizigo isiyowahusu
Samahani kama nitakuwa nimevuka mstari, kwa maoni yako, ni wazi hauko kwenye taasisi hii ya ndoa na huielewi vizuri inapoanzia na inapoishia.

Mahari ikishalipwa, kwa mila nyingi za kibantu, nyumbani kwa mwanamke ni kwa mume wake, na nyumbani kwa mume ni kwake na kwa wazazi wake.

Hii inadhihirishwa pia ule utaratibu uliokuwepo/uliopo wa mwanamke kutumia ubini w mume na watoto kutumia ubini wa baba. Wimbo maarufu ukisema , "ayaya kuolewa, kurudi nyumbani kutembea..."

Ukisema dini, hizi mbili, zinataja majukumu ya mwanamke kwenye ndoa na mwanaume kwenye ndoa, sijui unazungumziaje hapa?

Ukirudi kwenye sheria za nchi, zinasisitiza majikumu ya mwanaume yaliyoainisha kwenye dini, na sheria inasisitiza kuwa mali zote zilizochumwa kwenye ndoa ni za wanandoa wote wawili, hili likidhaniwa mwenye nafasi ya kutengeneza hizo mali ni mwanaume zaidi kuliko mwanamke.

Ukiachana na dini ambayo kimsingi inapinga mwanamke kutafuta na kumpa jukumu la kwanza na la msingi ambalo siku hizi amekabidhiwa beki tatu, sheria itaamuaje ikiwa mwanaume akawajengea wazazi wake ikiwa tayari kuna ndoa na mwanamke akijenga kwao ikiwa yuko ndoani endapo mmoja kati yao akaaga dunia? Nyumba hizo zitajumuishwa kwenye mirathi endapo aliyebaki akidai?

Mara nyingi, demokrasia ikishindikana kwenye ndoa, mfumo dume unashika hatamu na hakuna wa kupinga, ndio sababu ya BABA kuwa kichwa cha familia, hakuna kichwa kilicho juu ya mwili wa kiume kikawa na mawazo yasiyo na jinsia.

Asante.
 
Back
Top Bottom