Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

Mgogoro wa ndoa: Tuanze kuwajengea nyumba wazazi wa nani?

wazi hauko kwenye taasisi hii ya ndoa na huielewi vizuri inapoanzia na inapoishia.
Mkuu pengine mimi naifahamu ndoa vizuri kuliko hata mzee wako(sio wewe tu)
Mahari ikishalipwa, kwa mila nyingi za kibantu, nyumbani kwa mwanamke ni kwa mume wake, na nyumbani kwa mume ni kwake na kwa wazazi wake.
Naaaam anakokaa mume ndipo hapo atakapokaa mke,hiyo ni nyumbani kwake kwa mujibu wa kuishi na sio kwa mujibu wa kumiliki.

Mke wangu nyumba yangu mimi ndio nyumbani kwake kwa sababu ndo anatakiwa aishi hapo,na sio ni nyumbani kwake kwa maana ya kuwa anaimiliki ile nyumba naye ni yake hapana.

Hivyo neno "NYMBANI KWAKE" hutakiwi kiingia kichwa kichwa mkuu.
Hii inadhihirishwa pia ule utaratibu uliokuwepo/uliopo wa mwanamke kutumia ubini w mume na watoto kutumia ubini wa baba. Wimbo maarufu ukisema , "ayaya kuolewa, kurudi nyumbani kutembea..."
Hayo ni mambo ambayo hayahukumu juu ya kuwa mali ya mke ati mume aichukue bila ridhaa ya mke mwenyewe.

Yaani kuhalalika kwa baadhi ya mambo kwenye ndoa sio kwamba yamehalalika mambo mengine yote.

Mambo ya jina yatabaki kuwa jina,na mambo ya mali yatabaki kuwa mali,hakuna mahusiano hapo ati useme kwa kuwa kwenye jina mke ananasibishwa na mume basi na mali ya mke ni ya mume pia,hii haipo kabisa.

Utaratibu wa wapi wa ajabu namna hii.
Ukisema dini, hizi mbili, zinataja majukumu ya mwanamke kwenye ndoa na mwanaume kwenye ndoa, sijui unazungumziaje hapa?
Nazungumzia kama mwqnzo kwamba mali ya mwanamke ni ya mwanamke na mali ya mwanaume ni ya mwanaume maadamu bado mupo kwenye ndoa.

Tofautisha mambo haya.

Mali ya wanandoa wakati wanaachana.

Mali ya wanandoa endapo mmoja wao akifa.

Na mali ya wanandoa wakati wapo pamoja.


sheria inasisitiza kuwa mali zote zilizochumwa kwenye ndoa ni za wanandoa wote wawil
Hapa nimekupa mambo matatu mkuu.

1.mali za wanandoa endapo wakiwa pamoja.

2.mali hizo endapo mmoja akifa.

3.mali hizo wanapokuwa wapo katika ndoa.

Hakuna uhalali aw mwanamke kujichukulia mali ya mumewe atumie anavyotaka ilhi bado wapo katika ndoa hawajaachana.

Maadamu mtu hajaachana na mumewe basi mwanamke hana uhuru wa kusema hii mali yetu sote acha niifuje no no.

Na mwanaume pia huwezi kusema huu mshahara ni wa mke wangu acha niufuje tuu nifanyie mambo yangu,hiyo haiwezekani.

Ndio maana kama mfanyakazi hatoi huduma kwa watoto mke akienda kushtaki yule mume atakatwa kiasi fulani cha pesa cha kuwatosha watoto na mke then ingine anaachiwa mwenyewe.

Sio kwamba mume atakatwa pesa yote no no..
Nyumba hizo zitajumuishwa kwenye mirathi endapo aliyebaki akidai?
Maadamu umeuliza kisheria basi mimi sio mtaalamu wa sheria hizi za NCHI SIJUI zinasemaje.

Lakini hata katika sheria ya dini iko hivi..

Ikiwa mume au mke alishasema bayana wakati wa uhai wake kwamba hiyo nyumba sio yake kwamba kamjengea mtu fulani manake ameshaitoa mali hiyo katika milki yake wakati yupo hai kabla hajafa,hivyo hata akifa hiyo haiingii katika mirathi kwa sababu sio yake alishakwisha igawa.

Ni sawa na wewe umpe mtu zawadi ya gari leo alafu baada ya miaka 5 Mungu akuchukue eti watu watake kurudisha hii gari uliyogawa nayo waitie kwenye mirathi wakati ishampa mtu.

Katika uislamu nafahamu iko hivyo na Mola ndio mjuzi zaidi.
mfumo dume unashika hatamu na hakuna wa kupinga,
Mfumo dume ni jina baya lenye kutia chuki ambalo lina malengo ya kuleta usawa baina ya mwanamke na mwanaume usawa ambao haupo kiufupi.

Lazima kila sehemu awepo mtu ambaye atamzidi mwenziwe kikauli na mamlaka hivyo maisha ndo yanaenda vizuri.

Asante
 
Mkuu pengine mimi naifahamu ndoa vizuri kuliko hata mzee wako(sio wewe tu)
Nadhani ni mwandishi mzuri tu bila kujali kama una hoja ya msingi au la!

Ulipoamua kuiandika sentensi hiyo, ndipo ninapoishia mimi kwakuwa kufikia hapo unatabirika na sitajisikia vyema kukutana na huo upande wako.

Kila la kheri mkuu.
 
Nadhani ni mwandishi mzuri tu bila kujali kama una hoja ya msingi au la!

Ulipoamua kuiandika sentensi hiyo, ndipo ninapoishia mimi kwakuwa kufikia hapo unatabirika na sitajisikia vyema kukutana na huo upande wako.

Kila la kheri mkuu.
Kauli yangu hiyo nilikuwa naijibu kauli yako hii hapa chini....👇👇👇👇
ni wazi hauko kwenye taasisi hii ya ndoa na huielewi vizuri inapoanzia na inapoishia
Kwa bahati mbaya sana kauli yako hii mbovu hukuiona lakini tumeivumilia.

Nawe uwe na kila la kheri.
 
25m mbona wakiendelea kubishana wataila.Wasisahau wana mda mchache kabla ya kustaafu, wajenge ya kwao wazaz badae wawajenge rum 2 za kulala na sebule simple house kwa bajet ndogo
 
Mwanaume wajengee wazazi wako, ukisha maliza anza msingi wa nyumba yenu, mshahara wa mwanamke haukuhusu kabisa.. kama ataamua kujenga kwao ni makosa yako kuoa mke mbinafsi
Ubinafsi wa mke uko wapi hapo? Yaani wazazi wahangaike kunisomesha, nipate kazi then nishindwe kuwatunza kweli? Mwanamke kuolewa haimaanishi tukitaka kuhudumia wazazi wetu mpaka ruhusa ya mume. Kama mke ana kipato unampa hubby taarifa tu kwamba nafanya 1,2,3 basi, ili ajue kinachoendelea. Na yeye ana haki ya kufanya hivyo, siyo mpaka ruhusa ya mke. As long as mahitaji yetu kama familia tunatimiza, mf chakula, ada za watoto, etc
 
Wajenge nyumba yao coz mpaka waje wamalize kuilipa hiyo milioni 25, tayari watakuwa wameshakua 'vijana wazee'.
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti

Wote wanatokea familia masikini ila familia ya mwanamke ina ahueni kidogo maana wazazi wake wanaishi nyumba ya kudumu ingawa ni ya zamani na imechakaa ila kwa mwanaume wazazi wake wanaishi nyumba za tembe na makuti

Wote walikopa hela bank kama million 25 kwa kutaka angalau wawajengee wazazi na wakakubaliana kuanza kuwajengea wazazi wa mwanaume

Baada ya hela kuingia mwanamke amegoma kutoa hela anataka awajengee wazazi wake kwanza maana wamesumbuka kumsomesha

Mwanaume anakataa anasema makubaliano yaheshimiwe lakini mwanamke anakataa

Baadae mwanaume akapendekeza basi hiyo hela wanunue kiwanja wajenge nyumba yao,mwanamke akasema sawa wew kama mwanaume nunua kiwanja mimi nitajenga msingi wa nyumba panapobaki umalizie hela yangu inayobaki niwajengee wazazi maana wamenitoa mbali

Mwishowe mwanamke akasema hivi ungenioa bila kazi ungesema hayo unayotaka nifanye,wew kama mwanaume ajibika kuwajengea wazazi wako,kisha jenga nyumba yetu na mimi niwajengee wazazi wangu

Jamaaa anawaza sana anatishia kuvunja ndoa ,nini kifanyike ?

NB, Jamaa ana umri wa miaka 36 hivi mke wake miaka 27

Akili mbovu za kuwaza kukopa na kuizika pesa, hio ndoa bora ivunjwe, they had little experience of each inapokuja kuongea na kubishana, pesa ndio imewapa uhalisia, utiifu na unyenyekevu hupimwa na pesa. Yake yake yangu yetu hii ni bora kuzaa na mwanamke nje nimlee akiwa nje niwe baba tu. Kuoa raha sana na huleta baraka kama ni ndoa iliobarikiwa.
 
Ngozi nyeusi tuko na shida sana, uninafsi tunaorithishwa tangu enzi za kale utatusumbua mno! Ndio maana hata mali hupotea haraka sana mara tu baba anapotangulia mbele za haki tofauti na wazungu na waarabu ni vigumu sana kufilisika hata baba anapokuwa katoweka hapa duniani.

Sisi ngozi nyeusi tumejawa na umimi mwingi mpaka unamwagika na ndio sababu hata wanandoa tulio wengi hatuaminiani. Unaweza kuta baba ana biashara zake anaziendesha anavyojua lakini mke wala watoto hawajui undani wa ni namna gani mzee anahangaika kuhakikisha maisha yanaenda, sasa itokee bahati mbaya mzee akatangulia mbele za haki, biashara ndio inakuwa mwisho wake maana hakuna anayejua undani wake.

Kwa wale waliowaamini wake zao nao huishia kulia vilio maana mke badala asimamie ipasavyo kwa faida ya familia unaweza kuta anakazana kuchota kwa kificho na kufanyia mambo yake binafsi. Ubnafsi unatutesa sana ngozi nyeusi
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti

Wote wanatokea familia masikini ila familia ya mwanamke ina ahueni kidogo maana wazazi wake wanaishi nyumba ya kudumu ingawa ni ya zamani na imechakaa ila kwa mwanaume wazazi wake wanaishi nyumba za tembe na makuti

Wote walikopa hela bank kama million 25 kwa kutaka angalau wawajengee wazazi na wakakubaliana kuanza kuwajengea wazazi wa mwanaume

Baada ya hela kuingia mwanamke amegoma kutoa hela anataka awajengee wazazi wake kwanza maana wamesumbuka kumsomesha

Mwanaume anakataa anasema makubaliano yaheshimiwe lakini mwanamke anakataa

Baadae mwanaume akapendekeza basi hiyo hela wanunue kiwanja wajenge nyumba yao,mwanamke akasema sawa wew kama mwanaume nunua kiwanja mimi nitajenga msingi wa nyumba panapobaki umalizie hela yangu inayobaki niwajengee wazazi maana wamenitoa mbali

Mwishowe mwanamke akasema hivi ungenioa bila kazi ungesema hayo unayotaka nifanye,wew kama mwanaume ajibika kuwajengea wazazi wako,kisha jenga nyumba yetu na mimi niwajengee wazazi wangu

Jamaaa anawaza sana anatishia kuvunja ndoa ,nini kifanyike ?

NB, Jamaa ana umri wa miaka 36 hivi mke wake miaka 27
Nasema kila siku, masuala ya kuchanganya kipato katika ndoa ndiyo sumu ya ndoa. Kila mtu na kipato chake na majukumu yake. Baba ahakikishe familia yake ina pahala pa kuweka ubavu. Ni kosa kumlazimisha mwanamke akachange ili kujenga nyumba ya kuishi wanandoa. Kwa mtizamo hii ndiyo maana tumedumu na ndoa zetu hadi uzeeni
 
Nadhani kuna pahala sijaelewa.

Jina lililokopa pesa ni la nani au pesa iliingia kwenye jina la akaunti ya nani?
 
Wanandoa wangejenga ya kwao kwanza maana maisha yapo tu ukitaka kila kitu jinsi unavyowaza utaishia kufanya maamuzi yasiyo na mipango, hatimaye hizo hela wamekopa benki zitaelekezwa kwingine halafu wakawa watu wa madeni mpaka mnaondoka duniani... hakuna maisha mengine mahali pengine tofauti na haya unayoishi hivyo ni vizuri kuzingatia ustawi wa Ndoa ambayo tayari mlikubaliana.
 
Huyu mwanamke tunampopoa bure tu mawe wala hahusiki nayo. Mwanaume mwenzetu ni box tupu, tena box haswaa!!!! Mwanaume unaanzaje kujadiliana na mkeo kuwajengea wazazi wako!? Tena ujenzi wenyewe ni wa wazazi wako! Haya ndio matatizo ya kujifanya unataka kila kitu mkopromaiz ndani kabla ya kufanya.

NB. Hakuna Ndoa iliyowahi kuendeshwa Kidemokrasia ikafanikiwa! Msiwaone mama zetu wako pamoja na familia zao ukadhani ilikuwa rahisi kama hivyo.
 
Kuna mke na mume wameanza mgogoro mkali ambao unatishia ndoa kuvunjika

Miaka miwili iliyopita walioana na sasa wana mtoto mmoja na wote ni waajiriwa wa serikali na wote wameanza kazi intake moja ila idara tofauti.
Huyu jamaa falaaaaa nini? Yani mwanamke anataka ampande kichwani...hapo wala hamna cha kuzungumza either mwanamke ana tii makubaliano ama anaondoka.

Wanawake wa kisasa wanataka harusi na mtoto wakishapata hivyo wewe unabakia kuwa nothing kwake.
 
Back
Top Bottom