Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Kwa harakati hizi za kuvuana magamba katika vyama kuna dalili ya kuibuka kwa muswada bunge lijalo kuhusu MGOMBEA BINAFSI 2015 au kuibuka kwa chama kingine cha siasa.

Via
habari kutoka kwa makala mbalimbali za waandishi wa magazeti yasiyo ya udaku.
 
Hakika Mungu asaidie Watanzania tufanikishe mchakato wa kuundwa kwa katiba mpya uende kwa amani na hatimae tupate katiba mpya kwa niaba ya Watanzania.

Moja ya kiu kubwa ni kuona katiba inatamka haki ya kikatiba ya Mtanzania kama haki ya kuchagua na kuchaguliwa inafanya kazi hasa kwenye kipengelee cha Kuchaguliwa.Manake kwenye kipengele hicho ndiko tutapata mgombea binafsi au mgombea huru asiye na chama chochote cha kisiasa.

Kwa sasa vyama vya kisiasa vimeibuka na aina ya udikteta wa aina yake ambao umekuwa ni mfumo kuwa pasipo aina fulani ya Itikadi ambayo siyo itikadi lasmi ya chama basi mfuasi wa chama hicho hana haki dhidi ya chama chake.Wenye sale za kichama wanajua jinsi kwa baadhi ya watu katika vyama vya kisiasa wamegubikwa na tamaa ya fedha,mitandao, utiifu kwa viongozi hata kwa mambo ya kipuuzi, usengenyaji, wivu, ulaghai, ukosefu wa nidhamu, maadili, kutokuwa na miiko ya chama, uchonganishi na mengineyo mengi ya kuchefua. Mambo hayo chini ya usimamizi wa baadhi ya watu yameguka kuwa ndio itikadi ya chama na malengo makuu ya chama na sio sera na itikadi lasmi kama ndio misingi ya kuendesha chama.

Hakika ombi langu ni ujio wa mchakato wa katiba mpya kwa kuwa huo ndio utakuwa mwalobaini wa vyama vya siasa,kwa kuwa tuendako dunia ya watu ambao Integrity [If you have integrity, you are honest and firm in your moral principles.] watakuwa na nafasi kubwa sana na heshima kubwa sana kwenye jamii kwa kuwa wako genuine na wanakubalika kwenye jamii.

Hivyo vyama vya kisiasa itavibidi vifuate itikadi zao lasmi ili viwe na mlengo halisi na kuibua changamoto,kuwa mwanachama wake au mfuasi wake au mkeleketwa wake ni lazima awe na itikadi ya chama chake kama ndio mwongozo wake.Hivyo kupitia ujio wa mgombea binafsi ni nafasi ya kutengeneza CONFLICT OF INTEREST kati ya vyama vya kisiasa na nafasi za watu ambao watakubalika kwenye jamii ambao au kwa namna fulani wameshindwa kufanana na haiba [Persoality] au falsafa ya vyama vyao kwa wakati huo husika, hivyo wanaamua kujitoa na kusimama kama wagombea binafsi.

Ndio kwa vyama vya siasa legelege na sio makini mfumo huo ni mwiba lakini kwa demokrasia na ujenzi wa vyama makini vyenye mlengo sahihi bado hilo la mgombea binafsi ni changamoto ndogo sana,kwani usemi ule wa kiswahili palipo na wengi hakialibiki kitu,au kidole kimoja hakivunji chawa,hivyo hofu na mashaka ya vifo vya vyama ni hadithi na utastawi na kutoa matunda mazuri kwa vyama ni ubarikio unaojisimamia kwa wazi kabisa.Tunaweza kuona kwenye Taifa kama Marekani kuna mgombea binafsi lakini daima mbio za kisiasa ndani ya Taifa hilo kubwa ni la vyama viwili vikuu navyo ni Democratic na Republican kama vile hakuna nafasi ya mgombea huru.

Tukitazama sasa gumzo la wabunge wa NCCR na CUF,wabunge hao tungekuwa na mgombea huru au binafsi hakika vyama vyao vingepata shida sana kwenye chaguzi ndogo.Lakini kwa kuwa mchakato huo wa mgombe huru hatuna basi vyama vinakuwa na vulumai na michezo kauzu kibao na ukosefu wa maadili kwa kuwa baadala ya chama kuwa ni jumuiko la watu wenye nia moja kupitia Itikadi lasmi na sera zao lasmi za chama husika inakuwa ni kusanyiko la kundi au vikundi vya watu wenye malengo binafsi na si malengo ya jumuiya kama chama.

Hakika palipo na heri na majaliwa wanajf tuliangalie hili la mgombea binafsi kama kitu cha msingi kitakacholeta mabolesho kwenye vyama vya kisiasa.Tunaweza kujifunza kupitia malumbano yanayoendelea sasa kati ya NCCR,CUF, Mahakama,Msajiliwa vyama Tendwa,Wananchi ambao ndio waajili wa Mbunge, Vyombo vya habari, Bunge na Serikali kwa upande wao.Ni changamoto nzuri na mpambano mzuri wa kukuza maitaji ya mfum huo wa mgombe binafsi.

Nawasilisha
 
Athari zaweza kuwa aidha hasi ama chanya. Katika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015 pamoja na mchakato wa katiba mpya, kuna vuguvugu kubwa la kupendekeza kuwepo na kipengele cha mgombea binafsi.
 
athari zake ni kuwa ndilo kaburi la ccm.
hakuna demokrasia ndani ya chama mfano ni kura za maoni.
mfano mwingine ni linapotokea suala lenye maslahi ya nchi mafisadi ndani ya chama huwabana wabunge kwa vitisho ili kulipitisha.
kwa hiyo ikipitishwa mgombea binafsi ccm itabaki kama mmasai na fimbo bila ngombe.
 
Uzuri wake ni kuwa, ile tabia ya wabunge kuitana usiku na kuweka msimamo wa kichama na atakaebisha kufukuzwa hautakuwepo. CCM itakufa, maana hakuna anaeipenda ila tu kwa sababu hupitia huko ili agombee na huhonga wanchama ili wamuunge mkono. Lowasa atahama maana akiwa humo hakubaliki. Viongozi watawajibika kwa wananchi zaidi kuliko kuabudu chama. Mwisho wa kutishana.
 
Dawa ni kuhakikisha tunaweka fursa ya mgombea binafsi ndani ya katiba mpya,hili litapunguza migogoro ndani ya vyama na hapo tutapata mawazo na msimamo halisi ya wanasiasa si sasa wanaongozwa na unafiki wa vyama.najua wenyeviti kama wakina mbowe,mbatia,lipumba na Dr hawapendi kuona hili linatokea kunusuru vyama vyao.wajue sisi watanzania tunataka mgombea binafsi,tumechoka ukiritimba wa kuishi kwa fikra za m/kiti
 
kwa mantiki hii hiki kipengele ni mbinde sana kuwekwa kwenye katiba mpya. Na ninavyoona kwa upande mmoja italeta heshima serikalini ila kwa upande mwingine inaweza kujenga kiburi kwa watawala kwa kuwa hawakupitia kwenye vyama. Ndani ya bunge pia patakuwa hapashikiki kutokana na kutunishiana kwa hoja na mabavu. Katika mfumo kama huo, spika atatakiwa kuwa mtu makini sana, mbabe na mtu mwenye maamuzi ya haraka na sahihi
 
Itasaidia hile kasumba ya mb kukitumikia chama na si wapiga kura wake(yani jimbo)
 
Mgombea binafsi atasaidia sana kupunguza matatizo mengi ya sasa lakini kuna tatizo moja litaendelea kutusumbua, kwa wale wabunge/madiwani ambao walipata ubunge kupitia chama fulani then anahama au kufukuzwa na kwenda chama kingine, kuna wabunge wengi ambao wanapata ubunge kwa mgongo wa chama kiasi kwamba km chama kikimfukuza hata wananchi wanakuwa hawamtaki tena lakini kutokana na ugombea binafsi mbunge yule ataendelea kuwa mbunge.

Nini kifanyike kuzuia hilo:

Mbunge ambae amepata ubunge wake kupitia chama then akataka kutumia mwanya wa ugombea binafsi kuhama basi wananchi tupata nafasi ya kuamua kwanza iwapo bado na sisi tunamtaka mbunge huyo? km hatumtaki basi uchaguzi mdogo na km tunamtaka basi aendelee.

CASE I:
ukiweka ushabiki wa vyama pembeni ni wazi kwamba wale madiwani wa arusha pamaoja na kwamba wamefukuzwa na chama ila hata wananchi hawawati tena,

CASE II:
pamoja na kwamba Kafulila kafukuzwa na chama ila ni wazi kuwa wananchi bado wanamtaka ndio maana viongozi wa NCCR walizomewa.

Hizo cases nilizozitoa zinatupa anagalizo la nn tunapaswa kukifanya kabla hatujaacha loophole nyingine kwenye huyu mgombea binafsi.

IKUMBUKWE chadema walivyowafukuza madiwani walipokelewa kwa shangwe na wananchi wa arusha kwa uamuzi wao kiasi kwamba madiwani wakataka waweke pingamizi mahakamani wasitajwe majina yao ktk mikutano lakini NCCR wanazomewa na wananchi kwa kitendo km cha chadema ambao wao walishangiliwa.
 
Kuna watu wananguvu sana ya pesa hapa nchini na biashara zao zinahusiana sana na serikali sasa kwa misimamo ya upinzani wenu watu hawa watawaangusha sana wapinzani na kuungana na ccm kama watatokea wagombea binafsi wenye pesa mtashindana nao?,

Au mnashabikia tuu bila kujua kitakachotokea, watanunuliwa wapiga kura mpaka wasimamizi na mawakala. Na pindi wafanyapo makosa cjuwi mtawawajibisha vp maana ni dhamana yao ni wapiga kura cy chama.
 
Wakuu,
Inategemea "Sheria ya Mgombea binafsi" itakayotungwa itasemaje! Unaweza kukuta Sheria ikazalisha hali mbaya kiasi kwamba watu wakawa hawana hamu kabisa na ugombea binafsi! In general terms however, ni better kupanua wigo wa demokrasia ili kuruhusu ugombea binafsi!
 
itaondoa udikteta wa vyama vya siasa kwa wabunge.....
pia itasaidia wabunge kuwatumikia wananchi na si vyama vyao....
 
Pengine ruzuku kwa vyama vya siasa ifutwe hapo problem hakuna. Na ndio itakuwa mwisho wa vyama vyengine vina survive kwa ruzuku.
 
Kuna watu wananguvu sana ya pesa hapa nchini na biashara zao zinahusiana sana na serikali sasa kwa misimamo ya upinzani wenu watu hawa watawaangusha sana wapinzani na kuungana na ccm kama watatokea wagombea binafsi wenye pesa mtashindana nao?, au mnashabikia tuu bila kujua kitakachotokea, watanunuliwa wapiga kura mpaka wasimamizi na mawakala. Na pindi wafanyapo makosa cjuwi mtawawajibisha vp maana ni dhamana yao ni wapiga kura cy chama.

mfano mtu kama bakhresa au Mengi leo waamue kujitosa ubunge si tutajua wana lao jambo? Kama alivyosema Buchanan, inategemea sheria itakayoambatana na ugombea binafsi.
 
wandugu tujaribu kuipa uzito hii hoja maana ndiko mchakato unatupeleka. Na hii fukuza fukuza ya wabunge na madiwani inaweza pata mwarobaini pamoja na kuepuka gharama mara mbili mbili
 
Can we have independent candidance in our elections
can we in east africa have that?
 
We really don't need independent candidates, they will be bribed for votes and they will be very much unstable and selfish they will not have any policies so they will be feeding their stomach as they will have no Ideas on what to stand for
 
Wadau

naomba mnipe usahihi kiuchambuzi kwa haya maneno yanayotumika katika mchakato wa katiba mpya

Je Tanzania tunataka mgombea HURU (Independent Candidate) au Mgombea Binafsi (Private Candidate)?


Mnisamehe kama imekaa kisiasa lakini tatizo langu ni kwenye LUGHA
 
Back
Top Bottom