CCM na serikali yao lazima wapinge hiyo interpretation. Sababu ni simple, strategy imekuwa hivyo tangu tupate uhuru. Otherwise isingekuwa inawezekana kwa mtu mmoja, asiyekuwa na elimu yoyote ya kutosha, lakini anayo kadi ya chama, anakuwa waziri wa wizara saba(7!) tofauti ktk muda wa karibu miaka 30!
Hii haitokei popote duniani zaidi ya Tanzania! Ukitafuta kwa nguvu sana, unaweza kuikuta North Korea, Cuba, Syria, n.k.
Kwa ufupi katiba yote ya JMT inahitaji kubadilishwa, kwani ndiyo imekuwa ikitudumaza kwenye maendeleo tangu tulipoanza. Kwa kutumia udikteta wawe, baba wa taifa alijilimbikizia madaraka yote mikononi mwake, akidhani kuwa atakuwa "effective" ktk kutimiza "ndoto" zake za ujamaa wa kiafrika.
Alisahau au hakujua mambo mengi ambayo ni muhimu na hayabadilishiki, miongoni mwao kuwa hatoishi milele, na pia hao wakoloni wamekamata mpini na yeye na wenzie wamekamata makali. Matokeo yake tunayavuna hadi leo.
Waziri anapopinga interpretation ya High Court, anasisitiza uwiano uliopo uendelee kuwapo ambapo CCM wanamiliki kila kitu, kila mtu, kila sheria, kila uamuzi, kila uchaguzi.
Idumu CCM!! Idumu CCM! Idumu CCM! Wadumu MAFISADI!!!