Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Akili Kichwani,
Sasa unaanza kueleweka kuwa ni mabavu tu ya serikali yatatumika kuzuia hoja ya mgombea binafsi kwa hiyo kizingiti cha mahakama kitakuwa kimerukwa lakini kumbuka serikali hiyo hiyo ilikuwa inasema ni ndoto kuwa na serikali ya mpito kule zanzibar kwa vile katiba nasisitiza tena katiba hairuhusu wala si sheria

tofauti na hila la mgombea binafsi katiba inaruhusu kwa mtazamo wako lipi kati ya serikali ya mseto zanzibar na mgombea binafsi lilihofiwa zaidi na serikali kuu obvious ni serikali ya mseto ambayo rais na makamu wake wa zanzibar watakuwa na impact kubwa kwa serikali kuu zaidi ya huyu mgombea binafsi
 
Mgombea binafsi aumiza vichwa vigogo: Raia Mwema

UAMUZI Mahakama kuruhusu kuwapo mgombea binafsi unaelezwa kuwa tishio na sasa unaangaliwa kwa jicho la karibu na wanasiasa na wafanyabiashara wanaoweza kuamua kuingia katika kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa, Raia Mwema limegundua.

Wakati Mahakama ikiamini hakuna sababu za msingi za kuzuia mgombea binafsi, wabunge waliozungumza na Raia Mwema, wanaamini kumchagua mgombea binafsi katika ubunge au urais ni kujimaliza na wengine wakisisitiza, kilio cha umma kutaka mgombea binafsi ni dalili za kufeli kwa vyama vya siasa vilivyopo nchini.

Wanaamini ni dalili za kufeli kwa vyama vya siasa vilivyopo kutokana na vyama hivyo kuzongwa na rushwa, ubabaishaji, uonevu na mizengwe isiyo na mantiki wala maslahi kwa Taifa.

Tayari wananchi mbalimbali wameanza kuwaangalia wanasiasa na wafanyabiashara kwamba sasa vyama vya siasa vitalazimika kuwa na nidhamu na kuacha kuwatisha kwa kuwa kuna nafasi ya watu kuingia katika siasa bila kupitia vyama.

Wanaotajwa kuwa uamuzi huo unazidi kuwapa nguvu ni pamoja na wanasiasa wa pande zote zinazovutana ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na hata ndani ya vyama vikuu vya upinzani, ambavyo vilikuwa vikiwatisha baadhi yao kwamba vitawatimua kabla ama wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Miongoni mwa wanasiasa wanaotajwa ni pamoja na Spika wa Bunge Samuel Sitta, Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, pamoja na wabunge wanaowaunga mkono wanasiasa hao.

Wengine wanaotajwa kuwa tishio wakiamua kugombea bila kupitia vyama ni pamoja na mawaziri wakuu wastaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba na Frederick Sumaye, ambao wote wanaelezwa kuwatisha wanasiasa wa sasa.

Kwa upande wa wafanyabiashara, wanaotajwa ni pamoja na Reginald Mengi, Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, ambaye amekuwa akisema kuwa mwanachama wa CCM huku baadhi ya viongozi wa chama hicho wakitaka kumhusisha na vyama vya upinzani.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ni mmoja wa wanasiasa wanaotajwa kuweza kuamua kuingia katika uchaguzi bila kupitia chama chochote kutokana na kuwapo misuguano kati yake na chama chake cha CHADEMA.

Akizungumzia uamuzi huo, Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, amesema: kesi bado na tatizo wagombea binafsi waje au la, tatizo mahakama inapata wapi power ya kuamua suala linalogusa mabadiliko ya Katiba. Mwenye mamlaka hayo ni Bunge.

Wabunge waliozungumzia uamuzi huo ni pamoja na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye alisema anaamini kuwa kilio cha baadhi ya Watanzania kutaka mgombea binafsi ni dalili za wazi za vyama vya siasa vilivyopo kutokuwa katika kiwango cha juu cha utendaji, kisichotiliwa shaka na wananchi.

Hata hivyo, kwa upande mwingine mbunge huyo anaeleza kuwa mgombea binafsi si suala linaloweza kuwa na mshindo mkubwa katika Bunge au Serikali.

Katika nchi ambazo mfumo wa katiba unaruhusu mgombea binafsi sijawahi kuona serious impact inayotokana na wagombea binafsi, kwamba robo tatu ya Bunge kwa mfano iwe ni wagombea binafsi.
Nadhani wakati mwingine kunakuwa na uwoga usio wa lazima kuhusu kuwapo kwa wagombea binafsi, lakini ukitazama zaidi suala hili nchini unaweza kujiuliza kwa nini kuwa na kilio kikubwa cha mgombea binafsi?

Jibu ni kwamba, kilio hicho ni dalili za wazi za kushindwa kwa mifumo ya vyama vya siasa nchini. Demand ya mgombea binafsi ni dalili ya udhaifu mkubwa wa mifumo ya uendeshaji vyama.
Unajua mfumo wetu ni wa demokrasia ya uwakilishi wa kibunge, mtu anachaguliwa kuwa mbunge kuwakilisha na anawajibika kwa chama anachotoka. Sasa unapochagua mgombea binafsi, ni kupotosha dhana ya uwakilishi kwa mfano, huyo mgombea akikaidi ahadi zake au kufanya masuala ya ovyo, mtamwajibisha vipi au mtakwenda kwa mkewe?

Kwa hiyo nasema mgombea binafsi si mfumo wa maana kwa kuwa hau-reflect real democratic value, kilio hiki kipo kwa kuwa tu vyama vya siasa vilivyopo vimezongwa na uonevu, ukosefu wa uwajibikaji, rushwa, na ubabaishaji.

Naye Mwenyekiti Mstaafu wa Umoja wa Wanawake wa CCM- UWT na Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Abdallah, akizungumzia mgombea binafsi anahoji: Kwa nini watu walitaka mfumo wa vyama vingi? Na huyo mgombea binafsi atakuwa na sera zipi?

Anasema; Mimi naona mfumo mzuri na wa kidemokrasia zaidi ni kuwa na wagombea kutoka vyama vya siasa, mgombea binafsi ni ubinafsi.

Chama ndiyo kinatoa ahadi na ni jukwaa zuri la kumwajibisha kiongozi wake kwa niaba ya wananchi. Mimi hadi sasa sielewi na akili ya kawaida ya kuzaliwa inakataa kabisa, huyu mgombea binafsi atasimamia nini, na akiamua kufanya mambo yake binafsi itakuwaje. Hili suala halina maana yoyote, anasema Anna Abdallah aliyepata kuwa Waziri katika wizara mbalimbali nchini.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia anasema; Kuchagua mgombea binafsi ni kujimaliza kabisa, nani atamsimamia huyu na hasa utekelezaji wa ahadi zake. Ninavyojua chama cha siasa ndiyo chenye sera na katiba.

Kuchagua mgombea binafsi ni sawa na kuchagua kiongozi asiye na mfumo rasmi wa kudhibiti nidhamu yake. Na zaidi hakuna forum ya kumuadabisha anapoonekana kuyumba katika utekelezaji wa ahadi au kimaadili,.

Naye Mbunge Ludovick Mwananzila anaamini kuwa Tanzania haina haja ya kuwa na mgombea binafsi kwa wakati huu, kwa kuwa mazingira halisi ya kisiasa yanakataa.

Anasema: Nadhani tunataka vitu ambavyo bado hatujawa tayari kwa kiwango cha kuridhisha. Kuna vyama vya siasa 19, hivi kweli kuna Watanzania wanaokosa hiari ya kugombea kupitia chama chochote kati ya hivyo?

Alipoulizwa kwamba suala la mgombea binafsi ni la kikatiba kwa kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasisitiza kuwa kila raia ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa, Mwananzila alisisitiza; Haki hiyo inalindwa hata katika mfumo usio wa mgombea binafsi, kuna hivyo vyama 19 nimekwambiasasa si kweli mtu anakosa haki ya kupiga na kupigiwa kura hapo.

Kwa upande wake, Mbunge Richard Ndassa anasema mgombea binafsi si suala la maana sana kwa nchi inayotaka kupiga hatua katika tafsiri pana ya kidemokrasia.

Alisema: Hili ni suala la kuminya demokrasia. Demokrasia nzuri zaidi ni ile ya kwanza kuchujwa na wenzako, kushirikiana na wenzako kuanzia kwenye chama na baadaye kwenye umma.

Alipoulizwa kama mgombea binafsi ni suala linaloweza kubomoa vyama vya siasa kikiwamo chama chake cha CCM, alisema; Si rahisi iwe hivyo. Wananchi watapenda chama chenye ilani, ili wakishindwa kufukuzana na mgombea asiyewajibika basi wanakigeukia chama ambacho kilimdhamini huyo mgombea.

Kati ya viongozi wa CCM wanaounga mkono mgombea binafsi ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa sasa, Pius Msekwa, ambaye wiki kadhaa baada ya mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Butiama, alizungumza na gazeti moja la kila siku akisema anaunga mkono mgombea binafsi kwa kuwa huko ni kumuenzi kwa vitendo, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye ingawa hakuamini kuwa mgombea binafsi ni demokrasia bora zaidi kuliko vyama vya siasa, lakini hakuona mantiki ya kuzuia suala hilo.

Suala la mgombea binafsi lilifikishwa mahakamani na Mwenyekiti wa Chama Cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, akitaka aruhusiwe na Mahakama kukubaliana na hoja zake na hivyo kutoa hukumu inayoruhusu.

Hata hivyo, Serikali imekuwa ikionyesha kutokukubaliana na suala hilo kwa kutumia mianya ya kisheria na kuamua kukataa rufaa na rufaa hiyo kusikilizwa na Majaji saba, wakiongozwa na Jaji Mkuu, Augustino Ramadhani.
 
Kwa mujibu wa mwanasheria aliyebobea inaruhusiwa kuiomba mahakama iharakishe (expedite) hili suala!
 
Companero.. hili suala litaisha kabla ya juni na uamuzi wa mahakama kuu utathibitishwa na mpira utarushiwa serikali pale watakapofungwa na muda.. nyie ngojeni tu..
 
pasco,
Hivi mkitazama na kutafakari kwa MAKINI kabisa mnaona kweli tunayo mihimili miwili tofauti ya BUNGE na SERIKALI? Marmo ni Mbunge lakini wakati huohuo ni Waziri wa serikali.

Kimsingi Bunge letu ni kama halipo ndio maana serikali inalitumia kama inavyotaka kupitisha mambo yake likiwemo hili la kuidhalilisha wazi MAHAKAMA.
 
AK,
Unaposema mahakama ni chombo dhaifu, una maana gani? Ninachofahamu ni kwamba ni mahakamani pekee ambapo hata JK anaweza kushtakiwa.
 
Akili Kichwani,
Elewa kwamba mgombea binafsi atakaposhinda atatafuta chama atakachoshirikiana nacho kuunda serikali hivyo hicho chama kitakuwa kinawajibika kama vile rais anatoka kwao kwa vile kimeshirikishwa kuiunda serikali. Kwa maana hiyo mgombea binafsi wakati wowote anafaa.

Marmo ni mwongo sana kwani uamuzi wa mgombea binafsi ni wa muda mrefu sana kiasi ambacho naamini mpaka sasa sheria zote zinazohusiana na uchaguzi pamoja na katiba vingekuwa tayari vilisharekebishwa.
 
AK,
Unaposema mahakama ni chombo dhaifu, una maana gani? Ninachofahamu ni kwamba ni mahakamani pekee ambapo hata JK anaweza kushtakiwa.

Theoretically, sawa kabisa na practically inawezekana ktk serikali zilizo timamu. Kwa Tz si tumeshindwa hata jinsi ya kumshitaki Lowasa, hata Mkapa! Naamini hata mtoto wa Kingunge haiwezekani. Hivi kesi ya ajali ya Chenge iko wapi?

Itakuwa Rais
 
nilishatangaza hapa kugombea moshi vijijini kama mgombea binafsi nitafanya hivyo wakati wa kuchukua fomu, nitaichukua tume ya uchaguzi, na hakuna wa kunizuia kwa kuwa mahakama imeshaamua huo mchakacho wa kubadilisha katiba watauleta wenyewe mahakamani pindi tutakapoanza kukurupushana

Go man go, no one can stop you
if you go, we will support you
 
Serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais (Bunge na Uratibu) Philip Marmo amesema hakutakuwa na mgombea binafsi kwa mwaka huu 2010.

Akiwa Bungeni ambako anaendelea kunguruma, alisema kuwa mchakato wa kubadili katiba ya nchi ni mkubwa, hivyo hata mahakama itakuwa tayari imeridhia kuwepo kwa mgombea binafsi, muda hautatosha kuibadili.

Bado demokrasia inaminywa Tanzania? tujadili
Katiba ya nchi haijakataza mgombea binafsi na ndiyo maana Mtikila alishinda kessi on the ground that sheria mama ni katiba na sheria ya uchaguzi na ya vyama vya siasa haziwezi kuwa zaidi ya sheria mama ambayo ni katiba. Nadhani inatakiwa umma na wabunge waichallenge serikali.

Na zaidi wanaweza kutumia EU na US maana yake wakikohoa tu unasikia JK na Serikali yake wamekubali kila kitu. Hakuna haja ya kunyima mgombea binafsi kwani hiyo ni kuwanyima Watanzania haki yao mama! Mbona finance bill ya uchaguzi imepita haraka?

Au kwa vile CCM walishaagiza magari mia mbili kupitia sources zao wanazojua wenyewe na wanajua wameshawapiga wengine bao ndiyo maana wakagandamizia mwaka huu bila kujua kuwa inaweza pia ikawageukia wao wenyewe na kwa muda huo utakuwa "too late" na itabidi watumie mabavu ya serikali yao kama walivyozoea!

Inatakiwa serikali itoe fund kwa vyama vyote "at equal rates" kwa ajili ya uchaguzi na siyo kwa chama chenye wabune wengi maana by the time ya uchaguzi nafasi zote za ubunge zitakuwa wazi!!!! wakifanya hivi itasaidia vyama vichanga na kukuza demokrasia!
 
Mzee Mwanakijiji,

Amekuwa mtoto mtukutu anataka kuingia chumba kilichoandikwa " entry restricted". Analilia wembe mpeni tu.

Actually kinachotakiwa ni kuweka utaratibu wa jinsi wagombea binafsi watakavyoshiriki basi hakuna masuali, hakuna kuvimbisha misuli hapo dhidi ya tamko hilo.

Tumsamehe, kwa alilotamka ila aelimishwe (tuition) juu ya madaraka ya mahakama na mipaka ya kazi yake yeye kama waziri.
 
Pengine naliangalia hili suala vibaya ila ninapata hisia kwamba ipo athari kubwa ya kufanya kazi ya aina moja kwa muda mrefu kama mtu hautakuwa smart. Hilo linaweza kusababisha mtu akaanza kufanya kazi kwa mazoea.
Kwenye hili baraza la sasa la mawaziri wapo baadhi yao wanafanya mambo kwa mazoea sana, na Marmo anisamehe, maana inawezekana akawa ni mmoja wao.
Kama nia yetu sote ni kuijenga nchi kwanini anaanza kupingana na mahakama? Anataka kutufundisha nini?

Kama serikali inaweza kila kitu iache kuchagua majaji na mahakimu, so that they could properly run the show.

Ipo siku kwa tabia hii mbaya ya kupenda kujikweza kutokana tu na madaraka ya umma ambayo ni dhamana, baadhi ya watu wanaweza kuumbuka vibaya kwa kuona yale waliyoyasimamia na kujiaminisha nayo si lolote na si chochote.

Naomba tuwe na hekima ya kujua kuwa utumishi mwema wenye kutukuka lazima uzingatie haki na sheria. Kitakachoweza kutustahi mbele ya safari ni tabia yetu njema, uadilifu na utumishi uliotuka. Tunayadharau hayo..but times change.

Mungu ibariki Tanzania
 
Akili Kichwani,
Mkuu, mgombea binafsi alihitajika tangu miaka mingi iliyopita.

Tatizo sio kuwa kukitokea tatizo litashughulikiwaje kwa kutolea mifano yanayotokea sasa. Tatizo ni kuwa, haki muhimu ya kikatiba inaminywa na utaratibu wa sasa. Haki ya kila mtu kuchagua na kuchaguliwa. Uamuzi wa mgombea kuchaguliwa na kushinda uchaguzi utabaki kwa wananchi.

Kama mgombea binafsi atapata kura za kutosha kushika kiti cha uongozi, naamini atakuwa na nidhamu kubwa katika utendaji wake kiasi ambacho matatizo mengi yaliyopo yataweza kuepukwa. Atahitaji uungwaji mkono wa wananchi wote, na atafuata mahitaji ya wananchi badala ya chama cha siasa ambacho kimemteua kugombea.

Vile vile, mgombea binafsi akishinda uchaguzi, ataweza kuunda serikali ya umoja wa kitaifa zaidi ya mgombea mwingine yeyote wa chama cha siasa.

Vitu hivyo viwili ni muhimu sana kwa Taifa letu muda huu na baadae. Hakuna haja ya kuogopa kufanya mambo mema. Tuogope kufanya yasiyo mema, kwakuwa yana madhara.

Tatizo lililopo kwa sasa ni nia thabiti ya wanasiasa kupigia kura kukubali kuwepo kwa mgombea binafsi. Sioni kuwa kuna chama kinachoweza kuunga mkono mabadiliko ya Katiba kuruhusu mgombea binafsi, kwakuwa wananchi wengi wenye uwezo, nia na madhumuni ya kugombea uongozi wataamua kugombea bila kufungwafungwa na masharti ya vyama.
 
HOJA YA MGOMBEA BINAFSI :Bomani aishangaa serikali

Asema baba wa taifa Mwalimu Nyerere alibariki hilo mwaka1995

Salim Said na Nora Damin

MWANASHERIA Mkuu wa Kwanza mzalendo nchini, Jaji Mark Bomani amesema serikali inakwamisha bila sababu suala la mgombea binafsi katika uchaguzi, ambalo licha ya kupata baraka za mahakama lilishapata baraka zote za baba wa taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Mbali na kuitaka serikali kuacha kigugumizi katika kuruhusu utekelezaji wa suala hilo; alikosoa mfumo wa sasa wa uchaguzi na uteuzi wa mawaziri na kupendekeza kwamba, siyo lazima waziri awe mbunge.

Suala hili lilifunguliwa kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa DP, Christopher Mtikila ambayo ilitoa hukumu mwaka 2006 iliyoruhusu kuwepo mgombea binafsi, lakini serikali imeendelea kuweka ngumu kwa kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kuomba hukumu hiyo ipitiwe upya.

Februari 8, mwaka huu Jaji Mkuu, Augustine Ramadhan aliahirisha kusikiliza rufaa hiyo baada ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu kutojiandaa vizuri hivyo kuomba isogezwe mbele.

Akiahirisha rufaa hiyo, Jaji Ramadhan alisema hukumu ya Mahakamu Kuu itaendelea kama ilivyo hadi hapo rufaa itakapopitiwa na jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa na kumlaumu Naibu Mwanasheria Mkuu kwa kutojiandaa kikamilifu wakati wao ndiyo walioomba ipitiwe upya.

Katika taarifa yake maalumu aliyoitoa kwa gazeti hili jana, Jaji Bomani alisema mfumo wa mgombea binafsi katika chaguzi sio haramu kwa kuwa umeshakubaliwa na wataalamu mbalimbali.

Kauli hiyo ya Jaji Bomani imekuja karibu majuma mawili tangu jopo la majaji saba wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuitaka serikali kuwa makini katika rufaa waliyoikata dhidi ya hukumu ya mahakama kuu kuwepo kwa mgombea binafsi.

Walisema endapo serikali italegalega katika rufaa yake dhidi ya hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, suala la kuruhusiwa mgombea binafsi katika uchaguzi mkuu ujao, liko palepale.

Jaji Bomani ambaye alishawahi kushiriki katika kamati mbalimbali za kutafiti mfumo sahihi wa uchaguzi unaofaa Tanzania, alitoa changamoto kwa Rais Jakaya Kikwete kuwa ndiye anayepaswa kusimamia suala hilo.

Alisema Rais Kikwete ana nguvu na nafasi ya kihistoria kutekeleza uamuzi huo wa mahakama kwa kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi mkuu ujao.

Jaji Bomani alisema hatua nzuri na muhimu ya kuanzia katika utekelezaji wa suala la mgombea binafsi na kuboresha mfumo wa uchaguzi Tanzania, ni kupitia upya ripoti ya Jaji Kisanga, jambo alilosema kuwa serikali haijachelewa.

"Ripoti ya Tume ya Jaji Francis Nyalali ni moja kati ya kamati kubwa zilizoundwa na kulifanyia kazi suala hilo na kupendekeza kuwepo mgombea binafsi na kazi hiyo ilifanyika 1991.

Tume ya Jaji Kisanga nayo ikafuata nyayo, pia ripoti ya tume ya Elkit, Bomani na Maina wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa nguvu zote ilipendekeza kuruhusiwa mgombea binafsi," alikumbusha Jaji Bomani katika taarifa hiyo na kuongeza:

"Hata marehemu baba wa taifa, mwalimu Nyerere kwa nguvu zote naye alisimamia hoja hiyo katika hotuba yake kwenye sherehe za sikuu ya wafanyakazi zilizofanyika mkoani Mbeya 1995 na mahakama za sheria mara kwa mara zimekuwa zikiamua kwa uwazi kuhusu hoja hiyo na zinasisitiza kwamba ni kinyume na katiba ya nchi kuizika hoja ya mgombea binafsi".

Jaji Bomani alisema woga na hoja zinazotolewa na wapinzani kuhusu nafasi ya mgombea binafsi hazina msingi.

Ingawa Jaji Bomani hakuitaja serikali, kauli hiyo inaonyesha kuwa anayoizungumzia hapa ni serikali kwa kuwa ndiyo inayoendelea kuipinga hoja hiyo hata baada ya mahakama kuruhusu.

"Hakuna ushahidi wowote wenye nguvu wa kuonyesha kwamba, kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi kunaweza kuleta vurugu katika uchaguzi," alisema Jaji Bomani.

Akitoa mifano ya mgombea binafsi duniani, Bomani alisema woga huo hauna maana kwani hata historia inaonyesha kuwa nchi nyingi ambazo zimeruhusu mfumo huo, hazikuwa na vurugu na hata walioshinda ni wachache.

"Mwaka 1997 katika uchaguzi wa Bunge la Uingereza ni mgombea mmoja tu binafsi aliyeshinda na katika uchaguzi urais wa Marekani mwaka 1992 bilionea Ross Perrot ambaye alikuwa mgombea binafsi alipata asilimia 19 tu ya kura," alisema Jaji Bomani na kubainisha kuwa siku zote wagombea binafsi wana kuwa na kazi kubwa ili kushinda.

Kuhusu mfumo wa uchaguzi, Bomani alipendekeza kuwa mfumo bora na wa kidemokrasia ambao utakidhi mahitaji ya Watanzania kuwa ni wa mseto utakaochanganya kura za uwiano na kura za majimbo.

Alipendekeza kuwa kuna umuhimu wa kupunguza idadi ya majimbo kama njia moja wapo ya kuanzisha mfumo wa uchaguzi wa kutumia kura za uwiano.

"Mathalan kuzuia kupunguza idadi ya majimbo yaliyopo hivi sasa, kuanzisha kura za uwiano kwa ongezeko lolote lile la wabunge 100 Tanzania Bara na kwa upande wa majimbo ya Zanzibar yanaweza kupunguzwa kwa viti 50 hadi 30 kwa viti 20 vilivyotolewa katika kura za uwiano (PR)," alisema Bomani na kuongeza:

"Kuzungumzia uongezaji wa idadi ya majimbo kwa sasa hakuna maana yoyote, ni sawa na kufanya kazi isiyo na tija. Kwa mfano, Marekani wana watu 300 milioni, lakini bungeni kwao kuna wabunge 425 na India yenye watu bilioni moja ina bunge la wabunge 600 tu."

Bomani alisema mfumo wa kura za majimbo (SMC) unaofuatwa na Tanzania hivi sasa si wa kidemokrasia, una gharama kubwa na unasababisha rushwa na ufisadi wakati wa uchaguzi.

Alisema katika mfumo wa kura za majimbo siku zote kunakuwa na tatizo la kulinganisha majimbo kulingana na idadi ya wapigakura, ambapo baadhi ya majimbo yana wapigakura wengi na mengine wachache.

Alisema uchaguzi wa kura za majimbo unahusiana sana na uchaguzi mdogo ambao ni wa gharama.

"Inakisiwa kuwa kila uchaguzi mdogo Tanzania inatumia zaidi ya Sh300,000,000,â alisema Bomani na kusisitiza:

"Lakini, mfumo wa kura za uwiano ni wa kidemokrasia zaidi, ni rahisi, usiohitaji gharama kubwa na hauna rushwa wala ufisadi".

Alifafanua kuwa mfumo mzuri wa uchaguzi Tanzania lazima utoe uwiano wa kiuwakilishi kati ya wanawake na wanaume bungeni kwa kutumia vyombo maalumu, uhusiano maalumu kati ya majimbo na uwakilishi na uweze kupunguza idadi ya chaguzi ndogo au kuondoa kabisa.

Kuhusu hoja ya iwapo waziri lazima awe mbunge au la Jaji Bomani alisema sio lazima waziri awe mbunge.

"Maoni yangu binafsi ni kwamba sio lazima waziri awe mbunge, kwani rais anaweza kumchagua mtu yeyote kuwa msaidizi wake katika serikali," alisema Bomani na kuongeza:

"Matatizo yanayohusiana na hoja hii yamekwishawekwa wazi katika makongamano mbalimbali nchini."

Wakati huohuo, Chama cha Wanasheria wa Tanzania Bara (TLS), kimeunga mkono kuwepo kwa mgombea binafsi katika uchaguzi mkuu na kusema kuwa wananchi ndio wana uamuzi wa mwisho wa kuamua kama mgombea husika anafaa au hafai.

Kauli hiyo ilitolewa jana Dar es Salaam na Rais wa chama hicho, Dk Fauz Twaib alipokuwa akizungumzia mkutano mkuu wa chama chao unaoanza leo jijini Arusha.

Alisema dhana ya lazima mtu awe katika chama fulani si sahihi kwani kila mtu ana haki ya kugombea awe ana chama au la.

Alisema ingawa Mwanasheria Mkuu amekata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu iliyoruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi, ombi la rufani halizuii utekelezaji wa hukumu iliyotolewa.

"Kuna wasiwasi kwamba kuwepo kwa mgombea binafsi kutaleta hali ya kutokuwa na utaratibu maalumu yaani watu wengi watajitokeza kugombea, lakini sisi tunasema ni vizuri kila mtu akapewa haki ya kugombea," alisema Dk Twaib.

Rais huyo wa TLS alisema suala la mgombea binafsi ni mojawapo ya mambo yatakayojadiliwa katika mkutano wao utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi na wanazuoni ambapo mada kuu itakuwa ni suala la uchaguzi mkuu.

Tayari Mahakama ya Rufani Tanzania imetoa angalizo kwamba uamuzi wa Makamama Kuu, kuhusu suala hilo uko pale pale ingawa umekatiwa rufaa. 


Katika rufaa hiyo, serikali imetoa sababu sita za kukata rufaa, mojawapo ikidai Mahakama Kuu ilikosea kujipa mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, ilikosea kutengua vifungu vya katiba ya nchi, na ilikosea kisheria kupunguza matakwa ya lazima ya Ibara 30 (5) na 13 (2) ya Katiba ya nchi.

Sababu nyingine, ni kujipachika mamlaka ya Bunge ya kutunga sheria, kukosea kisheria kwa kuiweka Katiba ya nchi katika vyombo vya kimataifa na kuitolea uamuzi kesi hiyo bila kuweka suala hilo bayana. 
 Hata hivyo Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, na Bunge), Philip Marmo amesisitiza kwamba hata kama mahakama ikiamua kuwepo kwa suala la ugombea binafsi, halitawezekana mwaka huu kwa sababu maandalizi na mchakato wa uchaguzi huu yalianza mwaka jana na yamefikia hatua za juu.

Mwananchi; 02/9/2010
 
"Kuzungumzia uongezaji wa idadi ya majimbo kwa sasa hakuna maana yoyote, ni sawa na kufanya kazi isiyo na tija. Kwa mfano, Marekani wana watu 300 milioni, lakini bungeni kwao kuna wabunge 425 na India yenye watu bilioni moja ina bunge la wabunge 600 tu."

Hapa Mzee Bomani tuko wote.
 
Hoja ya Mark Bomani iko vyema kabisa.

Serikali inaogopa kivuli tu. Mtu mmoja atakae amua kugombea inabidi awe na ushawishi na uwezo mkubwa sana kiuchumi ili aweze kupambana na vyama vya siasa. Sijui uoga wa serikali unasababishwa na nini hasa.

Ni dhahiri kuwa kutokukubali watu kuomba kuchaguliwa bila shinikizo la kuwa na imani ya chama fulani ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
 
Jaji Mark Bomani alitakiwa kuwa Rais..Tatizo la wapuuzi wachache waliomzibia kwa sababu ametoka usukumani..kabila kubwa...
 
- Now you see, hawa kina Bomani wapo wengi sana nchini, yaani viongozi wanaoweza kusimama na kuhesabiwa, I mean this is what we are talking about unasema ukweli fast na tena bila kubabaika kama kina Msekwa, ndio maana mimi huwa ninasema hivi hawa maviongozi wengi tulionao magoi goi watoke waone kama hakuna wa kuwabadili na kufanya kweli, na huyu Bomani ni mmoja wapo anafaa sana huyu!

- Yani huyu Bomani lazima aingie kwenye vitabu vya historia kwa ksuema ukweli bila kubabaisha na bila kujali kwamba kwa ksuema ukweli against watawala atakosa mlo, saafi sana Mzee Bomani wako huu ni mfano wa kuigwa, and I love it!

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom