Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba


nadhani unaelewa natokea wapi na hoja yangu lakini; sipigii mtu debe hapa, naelezea jinsi gani matukio ya kisiasa yanayoendelea hivi sasa yatatufikisha huko; msingi wa mjadala huu sio uwezo wa January au Membe bali uwezekano mkubwa wa wao kuteuliwa kwa nafasi hiyo; Hoja nitazo jibu ni zile zinazojadili mchakato kwa kuzingatia vigezo nilivyoweka, vinginevyo kama wapo wenye nia ya kujadili personalities za hawa watu, uwezo wao, nadhani watapata wa kujadiliana nao; Lakini hoja yako imeeleweka;
 

Kama mmefikia kuwa desperate to the point ya kumsimamisha January kugombea urais bongo basi you guys need to see a doctor!
 
Uchambuzi mzuri!!!

Ila kwa uchambuzi wako huo wa wana CCM uliowataja Membe na January kwangu nawaona katika picha hii baada ya uchaguzi hii.

1: Membe
Huyu kwa picha sahihi ya sasa,,kwa mujibu wa uchaguzi huu wa NEC,ndie sign potential presidential candidate kwa tiketi ya CCM.Uzoefu wake kisiasa na michezo ya KIITIFAKI ambayo pia ameicheza na kuiishi inampa tiketi ya kuaminika kuwapredicted kwenye game hili la kinyanganyilo hicho.System uwa na nguvu yake pia katika kuamua nani apewe dhamana ya Nchi kwa mujibu wa mwelekeo wa Taifa kwa nyakati husika.Hata Rais mkapa maamuzi yake ya mwisho kumpa tiketi JK yalitegemea TAIFA linataka nini wakati ule husika.Hali ya kisiasa ya Taifa hasa kipindi cha nyakati za uchaguzi na mwelekeo mzima wa uchumi usukuma system kutoa uhitaji wa candidate atae endana na maitaji ya TAIFA.

Membe anavigezo vyote,vya kisiasa na uelewa unaompa tiketi ya kuaminiwa ukiachana na simulizi ambazo hatuna ushahidi nazo mpaka pale itakapothibitisha sivyo.Hivyo mwelekeo wa sasa kama si vinginevyo kwa mujibu wa mfumo wetu [System] basi sign ya nani kubeba bendera ya CCM kwenye uchaguzi wa 2015 ni Membe.


2: January;
Huyu ni kijana ambae kwa upeo wangu mimi,hastahiki hata kuwaziwa lolote zaidi ya vyeo vya utendaji,lakini sio dhamana ya mamlaka ya umma [watu na mali].Ukitaka kujua hastahiki ebu tafuta vigezo kafika hapo alipo mpaka leo tunamuona ni January jina kubwa kusikika kwenye siasa kubwa za dhamana ya TAIFA.Je amejiunda au kaundwa?Kama amejiunda/jijenga kisiasa basi anastahiki dhamana ya TAIFA lakini kama Kaundwa/kujengwa kisiasa sidhani kama tunahaja ya kujadili,kwa kuwa aliyemuunda anajua kamuunda kwa sababu gani?Rejea mtu anaetaka Urais kwa kutumia fedha Mwlimu anasema kazipa wapi/kwa nani na ataziludishaje pesa hizo.

Kuna wakati mkuu mmoja alipita sehemu akasema Rais wa Nchi ajae anapaswa kuwa
 

maswali yako nadhani yapo more relevant kwenye vikao vya mchujo, mimi nilicho present ni hatua za kufikia huko na nimejadili kwa hoja, sio ushabiki hasa kwa kuangalia jinsi gani mchakato wa NEC ulivyo unfold na unavyomalizika, na jinsi gani majina haya mawili yanaweza kuja ku stand out;
 
Huyu kazi yake ni ahadi tu toka hapo wizarani hadi jimboni mwake;utekelezaji ni ziro!

Kufikiria tu kuwa January anaweza kuwa Rais wa TZ ni ukosefu wa busara!!
 

Asante kwa mchango wako mzuri; Nimefurahi kwamba umeelewa mantiki ya hoja yangu na pia kwamba presentation yangu haijalenga kupendekeza hawa ndio wawe wagombea; Uchambuzi wako juu ya majina haya mawili ni mzuri kwani unatoa mifano, vigezo na vielelezo kwa HOJA, ni suala tu la watu wanaopingana na wewe waje na hoja badala ya ushabiki uliojaa viroja; Vinginevyo kama nilivyosema, bado sioni mgombea wa CCM ambae anaweza kusimama dhidi ya LISSU, na hata Dr. Slaa 2015, ingawa bado ni mapema kwani wagombea wa CCM wana muda wa kuanza kuonyesha umma wanasimamia masuala gani yenye maslahi kwa taifa badala ya hali ya sasa ambapo watanzania kutwa wanasikia tu majina yakitajwa bila ufafanuzi wa misimamo yao;
 
Huyu kazi yake ni ahadi tu toka hapo wizarani hadi jimboni mwake;utekelezaji ni ziro!

Kufikiria tu kuwa January anaweza kuwa Rais wa TZ ni ukosefu wa busara!!

Naamini humo CCM kuna watu ambao wana-qualify kuiongoza nchi hii, lakini sio January. Is this supposed to be a joke!
 
Pamoja na maelezo marefu bado hukuwa sahii kumtaja Januari kama mtu anaye weza kuwa mgombea urais, kwa Membe, na Lissu you are very right. Au unataka tuendelee kusikia tanzania imetokana na Zimbambwe?
 
Huyu kazi yake ni ahadi tu toka hapo wizarani hadi jimboni mwake;utekelezaji ni ziro!

Kufikiria tu kuwa January anaweza kuwa Rais wa TZ ni ukosefu wa busara!!

Kam ulinisoma kwa makini, hoja yangu ya msingi haikuwa kupigia debe hawa wawili bali kuelezea mchakato wa kufika huko upo vipi na jinsi gani mchakato husika so far unawapa hawa wawili nafasi kubwa;
 
Mchambuzi

Very good analysis - lakini umeharibu kidogo hapo mwisho kwa kudai humpigii mtu debe wakati huku mnampigia debe Tundu Lissu! haha

Mosi,
Tundu Lissu ni jembe lakini hana "temperament" ya kuwa Rais wa Tanzania. Period.

Pili,
Nakubaliana na wewe kabisa kwamba uchaguzi wa M-NEC CCM Viti 10 ni "referendum" au "test run" ya jinsi gani wale wenye nia ya kugombea urais ndani ya CCM watakavyoibuka mwaka 2015 kama wakijitosa. Tumeshuhudia matokeo kwamba Membe amepita katika Viti 10 Bara lakini hakupata kura za wingi kuliko wengine (amekuwa mtu wa 6 nyuma ya kina Wasira, Makamba, Nchemba, Shigela na Lukuvi). Mbona Membe ame-struggle hivi kuenea? Na je, hii ni inaashiria vipi kukubalika kwake na wajumbe wa Mkutano Mkuu, ukizingatia alifanya kampeni kubwa sana kupata kiti hiki?

Tatu, nadhani umeacha majina ya wengine ambao wanaweza kujitokeza au kuombwa kugombea Urais mwaka 2015 ndani ya CCM - nao ni Shein, Mwinyi na Pinda.
 
Last edited by a moderator:
Pamoja na maelezo marefu bado hukuwa sahii kumtaja Januari kama mtu anaye weza kuwa mgombea urais, kwa Membe, na Lissu you are very right. Au unataka tuendelee kusikia tanzania imetokana na Zimbambwe?

Soma vizuri msingi wa hoja yangu, hasa kuhusu jinsi gani mgombea anapatikana;
 

Lissu ndio kipimo changu kwa wagombea wengine wa CCM; Unaposema Lissu hana temperament ya kuwa Rais wa Tanzania, on whose terms?

Kuhusu kura za Membe kuwa chache, upo sahihi, lakini katika wote kumi waliopitishwa, membe ni top three ya presidential material; Mwinyi, Karume, Pinda, Shein, wont outshine hawa;
 
Ni sawa unavyosema Mkuu. Mimi nimeona mchakato unaoongelea unaishia kwa Bwana January na Membe,basi hata hamuikanitoka. nyway,tuendelee na mnakasha.
 
Mchambuzi

Nakubali kwamba Membe bado yupo katika nafasi nzuri kuelekea 2015. Lakini kama alitaka kujipima, basi matokeo haya ya kuwa wa mtu wa 6 kati ya 10 inaonyesha yupo "vulnerable" mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu, japokuwa ameweza kupenya na kupata ushindi. Ukizingatia hao 6 wa mbele yake hawatajwi kuwa na nia ya kugombea Urais, nilitegemea Membe angepata kura zaidi kwavile anatajwa-tajwa sana kwamba anakubalika.

Nasema Lissu hana temperament ya kura Rais kwa vile amejijengea image mbele ya wapira kura wengi ya kuwa too volatile na too combative. Its the same Dr Slaa syndrome. Naamini mwisho wa siku Watanzania wengi wanataka Rais ambaye kwa personality ni muungwana, ambaye kijamii sio mchonganishi bali ni mlezi wa umma (tazama hasa Nyerere na Mwinyi, hata Mkapa na JK wanazo sifa hizi kwa kiasi fulani). Kwa maoni yangu Lissu's "abrasiveness" is good in opposition politics but he would have to moderate it in order to be a viable presidential material for the whole electorate.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kwa nini mnamsahau Mulugo jaman
 

Watanzania wanahitaji raisi kichwa. Tena akiwa mababe na haangalii makunyanzi huyo ndie anafaa, no matter how ugly, temparamental, volatile or polarizing tha peson is, it really doesn't matter. tutaendelea kuuziwa sura hadi lini?
 
Mpaka hapa sikutaka kuendelea kusoma walaka wako ila CCM wakithubutu kumsimamisha Membe ili ashindane na Dr Slaa,Lissu basi wajue ndo mwanzo wa wao kuwa wapinzani!!pili wewe kwa mtazamo wako unajua EL atakuwa amelala tu anasubili wajumbe wa NEC wachague majina hayo mawili tu??wakati yeye kaisha wekeza!!Na kwambia kama tupo kati ya ulio wataja hapati hata mtu mmoja na kama ndo wanaambiwa wanaambiwa ili wasiongeze makundi ndani ya chama ila Mwenyekiti yeye anajua ninani atamsimamisha 2015!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…