Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Mchambuzi umefanya analysis nzuri.

January Makamba bado ni kinder CCM hawawezi kumpitisha 2015 kwa u-president. Anaweza kupanda na kua waziri kamili katika kumuandaa for president seat after 2015. For 2015 CCM wataangalia zaidi uzoefu+uadilifu Benard Memmbe na wengine wazoefu watanufaika na hilo.CCM wakimpitisha Makamba kwa kigezo number tano (ujana) wamekwenda na maji. Hicho kipengele kwa sasa kina picha hasi kwa jamii sababu mtangulizi wake (Kikwete) aliingia kwa kigezo hicho hicho but poor performance ndani ya chama na taifa kwa ujumla kimefanya wengi waone ujana sio kigezo pekee kwa upresidaa.

Kipengele number nne kitaendelea kutumika kuwachinjia wagombea wengine baharini ukichukulia kwenye Hotuba ya JK huko Dodoma amegusia ilo, ninanukuu "Kiongozi mzuri wa CCM lazima awe muaminifu na muadilifu na lazima wanachama na jamii imuone hivyo. Chama chetu kinashindania kushinda akili na mioyo ya Watanzania na hiyo ndiyo kazi tunayomtarajia kiongozi wetu afanye katika jamii. Hii ndiyo hasa kazi ya Chama ndani ya umma.

Lakini, ili kiongozi wetu aweze kuifanya kwa mafanikio taswira yake mbele ya jamii ni kitu muhimu. Awe na taswira nzuri mbele ya wananchi. Kama jamii inamuona kuwa si mtu muadilifu itakuwa taabu sana kwake kufanikisha jukumu la msingi la Chama chetu.

Hivyo ndugu zangu, lazima tuhakikishe kuwa viongozi wetu wanakuwa waadilifu ili wasigeuke kuwa balaa na hasara kwa Chama"(sources www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/352567-hotuba-ya-jakaya-mrisho-kikwete-tarehe-11-11-2012-a.html ). Pamoja na JK kugusia suala la maadili kwa wagombea wao lakini lolote linaweza kutokea ukichukulia CCM ya sasa ni chama cha kimaslai zaidi kuliko vitendo, vitendo vya rushwa ktk changuzi zake za sasa ni mfano mzuri.
 
Last edited by a moderator:
Hivi ni kwanini tunatumia muda mwingi sana kujadili nani atakuwa Rais wakati matatizo yanayokabili maisha ya kila siku tunapishana nayo bila kuyapa nafasi ya kuyajadili?
 
Mkuu uko vizuri, lakini umesahau kuwa kuna nguvu nyingine kubwa sana ambayo inaweza chukua nchi kabla hata ya 2015 ambayo ni wana nchi tuliochoshwa na hali ngumu ya maisha na siasa za bongo.
 
Mchambuzi

Nakubali kwamba Membe bado yupo katika nafasi nzuri kuelekea 2015. Lakini kama alitaka kujipima, basi matokeo haya ya kuwa wa mtu wa 6 kati ya 10 inaonyesha yupo "vulnerable" mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu, japokuwa ameweza kupenya na kupata ushindi. Ukizingatia hao 6 wa mbele yake hawatajwi kuwa na nia ya kugombea Urais, nilitegemea Membe angepata kura zaidi kwavile anatajwa-tajwa sana kwamba anakubalika.

Nasema Lissu hana temperament ya kura Rais kwa vile amejijengea image mbele ya wapira kura wengi ya kuwa too volatile na too combative. Its the same Dr Slaa syndrome. Naamini mwisho wa siku Watanzania wengi wanataka Rais ambaye kwa personality ni muungwana, ambaye kijamii sio mchonganishi bali ni mlezi wa umma (tazama hasa Nyerere na Mwinyi, hata Mkapa na JK wanazo sifa hizi kwa kiasi fulani). Kwa maoni yangu Lissu's "abrasiveness" is good in opposition politics but he would have to moderate it in order to be a viable presidential material for the whole electorate.

Naelewa hoja yako, lakini naomba nisisitize hoja yangu tena kama ifuatavyo kuhusu Membe:

Kwanza, tayari UMMA umepata taarifa nyingi sana kuhusu jinsi gani kulikuwa na mpambano mkali wa kumwangusha; How would you factor in suala hili katika matokeo yake ya kura 1,455 ambayo ni difference ya kura kama 680 kati yake na Wassira ambae ndiye aliepata kura nyingi kuliko wote?

Pili, nachosisitiza ni kwamba - kuna faida kubwa sana ya kugombania ujumbe wa NEC kupitia kundi hili la kifo kwani, whether you WIN or LOSE, tayari jina lako linakuwa exposed kwa wapiga kura mkutano mkuu wa taifa ccm wa mwaka 2015 wa kuteua jina; Kwa mtazamo wako, if we hold other things constant for a minute, mgombea yupi wa 2015 atakuwa kajirahisishia kazi kati ya hawa: Je ni yule aliye gwaya kundi hili la kifo na kukimbilia Wilayani au yule aliyethubutu kuingia kundi la kifo na akapita na kushika mkia katika nafasi zile kumi?

Kuhusu Lissu, watanzania tuna tabia ya ajabu, mtu akiwa mkali tunasema tunataka mpole, akiwa mpole tunasema tunataka mkali; Lissu ana ukali gani? Mbona nje ya vikao tunamwona ukali wake kwenye dance floor akitabasamu na kucheza kwa furaha kubwa na Mademe Makinda? Inawezekana huu ni mfano wa ovyo, lakini kwa kweli Ukali wa Lissu ni wa kikazi zaidi; Historia pia inatueleza jinsi gani Nyerere kufikia mwaka 1958 alivyogeuka kuwa millitant, hasa baada ya Mkutano Mkuu wa Taifa (TANU) Tabora 1958; Due to his millitancy... alikamatwa na serikali kwa kosa la kutukana wakuu wa wilaya na kuchochea vurugu na kupigwa faini kubwa wakidhania hatoweza lipa, hivyo kwenda jela, lakini wahindi na weusi kadhaa wakachanga hela na kumtoa.

Point yangu ya msingi hapa ni kwamba, Lissu akiwa na uzalendo na uadilifu ni BORA mara mia ya mtu mwingine ambae atakuwa muungwana, mpole, mcheshi lakini JIZI la mali ya umma; CCM ina viongozi wakali kama magufuli, aggrey mwanri n.k, lakini we need to see more on this and consistently...
 
CCM haitabiriki katika wagombea wake, pesa inazungumza zaidi kuliko vigezo vyovyote vya logic. Wakati wa Mwalimu, kauli ilitoka kwake wengine wakafuata, so far hakuna mchungaji ndani ya CCM kama alivyokuwa mwalimu. Sioni kama Membe au Makamba kama wanakipaji cha kutosha kufukuzia urais wa nchi.

If i have to bet i ll put my money kwa EL, against changamoto zote zinazomkumba na tuhuma tele lakini hadi mwaka huu uchaguzi wa CCM umeonekana kuwa na network kubwa ya EL. Just angalia namna nguvu kubwa inavyotumika na viongozi waandamizi wa serikali kuudhibiti mtandao wake na still ame managed kuwa na 2/3rd ya uongozi wa sasa ndani ya chama basi anaonekana hakamatiki.
TIME WILL TELL.
 
Naamini humo CCM kuna watu ambao wana-qualify kuiongoza nchi hii, lakini sio January. Is this supposed to be a joke!

Natumaini mnamjadili January mkiwa tayari mnaelewa kwamba hoja yangu ya msingi haikulenga kumjadili qualities zake ngazi ya Urais ingawa mjadala huo kuendelea ni sawa tu kama mkiamua hivyo; Hoja yangu ya msingi ni mchakato mzima wa kupata wagombea na jinsi gani hawa wawili stand a better chance kuliko wengine, na nimejadili hili kwa hoja;
 
Mpaka hapa sikutaka kuendelea kusoma walaka wako ila CCM wakithubutu kumsimamisha Membe ili ashindane na Dr Slaa,Lissu basi wajue ndo mwanzo wa wao kuwa wapinzani!!pili wewe kwa mtazamo wako unajua EL atakuwa amelala tu anasubili wajumbe wa NEC wachague majina hayo mawili tu??wakati yeye kaisha wekeza!!Na kwambia kama tupo kati ya ulio wataja hapati hata mtu mmoja na kama ndo wanaambiwa wanaambiwa ili wasiongeze makundi ndani ya chama ila Mwenyekiti yeye anajua ninani atamsimamisha 2015!!

Hoja yako inaeleweka, lakini kama umeamua kumalizia kusoma bandiko langu namba moja, unayoyasema nimeyajadili mwishoni, na ndio maana nikasema CCM inahitaji kumpata mtu wa kupambana na mtu kama Lissu kama sio Slaa kwani hawa wameonyesha uwezo wa kusimamia masuala pamoja na kuwa na vigezo vingine muhimu.

Pia nilisema kwamba inawezekana wapo wana CCM wenye uwezo wa kupambana na Lissu/upinzani, lakini tutabaini hilo muda ukifika, vinginevyo kwa sasa, tunachosikia ni majina tu, huku pia tukipata picha halisi ya mbio za ccm kupitia chaguzi za NEC 2012; Inabidi ifikie wakati wale wote wenye nia ya kuchukua fomu kupitia CCM waweke misimamo yao wazi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa (kisiasa, kiuchumi, kijamii - muungano, katiba mpya, uadilifu, utawala wa sheria, vision yao kuhusu a better Tanzania n.k) ili electorate iweze kuwachekecha na kuwafananisha na upinzani;
 
alles

Nashukuru kwa mchango wako ambao umeonyesha kwamba umeelewa hoja yangu ya msingi; Uliyoyasema yana mashiko, ila kikubwa ni kwamba, mgombea Urais atatokana na wajumbe hawa hawa wa Mkutano mkuu waliompa kura 2,093 January na kura 1,455 Membe; Usisahau pia kwamba tunachoambiwa na wenyewe huko juu ni kwamba safu hii (wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa, wajumbe wa NEC etc), ni safu iliyokamilika kufanikishia CCM ushindi 2015;
 
Last edited by a moderator:
Kwa upeo wangu mdogo wa siasa za Tanzania nadhani huyu January anahitaji muda zaidi ili akomae kama mwana siasa na kiongozi. waliokuwa nae karibu inawezekana kuna kitu wanakiona lakini bado mapema huyu CCM wamuandae kwa ajili ya uchaguzi wa 2020 uhai ukiwepo,ingawa hatuna utamaduni huo.
 
Mpaka hapa sikutaka kuendelea kusoma walaka wako ila CCM wakithubutu kumsimamisha Membe ili ashindane na Dr Slaa,Lissu basi wajue ndo mwanzo wa wao kuwa wapinzani!!pili wewe kwa mtazamo wako unajua EL atakuwa amelala tu anasubili wajumbe wa NEC wachague majina hayo mawili tu??wakati yeye kaisha wekeza!!Na kwambia kama tupo kati ya ulio wataja hapati hata mtu mmoja na kama ndo wanaambiwa wanaambiwa ili wasiongeze makundi ndani ya chama ila Mwenyekiti yeye anajua ninani atamsimamisha 2015!!

Umeelewa hoja yangu ya msingi lakini? Mgombea wa CCM atasimamishwa kwa vigezo viwili tu - kwanza mpambanaji wa Rushwa au Mwenye mvuto wa kura za vijana, hakuna lingine, kwani sasa CCM imeshagundua kwamba suala la mgombea wake kuwa rais wa nchi automatically limepitwa na wakati;

Swali lako kwangu kuhusu Lowassa kuwa macho au usingizini katika kupitisha jina hili na lile, mimi hayo sina interest nayo sana, ninacho tabiri ni kwamba mwisho wa siku hata yeye atahamia upande mmoja kati ya hawa wawili;

Kwahiyo kwa mtazamo wako Mwenyekiti atamsimamisha mtu anayemtaka? Yani ashindwe kuzuia mpasuko unaonukia CCM, ashindwe kuzuia rushwa zaidi ya kukemea, lakini aweze kumsimamsisha mgombea wake? uwezo huo hana, hilo liliisha na Mkapa wakati ule chama kipo intact; Jana kwenye hotuba yake alisema hana mgombea na hawezi kuchukua upande, lakini hata kama angekuwa na mtu wake, hatakuwa na uwezo huo hata akiamua; Chama kimefikia hatua ngumu sana;
 
Je, ni vigezo gani hutumiwa na CCM kumpata mgombea Urais? Najua wengi katika mjadala huu wataleta hoja khanga, kofia, n.k, kwani ukweli ulio wazi ni kwamba Chama kimechafuka; Lakini tukiweka hili pembeni kwa sasa, Vigezo vinavyotumika kuteua jina la mtu kuwa mgombea Urais (CCM) vipo vingi, na vingine ni very arbitrary na pia mchakato wake sio democratic; Lakini huo ni mjadala mwingine, na kwa sasa ningependa kujadili vigezo vifuatavyo:

  1. Awe na Sifa za Kuwa Mbunge Kufikia Kipindi husika
  2. Awe Mjumbe wa NEC Kufikia Kipindi Husika
  3. Jina lake liwe familiar miongoni mwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa
  4. Asiwe amethibitika kwamba ni mla rushwa (tetesi hazitoshi)/Awe na Sifa Za Kukemea Rushwa
  5. Na Awe na Umri utakaovutia Wapiga Kura Vijana
Mchambuzi,

Mada ni safi na quite objetive. Hapo nilipoweka red ni viongozi wangapi wa CCM waliothibitika kuwa ni wala rushwa na hawafai kuwa Rais wa nchi na wamechukuliwa hatua gani? Ingekuwa vizuri ukafafanua hil,i ili hiyo dhamira ya kumaliza rushwa kupitia chama tawala na serikali yake ifahamike kwa wananchi walioumizwa mno mno na mwenendo huu. Aidha itarudisha imani ya wananchi kwa CCM ambao wataendelea kukipa ridhaa ya kuendelea kutawala.

Umesema tetesi za rushwa hazina mashiko katika context ya hoja uliyoleta, sawa lakini hiki ni kitendawili!! Wala rushwa watathibitikaje ilihali hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa na vyombo husika? CCM imshukuru Mungu sana kwa umbumbu wa wananchi waliokosa elimu hasa wa vijijini na kuendelea kuridhika na CCM kwa kukosa uwezo wa kuelewa na kupambanua mateso waliyonayo kutokana na utawala mbovu wa miaka mingi chini ya chama hiki.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hotuba JK aliyoitoa, anaonekana amechoka na makundi na majina ya watu wanaotaka nafasi ya uraisi.

Japo, JK huwa hatabiriki katika kauli zake,nahisi sasa yupo tayari kuwatosa wote wanaotaka Urais (waliojitangaza au kuhisiwa kuitaka nafasi hiyo).

MEMBE:
Kwani kwa Nyakati tofauti, Membe naye amediriki kusema anawajua maadui zake(hii inaonesha yupo katika mchakato wa kuitaka nafasi hii ya urais!).

Mkuu wa nchi atakuwa anajua nia ya Membe,japo hasemi na hataki kuonyesha kuwa yupo kundi lipi,lakini kwa nyakati tofauti,Vijana wa mkoa wa pwani waliwahi kusema rais hata toka kaskakazini,kauli ambayo mpaka leo hamna aliyejitokeza kuikanusha.

Kwa sasa sio lazima tena Rais achaguliwe kwa vigezo vya kuwa na sifa ya kujua itifaki,kuwa waziri wa nchi za nje kwani bado vigezo hivi havisaidii kwani JK amekuwa anasafiri mara kwa mara na wananchi hawataki tena kuwa na mtu anasafiri huku mambo ya nchi hayaendi vizuri. Wananchi hawezi kushawishiwa na sifa za mtu anayetoka katika wizara aliyotoka mtangulizi wake.

Kwa vile tayari naye ni sehemu ya watu wenye makundi ndani ya chama,nahisi sasa hivi Chama kinweza kuondokana na makundi kwa kuteua Mgombea ambaye hatajwi wala hana makundi ili kulinda CCM isiendelee kugawanyika.

Kwa mantiki hii hata Membe hatapitishwa kugombea Urais 2015.


JANUARI MAKAMBA:
Jamii kwa sasa haitapenda ugombea Urais kwa kubebwa na hasa majina ambayo ni watoto wa waliokuwa wanasiasa, kama huyu Januari Makamba. Huyu labda anajiimarisha kwa ajili ya hapo baadae awe imara kisiasa kwani awamu hii imembeba, ndio alipoibukia katika siasa. Ujue kuna watanzania wengi wenye vipaji,lakini njia ya kufikia nafasi kama hizi inakuwa ngumu ndani ya CCM, kwa vile hawana fedha.

Januari, nahisi hawezi kuchaguliwa kugombea nafasi ya urais kwa vile jamii itakuwa nataswira ya WATOTO WA VIGOGO kubebwa, tena kurithishana madaraka ndani ya CCM, nafasi inatoka kwa baba kwenda kwa mtoto (Wazee wengi, kila mtu anataka mtoto wake awe na nafasi katika chama).
 
Ni muhimu tukaweka chuki na pia personal feelings pembeni, naombeni tujadili hoja iliyopo mbele yetu ambayo ni straight forward:

Wapiga kura kumchagua mgombea Urais (CCM) 2015 watakuwa ni hawa hawa waliompa January Kura 2.093 na Membe Kura 1,455;

Ujumbe wa NEC ni factor muhimu sana ya kiongozi kufikiriwa kuwa Rais; Ingawa hii sio kanuni rasmi ya Chama, imekuwa ni utamaduni unaokaribiana na Kanuni;

Ingawa wajumbe wa NEC wanapitia Jumuiya za Chama, Wilayani, na Pia ngazi ya taifa kupitia mkutano mkuu wa taifa, nafasi supreme kuliko zote ni ile ya kupitia kundi la kifo - majina kumi yanayochaguliwa na mkutano mkuu wa Taifa; Jumbe wa njia hii ni muhimu sana kwa aspirants wa Urais kwani kugombea kupitia hizi nafasi inaku expose kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa ambao ndio watakuwa ni wapiga kura tena kuchagua jina la mgombea urais kupitia CCM (2015); Hii ni tofauti na wagombea watakaojitokeza ambao walipata ujumbe wa NEC kupitia wilaya; Ingawa wao pia ni wajumbe wa NEC, majina na sura zao zitakuwa ni ngeni kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa 2015;

Ingawa January ameshikilia nafasi ya pili kwa wingi wa kura kati ya nafasi kumi huku Membe akishikilia nafasi ya sita, ukweli unabakia kwamba majina mengine yaliyopita - wassira, mukama, lukuvi, msome, mukangara, shigela na mathayo, haya yote sio presidential material kama January na Membe;

Kura za Membe kuwa chache haina maana kwamba he stands less of a chance, hasa ikizingatiwa kwamba kumekuwa na tetesi nyingi jinsi gani alihujumiwa, which means kura zake zingeweza kuwa nyingi zaidi;

Majina mengine yanayotajwa tajwa stand less of a chance kwa sababu mbalimbali:Lowassa; Nchimbi; Sumaye, Sitta, Migiro, Magufuli, Mwandosya, Mwakyembe, Karume, Pinda, Shein, Kigoda;

Wengi ya hawa, katika hatua tofauti watachagua upande baina ya Membe na January, hasa iwapo January ataamua kugombea;

Top Three ninayoitabiri ni kama ifuatavyo:

Bernard Membe
January Makamba
Amani Karume (kwa vile ni muhimu kukawa na mgombea kutoka Zanzibar)

Mshindi anaweza kuwa any of the three, ingawa utabiri wangu ume pick Membe au January; Membe, Karume na January watakuwa top three kwa hoja zifuatazo:

Agenda kuu itayotawala uchaguzi mkuu 2015 itakuwa ni kati ya hizi tatu:

Kwanza, ufisadi - iwapo CCM itashindwa kutoa watu kadhaa kama kafara ili ionekane inapiga hatua kuelekea huko, hivyo kupunguza makali ya Chadema juu ya hili; Iwapo Agenda hii itatawala, mteule atakuwa ni Bernard Membe;

Pili, mgombea Kijana - Nguvu ya Chadema ni Vijana, hivyo CCM kama itafanikiwa kuizima hoja ya ufisadi, agenda itahamia kwenye kura za Vijana, na kutokana na hili, hazina kubwa ya CCM katika hili ni January Makamba, hivyo huyu ndiye atakaepitishwa;

Na Tatu - inawezekana akahitajika mtu kutoka zanzibar iwapo suala la muungano litafikia hali tete, hivyo ili kuokoa muungano kuvunjika, Chaguo la CCM kwa hili litakuwa ni Amani Karume;

Natabiri kwamba Agenda namba moja na namba mbili ndio zitavuma zaidi;
 
Mada ni safi na quite objetive. Hapo nilipoweka red ni viongozi wangapi wa CCM waliothibitika kuwa ni wala rushwa na hawafai kuwa Rais wa nchi na wamechukuliwa hatua gani? Ingekuwa vizuri ukafafanua hil,i ili hiyo dhamira ya kumaliza rushwa kupitia chama tawala na serikali yake ifahamike kwa wananchi walioumizwa mno mno na mwenendo huu. Aidha itarudisha imani ya wananchi kwa CCM ambao wataendelea kukipa ridhaa ya kuendelea kutawala.

Umesema tetesi za rushwa hazina mashiko katika context ya hoja uliyoleta, sawa lakini hiki ni kitendawili!! Wala rushwa watathibitikaje ilihali hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa na vyombo husika? CCM imshukuru Mungu sana kwa umbumbu wa wananchi waliokosa elimu hasa wa vijijini na kuendelea kuridhika na CCM kwa kukosa uwezo wa kuelewa na kupambanua mateso waliyonayo kutokana na utawala mbovu wa miaka mingi chini ya chama hiki.

Upo sahihi lakini mimi nadhani mawili kati ya haya yatatokea:

Aidha, kuna mafisadi ambao watatolewa kafara kama njia ya kuokoa chama iwapo agenda ya ufisadi itaendelea kushika moto wa nyika come 2015; au

Mmoja wa wagombea au wanaotajwa tajwa atapasua bomu kubwa sana dakika za majeruhi kuhusu kina nani ni mafisadi na walihusika vipi na hiki na kile, na habari hiyo itabeba headlines kwa kipindi kirefu kuelekea uchaguzi mkuu na kufifisha sana agenda ya Chadema on Ufisadi; ndio maana ni muhimu Chadema wakaja na holistic approach ya kutatua matatizo ya wananchi kwani Ufisadi hauna itikadi, agenda hiyo can be robbed na mtu yoyote aliyeamua kulipuka;
 
Kwa hotuba JK aliyoitoa,anaonekana amechoka na makundi na majina ya watu wanaotaka nafasi ya uraisi.
Japo,JK huwa hatabiriki katika kauli zake,nahisi sasa yupo tayari kuwatosa wote wanaotaka Urais(waliojitangaza au kuhisiwa kuitaka nafasi hiyo).
MEMBE:
Kwani kwa Nyakati tofauti,Membe naye amediriki kusema anawajua maadui zake(hii inaonesha yupo katika mchakato wa kuitaka nafasi hii ya urais!!!!).

Mkuu wa nchi atakuwa anajua nia ya Membe,japo hasemi na hataki kuonyesha kuwa yupo kundi lipi,lakini kwa nyakati tofauti,Vijana wa mkoa wa pwani waliwahi kusema rais hata toka kaskakazini,kauli ambayo mpaka leo hamna aliyejitokeza kuikanusha.!!!Kwa sasa sio lazima tena Rais achaguliwe kwa vigezo vya kuwa na sifa ya kujua itifaki,kuwa waziri wa nchi za nje.kwani bado vigezo hivi havisaidii kwani JK amekuwa anasafiri mara kwa mara na wananchi hawataki tena kuwa na mtu anasafiri huku mambo ya nchi hayaendi vizuri.Wananchi hawezi kushawishiwa na sifa za mtu anayetoka katika wizara aliyotoka mtangulizi wake.

Kwa vile tayari naye ni sehemu ya watu wenye makundi ndani ya chama,nahisi sasa hivi Chama kinweza kuondokana na makundi kwa kuteua Mgombea ambaye hatajwi wala hana makundi ili kulinda CCM isiendelee kugawanyika.!!
Kwa mantiki hii hata Membe hatapitishwa kugombea Urais 2015.!!!!


JANUARI MAKAMBA:
Jamii kwa sasa haitapenda ugombea Urais kwa kubebwa na hasa majina ambayo ni watoto wa waliokuwa wanasiasa,kama huyu Januari Makamba.!!.Huyu labda anajiimarisha kwa ajili ya hapo baadae awe imara kisiasa kwani awamu hii imembeba,ndio alipoibukia katika siasa.Ujue kuna watanzania wengi wenye vipaji,lakini njia ya kufikia nafasi kama hizi inakuwa ngumu ndani ya CCM,kwa vile hawana fedha.Januari,nahisi hawezi kuchaguliwa kugombea nafasi ya urais ,kwa vile jamii itakuwa nataswira ya WATOTO WA VIGOGO kubebwa,tena kurithishana madaraka ndani ya CCM,nafasi inatoka kwa baba kwenda kwa mtoto(Wazee wengi,kila mtu anataka mtoto wake awe na nafasi katika chama).

Una hoja za msingi sana lakini kwa sasa naomba nikazie kwenye hoja yako kuhusu uwezekano wa CCM kuja na jina jipya kabisa la mgombea Urais dakika ya mwisho, ambalo hatulisikii hivi sasa:

Ukweli unabakia kwamba - CCM haina resources wala muda wa kumnadi mgombea atakayeibuliwa from nowhere a few months before elections; CCM ilifanya kosa hili mwaka 1995 kwa kumchagua Mkapa, na ikalazimika Nyerere azunguke nchi nzima kumuuza; Pamoja na intervention hii ya Nyerere katika kumuuza, Mkapa akapata the lowest victory in CCM's history (lower 60s in percentage); CCM haitaenda huko tena kama unavyofikiri, Rais ajae (iwapo CCM itahinda) atatoka miongoni mwa majina haya haya tunayoyasikia, na ingawa mbio hizi zinakemewa kwamba zinaharibu chama, kwa upande mwingine CCM inafurahia kwani inasaidia marketing ya candidates to its Members of National Congress lakini pia the electorate at large, na wakati muafaka ukifika, watachagua kati ya majina haya haya;
 
Una maana EL angegomebea kupitia kapu la taifa angeangukia pua?labda sijakuelewa vizuri!
 
una maana EL angegombea kupitia kapu la taifa angeangukia pua?ndivyo unavyoamini?labda sijakuelewa vizuri!

Sina majibu ya uhakika, lakini ufuatao ni mtazamo wangu tu:
It was not guaranteed kwa Lowassa kuibuka namba moja kwa wingi wa Kura kupitia nafasi hizi kumi za kifo, hivyo ilikuwa ni busara kwake kwenda kugombea wilayani; Kura za NEC zina heshima yake na zina send ujumbe mkubwa na tafsiri nyingi, hasa ikiwa uchaguzi unaofuata ni wa Urais;

  • Je unakumbuka matokeo ya kura kwa Lowassa na Kikwete ujumbe wa NEC kupitia nafasi hizi hizi za Kifo uchaguzi wa chama 2002?

Uchaguzi huu ulikuwa miaka mitatu kabla hawajaingia madarakani; Kwa mshangao wa wengi, wote wawili walipata kura chache sana tofauti na ilivyotarajiwa kwani katika uchaguzi wa 1997, 1992, wote wawili walikuwa wanapata kura nyingi sana, tofauti na ilivyotokea 2002; Kutokana na hli, wote kwa pamoja walilalamika kwamba hujuma imefanyika kuchakachua kura zao; Ingawa walipita, walishika nafasi za chini tofauti na chaguzi za awali, na hili lili affect sana mikakati yao kuelekea 2005, at least kisaikolojia;

Sidhani kama Lowassa was ready to go down this road again katika kipindi hiki cha siasa za fitina, kwani kama angewania kupitia mkutano mkuu wa taifa, mtu kama yeye needed nothing less than alichopata Wassira, if not more; Tazama jinsi gani kura za membe zinavyotafsiriwa, na ingawa amepita, bado ushindi wake haupewi heshima;
 
:nimekataa

Upo uwezekano wa kile ulichoandika kuwa kweli au si kweli. Sipendi pia nitoe msimamo kwani hili nalo ni sawa na kura za kapu la CCM. Kiukweli rushwa na ubinafsi ndo vinamaliza siasa za Tzania, mi nadhani sasa wa-Tz wote tuamke tu na kuangalia tulikotoka, tulipo na twendako ili tujiandae na ngwe ijayo kwa kuweka Rais bora na si bora RAIS.

Kuendelea kutetea ufisadi, rushwa, makundi, unafiki ni kuzika nchi ilotukuka katika lindi la matope na kuliangamiza taifa lakini tujue pia tunaipeleka nchi kutotawalika ambapo itafikia kizazi kijacho kuhoji nini walofanya walotangulia baadaye kuchukua sheria mkononi kwa sababu ya watu wapuuzi wachache wanaoangalia matumbo ya. Sipendi litokee na hivyo tujizatiti kukaza buti kuliepusha taifa hili linalong'ang'aniwa kuitwa changa kila siku.

:mwaaah:
 
Hujamuweka Lowassa??? Unatafuta ugomvi na Pasco and Co.

Mkuu ameshindwa kumzungumzia coz anaijua nguvu yake, haya yote mtayasema lakini Raisi mungu atamshusha toka mbinguni, na mtashangaa jiwe mlilolikataa ndo jiwe kuu la pembeni, Akina membe, January wote wanachekacheka tu. Hawawezi kutoa maamuzi magumu kama ya kumfukuza kiongozi dhaifu ilikuinusuru jamii, Tumechoka kutuletea wazaramo either wa bagamoyo, mtwara na wala wa tanga, Tunahitaji majembe yashike nchi na utawala wa serekali uheshimiwe na kuogopewa. Katika watu wako sijamuona hata mmoja anaeweza kulifanya hili.
 
Back
Top Bottom