Habari wakuu nipo mtaa wa mchikichi huku kariakoo maduka hayajafunguliwa hadi muda huu kuna nini kwani?
Ngoja niangalie na mitaa mingine.
UPDATES...
Muonekano wa maduka mbalimbali katika soko la Kariakoo hadi saa 8.23 asubuhi huku kufungwa kwa maduka hayo kukihusishwa na uwepo wa mgomo wa wafanyabiashara wa soko hilo kongwe na maarufu Afrika Mashariki.
Wafanyabiashara wa Kariakoo wanafanya mgomo wa kufunga maduka wakishinikiza kupungua kwa kodi wanazotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Your browser is not able to display this video.
WAFANYABIASHARA WAGOMA KUMFUATA WAZIRI MKUU DODOMA
Ni baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makala kuwataka kupeleka malalamiko yao kwa Kassim Majaliwa ambaye anatarajiwa kukutana na uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mawaziri husika na Kamati ya Wafanyabiashara ili kutafuta suluhu ya mgomo huo
Makalla amefika katika Soko Kuu la Kariakoo baada ya Wafanyabiashara kugoma kufungua biashara huku wakitoa malalamiko kadhaa ikiwemo madai ya uwepo wa utitiri wa kodi.
Wakizungumza baada ya Mkuu wa Mkoa kuondoka eneo la Kariakoo, wafanyabiashara wamesisitiza kuwa wanahitaji kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kutoa kero zao huku wakisisitiza kuendelea kufunga maduka yao
.............
Takwa la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla la wafanyabiashara kumfuata Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Dodoma limepingwa.
Wafanyabiashara hao walioitisha mkutano mwingine baada ya Makalla kuondoka wamesema wanalipa kodi hivyo Waziri Mkuu Kama anataka kuonana nao awafuate kariakoo na sio wafanyabiashara kumfuata.
Azimio la wafanyabiashara hao endapo mfanyabiashara atakayefungua duka leo ni halali yao.
"Mwenyekiti usiogope tupo nyuma yako usiogope chochote," ameeleza mmoja wa wafanyabiashara hao aliyepanda jukwaani na kutoa muongozo alioudai ni wa kisayansi.
Kuna ubaya gani TRA kuwataka muorodheshe store zenu mnazohifadhia mali? mnaficha kitu gani? wanataka wazifahamu ili wawe wanazikagua, kwasababu huko Kariakoo kuna ukwepaji mkubwa sana wa kodi.
Hata kama hizo kodi zinatumika hovyo serikalini, vyema store zenu zifahamike, ili mkiwatoroka bandarini mkakutane nao store, anyway niwapongeze hao wafanyabiashara kwa uthubutu wao, hata kama sikubaliani na madai yao.
NB.
Hao jamaa wanasema mfanyabiashara mwenzao yeyote atakayefungua duka ni halali yao, hivi wanazijua sheria za nchi?
otherwise umetumwa kuuvuruga. haya ni madai ya Wafanyabiashara dhidi ya Serikali na pengine kwa chini chini kuna mkono wa watu wa CCM kuhakikisha Serikali inasikiliza madai yao tupunguze ujuaji
Waache wakae na hela zao. Watu walipe kodi ili mabwanyenye na ma'mwinyi wakazitapanye na kuzila kwa kununua Mashangingi mapya ya 2023 na kujiongeza mishahara na marupurupu.
Wacha raia watumie hela zao wenyewe. Kodi kodi kodi .... Mxiem [emoji19] kodi ya nyoko.
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
Hebu twambieni kuna shida gani mkiorodhesha store mnazohifadhi bidhaa zenu? Shida iko wapi? Kwani ni kinyume na sheria? Kuna double taxation? Kivipi ni double taxation? Makadirio ni makubwa? Kivipi makadirio ni makubwa?
Sijawahi na pengine sitakuja kuwahi kuelewa hizi kodi zinavyokatwa
Mzigo ukifika bandarini unatokutana na tra
Mzigo huohuo ukifika dukani unakutana tena na tra
Sasa najiulizaga yule tra wa bandarini ni tofauti na huyu wa dukani????
Na km wote ni TRA, hizi kodi za mara mbilimbili zinalenga nini????
Hivi kweli hatuwezi kuja na mfumo mmoja tu TRA pale bandarini kuchukuwa kodi mara moja ili mzigo ukitoka basi watu wasisumbuane? mbona kwenye mafuta wameweza mzigo kwenye meli unakatwa kila kitu basi unaingia sokoni. Kuna nini hii kila siku kukimbizana wakati Tech imekuwa sana kuna njia za kuchukuwa mapato kwa njia ya kisasa tu badala ya haya mambo ya double taxation watu hakuna kuaminiana kwanini lakini? kodi kulipa ni haki basi tuweke mfumo utakaonekana ni wa haki.
Sio kila bidhaa inayouzwa inapitia bandarini, nyingine zinapitia mipakani ambapo Tanzania inazungukwa na nchi nyingi. Nyingine zinazalishwa ndani ya nchi
Kipindi cha JPM wafanyabiashara halali walikuwa wanasikilizwa vizuri na kero zao zinatatuliwa. Lakin sasa serikali ya KULA KWA UREFU WA KAMBA TRA wanakula kwa urefu wa kamba zao na hakuna anayejali sawa
Sio kila bidhaa inayouzwa inapitia bandarini, nyingine zinapitia mipakani ambapo Tanzania inazungukwa na nchi nyingi. Nyingine zinazalishwa ndani ya nchi
Mimi sijaongelea bandarini tu nimesema TRA kwani unaweza kupita mpakani, bandarini au airport bila uwepo wa TRA? wako kila entry ya nchi waweke mfumo wa kisasa kukusanya kodi sio mambo ya kuviziana madukani mambo ya kishamba sana.