lovely love
JF-Expert Member
- Dec 11, 2013
- 337
- 296
Khaaaa!!!
Smh
Smh
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Habari wakuu,
nimeipata hii taarifa ambayo sio rasmi kuwa kesho tarehe 14/09/2016 daladala za Daressalaam zinatarajia kugoma. Madai ni kukithiri kwa faini za barabarani au wengine wanaita vyeti au kifurushi cha wiki pia kitendo cha madereva wanapelekwa selo kwa kosa la barabarani kila kukicha.
Madereva wanahamasishana kwa SMS kutotoa gari kesho na endapo dereva akijifanya kukaidi gari lake litavunjwa vioo kwa kupigwa na mawe.
Haya wale wenzangu na mimi watumiaji usafiri wa uma nawaasa kuwahi kutoka ili kuepuka usumbufu.
Kisheria hutakiwi kuvaa kiatu cha wazi unapoendesha coz ikitokea dharula unaweza ukafa kiatu kikimbilia chini ya Pedal ya break.Siku hizi askari wamezidi, juzi kuna mtu kapigwa faini kisa kavaa ndala
HATA UKIWA KWA GARI BINAFSI HUTAKIWI KUVAA NDALA AU KUENDESHA PEKUPEKUNi kosa kuendesha gari ukiwa umevaa ndala
Utomaso mzuri sana wee hujui tuuTomaso on it's quality!!
kila traffick ana kitu kinachoitwa minus 3, maana yake akiwa kazin lazima akamate makosa matatu ndio akabidhi.Kisheria hutakiwi kuvaa kiatu cha wazi unapoendesha coz ikitokea dharula unaweza ukafa kiatu kikimbilia chini ya Pedal ya break.
Ila wanachofanya sasa traffic ni Kukomoana mradi tu pesa iingie serikalini ionekane kua serikali inakusanya pesa za kutosha, si hua mnamsikia Baba Jesca anasemaga hii nchi ni tajiri inapesa nyingi?
Yaani kinachofanyika ni kama vile wanapeana hesabu kwamba ukirudi jioni uje utoe Z-report iliyochangamka kidogo.
Mkuu unafahamu kanuni na sheria za usalama barabarani?Siku hizi askari wamezidi, juzi kuna mtu kapigwa faini kisa kavaa ndala
Hairuhusiwi ni kwasababu za kiusalama kuwa zile kamba za open shoes zinaweza kunasa kwenye pedals na ikawa hekaheka. So kwa ujumla si ruhusa kuendesha ukiwa umevaa sandalsHATA UKIWA KWA GARI BINAFSI HUTAKIWI KUVAA NDALA AU KUENDESHA PEKUPEKU
nakubaliana na weweMaisha yangu yote nimekuwa nikipingana na takwimu zinazotolewa na institutes mbali mbali Duniani kwamba sisi Waafrika tuna lowest IQ Duniani, lkn kila siku zinavyozidi kwenda nadiriki kusema kwamba Sayansi haidanganyi kwamba ni kweli kabisa sisi tuna lowest IQ Duniani!
Fikiria Mtuhumiwa anagoma kwa sababu hataki Askari amkamate kwa kufanya kosa, na hii ni nchi ambayo ukiondoka nyumbani kurudi salama kama haujavunjika mguu kwa ajali unashukuru Mungu!
Cha kushangaza kabisa kuna kundi la watu hapa watafurahia na kuwaunga mkono daladala wakifikiri kwamba wanamkomoa Raisi Magufuli kwa kuwa hawampendi kumbe hata huyo Magufuli anajaribu tu kuwalinda hao hao wanaompinga, Raisi Magufuli anasafishiwa njia na gari la lake huchunguzwa kabla hajalipanda, hivyo hahitaji daladala ...
Najua lakini kuna makosa mengine yanasameheka, tatizo siku hizi polisi wamekuwa traMkuu unafahamu kanuni na sheria za usalama barabarani?
Shida ni kuwa kila Siku wapo barabrani na gari kila Siku zipo na kila siku wanazikamata yaani haina kikomo,wiki,mwezi,miezi,mwaka.ukichunguza sana daah,in afadhali ingetoka amri wenye kumiliki hizi dala dala walete brand new buses sijuiKwa kweli Inabidi ufike wakati watanzania tuweke mazoea pembeni..ivi kama huna kosa,gari liko sawa kila kitu huyo trafic akukamate tu.Ingekuwa amri yangu ningepiga matufuku daladala zote maana hakuna hata moja iliyokamilika..iki tuanze upya na asiyetaka aache.pambafuu