Mgomo wa walimu na maamuzi ya Serikali, Mahakama

Mgomo wa walimu na maamuzi ya Serikali, Mahakama

Hivi ni kweli kwamba serikali yetu na busara zake zooote (!?) iliona kuwa suluhisho pekee ni kukimbilia mahakamani kuzuia mgomo wa walimu? kweli?....Kaaaaz kweli kweli!
 
Haya haya kumekucha,ukiona walinu wanagoma,hawa waliosifiwa wingi wa maadili,wingi wa uvumilivu wenye wito,wanakua vile walivyokua jana,ujue kunajambo lanukia,warasimuwa nchi mpo?mmeisoma clear msg pale ukutani?hamjaiona,hamjaisoma?washeni taa,mtaiona,hakika kuna jambo kuubwa laja,nalo litakua fundisho kuubwa,kwetui na vizazi vijavyo,mungu wabariki wagomaji,walaani waliochanzo cha matatizo haya tuyaonayo sasa,ibariki tanzania,na wana wa tanzania walio wema,walaani wote walio na hila mbaya na tanzania,na wana watanzania,japo pia ni watanzania wenzetu!
 
Waalimu wengi uchaguzi wa 2005 walionyesha mwamko wa mageuzi, wengine wakaenda kugombea udiwani kupitia vyama vya upinzani. Walitiwa moyo sana na waalimu wenzao.

Tunachokiona leo ni kulipiza kisasi. Nasikia JK ni bingwa wa visasi.
.

Wengine wanasema kuwa "Kamuulize Babu Seya.."
 
raismawe.jpg

Rais wa Chama cha Waalimu Tanzania (CWT, Gratias Mukoba
akikwepa mawe kutoka kwa waalimu waliojawa na jazba akikimbilia
gari la polisi , mkutano wa maandalizi ya mgomo ulivunjika, Makakama
Kuu Divisheni ya Kazi ilizuia mgomo wa walimu.


8436.jpg

Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bw. Gratian
Mkoba (kushoto) akikimbilia kwenye gari la Polisi jana wakati
risasi zikipigwa angani na polisi ili kutawanya walimu waliokuwa
katika mkutano wa kujadili mgomo uliotarajiwa kuanza nchi nzima leo.
Baada ya tamko la Rais huyo la kusitisha mgomo huo, kutolewa,
walimu walitaharuki na kufanya vurugu zikiwamo za kurusha mawe
kupinga tamko hilo katika ukumbi wa Diamond Jubilee. (Picha na Charles Lucas)
 
Jana nimeangalia taarifa ya habari ya Tv saa mbili usiku... kuna mwalimu mmoja mama mtu mzima hivi amelalamika kwa uchungu hadi kutoa machozi... na ule ni uchungu wa kweli si unafiki au mchezo wa kuigiza. Serikali yetu imeongeza shule nyingi za sekondari... tunasikia hazina walimu... na hawa walioko wamekata tamaa kiasi hiki!!! Hivi hii serikali ya Jakaya inamuhudumia nani?
 
si mara ya kwanza injuction order kutolewa nje ya muda wa kazi, katika ile kesi ya kusimamisha ucgaguzi wa meya kitwana kondo ilifanyika hivyo hivyo, jawabu nikuwa je mtu wa kawaida anaweza kupata huduma hii chaP CHAP KAMA SERIKALI ILIVYOIPATA HATA BAADA YA MASAA YA KAZI?

usisahau pia account ya mafisadi pale NMB tawi la barabara ya morogoro lilivofunguliwa tar 1 may (siku ya wafanyakazi)
 
raismawe.jpg

Rais wa Chama cha Waalimu Tanzania (CWT, Gratias Mukoba
akikwepa mawe kutoka kwa waalimu waliojawa na jazba akikimbilia
gari la polisi , mkutano wa maandalizi ya mgomo ulivunjika, Makakama
Kuu Divisheni ya Kazi ilizuia mgomo wa walimu.

na nimepata fununu kuwa baada tu yakudunda jamaa waalimu walimchagua raisi wao mwingine wa muda kwa hiyo bwana mukoba si raisi wao tena,

NOTE:kama taarifa hii, imeshaandikwa awali basi huna budi ya kuiignore yangu
 
Vijisenti wanavyodai waalimu ni vidogo saana, Coton man akiaahirisha tu safari zake za nje kwa miezi mitatu hawa wanalipwa malimbikizo yote wanayodai. Tatizo kwa sasa rais ni mdhaifu na kabineti yake asilimia 75 si uchafu ndo maana tunajionea haya.
 
Tunawahitaji sana walimu katika vita dhidi ya mafisadi kwani wanatumiwa sana kusimamia uchaguzi na kuwaingiza mafisadi katika madaraka. Ni high time kwao kujua kwamba this time imekula kwao na wakipewa dhamana ya kusimamia uchaguzi tena wasimamie haki na kuhakikisha mafisadi hawana nafasi tena.
 
Tunawahitaji sana walimu katika vita dhidi ya mafisadi kwani wanatumiwa sana kusimamia uchaguzi na kuwaingiza mafisadi katika madaraka. Ni high time kwao kujua kwamba this time imekula kwao na wakipewa dhamana ya kusimamia uchaguzi tena wasimamie haki na kuhakikisha mafisadi hawana nafasi tena.

ni miaka mi3 tu iliopita haya hhayakuweza kutokea au watu tulikuwa hatuna muamko.. the pace is good tusikate tamaa kila mtu akanyage mguu mahali pake na kuyakataa haya na kupreach kwa wengi wizi wa CCM naamini mpaka 2010 mambo yatakuwa ktk level nzuri na tutakuwa tumeshawazika kabisa CCM.. kama kunamtua ameangalia taarifa ta habari ya leo saa moja asbh chanel tena atanielewa ninaposimulia kuwa sikuamini macho yangu wazee watarime walivokuwa na mwamko mkubwa na naashilia kusema kuwa muamko wao ni mkubwa kiliko vijana wengi wa mjini
 
ni miaka mi3 tu iliopita haya hhayakuweza kutokea au watu tulikuwa hatuna muamko.. the pace is good tusikate tamaa kila mtu akanyage mguu mahali pake na kuyakataa haya na kupreach kwa wengi wizi wa CCM naamini mpaka 2010 mambo yatakuwa ktk level nzuri na tutakuwa tumeshawazika kabisa CCM.. kama kunamtua ameangalia taarifa ta habari ya leo saa moja asbh chanel tena atanielewa ninaposimulia kuwa sikuamini macho yangu wazee watarime walivokuwa na mwamko mkubwa na naashilia kusema kuwa muamko wao ni mkubwa kiliko vijana wengi wa mjini



Tarehe October 14, 2008 4:37 AM, Mtoa Maoni: Anonymous

HONGERA sana makamanda. Waongoze vyema wapiganaji wa tarime, wapate maisha bora, na wawe mfano wa kuigwa na majimbo mengine yanayodanganywa kwa kofia, fulana na khanga. Ninapendekeza Tarime itambuliwe na kutangazwe na wapiganaji wote wa tanzania kuwa MAKAO MAKUU ya kampeni tutakayoibatiza "TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA". Ukiwekwa utaratibu mzuri tupo wadau wengi ambao tuko tayari kuchangia linalowezekana. Hii maana yake ni kwamba, vijana watatumwa kutoka majimbo yote tanzania kuja tarime kujifunza mbinu za kuendesha kampeni hiyo. Wapiganaji mnasemaje?​



Comment hapo juu imetoka kwa mdau, website ya Michuzi
Mrithi wa chacha wangwe



.
 
HONGERA sana makamanda. Waongoze vyema wapiganaji wa tarime, wapate maisha bora, na wawe mfano wa kuigwa na majimbo mengine yanayodanganywa kwa kofia, fulana na khanga. Ninapendekeza Tarime itambuliwe na kutangazwe na wapiganaji wote wa tanzania kuwa MAKAO MAKUU ya kampeni tutakayoibatiza "TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA". Ukiwekwa utaratibu mzuri tupo wadau wengi ambao tuko tayari kuchangia linalowezekana. Hii maana yake ni kwamba, vijana watatumwa kutoka majimbo yote tanzania kuja tarime kujifunza mbinu za kuendesha kampeni hiyo. Wapiganaji mnasemaje?[/INDENT][/INDENT]



HII IMEKAA VIZURI SANA MKUU

I SECOND YOU!!!!!!!
 
Mi nadhani hata kama mahakama imetoa zuio la mgomo wao waendelee kugoma tu kwani watawafanya nini? Najua hata jeuri ya kuwafukuza kazi hawana kwani hao walimu wa kuziba hizo nafasi hata nusu yake hawatapatikana......Walimu wana hali mbaya sana jamani tuache utani nadhani hata ile morali ya kazi hawana tena.

1. Tunapojadili hili la walimu tufikirie pia sisi tunawasaidia vipi! kwani walimu wako peke yao nadhani wanahitaji support kutoka kwa kila mtu/asasi nk. katika maeneo yetu tutoe matamko na hata kuwaunga mkono kwa kuandamana nao.
2. Pia tufikirie haya malalamiko tunaya target wapi? Serikali ni kubwa sana na Raisi yupo juu mno. Huku chini huwa kuna watu fulani wanaoziba riziki za walimu mfano; walimu wakuu, wahasibu, ma afisa elimu/uajiri, wakurugenzi mbalimbali. Tupambane nao moja kwa moja hawa, kuna wengine ni wabaya sana wanakwamisha mambo mengi ya msingi bila woga.
Mfano mdogo; kuna matatizo ya mishahara UDSM ambayo yanatokana na watawala hasa Director wa Human Resources na Bursar. wanawanyanyasa wafanyakazi kwa kuwadhurumu mishahara na posho mbalimbali na huwa wanajitetea kuwa walikosea kwenye mahesabu!!!!!!! au sababu nyingine zisizo za msingi. huwa tunamlaumu Kikwete lakini wakati mwingine tunawaacha wanyanyasaji wakubwa!!!!! kikulacho!!
Nadhani na matatizo ya walimu yanasababishwa na baadhi ya mabosi wao ya kukataa kuidhinisha malipo kwani kuna wengine walikwishalipwa.
 
Walimu wafanya mgomo baridi
Maulid Ahmed
Daily News; Wednesday,October 15, 2008 @20:44

Maelfu ya walimu wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu jana waliendesha mgomo baridi katika maeneo mbalimbali nchini, licha ya amri ya Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi ya kuwazuia kugoma.

Mgomo huo baridi uliendeshwa kwa aina tofauti ambako katika baadhi ya maeneo walimu waliwaamuru wanafunzi warudi nyumbani, huku sehemu nyingine wakikusanyika katika maeneo maalumu na kufanya mikutano.

Wakati walimu hao wakiendesha mgomo huo baridi, Serikali imewaomba wavumilie na waendelee kusomesha wakati malipo yao yanaendelea kufanyiwa kazi. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Celina Kombani, alilieleza gazeti hili kuwa walimu wasiolipwa ni wachache na kuongeza; "Waziri wa Elimu (Profesa Jumanne Maghembe) ameshasema wanalipwa.

Nawaomba watuvumilie na wakiendelea na mgomo sheria zipo wanaweza kufukuzwa kazi." Akizungumza na waandishi wa habari jana, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba alisema kuwa walimu wameendesha mgomo baridi ambapo wamekuwa wakiingia darasani pindi wanapowaona wageni wanakwenda shuleni kwao pamoja na maofisa utumishi na maofisa elimu wanaowafuatilia.

Alisema serikali imepitisha fomu maalumu kila shule ambapo kila mwalimu alitakiwa kuijaza kuonyesha kuwa amefika shuleni na kufundisha na kuongeza; "Walimu wamezijaza fomu na wakaendelea kukaa pembeni bila kusomesha pale maofisa wa serikali walipoondoka tu eneo la shule".

Akitoa mfano alisema kwa Mkoa wa Lindi, Ofisa Elimu wa Mkoa huo alifuatana na polisi kwenda shule kadhaa kuwahimiza walimu waingie madarasani lakini walitii alipokuwapo na alipoondoka tu walitoka madarasani na kuendelea na mgomo wao baridi.

Mukoba alisema kuwa kutokana na walimu hao kuendesha mgomo baridi, CWT imekaa kimya na haijawachochea wala kuwakataza kuendesha mgomo huo na kuongeza; "Sisi hatuwezi kuwaambia waache mgomo kwani hatuna fedha za kuwalipa kama wenyewe wanavyotaka ili waache mgomo huo baridi".

Gazeti hili pia lilipotembelea shule kadhaa za jijini Dar es Salaam, lilibaini baadhi ya walimu walikuwa wakifundisha na wengine walikuwa wakiingia darasani wanapoona sura ngeni huku wengine wakikataa kuhojiwa wala kupigwa picha kwa madai kuwa wenzao wakiwaona wanaingia darasani watawaona wamewasaliti.

Mukoba alisema kuwa kutokana na walimu kufanya vurugu juzi na kuwashambulia viongozi wa CWT, kumewafanya wawe washindi kwa sababu serikali imeona kuwa walimu hawataki kusikia lolote isipokuwa haki zao na wanachotaka ni kugoma kufanya kazi.

Gurian Adolf anaripoti kuwa walimu wilayani Mpanda waliripoti shuleni asubuhi lakini muda mfupi badaye waliwarejesha majumbani wanafunzi na baadhi yao kuondoka katika vituo vyao vya kazi na kwenda majumbani huku wakiwaacha walimu wakuu pekee.

Mmoja wa walimu ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema wao wanaendelea na mgomo na hawatatii agizo la mahakama. Wamekubaliana kukukutana kesho kutathmini mgomo wao.
Makubo Haruni anaripoti kutoka Tarime kuwa mamia ya walimu jana walijikusanya Shule ya Msingi Turwa chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa (CWT) wilayani humu, Matinde Magabe na kuapa kuwa hata wakipigwa mabomu ya machozi darasani hawatakanyaga hadi walipwe haki zao zote wanazoidai serikali.

Ofisa Elimu wa Wilaya ya Tarime, Emanuel Johnson, alisema kuwa kugoma kwa walimu hao na kujikusanya ni kinyume cha sheria. Alisema kuwa wengi wa walimu ni wazembe na wameamua kutumia nafasi hiyo kufanya kazi zao binafsi.

Jacob Kambili anaripoti kutoka Mwanza kuwa mamia ya walimu walikusanyika mbele ya Jengo la Ukumbi wa Gandhi badala ya kwenda madarasani. Kutokuwapo kwao madarasani kulidhihirishwa pale maelfu kwa maelfu ya wanafunzi wa shule mbalimbali walipoonekana wakirandaranda katika mitaa ya hapa karibu kutwa mzima jana.

Baada ya majadiliano yasiyo rasmi walimu hao walisema wameazimia kwamba kuanzia sasa, hawataingia madarasani bali watakwenda tu kutia saini kwenye daftari la mahudhurio na kuondoka.

Agosti 12 mwaka huu, CWT ilitoa notisi ya kukusudia kugoma Oktoba 15 lakini Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi iliamuru kusitishwa kwa mgomo huo baada ya serikali kuwasilisha mahakamani hapo hati ya zuio la mgomo.

Walimu hao walikusudia kugoma hadi hapo serikali itakapotekeleza madai yao ikiwamo kuwalipa malimbikizo ya mishahara, posho za uhamisho, kujikimu, usafiri na kutaka upandishaji wa madaraja ufanyike kihalali na walimu walioondoshwa katika orodha ya malipo warejeshwe.
 
Migomo ni suluhisho la matatizo? Je haki za walimu zitapatikana kwa migomo? Nimesikiliza vyombo mbalimbali vya habari kuhusiana na sakata la madai ya walimu. Ninashindwa kuelewa madai ya walimu ni ya haki au la? Sidhani kama walimu ni wajinga wadai kitu ambacho si haki yao. Kilimanjaro nimesikia wahusika wa malipo ya walimu walikuwa wakihaha kuhakikisha walimu wanalipwa ili wasigome. Na pia kutishiwa wasigome. Ina maana serikali ni lazima iamshwe ndio ilipe haki za walimu?

Umefika wakati sasa wa kuwa na utaratibu wa kuhakiki haki ya kila mfanyakazi wa serikali na kulipwa kwa wakati na kwa haki yake. Kwa technologia iliyopo sidhani kwamba ni vigumu kutatua haki za walimu. Unajua mwalimu akienda likizo anatakiwa kulipwa nini na nini halipwi. Itengenzwe programme amayo ukiikomand inatoa kiasi cha kila mwalimu. Wanaofanya mahesabu ya malipo ya walimu kazi yao ni ipi.

Swali: Migomo ina madhara kwa nchi na kidunia?

Kwa wafanyakazi wengi duniani,mgomo ni last resort.
Tunakubali nchi yetu ni masikini lakini umasikini huo kwa kiasi kikucbwa unachangiwa na serikali yetu kukumbatia ufisadi.Hivi kama serikali ingedhibiti zile shs milioni 150 na upuuzi zilizokuwa zinalipwa kwa Richmond/Dowans ingeshindwa kutatua matatizo ya walimu?

Ifahamike kwamba malimbikizo ni moja tu ya matatizo ya walimu.Nenda mashuleni ukaangalie working conditions zao.Kama CCM inaweza kutumia bilioni moja kwa uchaguzi huko Tarime (na ikashindwa...mostly likely hiyo hela imetoka serikalini) inashindikana vp kuboresha mazingira ya kazi ya walimu?

Serikali imeshikwa pabaya na ndio maana imepigana kufa na kupona kujaribu kuzuia mgomo huo wa walimu.Ukitokea inamaanisha watumishi wengine nao watatangaza migomo.Madaktari na manesi are most likely to be next.Wanalipwa duni na working conditions ni poor.Kiama kitakuja pindi polisi nao watakapoacha siasa pembeni na kuingia mtaani kudai haki zao.Hawa watu wanatumika sana lakini mshahara ni kijungujiko.

Serikali inaweza kukimbilia mahakamani kuzuia mgomo,inaweza kutoa vitisho (sijasikia tishio la kufukuza kazi mwalimu atakayegoma) na kutumia mbinu nyingine kibao.Lakini hiyo yote ni kuahirisha tu ufumbuzi wa tatizo.Walimu wanaweza kwenda shule na wasifundishe.Au wanaweza hata kuingia madarasani na kuishia kutia stori tu.Unaweza kumlazimisha punda kwenda mtoni lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji.

Huu ni mwanzo wa mapinduzi ambayo baada ya vyama vya siasa kuchemsha,sasa ni zamu ya wafanyakazi.Tunacho-miss hapa ni akina Lech Walesa,lakini kuna kila dalili watazaliwa sooner than later.
 
Tunajua Tanzania ina uhaba wa waalimu, leo hii Serikali inadiriki kuacha kutoa mishahara na kutoa vitisho eti itafukuza kazi Waalimu watakao goma?

Mwankupuli, find us a win win situation kwa waalimu ili watoto wetu wapate elimu!
 
Date::10/20/2008
Walimu: Hatutazungumza tena na serikali
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi

RAIS wa Chama cha Walimu (CWT), Gratian Mukoba amesema kuwa hakuna mtu anayeweza kusema kuwa madai yao yametekelezwa, isipokuwa walimu wenyewe na kwamba hawatarudi kwenye mazungumzo kwa kuwa hatua hiyo ilishapita.

Walimu wanaidai serikali zaidi ya Sh16 bilioni, ambazo ni malimbikizo ya posho zao mbalimbali, fedha za nauli. Pia wanadai kupandishwa madaraja, lakini serikali katika taarifa yake ya Oktoba 15 ilieleza kuwa imeshalipa zaidi ya nusu ya fedha ambazo walimu wanadai na kwamba imeshaanza kutekeleza zoezi la kupandisha madaraja walimu, huku ikieleza kuwa inaendelea na uhakiki wa madai hayo kwa wale ambao hawajalipwa.

Jana, akizungumza kwenye kipindi cha televisheni ya Star asubuhi, Mukoba alisema CWT haitarudi kwenye mazungumzo kama Jaji William Mandia alivyoshauri kwenye hukumu yake ya kuzuia mgomo kwa muda, akisema kuwa hatua hiyo ya majadiliano ilishapita.

"Tunachosubiri ni utekelezwaji wa kile tulichokubaliana na si kuanza tena mazungumzo," alisema Mukoba. "Mazungumzo yalishafanyika na kulikuwa na makubaliano ambayo serikali inatakiwa iyatekeleze.

"Nilishangaa kuona serikali inadai kuwa ilikutana na CWT na kukubaliana kuwa serikali inatekeleza madai ya walimu. Ukweli ni kwamba sisi tulikaa nao kwa lengo la kutaka kujua serikali inatekeleza vipi makubaliano yaliyofikiwa. Ni hilo tu.

"Hatukukaa na kukubaliana kuwa eti serikali imefanya juhudi za kutosha. Tulitaka kujua jinsi inavyotekeleza makubaliano kwa kuwa yalishafikiwa. Kwa hiyo hatuko tayari kurudi kwenye mazungumzo kwa kuwa kufanya hivyo itakuwa ni kurudi nyuma.

"Tunataka twende kwenye mgomo hadi hapo serikali itakapowalipa walimu madai yao.

"Serikali kudai kuwa imetekeleza madai yetu ni uongo wa mchana kweupe, walichokifanya wao ni mambo ya hovyo hovyo tu, wanadai wamepandisha walimu madaraja, lakini siyo kweli unaweza kukuta walimu walioanza kazi pamoja, mmoja kapanda madaraja mawili, mwingine hakuna, sasa huu ni utaratibu gani, upandishaji madaraja una taratibu zake,"alisema.

"Huu ni mgomo unaotajwa na sheria. Ni mgomo halali kabisa kwa kuwa umefuata taratibu zote. Hivyo walimu wanayo haki ya kugoma ndio maana tumekata rufaa kutaka amri ya kuuzuia mgomo iondolewe.

"Juzi tulikuwa na semina ya Tucta kuhusu vyama vya wafanyakazi. Mtoa mada mmoja kutoka Nigeria, alishangaa kwamba serikali imekimbilia mahakamani kuuzuia mgomo. Alituambia kuwa hiyo ni mara ya kwanza kwa serikali kukimbilia mahakamani.

"Na sisi tunasema, kama serikali inadai kuwa imetekeleza madai ya walimu, ilienda mahakamani kufanya nini. Si imeshatekeleza."

Alikuwa akimaanisha kuwa kama ilishalipa madai ya walimu, basi mgomo ungekuwa batili na wale wote ambao wangehusika, wangeadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

"Kuna zile nyongeza za kila mwaka ambazo tulikubaliana ziongezwe, cha kushangaza katika mishahara waliyochukua walimu, hakuna hiyo nyongeza, sasa wanataka sisi tufanyeje,"alisema.

Kuhusu taarifa kuwa CWT na serikali walifikia maafikiano ambayo yalisainiwa na katibu wa chama hicho, Mukoba alisema taarifa iliyotolewa na serikali ililenga kupotosha umma.

"Anayeweza kusema kuwa walimu wamelipwa madai yao ni walimu wenyewe tu," alisema Mukoba katika kipindi hicho kilichorushwa moja kwa moja.

"Walimu ndio wanaoidai serikali na hivyo wakilipwa, ndio watakaoamua kuacha mgomo, lakini si mtu mwingine yeyote."

Mukoba pia alieleza kusikitishwa na kitendo cha serikali kuugeuza mgomo wa walimu kuwa wa viongozi wa CWT tu, akisema hizo ni mbinu za kuudhoofisha.

Mukoba alinusurika kupigwa wakati alipoenda kwenye mkutano, ambao ulikuwa uwe wa uzinduzi wa mgomo, kuwaeleza walimu kuwa Mahakama Kuu imeagiza mgomo huo usifanyike.

"Haikuwa kauli yangu mimi," alisema. "Nilikuwa natekeleza maagizo ya Mahakama Kuu ambayo iliagiza pande zote mbili zinazovutana kutoa matangazo kueleza wanachama wao kuwa mgomo umezuiwa na mahakama.

"Ile ilikuwa ni kauli ya mahakama na mimi ndio nilikuwa natekeleza amri ya mahakama. Lakini msimamo wa walimu umeonekana."

Pamoja na Jaji William Mandia wa Mahakama Kuu, kitengo cha kazi, kutoa amri ya muda ya kuzuia mgomo huo, walimu walipuuza na hadi sasa wanaendelea na mgomo baridi kwenye shule kadhaa, hasa za msingi.

Mukoba alisema CWT inasubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kuhusu ombi lao la kutaka amri ya kuzuia mgomo huo iondolewe ili serikali iwajibike kuwalipa walimu.

"Huu ni mgomo ambao unatajwa na sheria ya nchi," alisema kiongozi huyo. "Tumefanya.
 
Semina ya majaji yakwamisha rufaa ya walimu
Gedius Rwiza na Happines Matanji

SEMINA ya majaji inayoendelea mjini Same, imesababisha rufaa ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ya kupinga amri ya muda ya kuzuia mgomo, kutofanyiwa kazi na sasa suala lao litashughulikiwa Oktoba 27, ikiwa ni siku sita kabla ya majaji wote kuanza likizo ya mwaka.

CWT iliwasilisha rufaa hiyo Ijumaa ikitaka Mahakama ya Rufaa kutengua amri ya Jaji William Mandia wa Mahakama ya Kazi ya kuzuia mgomo wa walimu uliokuwa uanze Oktoba 15 kwa madai kuwa mgomo huo ungeathiri sekta nzima ya elimu, na hasa wanafunzi wa kidato cha nne waliokuwa kwenye mitihani ya mwisho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufaa, Sivangilwa Mwangesi alisema maombi ya CWT ya kutaka amri ya kuzuia mgomo iondolewe, hayajafanyiwa kazi hadi Jumatatu ijayo kwa sababu majaji wote wako Same mkoani Kilimanjaro wakihudhuria semina.

Mwangesi aliongeza kuwa, kwa sasa hawawezi kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo hadi jaji mkuu atakaposaini na kupanga jaji atakayesikiliza kesi hiyo na kwamba, majaji hao watarejea mwishoni mwa wiki hii.

“Hivi sasa hivi ndio napokea maombni hayo, lakini sina msaada zaidi ya kuwaambia kwamba maombi hayo yatashughulikiwa wiki ijayo kwa kuwa hapa hakuna jaji hata mmoja ambaye angeweza kuyafanyia kazi. Nawaomba walimu wavute subira hadi wiki ijayo kwa sababu majaji wote watakuwepo,” alisema Mwangesi.

Kwa kawaida majaji wote huenda likizo ndefu ya mwaka kuanzia Novemba 2, hivyo iwapo rufaa hiyo haitapangiwa jaji kabla ya tarehe hiyo, kuna uwezekano suala la walimu likaamuliwa Januari mwakani.

Akizungumzia suala hilo, rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema anashangazwa na kesi yao kupigwa kalenda wakati serikali iliomba siku moja kesi ikasikilizwa na kutolewa hukumu, lakini maombi ya rufaa hayapewi kipaumbele.

"Hii inanipa imani kuwa maombi yetu yanaweza kufanikiwa kulingana na taratibu tulizotumia katika kutangaza mgomo," alisema Mukoba.

Mukoba alisema kadri kesi yao inavyozidi kucheleweshwa ndivyo taifa linavyozidi kuharibika kwani walimu waliowengi wanasema kuwa hawataacha mgomo baridi hadi kesi yao itakaposikilizwa ingawa haijulikani itaisha lini.

Alisema serikali inaona imewaweza walimu, lakini wanaopata shida ni wanafunzi na jamii kwa ujumla kwani wahusika ambao wanaonekana kutojali suala hili haliwagusi kwa kuwa wako ngazi za juu na watoto wao wanasoma shule maalumu.

Tangu kuzuiwa kwa mgomo huo, walimu wamekuwa wakifundisha kwa utashi wao, huku baadhi ya shule wakikusanyika ofisini na kupiga soga na katika shule nyingine wakifundisha masomo mawili hadi matatu kwa siku.

Mukoba pia alisisitiza kuwa walimu wasisaini fomu yoyote inayotumwa na serikali kuhusu mgomo, kwani sheria hairuhusu kufanya uamuzi wowote wakati kesi ikiendelea.

"Kuna fomu zinazosambazwa katika shule mbalimbali ambazo zinawataka walimu wasishiriki mgomo huu. Walimu walio wengi wamepinga vikali kujaza fomu hizo kwa kuwa kufanya hivyo ni kuwarubuni walimu wasitishe mgomo bila kupata haki zao," alisema.

“Waache wazidi kupiga kalenda, lakini ipo siku tutapata mwafaka. Kadri wanavyozidi kupiga kalenda ndivyo wanavyozidi kuharibu taifa na wanafuzi kwa ujumla kwa kuwa walimu wameahidi kutoacha mgomo hadi kesi itakaposikilizwa.

Walimu wanaidai serikali zaidi ya Sh16 bilioni ambazo ni malimbikizo ya malipo yao mbalimbali, ikiwa ni pamoja na fedha za nauli, posho na pia wanadai kupandishwa daraja.

Serikali ilisema katika tangazo lake la Oktoba 15 kuwa imeshalipa zaidi ya Sh7 bilioni na kwamba zilizosalia zitalipwa baada ya uhakika wa madai ya walimu kumalizika, huku ikijitetea kuwa baadhi ya walimu wameshapandishwa daraja.

Lakini kauli hiyo ilipingwa vikali na Mukoba aliyesema kuwa hakuna mtu anayeweza kuwasemea walimu kuwa wameshalipwa haki zao zaidi ya walimu wenyewe na akahoji kuwa iwapo serikali ilishalipa, ilikuwaje ikakimbilia mahakamani.


Source:Mwananchi

 
Kwa habari hii nina uhakika mia kwa mia serikali haina nia njema na sekta ya elimu nchini kama kweli wanajali wanafunzi ambao ndio waathirika (Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi) fanya wanavyofanya sasa. Hongereni Majaji wetu mnakula allawances zenu kiulainiiiii wala hamgombwi lakini mjue watoto wetu wanakosa elimu na mwisho wa mwaka unaingia watajibu nini kwenye hiyo mitihani?kama itakuwepo?

Tunajua wanasiasa na majaji nyie sio wenzetu tena na watoto wenu hawasomi shule ya msingi kurasini shimo la udongo!Lakini muwe na utu japo artificial!hamuogopi kupigwa mawe?
 
Bwana Mukoba na walimu wengine mmekwishachemsha mambo yakishaingia mahakamani basi ujue yanaweza kuchukua hata miaka kufukia suluhisho kwani wao sio ndio wanapangiwa. Mlivyosema mgomo ulikuwa halali na ile mahakama haikuwa na uwezo wa kuwazuia kugoma kwanini msinge endelea kugoma na sheria ingefuata baadae?? hii ni kuonyesha hamna msimamo. Kama ni mtego basi naweza kusema mmeingia wazima wazima. Nafikiri mtakuwa mmesahau yale mliyokuwa mnatufundisha mashuleni kuwa mahakama ni muhimili mmojawapo wa serikali. Poleni sana naona mlikuwa mmelisahau hilo, sasa mmeshapata practical example bila shaka somo litakuwa zuri zaidi darasani maana naona mmeshaanza na kuingia madarasani kama kawaida. Poleni sana hii ndio "inji" yenu. Kidumu chama cha ma p i n d u z i ....???????? Dawa ya migomo imeshapatikana na ni very simple hakuna sababu ya kubishana na wagomaji kwenye vyombo vya habari, waziri anasubiri inabaki siku mbili anaingia mahakamani na kesho yake mahakama inatangaza kusitisha mgomo, simple like that mkikata rufaa basi ndio ule mchezo wa kalenda unaanzia hapo mpaka sirikali ipate uwezo wa kutatua ama mchoke kufuatilia.
 
Back
Top Bottom