Mhandisi Fatma Rembo Apania Kufanya Makubwa ndani ya UWT Mkoa wa Iringa

Mhandisi Fatma Rembo Apania Kufanya Makubwa ndani ya UWT Mkoa wa Iringa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MHANDISI FATMA REMBO - APANIA KUFANYA MAKUBWA NDANI YA UWT MKOA WA IRINGA

Mjumbe wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa 2022-2027 Kutokea Mkoa wa Iringa Ndugu Eng. Fatma Rembo amefanya ziara maeneo mbalimbali Mkoa wa Iringa na kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Katika ziara ya tarehe 09 Machi, 2023 Wilaya ya Kilolo, Eng. Fatma Rembo amechangia Shilingi 1,000,000 kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa UWT Wilaya ya Kilolo na kuahidi kununua Pikipiki Kwa ajili ya shughuli za UWT huku akionya vikali vitendo vya Ukatili na Unyanyasaji wa kijinsia wa Watoto wa kike na watoto wa kiume.

Eng. Fatma Rembo mnamo tarehe 08 Machi, 2023 aliadhimisha Siku ya wanawake Duniani kwa kutembelea Wodi ya Wanawake (wakina mama waliotoka kujifungua) katika hospitali ya Mkoa wa Iringa huku wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego. Maadhimisho kimkoa yaliadhimishwa Wilaya ya Kilolo.

Aidha, Eng. Fatma Rembo tarehe 04 Machi, 023 alishiriki Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) la Wilaya ya Iringa Vijijini ambapo alichangia Matofali 1000 na Mifuko 100 ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Mtendaji wa UWT wa Wilaya.

Pia, Uongozi wa UWT Wilaya ya Iringa Vijijini walimpatia Eng. Fatma Rembo Hati ya Pongezi pamoja na zawadi nyingine mbalimbali kutokana na mchango wake katika Chama Cha Mapinduzi na jamii inayomzunguka.

Eng. Rembo akizungumza katika baraza hilo, alisisitiza na kuhimiza Umoja na Mshikamano katika utendaji wa kazi za UWT katika wilaya ya Iringa Vijijini.

Vile vile, tarehe 03 Machi, 2023 Eng. Rembo alishiriki Kongamano la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Wilaya ya Iringa Mjini la kupinga vitendo vya Unyanyasaji wa Kijinsia, Ubakaji na Ulawiti kwa watoto, Kongamano lililoanza kwa matembezi kutoka ofisi za CCM Wilaya ya Iringa Mjini na kuhitimishwa katika ofisi za CCM Mkoa wa Iringa ambako kongamano hilo lilifanyika.

Aidha, tarehe 10 Februari, 2023 Eng. Rembo alipata fursa ya kushiriki Baraza Kuu la UWT la Mkoa wa Iringa chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Zainab Mwamwindi. Eng. Rembo alichangia hoja mbalimbali zilizojadiliwa zinazohusu masuala ya Umoja wa Wanawake wa Mkoa wa IRINGA.

Pamoja na wajumbe wengine, alikuwepo ni Mkuu wa Mkoa wa IRINGA, Mhe. Halima Dendego, Katibu wa CCM wa Mkoa wa IRINGA Ndugu Rukia Mkindu, Viongozi na Wajumbe wengine wa Mkoa wa Iringa.

#UWTImara
#WanawakeJeshiKubwa
#KaziIendelee

WhatsApp Image 2023-03-10 at 17.10.12(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-10 at 17.10.05.jpeg
 
Watu tunajadili issues za maana wewe unatuletea mambo ya kucheza na makopo
 
Halafu hatutumii neno ndugu kwa mwanamke tunatumia bi fulani sio ndugu fulani.
Ndani ya CCM, kama ni katika siasa za Chama huwa kila mtu ni Ndugu, wazee waliweka hivyo kwa sababu za msingi sana. Hata Mwenyekiti wa CCM Taifa haitwi Mhe., ila ni Ndugu Samia Suluhu Hassan.
 

MHANDISI FATMA REMBO - APANIA KUFANYA MAKUBWA NDANI YA UWT MKOA WA IRINGA

Mjumbe wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa 2022-2027 Kutokea Mkoa wa Iringa Ndugu Eng. Fatma Rembo amefanya ziara maeneo mbalimbali Mkoa wa Iringa na kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Katika ziara ya tarehe 09 Machi, 2023 Wilaya ya Kilolo, Eng. Fatma Rembo amechangia Shilingi 1,000,000 kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa UWT Wilaya ya Kilolo na kuahidi kununua Pikipiki Kwa ajili ya shughuli za UWT huku akionya vikali vitendo vya Ukatili na Unyanyasaji wa kijinsia wa Watoto wa kike na watoto wa kiume.

Eng. Fatma Rembo mnamo tarehe 08 Machi, 2023 aliadhimisha Siku ya wanawake Duniani kwa kutembelea Wodi ya Wanawake (wakina mama waliotoka kujifungua) katika hospitali ya Mkoa wa Iringa huku wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego. Maadhimisho kimkoa yaliadhimishwa Wilaya ya Kilolo.

Aidha, Eng. Fatma Rembo tarehe 04 Machi, 023 alishiriki Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) la Wilaya ya Iringa Vijijini ambapo alichangia Matofali 1000 na Mifuko 100 ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba ya Mtendaji wa UWT wa Wilaya.

Pia, Uongozi wa UWT Wilaya ya Iringa Vijijini walimpatia Eng. Fatma Rembo Hati ya Pongezi pamoja na zawadi nyingine mbalimbali kutokana na mchango wake katika Chama Cha Mapinduzi na jamii inayomzunguka.

Eng. Rembo akizungumza katika baraza hilo, alisisitiza na kuhimiza Umoja na Mshikamano katika utendaji wa kazi za UWT katika wilaya ya Iringa Vijijini.

Vile vile, tarehe 03 Machi, 2023 Eng. Rembo alishiriki Kongamano la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Wilaya ya Iringa Mjini la kupinga vitendo vya Unyanyasaji wa Kijinsia, Ubakaji na Ulawiti kwa watoto, Kongamano lililoanza kwa matembezi kutoka ofisi za CCM Wilaya ya Iringa Mjini na kuhitimishwa katika ofisi za CCM Mkoa wa Iringa ambako kongamano hilo lilifanyika.

Aidha, tarehe 10 Februari, 2023 Eng. Rembo alipata fursa ya kushiriki Baraza Kuu la UWT la Mkoa wa Iringa chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Zainab Mwamwindi. Eng. Rembo alichangia hoja mbalimbali zilizojadiliwa zinazohusu masuala ya Umoja wa Wanawake wa Mkoa wa IRINGA.

Pamoja na wajumbe wengine, alikuwepo ni Mkuu wa Mkoa wa IRINGA, Mhe. Halima Dendego, Katibu wa CCM wa Mkoa wa IRINGA Ndugu Rukia Mkindu, Viongozi na Wajumbe wengine wa Mkoa wa Iringa.

#UWTImara
#WanawakeJeshiKubwa
#KaziIendelee
Anavyotumia neno "Eng" kasajiliwa na bodi kama professional engineer? Au hajui kujiita engineer ikiwa haujasajiliwa ni kosa kisheria?
 
Anavyotumia neno "Eng" kasajiliwa na bodi kama professional engineer? Au hajui kujiita engineer ikiwa haujasajiliwa ni kosa kisheria?
Kwani ukiwa Registered kama Graduate Engineer hairuhusiwi kujiita? Mimi najiitaga Injinia na wala sijasajiliwa mbona, waje wanakamate tu, kusoma engineering nisome mimi, ada nilipe mimi, joho nivae mimi, cheti changu naitwa engineer halafu bado niwekewe masharti nisijiite injiniaaaa....bongo bhanaaa kuna mambo mengi kama unga wa ngano
 
Back
Top Bottom