Mhandisi John Nzulule Mtendaji Mkuu wa Wakala wa ndege za serikali amekua akishirikiana na nani?

Mhandisi John Nzulule Mtendaji Mkuu wa Wakala wa ndege za serikali amekua akishirikiana na nani?

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu.

Kwa uzoefu wake wa kutupiga sasa aliamua kutupiga kwa kipigo cha mbwa koko kwa kuweka cha juu cha mzigo wake wa dola 49 milioni katika ununuzi wa ndege ya mizigo ya ATCL. Fikiria badala ya kulipa dola milioni 37 akataka serikali ilipe dola milioni 86! Hii nadhani amevunja rekodi sijui tuite ya nchi au dunia!

Lakini bado natafakari kuwa ufisadi huu hafanyi peke yake. Lazima kuna mtu au genge la watu anashirikiana nao. Nashauri vyombo vinavyohusika na uchunguzi vimuhoji kwa kina mpaka ataje wenzake wanaohujumu nchi hii. Vinginevyo kundi hili litaendelea na ufisadi wake hadi nchi hii ifilisike kabisa!
 
Mhandisi John Nzulule

John Nzulule. Aircraft Engineer at Tanzania Government Flight Agency. TANZANIA GOVERNMENT FLIGHT AGENCY


March 28, 2023, 11:18 am
Waziri Mkuu Kassim akizungumza Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala la Ndege za Serikali (TGFA) John Nzulule, wakati alipotembelea karakana ya Wakala wa Ndege za Serikali, Machi 28, 2023 jijini Dar es Salaam.

WAZIRI MKUU AKAGUA UWANJA WA NDEGE TERMINAL I

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua uwanja wa ndege wa Terminal I ili kujiridhisha na kazi ya ukarabati unaoendelea kwenye eneo la kuegesha na kufanyia matengenezo ya ndege za Serikali.

Pia amewataka viongozi na wafanyakazi wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) wahakikishe wanashirikiana na mamlaka husika kuufanya uwanja huo wakati wote unakuwa nadhifu ili kukidhi hadhi ya viongozi wa kitaifa na kimataifa wanaoingia ama kuondoka nchini.

Akizungumza na viongozi na watumishi wa TGFA mara baada ya kufanya ukaguzi huo leo (Jumanne, Machi 28, 2023) jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa TGFA, Mhandisi John Nzulule ahakikishe ujenzi huo unakamilika haraka. “Serikali ilishatoa kibali kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa karakana hiyo ambayo nimeelezwa itakapokamilika itawezesha kuegesha ndege kubwa mbili kwa wakati mmoja pale zinapohitaji matengenezo.”

Pia amewaagiza Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwan Kikwete na Katibu Mkuu wa Utumishi, Bw. Juma Mkomi wafuatilie maslahi na motisha za watumishi wa taasisi hiyo ili kuinua ari yao ya utendaji kazi.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na watumishi hao, Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwan Kikwete alimweleza Waziri Mkuu kwamba Serikali ilitoa sh. bilioni 2.5 za ujenzi wa awamu ya kwanza ya ofisi za TGFA ambao umekamilika na ofisi zimeanza kutumika.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa TGFA, alisema kukamilika kwa jengo hilo kumesaidia kuboresha utekelezaji wa majukumu ya Wakala kwa idara zilizopo uwanja wa ndege kwa kuwa lina nafasi za kutosha na mifumo ya kisasa kwa ajili ya marubani, wahandisi, wahudumu wa ndege na watumishi wengine.

Alisema awamu ya pili ya ujenzi inahusisha ujenzi wa eneo la kuegesha na kufanyia matengenezo ya ndege na inatarajiwa kuanza hivi karibuni kwa sababu kibali cha ujenzi kimeshapatikana. “Taratibu za kumpata mkandarasi zimeshakamilika na taratibu zote za kimkataba zimekamilika.

Tunaahidi kusimamia kazi hii ili kupata thamani halisi ya fedha (value for money) katika mradi huu,” alisema
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
Daah! Mwenye pic yake atuwekee tumjadili vizuri.

Awesome hao walioshiriki upigaji huu. Na akamatwe sio aachwe!
 
Kama kweli kwenye ndege kapiga dili kubwa hivyo, kwenye ujenzi hakuna usalama.
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
Ripoti ya CAG umeiona alipozungumzia ujenzi wa reli toka makutopora kwenda tabora? Watu wamepiga hata huyo wa ndege haingii ndani mzee
 
Hizo pasenti za Cha juu, Jiwe alikuwa anazipiga kwa Kila ndege iliyonunuliwa, ndio maana alikuwa ananunua ndege kwa wingi kama kapata uchizi, kama alinunua ndege kumi, maana yake kapiga karibu trilioni, sema kwa Sasa dili limeiva na yeye kafa, hakuna wa kuziba kelele.
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
NCHI ILIKWISHA FILISIKA INA ISHI KWA MIKOPO NA TOZO WAJANJA WANAPIGA HIZO HIZO
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
Hapo Nwigulu na Makame hawachomoki, Ila Kwa vile ni vipenzi wa mama mhadisi amekuwa Scape goat
 
Kwa uzoefu wake wa kutupiga sasa aliamua kutupiga kwa kipigo cha mbwa koko kwa kuweka cha juu cha mzigo wake wa dola 49 milioni katika ununuzi wa ndege ya mizigo ya ATCL. Fikiria badala ya kulipa dola milioni 37 akataka serikali ilipe dola milioni 86! Hii nadhani amevunja rekodi sijui tuite ya nchi au dunia!
Wahenga walisema ukicheza na mbwa atakufuata msikitini. Sasa mbwa kaona bora avunje mwiko. Hakuogopa.
Sikua na lengo lakutumia lugha kali ila nimenukuu wahenga
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
unadhani kwa akili toka pale rais alipoongea jamaa itakuwa kaachwa?
 
Utatukana watu bure baadhi ya ufisadi ni mifumo mibovu
 
Ila hii bado mbichi! Kwa serikali mfumo wa malipo makubwa hivi hauanzii ama hauhitimishwi na Ceo peke yake,lazima uwe na baraka kwa walio juu yake.tutajua palipovuja tu ,tuwe na subra ilihali bunge linaendelea na mjadala bado mbichi.tunataka genge lote liwajibishwe siyo ...wa kafara🤣tu
 
Hizo pasenti za Cha juu, Jiwe alikuwa anazipiga kwa Kila ndege iliyonunuliwa, ndio maana alikuwa ananunua ndege kwa wingi kama kapata uchizi, kama alinunua ndege kumi, maana yake kapiga karibu trilioni, sema kwa Sasa dili limeiva na yeye kafa, hakuna wa kuziba kelele.
For your information, zile ndege zilikuwa za bei ndogo uliza uambiwe! JPM alikuwa mzalendo hasa ila inaonesha wewe ndugu zako walikuwa wapigaji ikazaa uhasama unaoonesha hapa JF
 
For your information, zile ndege zilikuwa za bei ndogo uliza uambiwe! JPM alikuwa mzalendo hasa ila inaonesha wewe ndugu zako walikuwa wapigaji ikazaa uhasama unaoonesha hapa JF
Huna ulijualo tusubirie mjadala wa bunge.
 
Daah! Mwenye pic yake atuwekee tumjadili vizuri.
Awesome hao walioshiriki upigaji huu. Na akamatwe sio aachwe!
Angalia hapo #3 ipo akiwa na Waziri Mkuu
 
Mbona unaongeza Chunvi penye sukari? Jamaa kakamatwa kwa kuongeza bei ya invoice ya wadai wa ndege ya ATCL ya mizigo.
Wewe umeenda mbele zaidi na kusema alipiga hata ndege za Serikali na zile za ATCL Je, una ushahidi wowote au ndio DHANA..
Unataka ushahidi gani zaidi ya hiyo invoice ya dola milioni 86?
 
Bila shaka yo yote huyu Mhandisi John Nzulule aliyetenguliwa na Rais si mara yake ya kwanza kutupiga katika ununuzi wa ndege za serikali. Nadhani ametupiga katika ununuzi wa ndege serikali na pia ndege za ATCL ambazo zimekuwa zikinunuwa na serikali kukwepa kukamatwa na wadeni wa ATCL huko majuu...
Nafikiri kutupisha tu haitoshii!
 
For your information, zile ndege zilikuwa za bei ndogo uliza uambiwe! JPM alikuwa mzalendo hasa ila inaonesha wewe ndugu zako walikuwa wapigaji ikazaa uhasama unaoonesha hapa JF
Dreamliner ni bilioni 500, alinunua ngapi? Na kickback ilikuwa ngapi? Acha zile Airbus na mengineyo
 
Back
Top Bottom