Watu8
Platinum Member
- Feb 19, 2010
- 73,773
- 102,126
......
Nawauliza wajameni, hivi hiki anachofanya Mhe. Lissu na wabunge wengine wa upinzani, kumsubulu Madam Spika ambaye ni mwanamke bila huruma, ni sawa kweli?!.
Kikao cha Bunge ni moja ya vikao vya Serikali vinavyozingatia kanuni na sheria kwa mujibu wa miongozo iliyowekwa.
Sidhani kama katika usimamiaji wa kanuni hizo kuna mahali panapoonesha jinsi gani inapaswa kuzingatia kanuni ipi, kiufupi wote wapo chini ya sheria "kanuni za bunge".
Hivyo mkuu dhana ya "kusulubu" inapaswa uiondoe akilini, kwa mantiki ya kwamba sheria ni msumeno hukata pande mbili.
Kawaida, KIONGOZI dhabiti anapaswa kuwa na uelewa na weledi mkubwa zaidi ya wale anaowaongoza ili kuepusha minyukano.
Kiafrika, wanawanake ni ni watu wa kubembelezwa na kuonewa huruma!, hivi hawa wabunge wa upinzani ni watu wa aina gani wasio hata na huruma kwa wanawake?!, leo ilibakia kidogo tuu madam spika angelia!, jee hiki wanachofanya ni sawa kweli?!. Ni haki?!....
Mwanamke ni mtu wa kubembelezwa si tu kwenye familia za Kiafrika, bali ni hulka ambayo wameumbwa nayo hivyo.
Sasa kwa mwanamke ambaye anapewa dhamana ya kuwa kiongozi, tena kiongozi wa Taifa lenye changamoto za siasa zenye mlengo wa kidemokrasia, anapaswa kuushinda udhaifu huo na kuonesha kuwa anaweza badala ya "KUBEBWA".
Bungeni si mahali pa "MAYAYA" kubembeleza watoto ni "platform" inayotoa mustakabali wa Taifa letu.
KAMA HANA UWEZO, BASI HAPASWI KUKIKALIA KITI CHA USPIKA, FULL STOP!!!