Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Na kweli wewe popoma, kama Rais mwenyewe anajulikana, sembuse dg tiss?! Nadhani ukikua utaelewa mambo ya aina hii, ma-dg wote wa tiss tangu enzi za mwalimu watu wanawajua mpaka wanakolala!! hebu kula erythromycine kidogo utulize kipindupindu.
MPE YA UTI
 
Ni kweli mkuu kuna logic flani ipo kwa usiri wa hawa watu.
Mfano mdogo tu idara hii ni only one ambayo ofisi zake hazitambulishwi, huwezi kukuta bango linalokuelekeza kwamba hapa au huku ni ofisi ya Usalama wa taifa.
Nilishawahi kumhoji jamaa kuhusu usiri wao na kazi zao mipaka yake ikoje.
Nikapewa maelezo kwamba shughuli zao zote ni Siri Ila Kwa wao watumishi akanieleza kwamba kuna public security officers na secret security officers.
Nilielezwa kwamba hawa public security officers mara nyingi inajumuisha wale watu wenye vyeo DSO,RSO na deputy ,DG na hata deputy.
Akanieleza kwamba hawa ni public kwani wanahudhuria shughuli nyingi za kijamii kulingana na muundo wetu wanakuwa karibu na ma dc na rc kama wajumbe wa kamati za ulinzi na Usalama hivyo mara nyingi hawatengwi wakati wa utambulisho.
Hawa published c security officers Kwa maelezo ni wachache.
Kwenye Idara watumishi wengi ni ma secret security officers hawa hata baadhi ya wenyewe Kwa wenyewe hawajuani, hawa unaweza ukakuta wamekuwa attached sehemu mbalimbali hata kwenye mabenki binafsi unaweza ukamuona mtu anafanya kazi za u benki officer kumbe pia ni tiss. Na benki husika hata haijui Hilo.
Hata hivyo kufahamika Kwa hawa watu zaidi kipindi hiki kunatokana na maendeleo ya teknologia ya mawasiliano sio kweli kwamba akina Nyerere au mwinyi alikuwa hawatembei nao,ma dg wa tiss wa vipindi hivyo, walikuwepo pamoja kwenye nyadhifa na shughuli mbalimbali za kiserikali na walikuwa wanawatambulisha Ila Kwa kuwa teknologia ya habari ilikuwa duni kipindi hicho watu wengi walikuwa hawawafahamu
 
Mkuu mimi nimewacha kusoma threads zako kwa sababu ya fonts zako zinaniumiza macho. Labda unataka uwe unique humu katika style yako, nakumbuka niliwahi kukueleza hili na ukanikubalia kuwa mimi sikuwa wa kwanza kuleta haya malalamiko kwako kuhusu hili. Kwangu mimi nimeona kumbe hata JPM akishauriwa, suala la kukubali au kukataa ushauri ni haki yake ya msingi. Hence, hatuna haki ya kumjadili, kwa sababu hakupewa kura kuchukuwa ushauri au kujadiliwa na kila anayejisikia.
 
ANGALIZO

Naomba kama unajijua kabisa kuwa uwezo wako wa kuona vitu vya umbali / unyeti / umuhimu wake basi katika huu ' Uzi ' kaa nao mbali kabisa na waachie wenye ' akili ' zao na ' Wachambuzi ' wa masuala haya ya Kijasusi ambao wapo ( tunao ) wengi humu na Sisi Mangumbaru na Mapopoma wengine tuwe watazamaji tu kuliko Kuchangia halafu ukajikuta umevapa / umekosea.

HOJA KUU

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwamba karibia awamu zote za nchi hii nilikuwepo japo ya Hayati Baba wa Taifa ilinikutia nikiwa bado katika Ndoo ya Kuogea na nalilia Uji wa Buruga ( namaanisha nikiwa bado Kichanga kabisa ) ila kwa awamu ya Mzee Mwinyi niliishuhudia bila kusahau ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete na sasa nipo hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli natiririka na naserereka nayo.

Katika Awamu zote hizo sikuwahi hata Siku moja kuwasikia hao Watangulizi wake Rais Dkt. Magufuli wakiwa na tabia ya kupenda ' Kumtajataja ' au hata kupenda kuonyesha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Idara Nyeti nchini ya Usalama wa Taifa ( TISS ) yupo eneo ambalo Wao wapo ila ilikuwa ni mpaka tu labda Mtu akutonye / akuambie.

Nimejuiuliza maswali mengi sana kwani Marais wote Wastaafu walikuwa hawapendi kuwatajataja Wakuregenzi wao Usalama wa Taifa ( TISS DG ) lakini kwa Awamu hii ya Gwala / Tano Rais Dkt. Magufuli anapenda mno ' Kumtaja ' na hata kupenda ' Kumuinua ' Kitini Mkurugenzi wa sasa Dkt. Modestus Kipilimba na bado sijapata jawabu / jibu ila najua kupitia ' Majiniasi ' waliotukuka wa Jamvi hili la JamiiForums leo nitayapata.

Sikuishia tu hapo kama kawaida yangu huwa napenda kwenda ' deep ' zaidi kufanya ' references ' na Mataifa mengine mbalimbali kuanzia na haya Jirani ( tunaofanana kwa Vingi ) kisha hupenda pia kuangalia na yale Mataifa makubwa ambayo yana uwezo mkubwa wa Kuanzia Uchumi, Kijeshi na Kiusalama kuliko Tanzania yetu hii na sijaona mahala ambapo Marais wao huwa wanawataja hovyo tena hadharani Wakurugenzi Wakuu wa Idara zao ' Nyeti ' za Usalama wa Taifa ila kwa Tanzania naona hii tabia inaanza Kuzoeleka.

Kwa maoni au mtazamo wangu mdogo tu ( mnaojua zaidi mtanisaidia ) kwa asili ya hizi nchi zetu tena ambazo zina ' Majaribu ' na ' Matatizo ' mengi ya Kimsingi huku kukiwa na ' Maadui ' wengi wa ndani na nje sidhani na siafiki kabisa tena kwa 100% kwa Wakurugenzi wetu hawa wa hii Idara / Taasisi muhimu kama si nyeti ya Usalama wa Taifa ( TISS ) kutajwatajwa hovyo kwa Watu na hata kujulikana kwakuwa Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye ' maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii hivyo kuna uwezekano na Wao wakaanza Kumjua na Kumzoea kisha hali ikaja kuwa mbaya zaidi huko mbeleni.

Na sidhani pia kama hata ' Kiuweledi ' hivi anavyofanya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. Magufuli la kupenda ' Kumtajataja ' Mkurugenzi Mkuu wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba ni sahihi na kama itapendeza nadhani Watu wa ' Itifaki ' ambao nina uhakika kuwa wengi wenu tunatiririka na kuserereka pamoja 24/7 hapa JamiiForums hili mtaliangalia kwa hayo mapana yake ili utaratibu ule ule uliozoeleka wa zamani wa hawa Wakurugenzi kutojulikana sana au kutajwatajwa hovyo uendelee kwani Kwangu Mimi kwa ' Mazingira ' ya nchi yetu ulikuwa ni utaratibu murua / mujarab / sahihi kabisa kuliko huu wa sasa aliouanzisha Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. Magufuli.

Huu ulikuwa ni mtizamo wangu Mimi kama GENTAMYCINE ila nitashukuru na Watu wengine nao wakija hapa wakichangia huku wale ambao ' watanikosoa ' basi wanikosoe ha ' Hoja ' nzito nzito kwani hata Mimi nataka Kujifunza jambo hapa kutokana na kwamba yawezekana huu utaratibu wa sasa ukawa ndiyo sahihi kuliko ule ambalo nimeukariri / nimeuzoea. Nia na madhamuni tupate afya ya Kimjadala na ya Kimantiki juu ya hili ' Suala ' kusudi mwisho wa Siku wote tupate ' maarifa ' na ' ufahamu ' zaidi.

Karibuni!

Nawasilisha.
Mwanazuoni usiri ulikua zamani. USA mkuu wa CIA kabla ya kuchukua nafasi anawekwa kikaangoni na Senate. Watu ambao hawahitaji kujulikana ni wale waitwao MOLE. Hawa ni ma agent ambao hupelekwa kukusanya data kutoka mahali wanapofanya kazi. Hivyo ni lazima kuficha cover zao. Lakini huyu Kipilimba hakuna asiyejua kuwa ni mkuu wa ama Mkurugenzi wa Usalama wa TAIFA. Labda SHUSHUSHU mkuu wa JF Mheshimiwa Evarist Chahali atatusaidia kwa hili ama rafiki yake mtunzi wa kitabu cha Amazoni Yericko Kiboko Nyerere
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.
Hoja ya mleta uzi, ilikuwa sabbu ya kumtaja taja...
na zaidi kuna wakati hata DDG naye alikuwa anamtaja..
so, kutajwa huku kunakuwa kunaleta viashiria gani ndani ya wasifu wa Rais na Nje ya wasifu wake???
 
Yawezekana ni hofu tu. Wakuu wa hizi taasisi.za usalama ni very public figures. Mara nyingi hasa kwa yale mataifa yenye demokrasia wanajulikana na kutakiwa kuwajibika kwa uma moja kwa moja au kupitia wawakilishi. Kinachokuwa siri ni wale operatives wa huku chini ambao hawatakiwi kujulikana au kuwa na uwajibikaji kwa uma ulio wazi sana. Mifano tunaiona hasa Ulaya na Marekani.

Ila kwa mataifa yenye uelekeo wa kikomunisti, kidikteta, kijeshi na kidini bado hofu zimewatawala. Mambo mengi huendeshwa kwa siri na hata hawa wakuu hujifichaficha. Sababu zinaweza kuwa pamoja na uhalifu mwingi hasa wa kisiasa unaotendwa na hizi taasisi (kwenye mataifa ya aina hii).

Watanzania inabidi tuendelee kupambana tusije tukaangukia kwenye udikteta au utawala wa kijeshi. Inatubidi tuendelee kudai katiba mpya na tasisi huru na zenye kuwajibika kwa uma na siyo kwa aliyewateua.

Uelekeo wetu ni kuwa taifa lenye maendeleo ya viwango vinavyotambulika na dunia na lenye kidemokrasia ya viwango vya nchi za Ulaya. Tusipende kukimbilia mambo ya kikomunisti, kidikteta, na mengine yanayoenenda kinyume na demokrasia.
 
KUMTAJA JAMAA HADHARANI HAKUNA MADHARA COZ HUYO NI KIONGOZI TU NA SIO OPERATIVE AGENT, HATA WA MATAIFA MAKUBWA HUYA WANAJULIKANA NA KWENYE MITANDAO WAPO ILA WALE WANAOTEKELEZA MAJUKUNU NDO HUWA SIRI KUBWA SANA,

KWA MFAN ISRAEL HATA RUBANI WA NDEGE ZA KIVITA SURA YAKE HUWA HAINONYESHWI HATA AKIHOJIWA ILA WAKUU WAO HUONEKANA.



Gina Cheri Haspel (née Walker, October 1, 1956) is an American intelligence officer serving as Director of the Central Intelligence Agency (CIA) since 2018
.
igres.jpg



Alexander Vasilyevich Bortnikov (Russian: Алекса́ндр Васи́льевич Бо́ртников; born 1951) is a Russian official. He has been Director of the FSB since May 12, 2008.

imgres.jpg




Director of Mossad
Incumbent
Assumed office

January 2016Prime Minister Benjamin NetanyahuPreceded by Tamir Pardo9th National Security Advisor (Israel) In office
August 2013 – January 2016Preceded by Yaakov AmidrorSucceeded by Yaakov Nagal (Acting)


220px-Yossi_Cohen_(cropped).jpg



The new head of MI6 has been named as Alex Younger, a career spy who has worked in the Secret Intelligence Service (SIS) for more than 20 years. He is replacing Sir John Sawers, who announced he was stepping down after five years as SIS chief earlier this year.Oct 3, 2014

imgres.jpg
 
Hiyo ni defending mechanism tu.
Anajaribu kupeleka ujumbe kwamba anawatumia sana vibarua wa DGoTISS, hawalali hivyo wakosoaji wake lazima watambue unavyoiba mifugo usifikiri kama umewini ila ukumbe yupo mchungaji anaeweka kikao na wenye mifugo.

Kwa hiyo hiyo ni kujaribu kutisha kama alivyo tumia jeshi katika kufanya manunuzi ya korosho na kufungia maduka ya FOREX .

Hatua hii ikizoeleka watesi wake wataona ni kawaida tu hivo hawatahofia kusonga mbele kwani hao wameshakuwa washikaji,wachumba tu!

Njia hii ya kutaja taka wakuu wa vyombo vya ulinzi, usalama na ujasusi hadharani na bila sababu au mazingira yeyote yanayo lazimisha kufanya hivo sio nzuri na mara nyingi huwa na mwisho mbaya kwa mtajaji na mtajwa!
Yaani nyie jamaa kila kitu mnahisi mnatishwa mara mnaonewa.Mnajihesabia haki hadi mnapitiliza.
 
ANGALIZO

Naomba kama unajijua kabisa kuwa uwezo wako wa kuona vitu vya umbali / unyeti / umuhimu wake basi katika huu ' Uzi ' kaa nao mbali kabisa na waachie wenye ' akili ' zao na ' Wachambuzi ' wa masuala haya ya Kijasusi ambao wapo ( tunao ) wengi humu na Sisi Mangumbaru na Mapopoma wengine tuwe watazamaji tu kuliko Kuchangia halafu ukajikuta umevapa / umekosea.

HOJA KUU

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwamba karibia awamu zote za nchi hii nilikuwepo japo ya Hayati Baba wa Taifa ilinikutia nikiwa bado katika Ndoo ya Kuogea na nalilia Uji wa Buruga ( namaanisha nikiwa bado Kichanga kabisa ) ila kwa awamu ya Mzee Mwinyi niliishuhudia bila kusahau ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete na sasa nipo hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli natiririka na naserereka nayo.

Katika Awamu zote hizo sikuwahi hata Siku moja kuwasikia hao Watangulizi wake Rais Dkt. Magufuli wakiwa na tabia ya kupenda ' Kumtajataja ' au hata kupenda kuonyesha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Idara Nyeti nchini ya Usalama wa Taifa ( TISS ) yupo eneo ambalo Wao wapo ila ilikuwa ni mpaka tu labda Mtu akutonye / akuambie.

Nimejuiuliza maswali mengi sana kwani Marais wote Wastaafu walikuwa hawapendi kuwatajataja Wakuregenzi wao Usalama wa Taifa ( TISS DG ) lakini kwa Awamu hii ya Gwala / Tano Rais Dkt. Magufuli anapenda mno ' Kumtaja ' na hata kupenda ' Kumuinua ' Kitini Mkurugenzi wa sasa Dkt. Modestus Kipilimba na bado sijapata jawabu / jibu ila najua kupitia ' Majiniasi ' waliotukuka wa Jamvi hili la JamiiForums leo nitayapata.

Sikuishia tu hapo kama kawaida yangu huwa napenda kwenda ' deep ' zaidi kufanya ' references ' na Mataifa mengine mbalimbali kuanzia na haya Jirani ( tunaofanana kwa Vingi ) kisha hupenda pia kuangalia na yale Mataifa makubwa ambayo yana uwezo mkubwa wa Kuanzia Uchumi, Kijeshi na Kiusalama kuliko Tanzania yetu hii na sijaona mahala ambapo Marais wao huwa wanawataja hovyo tena hadharani Wakurugenzi Wakuu wa Idara zao ' Nyeti ' za Usalama wa Taifa ila kwa Tanzania naona hii tabia inaanza Kuzoeleka.

Kwa maoni au mtazamo wangu mdogo tu ( mnaojua zaidi mtanisaidia ) kwa asili ya hizi nchi zetu tena ambazo zina ' Majaribu ' na ' Matatizo ' mengi ya Kimsingi huku kukiwa na ' Maadui ' wengi wa ndani na nje sidhani na siafiki kabisa tena kwa 100% kwa Wakurugenzi wetu hawa wa hii Idara / Taasisi muhimu kama si nyeti ya Usalama wa Taifa ( TISS ) kutajwatajwa hovyo kwa Watu na hata kujulikana kwakuwa Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye ' maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii hivyo kuna uwezekano na Wao wakaanza Kumjua na Kumzoea kisha hali ikaja kuwa mbaya zaidi huko mbeleni.

Na sidhani pia kama hata ' Kiuweledi ' hivi anavyofanya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. Magufuli la kupenda ' Kumtajataja ' Mkurugenzi Mkuu wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba ni sahihi na kama itapendeza nadhani Watu wa ' Itifaki ' ambao nina uhakika kuwa wengi wenu tunatiririka na kuserereka pamoja 24/7 hapa JamiiForums hili mtaliangalia kwa hayo mapana yake ili utaratibu ule ule uliozoeleka wa zamani wa hawa Wakurugenzi kutojulikana sana au kutajwatajwa hovyo uendelee kwani Kwangu Mimi kwa ' Mazingira ' ya nchi yetu ulikuwa ni utaratibu murua / mujarab / sahihi kabisa kuliko huu wa sasa aliouanzisha Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. Magufuli.

Huu ulikuwa ni mtizamo wangu Mimi kama GENTAMYCINE ila nitashukuru na Watu wengine nao wakija hapa wakichangia huku wale ambao ' watanikosoa ' basi wanikosoe ha ' Hoja ' nzito nzito kwani hata Mimi nataka Kujifunza jambo hapa kutokana na kwamba yawezekana huu utaratibu wa sasa ukawa ndiyo sahihi kuliko ule ambalo nimeukariri / nimeuzoea. Nia na madhamuni tupate afya ya Kimjadala na ya Kimantiki juu ya hili ' Suala ' kusudi mwisho wa Siku wote tupate ' maarifa ' na ' ufahamu ' zaidi.

Karibuni!

Nawasilisha.
Kaka mimi hii kitu nishaiona muda sana na inanitatiza lakini naamini jiwe hajui namna jamaa wanavyotakiwa kufanya kazi,ndo hoja ya wale wanaodai jiwe hakuandaliwa na mfumo kuwa state man inapata nguvu.
Wakati mwingine akimuinua hadi mimi nayefatilia kupitia TV naona aibu. Kwa mfumo wetu na muundo wa idara sio kila mtu anatakiwa kuonekana /kujulikana, ndo maana wenzetu kama UK wana idara zaidi ya moja kama MI5 na MI6 au kule US wana FBI na CIA.
Naamini mkuu alivyoanza phase one kuna vitu vingi alikuwa hayuko familia navyo na kadri muda unavyoenda naona pase ya kujifunza inaongezeka, kumbuka hata aina ya speech na approach ya mambo.
Kupitia jukwaa hili tunafikisha ujumbe sehemu husika, amini kupitia hapa JF tunaelimisha na utaona changes.

Asante kwa uzalendo mkuu, unaipenda Tanzania.
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.
Juzi nimehoji hivi ni lazima mtu kila siku apost thread humu?Kuna watu yaani wanapost vitu vya ajabu sana na wengi ni kutaka sifa za likes tu.Kiujumla jamaa ujuaji mwingi sana na akiambiwa ulichopost ni pumba anakuja juu kwa matusi.
 
Kuna vyeo vya idara ya usalama watu wanajulikana na siyo siri kama huyo DG wa usalama wapo hata mikoa RSO na wilayani DSO kila mtu anamjua na anajua kazi zake.Sioni kama ni tatizo hata pale anapotajwa hadharani.na hata huwa wana mikutano yao ya kimataifa duniani huko wanakutana na picha wanapiga za pamoja na zinasambaa pia mfano nakumbuka walikutano Kigali Rwanda wakuu wote wa Idara ya usalama kwa nchi za africa.
 
Nilikuja kumjua mkuu Wa tiss baada ya Ulimboka kunatwa na huyu Wa sasa lkn huko nyuma sikuwahi kuwasikia wala kuwaona nami nahitaji kuelewa zaidi kulikoni
 
Amtaje au asimtaje hadharani, watu wakihitaji kumjua watamjua tu. Ifikie wakati tuamini integrity ya watu wetu. Hata hivyo TISS ni chombo halali cha serikali kwahiyo hakuna ubaya mkuu wao kufahamika. Kazi zao kua siri ni sawa ila sio executives.
Pamoja na mambo mengine, Rais JPM anajivunia kazi aliyomkabidhi na anayoifanya DG wa TISS hususan kwa tempo na mfumo wake wa utawala.
Akiwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, nadhani pia ndiye aliyemshauri kuwa na walinzi wengi zaidi kuliko viongozi waliomtangulia. Hali halisi ya usalama wake, Rais Magufuli anahitaji ulinzi mkubwa sana wakati wote na popote dhidi ya wanaopinga juhudi za kuwaletea watanzania nchi ya viwanda, na asali na maziwa.
 
GENTAMYCINE

Kindly ondoa wasiwasi ndugu; hakuna madhara/makosa yoyote wala hakuna uweledi uliuvunjwa kwa kutajwa kwa DGIS au ata akitajwa DDGIS wote hao ni just Public Figures...

Makosa yanaweza kutokea endapo kama wakitajwa vijana wafanyao kazi mbalimbali (Ops) kwa majina...kitu ambacho usitegemee kutokea ata siku moja...

Mataifa mbalimbali makubwa ambayo umeyazungumzia kama mifano, siku zote uwataja viongozi waandamizi mbalimbali wa Idara zao za kijasusi siku wanapoteuliwa na ata ktk mambo mengine mbalimbali...e.g.Kama ulifuatilia teuzi za Brennan, Pompeo mpaka Gina Haspel kama D/CIA...

Mfano ata asipotajwa DGIS au kutambulishwa, atakaeweza kufichwa hapa ni yule raia wa kawaida ila kwa wale ambao ni wajuzi wa haya mambo eidha wa ndani au wa mataifa mengine siku zote watawajua tu au ata mkitoa mtu nje ya nchi aje kuchukua nafasi watamjua (kwa majina, familia zao, makazi yao, weakness zao, uchafu wao, nk) ata kabla hawajateuliwa au majina yao hayajakuwa recommended kwa uteuzi...Chief of Stations (COSs) wa mataifa yote na vijana wao waliojificha kwa kivuli cha balozi hii ndio moja ya kazi zao...

Ata raia wa kawaida akijua DGIS au DDGIS ni nani au ata wakiwazoea hakuna lolote baya litaweza kutokea...narudia tena hakuna lolote baya linaweza kutokea...everything is under control, and anything will be dealt accordingly.
Nimefurahi kuskia maneno yako mkuu, naamini kama ulivyosema terms and conditions are applied. Pitia comments zote na yule mjinga wa Kilombelo aliyepo Ng'ambo akijibu nitag
 
GENTAMYCINE

Kindly ondoa wasiwasi ndugu; hakuna madhara/makosa yoyote wala hakuna uweledi uliuvunjwa kwa kutajwa kwa DGIS au ata akitajwa DDGIS wote hao ni just Public Figures...

Makosa yanaweza kutokea endapo kama wakitajwa vijana wafanyao kazi mbalimbali (Ops) kwa majina...kitu ambacho usitegemee kutokea ata siku moja...

Mataifa mbalimbali makubwa ambayo umeyazungumzia kama mifano, siku zote uwataja viongozi waandamizi mbalimbali wa Idara zao za kijasusi siku wanapoteuliwa na ata ktk mambo mengine mbalimbali...e.g.Kama ulifuatilia teuzi za Brennan, Pompeo mpaka Gina Haspel kama D/CIA...

Mfano ata asipotajwa DGIS au kutambulishwa, atakaeweza kufichwa hapa ni yule raia wa kawaida ila kwa wale ambao ni wajuzi wa haya mambo eidha wa ndani au wa mataifa mengine siku zote watawajua tu au ata mkitoa mtu nje ya nchi aje kuchukua nafasi watamjua (kwa majina, familia zao, makazi yao, weakness zao, uchafu wao, nk) ata kabla hawajateuliwa au majina yao hayajakuwa recommended kwa uteuzi...Chief of Stations (COSs) wa mataifa yote na vijana wao waliojificha kwa kivuli cha balozi hii ndio moja ya kazi zao...

Ata raia wa kawaida akijua DGIS au DDGIS ni nani au ata wakiwazoea hakuna lolote baya litaweza kutokea...narudia tena hakuna lolote baya linaweza kutokea...everything is under control, and anything will be dealt accordingly.
Mkuu hivi Mzee hawezi kudhuliwa na wabaya wetu kupitia kupeana mikono?
 
Usalama wa Taifa si kila jambo ni siri, DG na Deputy wake ni lazima wajurikane.

Kwa mfano Usalama wa Taifa zonal wanafanyakazi na public, hata wewe kama una jambo la kushare nao unaweza kwenda ofisini kwao hawapo kwa kificho.

Kuna manyoka yamejaa BOT na TRA hao ndio siku zote hata familia yake haijuwi kama ni wa kitengo.
 
Wewe Husikii fahari kumtambulisha Baba yako aliyekuzaa?Aliyesababisha uwepo Duniani?Yaaani unajijua kabisa pasipo huyu(japo hakuwa yeye bali Taasisi) nisingekuwepo Duniani kutumbua maraha haya.
 
Kutambulika sio hoja mbaya, ni watumishi wetu wa umma. Ni sawa na Wapenzi wawili mke na mume tunawajua na tumeshuhudia mpaka ndoa yao, lakini wayafanyayo wakiwa faragha hatuyajui hivyo haijalishi huyu kumjua ilimuradi ayatendayo tunaona matokeo tu
 
Back
Top Bottom