Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaama ajirusha kutoka ghorofani na kufa kutokana na kukosa ajira

Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaama ajirusha kutoka ghorofani na kufa kutokana na kukosa ajira

Haya Ndio Matatizo Ya Mfumo Wa Elimu Ya Kwetu Tumejengwa Au Kutayarishwa Kuajiriwa Tu Baada Ya Kuhitimu Elimu Zetu! Hata Wale Wanaosomea Masomo Ya Sanaa, Biashara Nao Wanatoka Wakijua Wanaenda Kuajiriwa Mwisho Wa Siku Ndio Hayo Ya Kujiua Au Ulevi Wa Kupindukia, Unakuwa Na Msongo Wa Mawazo Unaharibika Kisaikolojia. Elimu Imekupa Maarifa, Imepanua Uelewa Wako Wa Kufikiri Na Kutatua Matatizo Itumie Kufanya Mambo Mengine Kama Kilimo,biashara, Ufugaji, Sanaa Nk. Unaanzaje Kujiua Kijana Mdogo Tena Mwenye Elimu? Ni Upumbavu.
 
Ni muda muafaka wenye utaalamu wa afya ya akili (mental health) waione fursa na kufungua vituo vya ushauri na tiba mbadala (therapy).

Watanzania kama zilivyo nchi nyingi wanamatatizo mengi kama msongo wa mawazo (depression), kukata tamaa, kuvunjika moyo na matatizo mengine yanayosababishwa na changamoto za maisha. Hivyo kukiwa na sehemu za kuwatia moyo na pengine kufunguka matatizo ya ndani inasaidia kupata unafuu (heal) na maisha yanasonga.

Mara nyingine mtu akiwa na changamoto anaona kama wote wanaomzunguka hawafai na wanamhujumu hivyo hawezi kuwaeleza yanayomsibu. Hatimae akili ikishindwa kuhimili anaona hakuna namna anafikia maamuzi ambayo sio mazuri.
 
Ally (25), mkazi wa Kiloleli wilayani Ilemela jijini hapa anayedaiwa kuwa na elimu ya chuo kikuu, amejirusha katika jengo la la Rocky City Mall na kufariki dunia.

Imeelezwa kuwa Musa alichukua uamuzi huo kutokana na kuwa na msongo wa mawazo, kukosa kazi.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Desemba 21, 2018 kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza, Advera Bulimba amesema tukio hilo limetokea leo saa saba mchana.

Bulimba amesema kijana huyo alionekana akiwa amelewa kupita kiasi na tangu Desemba 16, 2018 na alikamatwa na kuwekwa kituo cha polisi Kirumba, kilevi kilipopungua aliachiwa.

Amesema katika uchunguzi wa awali marehemu alibainisha kuwa alikuwa na msongo wa mawazo kwa sababu ya kukosa kazi licha ya kuwa na elimu ya juu.

Bulimba amesema baada ya polisi kumuachia alikwenda kunywa tena pombe na baadaye kujirusha kutoka ghorofa ya tatu na kukutwa na pombe kali na ugoro.

“Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa kijana huyo amesema amejiingiza kwenye ulevi na asilaumiwe mtu yeyote.

Amesema amechukua uamuzi huo yeye binafsi, pia akidai yeye ni masikini hana baba wala mama,” amesema Bulimba.

Amesema mwili umehifadhiwa hospitali kwa ajili ya uchunguzi zaidi licha ya kutotaja jina la hospitali hiyo.

Bulimba amesema, maandishi aliyokutwa nayo marehemu yalisomeka kwamba “yeye ana shahada sayansi ya kompyuta aliyoipata Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).”

Chanzo:Mwananchi.

Police wamesomba Picha zimekataa kuupload. Ila nimeattach kwenye comment no 6 na 7.
Hii ni habari mbaya sana kwa serikali ya CCM baada ya kushindwa kuajiri kwa miaka 8 sasa....mnataka wasomi waliohitimu wakale wapi? Waingie kwenye siasa? MiCCM ni mijitu ya ajabu sana.
 
Popoma hizo sababu namba 1 na 2 ndo zinawezekana zaidi kwa mtu wa umri huo.

Moja wapo laweza kuwa jawabu sahihi:

1. Kagundua ana tatizo la Nyuzi la Gitaa la ' Dally Kimoko '.
2. Kafumania Demu wake ' Wanamume ' wakifanya yao kwa Kusimamia Ukucha
3. Masela wamemkuta na Demu wa mwenzao kisha wakafanya yao na kwa msaada wa ' Video Shooting '
4. Stress za Maisha ( japo tupo wenye hizo Stress lakini bado tunakomaa tukiamini kuwa ipo Siku tutatoboa tu )
5. Kasababisha Kifo au hasara Kubwa mahala
6. Karogwa
7. Uwendawazimu wa ghafla umempata

R.I.P sana Marehemu.
 
Mimi Tumaini Geofrey Temu limbukenitutababanana humuhumu nilisha tibiwa kichaa niwemuachia nyie na raisi wenu,, 2020.. Mrema agustino wariri mkuu Mama Maria Malkia Amitipal Sing Bhogal,,,
1545910926798.png
Temu akili bado haijakaa sawa hebu rudi tena ukatibiwe au Mirembe ipo hapa Nchini, mwenzako Mrema si Waziri Mkuu tena ni Boss wa Parole . Mama Maria kwa sasa yupo Msasani
Duh kazi kwelikweli vijana watajimaliza awamu hii
 
1. Kama kweli polisi walibaini ana msongo wa mawazo na wakamwacha basi walipoteza weredi katika kazi yao.


2. Watalaam wa Counselling waichungulie hiyo fursa ya msongo wa mawazo na kuanzisha ofisi ili watoe huduma hiyo kwa hitaji na kuajiri wengine
 
Hii ni habari mbaya sana kwa serikali ya CCM baada ya kushindwa kuajiri kwa miaka 8 sasa....mnataka wasomi waliohitimu wakale wapi? Waingie kwenye siasa? MiCCM ni mijitu ya ajabu sana.
Serikali tangu imeingia madarakani imeajiri watumishi 6000's only,ajabu sana yaani on avarage inaajiri watumishi 2000's/year wkt wasomi ni maelfu wanaotoka ma vyuoni huko.
 
Mmmhhh! Sidhani kama angekosa kitu cha kufanya; kuna uwezekano mkubwa alikuwa anachagua ajira ndiyo pale anayoitaka haitokei.
Mbaya zaidi kuona pombe ndiyo suluhu ya alichokuwa akiwaza; wahenga walikwisha sema pombe si chai. Makosa ni yake mwenyewe kwa kuchukua uamuzi dhaifu mno.
 
Back
Top Bottom