sikatai boss inawezekana umri na kutokea shule kulichangia
Yeah,22 yrs ni mdogo mno kukamata noti za kila mwezi plus marupurupu ungezisotea usingezichezea na hata kama ungezichezea basi zingeacha alama mfano nyumba,gari mbovu mashamba,ila kule kutoka tu shule na bado unawaza kuendelea kusoma ajira hii hapa,pesa mingi usingerudi viunzi na upo kwenye right track andiko lako limesaidia weng hasa waajiriwa.
Mkuu kwa sisi(mimi) nimepitia msoto sana katika maisha yangu nimetokea familia ya kimasikini mno yaani basi tu tena ya single mother mwenye 5 kids na mimi nikiwa first born nimeparangana sana kusoma lakini hata kidato cha nne nmekimaliza kwa mateso sana,mazingira yalichangia sana kufeli nikachaguliwa vyuo vya ualimu,utumishi wa umma,afya na ugavi hakuna nilichofanikiwa kujiunga nacho maana hata mia mbovu sikuwa nayo,nikaingia mgodini mwaka na ushee hollah,
Nikaingia kutafuta mali za mjerumani sijui pasi,rupia,n.k hollah
Nikarudi shamba kulima miaka mitatu hollah
Nikabuni mbinu ya kutafuta pesa kwa kutumia taaluma yangu ya kidato cha nne tu,nikaajitolea kufundisha nursery mwaka na nusu,.............
Mpaka muda huu naandika namshukuru sana Mungu,amenithibitishia kwamba akiamua kukupa ridhiki hachagui akupe kupitia ulichokitarajia,........
Nimejenga nyumba nzuri tu ya kuishi,nina shule yangu ya English medium nursery mpaka primary.
Ukinikuta nafundisha hutakaa uamini kama nimeishia kidato cha nne, mimi siyo mkurugenzi mwenye shule mpaka leo hajulikani,kuna mkuu wa shule ndiyo meneja yeye anajua mimi ni mwangalizi tu kuna utawala pia,walimu na wafanyakazi wanalipwa na my Mrs ambaye ndiye mhasibu wa shule na yeye anafahamu kuwa mimi nina asilimia kidogo tu za umiliki kama 25% zilizobaki ni za wafadhili,kumbe ninaown hisa 100%.
Ninafundisha kama mwajiriwa na ninalipwa kama walimu wengine.
Mkuu naomba niishie hapa ila katika maisha kuna mambo mengi watu tunatembea nayo tu.