Miaka 10 ya Utumishi: Kumbukizi mbaya ya matumizi ya pesa isiyofutika katika historia ya maisha yangu


Mmmh technician hiyo hela ndo ulikuwa unapata kwa mwezi,shirika gani hilo?
 
Hicho kipato chako kinaonesha hukua mtumishi wa umma ( civil servant) tuulize sisi watumishi wa umma tukung'ate sikio vipato vyetu lazima utahoji naishije! Acha kaka halafu huu no mwaka wa tank hakuna ongezeko !utasikia mwenyewe anasema kama hutaki acha ikazi!!!!/ kwa kweli watu wamechakaaa mioyo
 
Mkuu jamaa aliajiriwa kwenye taasisi ya umma.. taasisi nyingi za umma kama tcaa, sua, muhas, toa, tra zina madaraja yao ya mshara ..ya grade zao za mishara siyo kama hizi common za waalimu
 
Andiko lako ni zuri sana, Kama litafanyiwa kazi litawasaidia wenfi sana. Wengi hatuna AKILI ya saving katk kidogo au kingi tunachopata.

48M + 15M = Kwangu ningehesabu Kama pensheni. Daaah . Take it easy jitahidi mwanao asifuate makosa yako. Mpende sana mkeo. Asingekuwepo ingekuwa chizi tayari.
 
Wazazi wanatakiwa sana kuangalia vijana wanaoajiriwa katika umri mdogo, ni bora hata kuwaelekeza kwa muda fulani juu ya matumizi ya pesa, saving and all na sio kukuona umeajiriwa basi ushakua mtu mzima wakati kiasi hicho kikubwa cha pesa za kila mara hujawahi kipata. Mwenyewe niliajiriwa at 22 first salary was 925k plus 1million per diem kila baada ya wiki 2 na hivi niliajiriwa mkoani yani kila ijumaa nipo airport naenda nyumbani kuona wazazi na mchumba. Looking back miaka mitano nyuma naona ningekuwa mbali sana tofauti na hapa nilipo leo maana umri unasonga na majukumu yanaongezeka
 
Pole sana ndugu yangu, mimi nimeajiriwa na shirika la serikali yawezekana huelewi kuhusu utofauti wa maslahi kwenye taasisi za umma, ngoja nikupe mifano hai ya ndugu zangu wa karibu kabisa wanne ambao wameajiriwa hivi karibuni baada ya kutoka kapa huko JKT kupitia pale utumishi na wote wako cheo kimoja na elimu yao ni kidato cha nne tu, wameajiriwa taasisi tofauti, tuwape majina A,B,C na D.

"A" alitangulia kuajiriwa TPA mwaka jana japo usaili walifanya wote na akafanikiwa yeye tu kupata ajira hapo miongoni mwao wote kama "Security Guard", amefika kule akakuta mshahara 800+k ukiongeza na overtime ambao wao inachanganywa kwenye mshahara pamoja at the end mshahara unasoma 1.3+m na wana posho 150k kila mwisho wa mwezi,alipelekwa mtwara kituo chake cha kazi na alipewa pesa ya kujikimu zaidi ya 3m.

"B" aliajiriwa Mahakama na akapelekwa mahakama ya wilaya flani huko kama Mlinzi pia mwaka jana hiyohiyo akapewa 500k ya kujikimu na akakuta mshahara laki tatu tu yaani 300k kwa mwezi na hakuna posho yoyote.

"C" Yeye aliajiriwa nadhani mwaka huu hapo DDC (Dar Es salaam Development cooperatin) kama "Security officer" pia, amefika kakuta mshahara 696k kwa mwezi na posho za zaidi ya 300k per month na pesa za kujikimu kapewa 900k

Huyu "D" na yeye ameajiriwa mwaka huu huko Ngorongoro Conservation kama mlinzi ( Askari wa wanyamapori) huyu kafika kule kakuta mshahara 960k na overtime inategemea na masaa yako ya ziada, na posho zingine nyingi na akapewa pesa ya kujikimu 3.4m

Nimejaribu kukupa mifano hii ya watu walioajiriwa vyeo vya chini kabisa ambao ni ndugu zangu wa karibu walioajiriwa hivi majuzi pamoja na kwamba ni kada moja na elimu yao ni sawa lakini unaona hapo kabisa kuna mmoja anaweza kumlipa mwingine mshahara wake wa mwaka mzima kutumia mishahara na posho zake za miezi isiozidi mitatu.

NADHANI UMEGUNDUA KITU HAPA.

Maslahi na mishahara inatofautiana kulingana na taasisi uliyopo boss
 
pole sana ndugu lakini bado hujachelewa sana.
umri wetu bado unaruhusu kufanya makubwa.
 
Upele humuota asikuwa na kucha. Nalipwa 716k per month, take home 454k yaan nije nilipwe 1.2M kwa mwezi na hiyo 48M mkopo wa masharti nafuu kama hayo uliopewa nadhani ningekuwa mbali sana. Nafanya mambo yalio muhimu. Napanga bajeti yangu ambayo itakuwa chini ya mstari wangu wa matumizi. Nafanya biashara ambayo inamtaji wa wateja na inaleta faida nzuri kulingana na nilichowekeza.

Pole sana. Umri wako bado. Anza upya sahihisha makosa yako. Umewapa vijana somo zuri sana.
 
boss, umri nao unachangia kwa sasa kila kitu kimebaki historia huo ujinga umebaki kuwa kumbukumbu mbaya tu kwenye maisha yangu
 
umepata pesa bado kijana mdogo sana ni halali yako kufanya hivo.
kwenye maisha kila mtu ni lazma apite hii stage, wachache sana ambao hawapitii huku na uzeeni wengi wao lazma fanya upuuzi wa kushangaza hapo ndio unakuta mtu anachukua mafao anaenda kuolea mke wa pili.

Pambana kwa vile tayari ulishashtuka karibia miaka 5 iliyopita
 
[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Hongera Sana lakini experience inachangia maana umepitia mengi..shida Ni ujana..wengi ujana ulituangusha
 
Jaribu kutafuta njia ya kuendesha miradi yako ukiwa ndani ya hiyo ajir.... Nawaza tu kama mkeo anauwezo mpe kazi ya kuisimamia hiyo miradi ila uhakikishe umeiweka sawa kisheria kuhusu umiliki wake. Pia Jenga tabia ya kuifanyia ukaguzi wa kimahesabu Kila baada ya muda Fulani hata kwa kuajiri mtaalamu (USIIAMINI SANA JINSIA KE na umeshasema she is smart than you)

Kwanini nimekwambia endesha miradi ukiwa kazini??

Emagine mtu Alie acha kazi 2018 akawekeza katika bishara ya kununua vitu online na kuuza na kapiga pesa sanaaa kipindi hicho kwa Sasa anahali gani??

Sio kwako tu hua nashauri Kama unauwezo wa kufungua miradi na una mtu sahihi wa kuisimamia fanya hivyo ila sio kuacha kazi completely. UTATESEKA ifanye Kazi yako kuwa chanzo kingine Cha mapato.
 
Boss Ahsante sana kwa huu ushauri wako
 
haya mambo haya ni mungu tu mda mwingine anatenda, unajikuta unaoa pale ulipokuwa huna mapenzi napo
 
Kuna mda mwingine nawaona watunga sera wa hii nchi ni wapumbavu sana, mtu mwenye shahada kwenye taasisi za kawaida na serikali kuu anazidiwa mshahara mara mbili na Mlinzi, msaidizi wa ofisi au Telephone Operator mwenye elimu ya kidato cha nne tu.
Na ile kamati ya mishahara sijui hata imeishia wapi, Miongoni mwa vitu ambavyo vinanitia kero ni huu utofauti mkubwa wa mishahara serikalini


Ofisini kwetu kuna Telephone operator amehania taasisi nyingine mshahara anaolipwa sisi na degree zetu hatumfikii hata nusu unabaki kuduwaa tu, sijui waliwaza nini hawa viongozi kwenye hii miongozo ya mishahara serikalini... PUMBAVU ZAO
 
Mkuu ulifaidi ila vyema umesharekebisha uliokosea.
Mimi sina nilichokosea wala kupoteza sijawahi kula bata au kuwa na unafuu wa maisha,Ni mwajiriwa ila kutokana salary haikidhi hadi sasa sina asset yoyote wala biashara majukumu ya familia(mama pamoja na wadogo zangu) yamenibana kiasi kwamba hadi kununua nguo unaona ni dhambi,dogo yupo semester ya mwisho chuo ila hadi saivi naandika hapa sielewi ada anaipataje,kama benk nilishakopa ili niwalipie ada na 1 june anatakiwa chuo, kwa kiasi fulani nashukuru Mungu hata ili naamini atanisimamia litapita tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…