Miaka 100 baada ya kifo chako, utazaliwa kwa mara nyingine ukiwa na mwili mpya

Lacks scientific evidence or verifiable data
Mkuu, kwa sisi tuliopitia mafunzo ya kibudha, tahajudi, yoga, ashart, menio, sminla na chandral tunaufahamu ukweli wa mambo. Ukitaka vingi zaidi unatakiwa kuwa na access ya Dark Web. Wengine tumekuwa tukizungumza na mizimu, majini mpaka malaika wa mashetani kwa kiebrania. Upo hapo mkuu!
 
Sasa Kama kipindi cha LRP kumbukumbu zote hupotea na mtu Kuzaliwa upya, we umejuaje? Au huyo aliyekwambia alijuaje, bila uwepo wa kumbukumbu?
Ooh yes! utakuwa uko ndotoni; tunashukuru kwa ndoto yako nzuri.
Nafsi nyingi huzaliwa miaka mia baada tu ya kufa ikiwa 80% ya nafsi hizo hurejea ubinaadamu wa kawaida ukiwa na ujinsia uleule pia ikawezekana ndani ya ukanda ule ule wa maosha yaliyopita. 20% ya nafsi huzaliwa kwenye nafsi tofauti kabisa za wanyama wengine

Miaka 100 ni wastani halisi, lakini kama itatokea umezaliwa kabla ya miaka 100 kutimia vyema, baadhi ya kumbukumbu utakuwa nazo
 

Attachments

kwaiyp ww hapo ni kuwa ulikufa miaka zaidi yà 100 ilopita saiv upo umezaliwa tena?? ujinga ni mzigo
 
Kwa hiyo ongezeko la population linatokana watu kutoroka huko walikolala?
 
Ingawa idadi ya binadamu huongezeka, kuna baadhi ya viumbe idadi yao hupungua. Uzao mmoja wa chatu una range mayai 20 hadi 100. Hivi umewahi jiuliza ni kwanini nyoka hawa wasiwe wengi zaidi ulimwenguni, ni issue nzima ya natural selection. Baadhi yao hubeba nafsi za walio wahi kuwa binadamu. Kupotea kwao ni ujio wa binadamu wengi zaidi ambao wamewahi kuishi kabla

Unaweza ukafa leo, baada ya karne nafsi yako ikazaliwa ndani ya ngamia, ngamia huyo ukafa, kisha baada ya karne ukazaliwa tena kama binadamu wa ukanda ule ule wa karne mbili zilizopita
 
Simply idadi ya watu isinge ongezeka
 
Nizaliwe marekani huku nilipo nimepachoka
 
Mkuu Melki, hii nadharia yako ni yenye kutafakarisha na kuamsha tafakuri pana zaidi juu ya hatma ya maisha ya mwanadamu baada ya kifo chake. Hii ni kutokana na mantiki ya kuwa mchakato mzima wa roho kutengana na mwili, kisha roho hiyo ku "perambulate" kwa miaka 100, kufutika kwa kumbukumbu za awali kutoka katika nafsi iliyopata kuishi hapo awali, kuhama na kuzaliwa kwa nafsi mpya yenye mwili mpya. Nyuma ya mchakato huu ni lazima kuwe na uwepo wa nguvu kuu ama "grand master" anayeusimamia, kuuendesha, na kutafuta "balance".

Dhana yako hii ni lazima itapata upinzani mkubwa sana kutoka kwa waumini wa dini zinazojitambulisha kuwa ni za asili kutoka kwa Abraham ama Ibrahim. Hii ni kutokana na ukweli ya kwamba dini hizi zote zinaamini kuwa chanzo cha uhai wa nafsi ya mwanadamu kinatokana na Muumbaji mmoja ambaye ndiye Mungu wa kweli wa Abraham, na hatma ya maisha ya nafsi yake ya umilele, inategemea hukumu yake mbele ya Muumba wake, ama itakuwa ni tuzo ya uzima wa milele ama laana ya umauti wa milele.

Nathamini sana mchango wako ijapokuwa unakuwa mgumu sana kueleweka kwa watu wengi ambao akili zao zipo "biased" kutokana "dogma & doctrines" tofauti ambazo hupelekea watu kuwa na mitazamo na itikadi tofauti za kidini na kiimani. Ndiyo! Katika "body of knowledge" zipo nadharia nyingi mno ambazo huchochea udadisi wa "scholars" tofauti kupata elimu ya ziada kuhusu mambo ya kiroho kama haya. Lakini hii uliyoiibua hapa jukwaani ni ngeni kwa wengi, hivyo ni lazima itachokoza mihemuko hasi kwa baadhi ya wachangiaji.

Niombe tu, kwa mjadala kama huu uliouleta tukubali kutofautiana kiimani, hii ni kutokana na ukweli ya kwamba "we share different historical backgrounds, associated with different perceptions backed by our different environmental and ecological inclinations"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…