Miaka 20 Baada ya Kufika Pwani ya Kipumbwi: Historia ya Kipumbwi Katika Mapinduzi ya Zanzibar

Miaka 20 Baada ya Kufika Pwani ya Kipumbwi: Historia ya Kipumbwi Katika Mapinduzi ya Zanzibar

Ilikuaje wazanzibar walidai uhuru kwa Mwingereza wakaupata then wakatawaliwa na mwarabu? Au ni mwarabu alipambana kudai uhuru baada ya kupata wazanzibar wakampindua?
Mwarabu ndo alidai uhuru na walipoupata wakaweka utawala ea kisultani..
The sultanate Government kama sikosei ndo iliyokuwepo na ilikuwa ina nguvu kweli kweli mpaka mwaka 1964 ilipopinduliwa
 
Okelo hakuwahi kuwa mwanajeshi,bwana yule alienda kule kisiwani "kubangaiza" tu maisha.

Baadhi ya maandiko yalidai kwamba Okelo alitumika tu sababu alikua na lafudhi ya kutisha sana na sura yenye matisho hivyo kuogofya wapinzani lakini hakuna .

Kumbukumbu rasmi inayoonyesha hakuwahi kupata training yoyote ya kijeshi.
Mkuu nimeweka magazeti ya kipindi hicho yanamuita Field Marshal au Marshal Okello...

Je unakijua hicho cheo na Picha alizopoga kipindi hicho umeziona nimeongea na Mzee wangu ambaye kipindi hicho alikuwepo na kanihakikishia na ninamuamini..

Unless ulete ushahidi wa unachosema maana nimeleta ushahidi wa Picha na Magazeti ya wakati huo...

Na unaweza ukamgoogle pia
 
Okelo hakuwahi kuwa mwanajeshi,bwana yule alienda kule kisiwani "kubangaiza" tu maisha.

Baadhi ya maandiko yalidai kwamba Okelo alitumika tu sababu alikua na lafudhi ya kutisha sana na sura yenye matisho hivyo kuogofya wapinzani lakini hakuna .

Kumbukumbu rasmi inayoonyesha hakuwahi kupata training yoyote ya kijeshi.

Unaweza ukapitia hapa
 
Baada ya wamakonde kuwasaidia kumtoa nduki muarabu ni kwa nini karume baadae alitaka kuwafurusha wamakonde Zanzibar? Na wakati historia inasema karume alijificha wakati wa mapinduzi hakushiriki vita ile, lakini pia ni kwa nini alimfukuza John Okelo baada ya vita kuisha ?
 
Mwarabu ndo alidai uhuru na walipoupata wakaweka utawala ea kisultani..
The sultanate Government kama sikosei ndo iliyokuwepo na ilikuwa ina nguvu kweli kweli mpaka mwaka 1964 ilipopinduliwa
Anhaaaa bas kama ni hvo mapinduzi yalikua sahihi kbs
 
Likizo yangu ya mwaka jana Mwaka mpya nilikua Pangani (pale beach kuna guest ziko ukingo wa bahari) baade nikaenda kipumbwi. Mazingira, aina ya watu na mishemishe zinazoendelea unaweza jua sio Tanzania. Pako tofauti kabisa
 
Ni serkali ambayo wazanzibar waliipenda kweli kweli kuliko waliyo nayp sasa hivi ukiwauliza watakuwambia hivyo
Sisi watanganyika tuliwasaidia wajitawale wao sio kuleta utawala wa mwarabu....kote lengo ni kuondoa mkoloni
 
MIAKA 20 BAADA YA KUFIKA PWANI YA KIPUMBWI: HISTORIA YA KAMBI YA KIPUMBWI KATIKA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Miaka 20 iliyopita tarehe kama ya leo 9 December, 2003 ndiyo siku Mohamed Omari Mkwawa alipotufikisha mimi na Dr. Harith Ghassany Kipumbwi.

Siku hii iliangukia kuwa siku Tanganyika ilipopata uhuru wake.
Kipumbwi ni kijiji kidogo cha wavuvi kilomita chache kutoka Tanga.

Hapa Kipumbwi ndipo ilipowekwa kambi ya askari mamluki wengi wao Wamakonde waliokuwa wanapewa mafunzo ili washiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Historia hii si ngeni kwa sasa kwani Dr. Ghassany kaieleza kwa kirefu katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," (2010).

Lakini kabla ya yeye kufika Kipumbwi na kushuhudia kwa macho yake yale aliyoelezwa na Mzee Mkwawa Tanga mjini kuwa alihusika katika kuwavusha Wamakonde kwa siri kuingia Zanzibar kushiriki katika mapinduzi hii ilikuwa siri kubwa sana.

Sikupata siku kumuona Dr. Ghassany kafurahi kama siku ile.

Kwa hakika kabisa alikuwa na haki ya kufurahi kwani alikuwa amekitegua kitendawili kikubwa; kwanza kuwa kuwa kulikuwa na kambi ya mamluki katika ardhi ya Tanganyika waliovushwa na kuingia Zanzibar kusaidia mapinduzi.

Kafika Kipumbwi na Mzee Mkwawa akatupitisha sehemu zote kuanzia pango la chini walikukuwa wanaficha majahazi yao hadi kutuonyesha mgahawa mdogo walipokuwa wakila usiku kabla ya kuingia katika vyombo na kuanza safari.

Pili Kipumbwi ilisaidia kueleza mauaji yaliyotokea mashamba ambako Waarabu wengi waliuliwa.

Leo naikumbuka siku hii miaka 20 iliyopita na naweka picha tulizopiga Kipumbwi.

PICHA: Picha ya mwisho ni Mzee Mohamed Omari Mkwawa na mkewe.

View attachment 2838139
Uhusika wa serikali ya Tanganyika kwenye mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 upo ila hauwekwi wazi.

Pascal Mayalla
 
MIAKA 20 BAADA YA KUFIKA PWANI YA KIPUMBWI: HISTORIA YA KAMBI YA KIPUMBWI KATIKA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Miaka 20 iliyopita tarehe kama ya leo 9 December, 2003 ndiyo siku Mohamed Omari Mkwawa alipotufikisha mimi na Dr. Harith Ghassany Kipumbwi.

Kwa hakika kabisa alikuwa na haki ya kufurahi kwani alikuwa amekitegua kitendawili kikubwa; kwanza kuwa kuwa kulikuwa na kambi ya mamluki katika ardhi ya Tanganyika waliovushwa na kuingia Zanzibar kusaidia mapinduzi.
Asante sana kwa kumbukumbu ya Maskani Kipumbwi.

Mimi ni muumini wa karma, what goes around, comes around.

Wakaazi halisi wa Zanzibar kabla ya ujio wa Waarabu ni Wakwezi na Wahadimu ambao wote ni Wamatumbi. Wareno wakaivamia Zanzibar, Kiongozi wa Wamatumbi, Mwinyimkuu akaomba usaidizi wa Waarabu kuwapiga Wareno, wakakubali na baada ya kuwashinda Wareno, haijulikani hawa Waarabu walimfanya nini Mwinyimkuu, maana hakuna kukumbukumbu yoyote hata ya uongo uongo kuonyesha ilikuwa Sultan Seyyid Said akahamishia The Sultanate yako toka Oman kuja Zanzibar ile 1732. Kwa Tanganyika Karl Peters alisainisha mikataba kwa kina Chifu Mangungo, kwa Kilwa Hassan Bin Amiri, alikinunua kisiwa cha Kilwa kwa kitambaa kinachozunguka Kilwa yote, lakini kwa Zanzibar, Mwarabu aliipataje Zanzibar!, no one knows Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu waliteswa, hasiwa, bakwa, na kuuawa kinyama

Hivyo Sultan Seyyid Said wa Oman, alivivamia visiwa vya Zanzibar, akajimilikisha na kuvifanya mali yake, bila kubisha hodi!.

Hivyo hakuna ubaya wowote kwa Wamatumbi wa Zanzibar, kuomba msaada kwa Wamatumbi wenzao wa Tanganyika kuwasaidia kuvikomboa visiwa vyao dhidi ya uvamizi wa Sultan of Oman ambaye baada ya kuitwaa Zanzibar, akawa Sultan of Zanzibar.

Hivyo ile usiku wa January 11 kuamkia January 12, Wamatumbi wakafanikiwa kuvikomboa visiwa vyao, na Mwarabu, kama alivyokuja pasi hodi, aliondoka pasi kuaga! Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari

Kama ikithibitika Kipumbwi ilitumika kuikomboa Zanzibar, inastahili kupewa hadhi na heshima yake katiba ukombozi wa Zanzibar.
P
 
Hakuna.
Halafu wapo asilimia mbili tu. Interesting.
Mkuu Asilimia 2.ni negligible in science where the sample size is large than the Required value...
Kwa mfano wanaposema hakuna Dawa mahospitali wanamaanisha Dawa zilizopo hazikidhi Matakwa wa kiasi kinachotakuwa kuwepo...

Mfano mwingine...unaohusu Siasa..

Unapoambiwa kuwa Tanganyika haikuwa Huru kabla ya 1961,Haimaanishi kwamba waliishi kama jela ila walikuwa na uhuru ila haukutosha kusema walikuwa huru moja kwa moja...
 
Back
Top Bottom