Miaka 55 ya BAKWATA: Tujikumbushe Historia Yake na Yaliyotokea October - December 1968

Miaka 55 ya BAKWATA: Tujikumbushe Historia Yake na Yaliyotokea October - December 1968

Papasa,
Mbona ghafla umeghadhibika?

Maraisi Waislam hawakuchaguliwa na wananchi kuja kuudumia Uislam.

Wangefanya hivyo wangesababisha vurugu nchini.

Ingekuwa hatujatia maanani elimu EAMWS isingetaka kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968.

Hapa unelalama ni wewe mimi nakueleza historia ya kweli kumekuwa na njama ndani ya serikali kuwazuia Waislam wasipate elimu.

Waislam wamefanya maandamano mwaka wa 2012 kupinga hujuma za NECTA dhidi ya shule za Kiislam.

Katika miaka ya 1970 OIC ilitaka kujenga Chuo Kikuu serikali ikakataa kutoa kibali.

Huna unachokijua.
Wacha uwongo wewe mzee. Waisalmu wenye kutaka kusoma wanajuwa mahali pa kupata elimu siyo lazima wakasome chuo kinachoitwa cha Kiislamu.

NECTA unailamumu bure. Ulitaka wakupe alama "B" wakati umepata "F"? Zitaje hizo shule za Kiislamu unazofikiri zilionewa tuzijadili hapa.
 
Mleta mada serikali ilikuwa sahihi kuvunja Hicho kitu kinaitwa Eamws kama kweli huo ukikuwa mradi wa kitapeli wa Agha Khan kiongozi wa dini ya kishia akiwalaghai waislamu walio wengi wa Tanzania ili wajiunge na shule zake za Agha Khan waliipe mihela kibao

Akipojitia kuanzisha hiyo Taasisi ya waislamu ya Afrika mashariki kusaidia Waislam mojawapi lengo likiwa elimu na afya nk serikali ikafanya tathmini ilipoomba usajili kuwa je watanzania wangapi wamesomeshwa bure primary au sekondary shule za Agha Khan au kutibiwa bure hospital za Agha Khan wakakuta hakuna
Shule na hospitali zake zilikuwa kwa ajiki ya wahindi waislamu wa madhehebu ya Shia Usmailia na wahindi wengine sio waafrika ngozi nyeusi

Serikali ikaona utapeli wa Agha Khan wakafuta hiyo taasisi Tanzania
Uliza hata humu wangapi waislamu waliosomeshwa bure au kutibiwa bure taasisi za Agha Khan ziwe shule au kutibiwa bure hospitali za Agha Khan baada ya yeye kunyimwa usajili au kufutiwa?
Ila kitu cha ajabu kuna waandishi wajitia jutetea uislamu Mohamed Said akiongoza hutetea sana kuwa ohhh hiyo Agha Khan alikuwa na malengo mazuri na waislamu OK alizuiliwa kusajili hiyo taasisi serikali ok serikali ilifuta hiyo taasisi lakini haikumzuia kusomesha waislamu bure shule zake za Agha Khan wala kuwatibu waislamu bure hospital za Agha Khan

Mbona hilo hakulifanya hadi leo ? Lengo lake si lilikuwa kusaidia waislamu? Mbona hadi leo hakuna kusoma bure au kutibiwa bure taasisi za Agha Khan kwa waislamu?

Binafsi katika watu wapotosha historia wasioenda ndani sana Mohamed Said anaongoza muongo mno na hayuko deep kwenye analysis za hoja zake
Uzuri yuko hai hivyo ni vizuri ajue uongo waje akiwa hai

Agha Khan alikuwa tapeli alitaka kutapeli waislamu wa Afrika Mashariki akastukiwa na nchi zote za Africa Mashariki kote kuna mabaraza ya nchi zao ya waislamu siyo Tanzania pekee iliyogoma kote serikali Afrika Mashariki zilimpiga teke Agha Khan aondoke na utapeli wake wa kutaka kutapeli waislamu

Tanzania tuna viongozi wakubwa kibao waislamu hakuna hata mmoja aliyesoneshwa bure na Taasisi ya Agha Kan
Mkuu umeliweka vizuri sana. Ika huyu mujahidina Mohamed Said atabisha tu kwa vile kichwa chake kilishajaa bangi ya udini
 
Yehoda,
Hili lilikuwa moja ya mabango katika maandamano dhidi ya NECTA chini ya uongozi wa Dr. Ndalichako.

Unasemaje?

Kuna maandamano yalifanywa kumkataa Aga Khan au Aziz Khaki au Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Waislam waliikubali BAKWATA?

Huna unachokijua kuhusu historia ya Waislam.

Isome kwanza ndiyo uje kujadili.
Wahusika wakuu wako kimya hawana mdomo wa kujadili haya.

Wanaogopa.
Unajibu wewe usiyohusika.

Katika mambo ya hovyo wewe mzee unafanya ni kuwa mwanaharakati wa kiislamu. Tanzania huna nafasi, nenda Somalia kajiunge na Al Shabab kama hawajakupoteza ndani ya Lisaa limoja.

Kweli mtu mwenye akili anaweza akasema NECTA ni Parokia? Kwa taarifa yako shule za Kikristu kwenye mambo ya shule hazina mzaha. Usione St Francis Mbeya au Marian Bagamoyo wamemiliki top spot ya O-Level na A-Level kwenye mitihani ya NECTA kwa miaka 30 sasa ukadhani kuna upendeleo.

Nafahamu viongozi wa juu ambao ni Waislamu waliopeleka watoto wao huko St Francis na Marian. Walipeleka kwa vile wanajuwa thamani ya elimu. Tofauti na wewe unataka tuwe na Chuo Kikuu cha Madrassa. Hovyo
 
Yehoda,
Hili lilikuwa moja ya mabango katika maandamano dhidi ya NECTA chini ya uongozi wa Dr. Ndalichako.

Unasemaje?

Kuna maandamano yalifanywa kumkataa Aga Khan au Aziz Khaki au Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Waislam waliikubali BAKWATA?

Huna unachokijua kuhusu historia ya Waislam.

Isome kwanza ndiyo uje kujadili.
Wahusika wakuu wako kimya hawana mdomo wa kujadili haya.

Wanaogopa.
Unajibu wewe usiyohusika.

Mwinyi, kikwete, na sasa samia wote hawa ni marais waislamu sasa hapa mnaonewaje acha upotoshaji na uongo

Kuhusu elimu matokeo ya wanafunzi yanatolewa kwa number hapo waislamu wanaonewaje
 
Katika mambo ya hovyo wewe mzee unafanya ni kuwa mwanaharakati wa kiislamu. Tanzania huna nafasi, nenda Somalia kajiunge na Al Shabab kama hawajakupoteza ndani ya Lisaa limoja
Walishaona hana madhara, afu hizi harakati zake ni humu tu nje ya jf hana uzito wowote wa kutisha
 
Yehoda,
Mimi si mtu wa ubishani wa staili hiyo yako ya kutoa matusi kuwa ''Waislam ni sifuri kichwani.''

African Association iliasisiwa mwaka wa 1929 na hawa: Kleist Abdallah Sykes, Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Suleiman Majisu, Ibrahim Hamisi na Cecil Matola, Raikes Watts na Raikesi Kusi.

Waislam hawa unaowatukana mwaka wa 1933 wakaunda Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Vyama vote hivi viwili vilitumika kupambana na ukoloni wa Muingereza.
Safari ya kwanza ya Nyerere UNO dhifa ya kumuaga Nyerere ilifanywa ndani ya jengo hili la Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika.

Mkusanyaji wa fedha za safari ya Nyerere alikuwa Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyy fi Tanganyika na Mweka Hazina wa TANU kadi yake ya TANU ni no. 24.

View attachment 2853181
Kulia ni Haruna Iddi Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramiyya na Iddi Faiz Mafungo wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.​

Sasa tunaweza kuendelea na Aga Khan
Ilibidi tufahamiane kwanza:

Tuanze na makala hiyo hapo chini kisha In Shaa Allah tutaendelea na mengine ikiwa utapendezewa na sharti kuwa hutawatukana wazee wangu waliopigania uhuru wa nchi yetu kwa hali na malii zao:

AGA KHAN PATRON WA EAMWS ALIPOKUTANA NA VIONGOZI WA BAKWATA MIAKA YA 1980
Nakusudia In Shaa Allah kuweka hapa makala mbili au tatu hivi kueleza yaliyotokea baada ya miaka mingi na Aga Khan aliyekuwa Patron wa EAMWS kujaribu upya kusaidia Waislam wa Tanzania lakini safari hii kupitia BAKWATA.

Naamini yapo mafunzo makubwa kwetu na Waislam na wananchi kwa ujumla wataielewa historia ya BAKWATA na viongozi wake.

Aga Khan si mgeni Tanzania na waliomuingiza nchini ni Waislam katika miaka ya 1930 kwa ajili ya kutoa misaada kwa Waislam.

Katika miaka ya 1930 baba yake huyu Aga Khan wa sasa Shah Karim Al Hussein, Sir Sultan Mohamed Shah alitembelea Tanganyika na katika mradi mmoja wapo aliofika kuuangalia ulikuwa ujenzi wa shule ya Al Jamiatul Islamiyya School, Mtaa wa Agrrey na New Street uliokuwa ukijengwa na Waislam chini ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Katika hafla ile mwanafunzi aliyesoma risala mbele ya Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.

(Miaka mingi baadae Abdulwahid Sykes sasa kijana na mwanasiasa akajachaguliwa kuwa mjumbe katika Bodi ya Elimu ya Aga Khan).

Aga Khan alivutiwa sana na juhudi zile walizoonyesha Waislam wa Tanganyika za kutaka kujiendeleza katika elimu na akatoa fedha zilizowezesha kumaliza ujenzi wa shule yote kwa ukamilifu wake.

Aga Khan akatoa changamoto kwa Waislam wa Afrika Mashariki kuwa Muislam akichanga shilingi moja kwa ajili ya maendeleo ya umma yeye ataoa shilingi moja vilevile juu yake.

Huu ulikuwa sasa wakati wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).

Kitendo hiki cha Aga Khan kilikuwa msaada mkubwa kwa Waislam kwani wakati wa ukoloni ni Ukristo pake yake ndiyo ulikuwa na fursa ya kupata misaada kutoka nje.

Ushirikiano huu wa Aga Khan na Waislam wa Tanganyika uliendelea vizuri sana.
Aga Khan kupitia EAMWS alijenga shule nyingi hadi kufikia sasa kutaka kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam chini ya usimamizi wa Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Tewa Said Tewa na Aziz Khaki aliyekuwa mwakilishi wa Aga Khan Tanzania.

Hii ilikuwa mwaka 1968 baada ya Tanganyika kuwa huru.

Aga Khan na EAMWS kutaka kujenga chuo kikuu hapo ndiyo matatizo yakaanza baina ya Nyerere na uongozi wa EAMWS.

Kisa hiki ni maarufu hapana haja ya kukirejea.

Sasa tuingie kwenye kisa chenyewe.

Miaka mingi ikapita na mwishowe Nyerere akatoka madarakani na serikali ikashikwa na Ali Hassan Mwinyi.

Kwa takriban miaka 20 Aga Khan hakupata kutia mguu Tanzania.
Katika utawala wa Mwinyi Aga Khan akaja Tanzania.

Katika mazungumzo na Rais Mwinyi, Rais Mwinyi akaomba msaada wa Aga Khan katika nyanja tatu - Elimu, Kilimo na Afya.

Aga Khan akamueleza Rais Mwinyi kuwa Aga Khan walikuwapo Tanzania miaka ya nyuma wakisaidia katika elimu kupitia EAMWS.

Hili suala la elimu likamgusa sana Aga Khan kiasi cha yeye alipomaliza mazungumzo na Mwinyi akamwamrisha Katibu wa Elimu wa Aga Khan Tanzania, Riyaz Gulamani awakaribishe viongozi wa Waislam wa iliyokuwa EAMWS pamoja na viongozi wa BAKWATA katika chakula cha jioni ili wajadili maendeleo ya Waislam.

Katika viongozi wa EAMWS walioalikwa katika hafla ile alikuwa Tewa Said Tewa.
Kutoka BAKWATA walioalikwa walikuwa Sheikh Mkuu wa BAKWATA Hemed bin Jumaa, Adam Nasibu aliyekuwa katibu wa BAKWATA, Mustafa Songambele mzee wa CCM na mwanakamati katika BAKWATA na Waislam wengineo.

Kutoka EAMWS aliyealikwa alikuwa Tewa Said Tewa.

Baada ya chakula Aga Khan akawaeleza nia yake ya kuwaita na akawataka watoe wanachotaka wafanyiwe na Aga Khan katika elimu.

Hapa ndipo ''drama,' ilipoanza.

Akasimama kiongozi mmoja wa BAKWATA na mzee wa CCM, Mustafa Songambele, akamwambia Aga Khan, ''Serikali ya Tanzania inawatosheleza Waislam katika elimu na hawahitaji msaada kutoka kokote.''

Mustafa Songambele...

Naomba nisimame hapa.

Mkasa huu kwa mara ya kwanza alinihadithia Riyaz Gulamani.
Sikuamini kama inaweza kuwa kweli.

Kisa hiki nikaja kuhadithiwa tena na Tewa Said Tewa kama vile alivyonihadithia Riyaz Gulamani.

Hapo ndipo nikaamini kuwa kisa kile hakika kilitokea na Mzee Tewa akanipa na jina la huyo aliyesema maneno yale.

Tuendelee.

Aga Khan kwa upole kabisa akajibu kuwa jana yake alikuwa na Rais na yeye kaomba msaada wa elimu.

Hapo sasa ndipo likazuka zogo baina ya viongozi wa BAKWATA na Waislam wengine mbele ya mgeni Aga Khan.

Kufupisha mkasa.

Kabla hajaondoka kufuatia yale aliyosikia na aliyoshuhudia, Aga Khan akamwambia Riyaz, ''Inaelekea hawa ndugu zetu bado hawajawa tayari lakini ushauri wangu ni kuwa uache mlango wetu wazi.

Siku yoyote watakapokuwa tayari basi tutatoa msaada.''
Kwa maneno yako mwenyewe, kumbe Agha Khan alishagundua kiwa "Waislamu wa Tanzania HAWABEBEKI". Maana Rais Mwislamu Mwinyi kamkaribisha kiongozi wa dini ya Kiislamu Agha Khan. Naye Aga Khan kaitisha mkutano wa Waislamu ambao una mchanganyiko wa BAKWATA na EAMWS. Na kwenye mkutano huo HAKUKUWA na MKRISTU hata mmoja. Mumeshindwa KUELEWANA, bado Mohamed Said unawalaumu JK Nyerere na WAKRISTU.

Wewe ni mzee wa HOVYO
 
Mumepewa na B W Mkapa chuo cha TANESCO Morogoro ili kiwe Chuo cha Kiislamu. Niambie nini kinaendelea pale toka mupewe yapata miaka 20 sasa.

Mzee unalalamika sana mpaka unadhalilisha Uislamu
Stunex,
Mimi silalamiki na laiti ningekuwa hivyo ningepata sifa ya ulalamishi.

Mimi nina heshima yangu katika utafiti wa historia ya Tanzania.

Kitabu nilichoandika cha Abdul Sykes kimebadilisha historia ya Julius Nyerere na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Utafiti wa tatizo la elimu kwa Waislam limeonyesha yale ambayo waliokuwa wakifanya hujuma wamefahamika.

Nimeweka Research Papers hapa nilizowasilisha vyuo vikuu ndani na nje ya mipaka yetu bahati mbaya hajatokea mtu kati yenu aliyetaka kujadili paper hizi.

Kilicho chepesi kwenu ni uandishi wa jeuri na kejeli.

Stunex,
Mohamed Said kalamu yake haijadhalilisha Uislam.

Picha kutoka Maktaba yake zimethibitisha ukweli wa aandikayo.

Nimekuwekeeni hapa video clips mtazame.

Jukwaa zima likawa kimya.

Nimekuwekeeni clip hapa nazungumza Ikwiriri katika Bibi Titi Festival mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa naeleza yaliyotokea nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata Nyerere alipokwenda kutoa taarifa kuwa Waingereza wamekataa kusajili TANU kwa kisingizio kuwa chama hakina wanachama.

Hiki kilikuwa kikao cha watu wanne siku ile: Mama mwenye nyumba Bi. Zainab mke wa Ally Sykes. Huyu Ally Sykes kadi yake ya TANU No. 2, Abdul Sykes kadi ya TANU No. 3 na Julius Nyerere kadi ya TANU No. 1 ya Territorial President wa TANU.

Katika kikao hiki cha kujadili usajili wa TANU nikamleta Said Chamwenyewe.

Huyu ndiye Mohamed Said.

Waziri Mkuu alipozungumza kufunga Bibi Titi Festival alisema historia ya kweli isomeshwe wanafunzi wawajue wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.
 
Papasa,
Mbona ghafla umeghadhibika?

Maraisi Waislam hawakuchaguliwa na wananchi kuja kuudumia Uislam.

Wangefanya hivyo wangesababisha vurugu nchini.

Ingekuwa hatujatia maanani elimu EAMWS isingetaka kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968.

Hapa unelalama ni wewe mimi nakueleza historia ya kweli kumekuwa na njama ndani ya serikali kuwazuia Waislam wasipate elimu.

Waislam wamefanya maandamano mwaka wa 2012 kupinga hujuma za NECTA dhidi ya shule za Kiislam.

Katika miaka ya 1970 OIC ilitaka kujenga Chuo Kikuu serikali ikakataa kutoa kibali.

Huna unachokijua.
Wewe ambae unajikuta unajua Sana unatuletea hadithi za abunuasi zisizokua kua na maana, unakuja kusema wali dhurumiwa ili iweje sasa🤔🤔 haya maandiko yako hayana maana hata kidogo kwenye ulimwengu tulio nao sasa hivi kakusanye wafia dini wenzio ukawahadithie hizo hadithi zako za abunuasi, tena unapaswa kuupuzwa kabisa huna maana
 
Stunex,
Mimi silalamiki na laiti ningekuwa hivyo ningepata sifa ya ulalamishi.

Mimi nina heshima yangu katika utafiti wa historia ya Tanzania.

Kitabu nilichoandika cha Abdul Sykes kimebadilisha historia ya Julius Nyerere na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Utafiti wa tatizo la elimu kwa Waislam limeonyesha yale ambayo waliokuwa wakifanya hujuma wamefahamika.

Nimeweka Research Papers hapa nilizowasilisha vyuo vikuu ndani na nje ya mipaka yetu bahati mbaya hajatokea mtu kati yenu aliyetaka kujadili paper hizi.

Kilicho chepesi kwenu ni uandishi wa jeuri na kejeli.

Stunex,
Mohamed Said kalamu yake haijadhalilisha Uislam.

Picha kutoka Maktaba yake zimethibitisha ukweli wa aandikayo.

Nimekuwekeeni hapa video clips mtazame.

Jukwaa zima likawa kimya.

Nimekuwekeeni clip hapa nazungumza Ikwiriri katika Bibi Titi Festival mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa naeleza yaliyotokea nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata Nyerere alipokwenda kutoa taarifa kuwa Waingereza wamekataa kusajili TANU kwa kisingizio kuwa chama hakina wanachama.

Hiki kilikuwa kikao cha watu wanne siku ile: Mama mwenye nyumba Bi. Zainab mke wa Ally Sykes. Huyu Ally Sykes kadi yake ya TANU No. 2, Abdul Sykes kadi ya TANU No. 3 na Julius Nyerere kadi ya TANU No. 1 ya Territorial President wa TANU.

Katika kikao hiki cha kujadili usajili wa TANU nikamleta Said Chamwenyewe.

Huyu ndiye Mohamed Said.

Waziri Mkuu alipozungumza kufunga Bibi Titi Festival alisema historia ya kweli isomeshwe wanafunzi wawajue wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Hicho kitabu cha Abdul Sykes ni novel yako tu wewe, haiwezi kamwe ikabadilo historia ya Nyerere na uhuru wa Tanganyika.

Hata hao unaowalilia kama wazee wako mbona Nyerere aliwapa nafasi nyingi tu Serikalini mpaka umauti ulipowafika??

Ajabu unalalamika wewe lakini wao HAWAKUWAHI kulalamika hata Nyerere alipotoka madarakani.
 
Wewe ambae unajikuta unajua Sana unatuletea hadithi za abunuasi zisizokua kua na maana, unakuja kusema wali dhurumiwa ili iweje sasa🤔🤔 haya maandiko yako hayana maana hata kidogo kwenye ulimwengu tulio nao sasa hivi kakusanye wafia dini wenzio ukawahadithie hizo hadithi zako za abunuasi, tena unapaswa kuupuzwa kabisa huna maana
Papasa,
Si rahisi kunipuuza na ndiyo sababu wewe hujaweza kufanya hivyo.

Uko hapa unanisoma.

Niandikayo si hadithi ni historia ambayo walijaribu watu kuifuta.

Leo kitabu changu kilichochapwa mwaka wa 1998 kiko toleo la nne kinakwenda la tano.

Kitabu kinajadiliwa hapa JF sasa zaidi ya miaka 10 na kimesababisha niwe Mwandishi Bora Jukwaa la Historia kwa miaka miwili mfululizo 2021 na 2022.

Kitabu changu kiko katika Cambridge Journal of African History kupitia mabingwa wa African History: John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Utanikuta vilevile ndani ya Dictionary of African Biography (DAB).

Jiulize imekuwaje?
Nini sababu ya haya yote?

Haya hayapatikani kwa kuandika hadithi kama unavyodai.

Uandishi wa riwaya una watu wake lakini mimi sikujaaliwa kuwa kwenye kundi hilo.

Haya yanapatikana kwa kuandika mambo yanayoongeza elimu katika duru za Vyuo Vikuu na kwengineko.
 
Kwa maneno yako mwenyewe, kumbe Agha Khan alishagundua kiwa "Waislamu wa Tanzania HAWABEBEKI". Maana Rais Mwislamu Mwinyi kamkaribisha kiongozi wa dini ya Kiislamu Agha Khan. Naye Aga Khan kaitisha mkutano wa Waislamu ambao una mchanganyiko wa BAKWATA na EAMWS. Na kwenye mkutano huo HAKUKUWA na MKRISTU hata mmoja. Mumeshindwa KUELEWANA, bado Mohamed Said unawalaumu JK Nyerere na WAKRISTU.

Wewe ni mzee wa HOVYO
Stux...
Hakuna sababu ya kunitukana.
Hivyo utavuruga mjadala.

Tunaweza tukafanya mjadala wa heshima na adabu.

Huu mkutano wa Aga Khan haukuwa kati yake na EAMWS na BAKWATA.

Kikao hichi kilikuwa kati ya Aga Khan na BAKWATA.

Rejea ondoa ghadhabu katika kifua chako na usome upya.

EAMWS ilishapigwa marufuku na Tewa Said Tewa alialikwa kama kiongozi wa zamani wa EAMWS.
 
Papaya,
Tuchukue jambo moja kisha lingine.

Tuanze na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Historia ya kweli ilifutwa ikapachikwa nyingine.

Hii ilikuwa shida.

Kuondoa hii shida nikaandika kitabu cha Abdul Sykes.

Kitabu hiki ni maarufu naamini unakifahamu.
Historia ya kweli ni ipi?
 
Sijasoma yote ila Bakwata ...ni Taasisi?
Wako serious?

Wana katibu kabisa anaelipwa mishahara?
Au anajitolea?
Wana plans?
Source ya income?
Wana shule ngapi?
Vyuo?
Wana mkurugenzi wa elimu?
Wana vitabu au waandishi vitabu?
Bakwata yote ina PhD ngapi?

Nikipata majibu haya ndo ntakuja kuwachukulia serious..

Wana hata ripoti ya fedha na matumizi ya kila mwaka?
 
Kuwa na adabu. Jibu hoja zake kama huwezi kaa kimya.
Wacha jazba mzee wangu.Historia ya Tanzania imeandikwa na iko sahihi.Tatizo lako ni kutazama.kila kitu katika miwani ya Uislamu.
Unataka kuwa na hati miliki ya ukweli kuhusu Uhuru wa nchi yetu.Acha ushamba
 
Uzalendo....
Kwanza Reseach Paper hii ni Sehemu ya Tatu ya kitabu cha Abdul Sykes.
Research Paper yenyewe ni hiyo hapo chini:
Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)

Nakuwekea nyongeza:
Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
Duh
 
Yehoda,
Hili lilikuwa moja ya mabango katika maandamano dhidi ya NECTA chini ya uongozi wa Dr. Ndalichako.

Unasemaje?

Kuna maandamano yalifanywa kumkataa Aga Khan au Aziz Khaki au Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Waislam waliikubali BAKWATA?

Huna unachokijua kuhusu historia ya Waislam.

Isome kwanza ndiyo uje kujadili.
Wahusika wakuu wako kimya hawana mdomo wa kujadili haya.

Wanaogopa.
Unajibu wewe usiyohusika.

Historia ya waislam eeeeeh?Tutajie wasome watano wazalendo waliosomeshwa bure na taasisi za Agha Khan
 
Hicho kitabu cha Abdul Sykes ni novel yako tu wewe, haiwezi kamwe ikabadilo historia ya Nyerere na uhuru wa Tanganyika.

Hata hao unaowalilia kama wazee wako mbona Nyerere aliwapa nafasi nyingi tu Serikalini mpaka umauti ulipowafika??

Ajabu unalalamika wewe lakini wao HAWAKUWAHI kulalamika hata Nyerere alipotoka madarakani.
Stux...
Cambridge Journal of African History haichapi mapitio ya vitabu vya riwaya.

Inawezekana wewe unataabika na ukweli lakini walimu wa historia ya Afrika vyuo vingi wanaposomesha historia ya utaifa wa Tanganyika huanza na Kleist Sykes na Dr. Kwegyr Aggrey mwaka wa 1924.

Hapa huwaelekeza wanafunzi kusoma maisha ya wazalendo hawa wawili katika Dictionary of African Biography (Oxford University Press New York 2011) kisha huwaelekeza pia kusoma, Modern Tanzanians, (Tanzania Publishing House, Dar es Salaam 1973) kitabu alichohariri John Iliffe wasome, ''The Townsman Kleist Sykes,'' mwandishi Aisha ''Daisy'' Sykes.

(Unaweza kusoma historia hii Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam East Africana: ''The Life of Kleist Sykes,'' Ref. No. JAN/HIST/143/15).

KIsha anawapa rejea ya kitabu cha Abdul Sykes (1998) wasome.

Hakuna mwalimu atakaegusa Historia ya TANU ya Kivukoni na vitabu vingine labda kwa kupita kuwaonyesha wanafunzi umuhimu wa kuandika ''Corrective History.''

Kuna mengine unayoandika nayanyamazia kwa kuwa si maudhui ya mjadala wetu.

1703589904031.png

1703590094605.png

1703590227694.png
 
Back
Top Bottom