Miaka 61 ya Uhuru: Japo Tumefanikiwa sana kielimu, shule, vyuo na wasomi (Madaktari na Maprofesa kibao), mbona bado adui ujinga yupo? Tunakwama wapi?

Hakuna mahala tulipofanikiwa kwenye elimu. Toka uongozi wa mkapa kulikuwa na mkakati kabisa wa chini chini wa kushusha kiwango cha Elimu ama kwa kuelewa au bila kuelewa.
Elimu ya ukweli iliishia enzi za Makweta. Kipindi hicho watoto wote wanasoma shule Aina moja,kuanzia watoto wa viongozi,machief wa masikini wote ilikuwa shule moja. Na elimu iliyokuwa inatolewa ilikuwa Bora sana na ndio maana hata viongozi watoto wao tulichanganyikana nao kwenye hizo shule.
Enzi hizo mwanafunzi wa darasa la Saba alikuwa ana uwezo wa kuongea kiingereza vizuri tu hata masomo mengine walikuwa na uwezo pia. Muhimu enzi hizo walikuwa wanaandaliwa pia kujitegemea. Ilikuwa ukishindwa kuendelea na masomo lazima utatoboa kwenye stad zingine kama biashara,ufundi n.k.

Lakini elimu ya sasa mtoto wa form four hamna kitu. Hata mwandiko wake tu kama wa darasa la 5 wa zamani. Pia hawa wa sasa akishindwa tu darasani au hata akimaliza chuo,hana uwezo wa kujitegemea na kujiajiri ndio hawa panya rod na wengine. Na hiyo yote ndio maana nimesema elimu inashushwa makusudi ili familia kubwa zenye uwezo waendelee kuwatawala watoto wa masikini ambao hawajasoma shule nzuri. Viongozi wanajenga madarasa mengi lakini watoto wao wanawapeleka kusoma nje. Huko wanapata elimu Bora kuliko hawa walioshushiwa elimu.

Na ndio maana ni vigumu kwa sasa kwa waliohitimu vyuo bongo kupata ajira nje ya nchi. Tofauti na zamani akina Mseven,Kabila na wengine wamepitia vyuo vyetu walikuwa bora. Pia ndio maana ni vigumu kupambana na nchi jirani kama Kenya kwenye ajira.

Pia hizi shule binafsi kwetu zimechangia sana zimeharibu sana elimu yetu. Ksbb wao wanamfundisha mwanafunzi kukariri sio kuelewa. Pia mwanafunzi wetu ndani anafundishwa namna ya nyingi ya kupata mafanikio tu katika maisha ,ndio maana wengi utasikia somea hii ksbb ina ajira baadae.

HATUJAFANIKIWA KWENYE ELIMU KABISA. KUFANIKIWA KWA ELIMU KIGEZO CHAKE NI WAHITIMU WA VYUO VYETU KUJITAFUTIA AU KUPATA AJILA NJE YA NCHI BILA SHIDA. YAANI MHITIMU AJIUZE KIAJILA NJE YA MIPAKA YA TZ KAMA ILIVYO KWA WAKENYA,NIGERIA,GHANA N.K

NB; UKIKUTANA NA MBONGO NJE YA NCHI KAMA DUBAI NI MUOGA HATARI. YAANI KILA WAKATI ANAOGOPA ANAONA KAMA ATAVUNJA SHERIA YA HUKO. WAKATI HUO HUO KUTANA NA M-NIGERIA,YUKO HURU SANA KSBB NYINGI KWANZA ELIMU,PILI WANAFUNDISHWA SANA NCHINI MWAO NAMNA YA KUJITEGEMEA PIA KIKUBWA WANAFUNDISHWA SANA SHERIA ZA KIMATAIFA. UKIWA NCHI NYINGINE UISHIJE. NA NDIO MAANA WANIGERIA WAMETAPAKAA ULAYA NA AMERICA NA KWINGINEKO KWENYE FURSA NZURI. NA WANA MAFANIKIO MAKUBWA SANA. SISI HATUNA HATA HIYO NDOGO TU KUFUNDISHWA SHERIA NAMNA TU KIDOGO UISHIJE UKIWA NCHI NYINGINE.
 
Kwanza wasomi wengi wamegundua pesa ni bora kuliko elimu na hivyo kuamua kutumia elimu yao kujipatia pesa kwa kila njia (wizi,ufisadi,uongo na uchawa),watu wanaakili nzuri lakini pesa mbele.pili demokrasia nzuri hakuna ambayo ingewasaidia watu wote kuwa huru kuhoji na kushindana kwa hoja kwa uhuru. Nashauri itungwe sheria ya kuwalazimisha wagombea wote wa Urais,ubunge na udiwani kuwa na mdahalo wa live mbele ya wananchi mara 3 katika muda wa kampeni ili tushindanishe hoja na kuangalia hisia zao wakiwa pamoja.
 
Safi sana tuanzie na hili. Kwa walioelimika wote kuanzia Paskal Mayala tukianzia kwenu kuikataa ccm iliyodumaza mifumo yetu yote kuanzia elimu.
 
Ukiachana na wale maadui watatu aliowataja baba wa Taifa yaani ujinga , umaskini na maradhi .

Sasa ameongezeka adui mwingine " UCHAWA" , huyu amekula akili za watu mpaka pamoja na elimu zao wanashindwa kusaidia Taifa kwa kuendekeza kujipendekeza kwa wenye mamlaka kwa manufaa yao.
 
Ma Professa kama Mwigulu anaechanganya deni la makampuni binafsi na deni la serikali.
 
Walioelimika ndo hawa wanaigeuza nchi kuwa soko la China badala ya kuwa wazalishaji malighafi kwa Kilimo?
Hao walioelimika wanashindwa kuleta Uwekezaji mkubwa wa Kilimo kwenye Nchi inayolimika Kila Wilaya na wanaendelea kung'ng'ania VIWANDA vya YEBO YEBO ambavyo ni mabomba ya hela yetu kwenda China??
Wasomi wasifu Ujenzi wa VIWANDA kwenye Nchi isiyo na Malighafi...
 
Inawezekana ule ujinga wa kutojua kusoma na kuandika umetoka, nadhani tafsiri ya ujinga iende mbele zaidi ya kujua kusoma na kuandika.

Kusoma na kuandika ni tools za kuondoa ujinga, baada ya kuwa na hizo tools, kama taifa, Sasa tujue ni ujinga gani tunao ili tukaufute.
 
Umenikumbusha kisa cha dada mmoja muhitimu wa PhD muhimbili alipomugomea rais Mwinyi.
 
Umenikumbusha kisa cha dada mmoja muhitimu wa PhD muhimbili alipomugomea rais Mwinyi.
Naomba utukumbushe, mdada, msomi, kamgomea rais wa nchi?!. Sio lazima kumtaja jina ila tukumbushe kisa.
P
 
Tafsi ya kawaida ya MSOMI ni hali ya kukabiliana na matatizo na kuyachanganua kwa mapana na si, vinginevyo.
kama tukishidwa kujua nadharia hii ni vyema tungepunguza idadi ya Dr na prof,kwa maana ya uhaba wao kulitumia vizuri maarifa waliyo yapata.
Kuleta madhara kwenye jamiii zetu na Taifa kwa ujumla
 
Paskali asante kwa mada nzuri na imenipa kutafakari kiasi. Matokeo ya kutafakari kwangu nimeona pana shida moja kubwa kwamba kupiga vita adui ujinga kulihusisha eneo moja tu kusoma na kuandika na maeneo mengine yakaachwa. Hili la kuhimiza kusoma na kaundika halikuja kwa bahati mbaya ilipangwa kwa matarajio kuwa watu wakijua kusoma na kauandika ni rahisi kutafuta na kutumia maarifa. Sasa waliosoma na kujua kuandika wamebaki na kujua kusoma na kuandika tu hawatumii silaha zao; wanaozitumia 90% wanazitumia vibaya. Hapa ndipo tatizo lilipo, tukijinasua hapo tutafanikiwa vinginevyo vita ya kupiga ujinga ni endelevu na kibaya sana binafsi
 
Hatujakwama. Ni kwamba binadamu wapya wanazaliwa kila siku, na wanazaliwa wakiwa wajinga (yaani hawajui kitu) na wakiwa maskini (yaani hawamiliki mali yoyote).

Kwa hiyo kazi ya kupiga vita ujinga na umaskini ni kazi ya kudumu. Haina mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…